Bernard Membe: Nina maadui 11, ikifika 2016 watakimbilia Kenya!

Kampeni hizo za uraisi 2015, na hawatamuacha......watauana hiyo 2015. Ameomba kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni awe anaulizwa maswali kama ambavyo waziri mkuu huwa anaulizwa......hapo napata kigugumizi kidogo Mh. Mamba, nafahamu kuwa waziri mkuu huwa anaulizwa maswali kwa kuwa yeye pale anaiwakilisha serikali kwani yeye ndie msimamizi wa shughuli zote za serikali bungeni. Lakini pia waziri mkuu huulizwa maswali yanayohusu serikali kwa ajili ya kujua utekelezaji wa mambo mbalimbali kwa walipa kodi ambayo serikali inayasimamia. Ni vizuri pia Mhe. Mamba akafahamu kuwa waziri mkuu huulizwa maswali ali atoe majibu kwani yeye (serikali) ndio hukabidhiwa fungu (bajeti) ya utekelezaji wa shughuli zote za serikali. Sasa iweje leo Mh. Mamba atake kiongozi wa upinzani nae aulizwe maswali na wabunge!!?? Atakuwa anaulizwa juu ya nini?? Hivi lengo la yale maswali ni kutaka kujua uwezo wa waziri mkuu kuyajibu ama kupata majibu ya hoja za msingi zinazohusu utekelezaji wa waliokabidhiwa fedha za walipa kodi?? Namuomba Mh. Mamba kama kweli anataka kiongozi wa upinzani aulizwe maswali basi wamuachie bajeti ya serikali kiongozi wa upinzani ili aisimamie then waje kumuhoji serikali yake imefanya nini. Lakini pia napata picha kuwa kumbe yale maswali huwa ni kupoteza muda tu, kwani kwa mujibu wa mamba, kama hata kiongozi wa upinzani anaweza ulizwa basi huwa si kujibu hoja za walipa kodi bali ni kutaka kujua uwezo wa waziri mkuu kujibu!!!!!!!!...........KAZI NI KWETU
 
Kama hupendi! Fungua fb au eatv kapoteze muda! Unakuja kumlalamikia nani hapa? Mpigie simu semunyu umwambie na sio kuja na hoja zisizo na kichwa wala miguu hapa!
 
Eti huyu naye anataka kuwa rais!!

Yaani tulipokuwa na rais Mwinyi tulifikiri he was the worst president possible, akaja Kikwete tukaona afadhali hata Mzee Ruksa, sasa akija Membe amini usiamini tutaona bora hata Kikwete.
 
hajui Cameron aling`aa wapi?hajui wabunge wa CDM huwa wanafany kazi za kitaifa kuliko kijimbo, kwa vile rasilimali za majimbo zinatoka katika mfuko wa taifa na majimbo yanategemeana.Kasahau kuwa alichosema kinapinga propaganda za CCM.

Hakuna waandishi bongo.Labda akina Generali Ulimwengu na masako wanaweza waweka pazuri hawa vilaza.wengine wote wanakuwa interviewed wao kama si kufany amaigizi na kujichekesha tuu. Hichi kijamaa hakina tofauti na Kale kabunge ka kondoa.Nina wasiwasi kama wakimwita atatokea.

Hivi biandishi vyenye asili ya TBC huwa vikihoji mtu ni kama kumpa kazi mtu amhoji role model wake.
 
Sifa za Kijinga anataka apewe kipindi kingine ndo awataje Jamaa alifanya kipindi part2 ili ataje na tumechoshwa na sound zako oooh!ole wao nikioteshwa ...mara Bae wajisafiche.Wenzako waliona mbele wakakupa zigo la mavi ukatwisha kichwa kichwa issue ya OIC ukajikutaa upo pekee yako.
 
Chezea Membe wewe Dogo ametimba Ethiopia kwa tiketi ya membe kwa mwaka huu tu membe ameshaapear zaidi ya mara 3 kwenye kipindi cha 45 mpaka anaboa. hata kipindi chenye kinapoteza mvuto leading question no research anatumia udaku na story za mitaani/vijiweni kubuild maswali.
 
