beta testers for E-commerce site

Kivuko

Member
Jul 12, 2009
66
4
PM me if you are interested to test-drive a Tanzanian E-commerce Site.

for general Viewing take a look here.

regards.
 
Tunaandaa toleo la Kiswahili,likiwa tayari watumiaji watakuwa na uwezo wa kuchagua lugha waipendayo.

Upande wa customer service na support staff wetu wanaweza kukusaidia kwa kiswahili au English.
 
Last edited:
seen some issues,paypal express checkout has some issues,wont go through with the transaction, and it fails to redirect back as well.

others aspects are just fine,still testing..,
 
seen some issues,paypal express checkout has some issues,wont go through with the transaction, and it fails to redirect back as well.

others aspects are just fine,still testing..,

THANKS FOR DISCOVERING THAT.

It was caused by paypal system not accepting Tanzanian Shillings as one of the preferred currencies.one of the things we have to trade off to support Tshs.

Now it is fixed and working.

welcome.
 
Last edited:
Wakuu hebu nijuzeni kuhusu kivukoni dot kom, hivi hili ni duka au soko? napenda kufahamu kuhusu huduma zao, je wanaaminika? kuna watu walishawahi kkununua huko? Nimeona kuna mtu wa kivukoni humu ndani, atafanya vizuri zaidi kama akiwafafanulia watu wote humu ndani. Kama ni duka wapi physical adress? Kama ni soko security yake ikoje?
 
Wakuu hebu nijuzeni kuhusu kivukoni dot kom, hivi hili ni duka au soko? napenda kufahamu kuhusu huduma zao, je wanaaminika? kuna watu walishawahi kkununua huko? Nimeona kuna mtu wa kivukoni humu ndani, atafanya vizuri zaidi kama akiwafafanulia watu wote humu ndani. Kama ni duka wapi physical adress? Kama ni soko security yake ikoje?


Ndugu Amoeba,

nakushukuru wewe na wengine wote waliotuma PM zao kuuliza maswali tofauti.

Kivuko.com ni "duka" au "soko"?

Kivuko.com ni zaidi ya duka na si kama soko ulilolizoea.
Hatuuzi bidhaa zetu kwenye "traditional brick and mortal shops".Duka letu lipo www.kivuko.com.
Ofisi zetu haziifadhi bidhaa za wateja,zinatumika kama kiunganisho cha "end suppliers" na mtumiaji.Kwa hiyo ofisi yetu haifanani na maduka tuliyoyazoea,ingawa tunauza bidhaa.
kwa anuani ya ofisi zetu tazama hapa.

Pindi mtu anapoweka oda yake kivuko.Sisi hupitia mlolongo maalum wa kuitoa bidhaa hiyo kutoka kwa watengenezaji/wasambazaji (distributors/suppliers) hadi kwa mtumiaji.
Kwa lugha rahisi kivuko.com inafanya kazi ya kuunganisha watumiaji na vyanzo bora vya bidhaa.


Je kivuko ni "soko?"

Bidhaa zinazouzwa kivuko ziko chini ya usimamizi wa kampuni ya kivuko,ambayo inachukua "responsibility" ya bidhaa zote tunazoziuza.

Ingawa kuna Baadhi ya bidhaa zinapatikana kupitia ma-vendor wetu.kwa sasa idadi yao ni ndogo na asilimia kubwa ya wasambazaji wetu wako nje ya Tanzania.

Ingawa kuna uwezekano wa kuwa na mavendor sio kila mtu anaweza kuwa vendor/supplier wa kivuko.Nia yetu ni kufupisha "supply chain" ya bidhaa ili kupunguza gharama kwa mtumiaji.Tunazingatia sana authenticity,kiwango,ubora na uhalisi wa bidhaa kabla ya kukubali mtu/kampuni kuwa vendor wetu.(lakini tunapenda kuwakaribisha wote wenye nia na wanaofikia vigezo kuwa ma-vendor wa kivuko)

kwa hiyo ingawa kivuko ina tabia za duka na soko kihalisia haifananani na duka wala soko.

Kivuko kwa lugha ya kigeni ni B2C au Business 2 consumers.

Tunamuunganisha mteja na chanzo cha bidhaa halisi,bila kutumia "middle men".

sasa kama hatuweki bidhaa dukani zinamfikiaje mtumiaji?wa zanzibar kwa mfano?

Wakati wa kuweka oda yako,utahitajika kujaza anuani yako na namba ya simu.Taarifa hizi zinatusaidia kufikisha Bidhaa kule inakotakiwa kwenda.

Bidhaa nyingi zina "option" ya "free shipping",kutoka kwa Msambazaji/mtengenezaji hadi kwako mtumiaji,na nyingine zinahitaji kulipia gharama kidogo za usafirishaji.
kwa mfano laptop itahitaji $10 kwa "standard shipping".

Kivuko ni Salama?

Kwa tafisri ya kimtandao,kivuko ni moja kati ya mitandao salama zaidi hapa nchini kwetu kwani tumejitahidi kutumia "industry standard" security measures ili kuwezesha watu na taarifa zao binafsi kuendelea kuwa salama katika kipindi chote wanachokuwa kivuko.com.

Moja ya vitu tunavyotumia ni 256-bit secure encryption SSL kulinda taarifa zako ukiwa kivuko.com.

njia za malipo?

Tunatumia payment gateways za "paypal" na "2checkout".hii inamaanisha kwa wale wanaotumia Credit Cards.Taarifa zao zinalindwa na na makampuni bingwa ya E-commerce duniani".

Na kwa wale wasio na Credit card, hamna shaka tunapokea malipo kupitia M-PESA,Z-PESA,Paypal,Kulipia ukipokea (Cash on Delivery),gift certificates, na kupitia Benki.

Vipi kuhusu ubora wa Bidhaa?

Bidhaa zilizopo Kivuko.com ni za "genuine" na zenye "warranty za muda mrefu.na kama ukipokea bidhaa yenye matatizo basi unaweza kubadilisha mpya ndani ya siku 7.

kuna tofauti kati ya kivuko na mitandao mingine ya E-commerce?
Tofauti zipo nyingi,kwani kivuko.com tunaamini katika uboreshaji wa huduma kama njia bora ya kuhudumia wateja wetu.Tunatoa pia huduma za "after sales Consultancy" na online live chat na mmoja kati ya wahudumu wetu.

zaidi ya hapo hauhitaji kuwa mwanachama wa kivuko.com ili kuweza kufanya manunuzi ya bidhaa zako, ingawa wanachama wa kivuko.com watajipatia faida za ziada zinazokuja na uanachama wao.moja kati ya faida hizo ni kuweza kukusanya point kwa kila bidhaa wanayonunua kivuko.com,kujipatia mapunguzo na promosheni nyingine nyingi zinazoelekezwa kwa wanachama.

Kwa wana JF napenda kuchukua nafasi hii kuwakaribishaKivuko.com,Tanzania Online Gateway.

Endelea kutazama ukurasa huu kwani watumiaji wa JF watapokea punguzo maalum kwa kuelewa umuhimu wao katika ukuaji wa teknohama.

wasalam,

cheers!

Kivuko.com
 
Back
Top Bottom