Bernad Membe Ole Wako Utie Mguu Wako Hapa New York, Tutakuzomea Kabla Ndege Haijatua!

Membe atakuja New York na tuone hayo maandamano, labda umzomee ukiwa chumbani kwako, thubutu utoke nje uone kilichonyoa kanga manyoa, unafanya mchezo wewe?
 
Kama ndio munavyodanganywa na wamarekani eti mupinge wale wote wanaolaani kifo cha Col. Gadhafi basi muwaambie kuwa kwa Tanzania sio hivyo, hili ni Taifa linaloheshimu utu wa mtu. Ujinga huo mubaki nao huko huko munakoishi kwa kuabudu kipato cha mtu.
 
Nyinyi si vibaraka wa Marekani tu, si ajabu hata Tanzania huijui. Hao Marekani na NATO wanakudanganya. Ni wauaji, wananyemelea maliasili ya frican resources for Africa. He was sentensed by your Ameracans and NATO because of his just African course.

As for Membe hiyo statement aliyoitoa inawakisha mawazo ya Watanzania minus wapuuzi nyie na wenzako. Kwani kama ni udikteta huo unaofanywa na Marekani na NATO kuutiisha ulimwengu kwa maslahi yao utauitaje.

UMENISIKITISHA KUPINDUKIA KAMA MPO NA WENZIO FIENI HUKO HUKO KWANI HAMANA HATA CHEMBE MOJA YA UAFIRIKAn ACHA UTANZANIA.

mvuta bange wa kwa gude huyo hana lolote huko marekani. Alikuwa kaba.. Ro ..ba leo kazamia ma anatamka kama mwakilish wa wa tz marekan. Kwel watz wa Us mnataabu.
 
mna vibali vya kuishi marekani?/manake na nyie kw maneno ndio wenyewe,mbona mlisema mtaandama kuhusu mkweree,mtabebwa jujuu na wazungu,shauri yenu
 
leo hii mmesahau wazungu walivyotutenda enzi za ukoloni mnawathami watulawale tena,, kama cyo mkono wao libya pasingetokea mauwaji makubwa na uharibifu mkubwa namna hy,, sasa nato wanataka fidia ya vita hvy nina aliyewaita?

Au wanatufanya wajinga? Membe upo sawa kulaani kuuwawa kwa gadaffi kiongozi aliyependa AFRIKA iungane,, muwe na mtazamo wa kimataifa acheni U ccm NA uchadema wetu katika masuala ya Kimataifa.
 
Mtakalia hayohayo kulalama kwamba mnaonewa huku wengine wanapiga hatua.
Ghadafi kaondolewa na wananchi wa Libya kwa utawala wake wa kishenzi.
Hatumhitaji mtu kama Ghadafi Afrika. Mi niko hapa hapa Tz lakini najua tatizo c wazungu kwa kutoendelea kwa Afrika bali Waafrika wenyewe kutokana na viongozi kama Ghadafi na mawazo mfu ya mwafrika ya kuamini matatizo yake yanasababishwa na wazungu.
Hivi tulimwona Ghadafi akitangaza bila aibu yoyote ya kuwaua raia zake na akaanza kufanya hivo ulitaka wazungu wakae kimya halaf badae muanze kuwalaumu kama kawaida yenu? Hawakutusaidia kumzuia Ghadafi asituue!!! Ningekuwa viongozi wapya ws Libya ningefunga kabisa mahusiano na serikali hizi dhalimu za Kiafrika zisizoguswa na mauji ya raia. Eti Ghadafi kuua raia ni sawa hata awateketeze kwa mabomu ya sumu ila kumwondoa madarakani kwa vitendo hivo ni haramu.
Membe anafaa kuzomewa sana. MBONA YEYE NA KILAZA WAKE JK HAWAKUMKEMEA GHADAFI ALIPOKUWA ANAUA RAIA WAKE?
Nawapongeza wazungu na wasiishie tu kwa Ghadafi ila kwa mafadhuli wengine katika club cha pombe cha AU.

Nakushukuru kwa kudhihirisha umbumbu na utumwa wa mawazo yako. Kinachozungumziwa ni "statement ya nchi ya Tanzania kuhusu kifo cha Gaddafi, Upuuzi wa Marekani, NATO na Umoja wa Mataifa kuidhalilisha AU kwa hoja ya msingi.

Utumwa unakufanya usiamini solution ya kiafrica kwa waafrica, umbumbu unakufanya uwe na very shallow judgement ya local na global issues. Mimi ni mshabiki wa siasa, siiungi mkono CCM na serikali yake; lakini Statement ya Membe ni halali na inawakilisha msimamo wa Kitanzania usioyumba wa baadhi yetu minus wewe na wenzio. Ila usisahau Tanzania ni yetu sote na kauli ya serikali ni yetu hata kama hatuipendi serikali yenyewe.

Kwani ni kila kitu kinachofanywa na serikali ni kibaya? Hivyo hivyo kwani kila kitu kifanyacho na Waafrica ni kibaya?

