Oloronyo
Member
- Mar 29, 2009
- 80
- 9
Yule Nguli wa miziki yenye mahadhi ya Pwani yaani Taarab amefariki dunia,Jijini Dar. Hii ni kwa mujibu wa mtangazaji wa Leo tena wa Clouds FM Dina Marios.
Nasma Hamisi 'Kidogo' amefariki dunia juzi usiku katika hospitali ya Temeke jijini Dar.
Kwa habari za uhakika zilizopatikana kutoka kwa ndugu wa karibu wa marehu zinaeleza kuwa Nasma alilazwa katika hospitali ya Temeke ijumaa mchana akisumbuliwa na malaria pamoja na presha ya kushuka,ugonjwa huo ulikuwa ukimsumbua kwa takriban miaka miwili.
Msiba upo kwa baba yake mdogo,Mzee Kaniki.Kinondoni maeneo ya ya hananasifu karibu na shule ya TAPA,Mazishi yanatarajiwa kufanyika leo saa saba mchana kwenye makaburi ya kisutu jijini dar.
Baadhi ya nyimbo alizotamba nazo msanii huyo ni Mwanamke mazingira,Subira Heri,Mpenzi na sanamu la michelin,pia enzi za uhai wake aliimbia vikundi kadhaa kikiwemo Egyptian,Babloom,Tanzania One Theatre na Muungano Cultural Troup.
Nasma ameacha watoto sita, wanne wa kike na wawili wa kiume.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-AMIN
Nasma Hamisi 'Kidogo' amefariki dunia juzi usiku katika hospitali ya Temeke jijini Dar.
Kwa habari za uhakika zilizopatikana kutoka kwa ndugu wa karibu wa marehu zinaeleza kuwa Nasma alilazwa katika hospitali ya Temeke ijumaa mchana akisumbuliwa na malaria pamoja na presha ya kushuka,ugonjwa huo ulikuwa ukimsumbua kwa takriban miaka miwili.
Msiba upo kwa baba yake mdogo,Mzee Kaniki.Kinondoni maeneo ya ya hananasifu karibu na shule ya TAPA,Mazishi yanatarajiwa kufanyika leo saa saba mchana kwenye makaburi ya kisutu jijini dar.
Baadhi ya nyimbo alizotamba nazo msanii huyo ni Mwanamke mazingira,Subira Heri,Mpenzi na sanamu la michelin,pia enzi za uhai wake aliimbia vikundi kadhaa kikiwemo Egyptian,Babloom,Tanzania One Theatre na Muungano Cultural Troup.
Nasma ameacha watoto sita, wanne wa kike na wawili wa kiume.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-AMIN