Kasau kuwa mbunge ni coordinator zaidi ya mtoa pesa.Hajui kuna wadau wengi wa maendeleo ndio maana baadhi ya mikoa n majimbo mambo yao yapo juu bila kujua msaada wa serikali.Sasa kama yeye anachukua hela ktk sehemu zisizostahili na kwenda mwaga jimboni kwake asidhani ndio kuleta maendeleo kwa watu wasiokuwa namaendeleo katika nynja nyingine.hajui kuwa ngoma na mimba za kiholela zinaweza angamiza watu wake ingawa kapeleka kiwanda kwa hela ya ghadafi.Pia hajui kuwa kiwanda kinaweza kuwa kule ila watakaokifaidi wawe watu wengine kabisa na wasio na mchango katika kura zake za ubunge na hata urais.asidhani kiwanda mtwara kitampa kura mbeya, arusha, mwanza, dar, Moshi, tanga ,Iringa, singida, achilia mbali siasa za ukabila na vijiji huku jimbo kwake.

Kasahau kuwa wabunge wa cdm ni mawaziri wa kivuli na ni wa kitaifa achilia mbalia nafasi zao katika chama ni za kitaifa.Jama na personality ya masanamu wa kuvalishwa nguo katika maduka ya nguo anachelewa sana kuona vitu kwa haraka.
 
Ulevi wa madaraka umekolea. Taratibu ya kubadilisha mgombea rais bara visiwani umesahaulika. Hili la mgombea urais kutoka bara mara tatu mfululizo ni sensitive sana and it may very well be the straw that broke the camels back,
 
Ulevi wa madaraka umekolea. Taratibu ya kubadilisha mgombea rais bara visiwani umesahaulika. Hili la mgombea urais kutoka bara mara tatu mfululizo ni sensitive sana and it may very well be the straw that broke the camels back,

habari za kubadilisha rais kwa basis ya bara na visiwani ni regionalism, sio mbali sana na ukabila. Mtanzania awe Mtanzania tu, mkianza kum qualify tutafika hata kusema safari hii kapata mtu wa bara wa kaskazini, safari ijayo apate wa kusini, mwishowe safari hii ******, safari ijayo Muhaya. Hata kama atatokea ****** mwenye sifa zote!

I notice JF is blocking M.kwere, hivi M.kwere ni tusi siku hizi?
 
Tatizo letu tunaangalia sana theatrics kuliko substance.

Ndizo habari hizi hizi za "Membe ana confidence" zilizofanya watu wamchague "JK handsome".

Kwa kweli mie sijaona kitu hata kimoja alichofanya Membe ambacho kina merit presidential ambitions hata za kuota tu.

Labda mniambie, kipi kikubwa alichofanya? Sanasana naona blunders na corruption tu, fiasco na flops tu, hakuna anachoweza kujivunia kwamba kafanya cha kueleweka mpaka sasa.

Tatizo letu wengi hatuwezi kuona past the theatrics na kuchambua mantiki i wapi na maigizo yaso mshiko ya wapi.
Mkuu Kiranga, please usitake kum downplay Membe, kwani Mwinyi kabla hajachaguliwa, alikuwa amefanya nini?. Kwani Ben kabla hajachaguliwa alikuwa amefanya nini?. Kwani JK kabla hajachaguliwa alikuwa amefanya nini?, why tuweke kigezo cha Membe amefanya nini?.


Katika ule wangu wa Mazuri ya JK, tena nakumbuka ni wewe wewe uliuliza kuhusu track record na leadership integrity, nilikuuliza "kwani Watanzania tunachagua nini?" Saikolijia ya uchaguzi inasema mtu anaejieleza vizuri anachagulika zaidi hata kama hayo anayoyaeleza hayana any substance!. Mtu anayetazamika zaidi vizuri zaidi, (HB) anachagulika zaidi kuliko grummy faces, hata kama ni empty upstairs!.

Siku zote debe tupu hutika!, simba mwenda kimya ndio mla nyama!, ukiona watu mnataka kupigana, adui yako akinyamaza tuu kimya huku amekunja ngumi, muogope zaidi kuliko mpiganaji anayepiga kelele, "mshikeni nitamuumiza!' mtu anayepiga kelele sana ujue ni muoga!. Ukitembea usiku peke yako wakati wa giza, uli kuondoa uoga, utajikuta unaimba kwa sauti kubwa!. Kwa jinsi Membe alivyoongea, ameonyesha confidence kubwa, na ni kwa confidence kama hiyo, anaonyesha wazi kuwa kama tutamkosa EL, huyu atatufaa sana kuwa mgombea wa CCM 2015!.

