EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
UPDATE
Mila na desturi kisa cha harusi kutofungwa
Hii ni update kuhusu yule Bi harusi aliyeingia mitini. Chanzo cha harusi kutofungwa kilitokana na kutokuwa na mawasiliano mazuri na washenga wake ambao ni Bwana Amoni Mwangosi ambaye ni mshenga wa Bibi harusi na Bwana Angolile Mwakisilwa ambaye ni mshenga kwa upande wake wa Bwana harusi.
Bwana harusi alitumia watu wengine kupeleka nauli ya Sh. 24,000/= ya kumchukua bi harusi na mpambe wake bila kufuata taratibu za kimira za kuwajulisha washenga wake ndiyo waende kumchukua mchumba wake hata hiyo watu hao walikataliwa kwa kutotambuliwa na familia hiyo ya bi harusi na kutaka wahusika wafike ili wakabidhiane kwa taratibu zinazotambulikana.
Kwa upande wake wa Mzazi wa Bibi harusi Mzee Akimu Mwalukosya, amesema hana kinyongo bali yaliyopita si ndwele na wagange yajayo kwani makosa yaliyofanyika yanazungumzika.
Jana (Jumanne) jioni kamati ya maandalizi upande wa bwana harusi walikutana kujadili suala hilo. Hata hivyo kamati ya sherehe ya bwana harusi itakutana leo (Jumatano) kupata hatima ya harusi hiyo.
Bi harusi wakiwa na mama yake
Wakati wakichumbiana
Hii ni kwa mujibu wa blogu ya Mbeya Yetu. Jana Bi harusi mmoja aliingia mitini; hakutokea kabisa kanisani wala kwenye ukumbi wa sherehe. Wanakamati walishikwa na butwaa huku wengine wakilia. Licha ya Bi harusi kuingia mitini, sherehe iliendelea kama kawaida ukumbini jana usiku. Bwana harusi alishindwa kuja ukumbini kwa machungu aliyokuwa nayo. Kwa mujibu wa blogu hiyo sababu ya Bi harusi kuingia mitini bado haijafahamika. Sikupenda kuweka picha lakini kwa vile leo ni April fool watu wasingeamini hii habari.
Maandalizi ya ukumbi wa harusi kama yalivyokuwa yanaonekana jana.
Wanakamati wa harusi baada ya kupewa taarifa yakuingia Bi harusi kuingia mitini. Baadhi yao waliangua kilio ukumbini hapo.
Wazazi wa bwana harusi wakishuusha maombi ukumbini hapo.
Wazazi na ndugu wa bwana harusi wakiwa mbele ya wageni waalikwa.
Dada za bwana harusi pamoja na wazazi wakipokea zawadi kwa niaba ya bwana harusi ambaye naye alishindwa kuja ukumbini kwa machungu aliyokuwanayo
Baadhi ya waalikwa wakiwa haamini kilichotokea
Mama mzazi wa bwana harusi akitambulishwa bila kuwepo kwa maharusi.
Kwa picha na habari zaidi tembelea blog ya Mbeya yetu: Mbeya Yetu
Mila na desturi kisa cha harusi kutofungwa
Hii ni update kuhusu yule Bi harusi aliyeingia mitini. Chanzo cha harusi kutofungwa kilitokana na kutokuwa na mawasiliano mazuri na washenga wake ambao ni Bwana Amoni Mwangosi ambaye ni mshenga wa Bibi harusi na Bwana Angolile Mwakisilwa ambaye ni mshenga kwa upande wake wa Bwana harusi.
Bwana harusi alitumia watu wengine kupeleka nauli ya Sh. 24,000/= ya kumchukua bi harusi na mpambe wake bila kufuata taratibu za kimira za kuwajulisha washenga wake ndiyo waende kumchukua mchumba wake hata hiyo watu hao walikataliwa kwa kutotambuliwa na familia hiyo ya bi harusi na kutaka wahusika wafike ili wakabidhiane kwa taratibu zinazotambulikana.
Kwa upande wake wa Mzazi wa Bibi harusi Mzee Akimu Mwalukosya, amesema hana kinyongo bali yaliyopita si ndwele na wagange yajayo kwani makosa yaliyofanyika yanazungumzika.
Jana (Jumanne) jioni kamati ya maandalizi upande wa bwana harusi walikutana kujadili suala hilo. Hata hivyo kamati ya sherehe ya bwana harusi itakutana leo (Jumatano) kupata hatima ya harusi hiyo.
Bi harusi wakiwa na mama yake
Wakati wakichumbiana
Hii ni kwa mujibu wa blogu ya Mbeya Yetu. Jana Bi harusi mmoja aliingia mitini; hakutokea kabisa kanisani wala kwenye ukumbi wa sherehe. Wanakamati walishikwa na butwaa huku wengine wakilia. Licha ya Bi harusi kuingia mitini, sherehe iliendelea kama kawaida ukumbini jana usiku. Bwana harusi alishindwa kuja ukumbini kwa machungu aliyokuwa nayo. Kwa mujibu wa blogu hiyo sababu ya Bi harusi kuingia mitini bado haijafahamika. Sikupenda kuweka picha lakini kwa vile leo ni April fool watu wasingeamini hii habari.
Maandalizi ya ukumbi wa harusi kama yalivyokuwa yanaonekana jana.
Wanakamati wa harusi baada ya kupewa taarifa yakuingia Bi harusi kuingia mitini. Baadhi yao waliangua kilio ukumbini hapo.
Wazazi wa bwana harusi wakishuusha maombi ukumbini hapo.
Wazazi na ndugu wa bwana harusi wakiwa mbele ya wageni waalikwa.
Dada za bwana harusi pamoja na wazazi wakipokea zawadi kwa niaba ya bwana harusi ambaye naye alishindwa kuja ukumbini kwa machungu aliyokuwanayo
Baadhi ya waalikwa wakiwa haamini kilichotokea
Mama mzazi wa bwana harusi akitambulishwa bila kuwepo kwa maharusi.
Kwa picha na habari zaidi tembelea blog ya Mbeya yetu: Mbeya Yetu