Kama Mwinyi tulimchagua kwa ukimya wake!
Mkapa tukamchagua kwa kuongea kwa ukali wake wakati wote!
JK tukamchagua kwa sura, cheko na bashasha zake!
Why not Membe kwa maconfo yake ya kusubiria kuoteshwa?!.
 
Nimemsikia for the first time he looks genuine and determinant kuwalipua!. Kwa vile alishagabatizwa kuwa yeye ni "Joka la mdimu", wakimaanisha he is only a "barking dogs, seldom bite", kwa jinsi nilivyomsikia akiongea kwa msisitizo, naamini this time itakuwa kweli, na ata prove beyond reasonable doubt kuwa yeye sio "joka la mdimu"!.

Sikufurahishwa alipowataja "Chadema wameenda kwake na njaaa zao, akawapa chakula"!.
Nimependa alipowataja wabaya wake 11 wakiwemo waandishi wa habari wawili na kuahidi muda muafaka ukiwadia, atawalipua kwa kuwataja hadharani!.

Pia nimeipenda ile ya sababu za yeye kuandamwa na hao wabaya wake, ni kwa sababu wao wana jicho la tatu la kuona 2015 itakuwaje, hivyo fitna zote ili ili kumzuia` na kitakachotokea 2015 na kutoa 'ole' kali kuwa "ole wao asioteshwe" kwani akioteshwa...(watakiona cha mtema kuni-emphasis mine!)

Pia nimeipenda confidence aliyoionyesha na sound ya "commanding voice" na "authority" kuthibitisha anaweza kuwa amiri jeshi mkuu!.

Kwa sisi tunaopenda mageuzi ya kweli ya nchi hii, nawashauri tuweke sala zetu kwa umoja wetu ili Membe aoteshwe na tumpigie debe la nguvu ili awe mgombea wa CCM, candidature yake ni muhimu sana kutupeleka kwenye ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania!.

Kama tutamkosa EL, then Membe atatufaa sana!.

Membe for 2015!.
Mkuu Pasco. Tanzania ya 2016 itaongozwa na chama tofauti na CCM hata wao wanafahamu hilo ukiondoa wale wasiotaka kukubaliana na ukweli. Lakini kuna jambo muhimu ambalo litabidi lifanyike. Makabila makubwa ya nchi hii,wachagga,wahaya,wanyakyusa na wasukuma hawana budi kujitokeza na kuchukua jukumu la uongozi wa nchi.
 
habari za kubadilisha rais kwa basis ya bara na visiwani ni regionalism, sio mbali sana na ukabila. Mtanzania awe Mtanzania tu, mkianza kum qualify tutafika hata kusema safari hii kapata mtu wa bara wa kaskazini, safari ijayo apate wa kusini, mwishowe safari hii ******, safari ijayo Muhaya. Hata kama atatokea ****** mwenye sifa zote!

I notice JF is blocking M.kwere, hivi M.kwere ni tusi siku hizi?
Nadhani lengo ni kuondoa sumu ya ukabila kuepuka kuwatambulisha watu kwa makabila yao!.
 
Huyu mheshimiwa anataka kuwa kama babu wa Loliondo kwani anategemea kuoteshwa ili agombee urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Je naye atapotea kama babu??
 
Mkuu Pasco. Tanzania ya 2016 itaongozwa na chama tofauti na CCM hata wao wanafahamu hilo ukiondoa wale wasiotaka kukubaliana na ukweli. Lakini kuna jambo muhimu ambalo litabidi lifanyike. Makabila makubwa ya nchi hii,wachagga,wahaya,wanyakyusa na wasukuma hawana budi kujitokeza na kuchukua jukumu la uongozi wa nchi.
Mkuu Timbilimu, please usituletee ukabila hapa!. Japo haijaandikwa popote but it goes without saying, kamwe makabila haya wachagga,wahaya,wanyakyusa na wasuku, hayawezi kutoa rais wa nchi hii!, hapa tuu urais hawaushika makabila hayo ndio yanayotawala Tanzania!, tuwape na urais?!. No way!. Niiteni mkabila lakini that is a fact!, a bitter fact we have to swallow tupende tusipende!.
 
Back
Top Bottom