EBU JICHUNGUZE UELEWA WAKO KAMA UNA TIJA
 
Kwa ufupi wewe ni FIMBO YA MBALI huwezi kuua nyoka. Na kwa sababu hiyo hatutaweza kamwe kuongea lugha moja kwa habari ya kuleta maendeleo ya nchi yetu Tanzania. Hii tabia ya kujidai unaungana na Wamarekani kummwona Gaddafi kama mtu ambaye hajawahi kuwa na mchango wowote kwa maendeleo ya Libya na Afrika ni kielelezo kwamba si mwenzetu. Sisi huku hatujafurahia kifo cha Gaddafi kuuawa vibaya kuliko kibaka. Angalau wangemwacha angalau aende The Hague kuheshimu yote aliyoitendea Libya ikiwemo kujenga mto wa kilometa 500 chini ya jangwa

Huu msemo wa FIMBO YA MBALI HAIUI NYOKA kwa sasa hauna maana sana kwani kuna uendelezaji mkubwa wa technology na hasa "social media" au mtandao jamii.

Kama hufahamu kuna aina mbili ya "social media", moja ni ile ya hapa JF ambapo tunaandikiana ujumbe na kupokezana mawazo au "interactive" na pili ni kutandaza mtandao au "expanding your network" ambapo ujumbe unatumwa na kusambazwa ndani ya sekunde chache sana.

Sasa kama wewe ni jasusi au mtu wa intelligence nenda ukaifanyie kazi hii aina ya pili ambayo ni hatari sana.
 
JF kuna mambo ya ajabu sana, yaani bila hata ya kuchunguza habari watu wanamwaga upupu tu. Huyu mtoa mada yupo Manzese kwa 'mfuga mbwa' lakini watu wame-react utafikiri wanamfahamu kuwa yupo Marekani.
 
Richard. Nashukuru kwa mchango wako mzuri. Ni kweli huko nje baadhi yenu ni wazalendo na mmeifanyia nchi mambo makubwa. Lakini ndugu yangu mimi nadhani hasira zinazoonyeshwa dhidi yenu mlioko nje,ni mchango wenu mdogo katika Tanzania yenye demokrasia,haki na usawa.

Hamuonekani kujali hayo mambo hapo juu,nyie mko busy kuwabana watawala wetu ili mpate uraia wa nchi mbili. Mimi sina tatizo na nyie kupewa uraia wa nchi mbili,tatizo langu ni kwanini mambo kama tume huru ya uchaguzi,uchaguzi huru, utawala bora na ufisadi siyo vipaumbele vyenu?

Ama kwasababu mambo yakiharibika nyie mna pakwenda?
 
Huyo anamuunga mkono Gaddafi kwa maslahi ya tumbo lake, na sio kwa maslahi ya Watanzania. kwa kauli yake haituwakilishi Watanzania wote.
 
hiyo mnaweza kuwa mmesaidia lakini ni majuzi tu mlituahidi kuandamana kumpinga JK na tukaishia kuwaona mkimuandalia mkutano! tatizo la Membe linaweza kuwa ni sehemu mojawapo ya haya makundi katika hii quote.

View attachment 39769
 
Sisi watanzania tuishio mjini New York tumekerwa na kitendo cha waziri wetu wa mambo ya nje huko nyumbani Tanzania mseminaristi aliyepotoka(Bernard Camillius Membe) kwa kitendo chake cha kuunga mkono udikteta wa Ghadaf.

Dunia nzima imeshangazwa na kitendo cha huyu Bwana, sijui karogwa? au ndiyo anataka kura za ndugu zetu wai.....mu? 2015? kwa maana sio jambo la kawaida kwa viongozi wa Tanzania kuunga mkono udikteta kama alivyothubutu.

Sasa sisi watanzania tuliopo hapa tunatoa TAMKO RASMI kuwa Membe asikanyage hapa! kwa maana akitia tu mguu ataipatapata, tunaapa kuwa kabla hiyo ndege atakayopanda haijatua sisi tutaanza kumzomea.

KIFUPI KATUKERA SANA, HATUHITAJI HATA MSAMAHA WAKE


Nadhani ninyi ndugu mna takiwa kusaidiwa.Sioni kosa la membe.Acheni ushabiki.Fanyeni utafiti kama hamna taaluma ya masuala ya mambo ya nje.Kwanza muelewe na muwaeleze kuwa Tanzania ni Taifa lenye bendera yake,hatuburuzwi na yeyote.Mbona watu hawataki kujadili hoja za Membe alizotoa? hebu na ninyi muache mawazo ya kitumwa

Unajua kuna wakati vijana wa Tanzania tunajiandaa kuwa watumwa wa Fikra hadi inatia aibu,loh!
 
sio nyie tu wa ughaibuni... huy bwana hata sie huku nyumbani ametukera...

anaweweseka kwani alikuwa allien wa ghadafi mzuri.... na nadhani kwa kuwa swaiba wake aliyekuwa anamtegemea alikufa ghafla hawezi kabisa kupambana na lowassa..... hilo analijua wazi na anaweweseka....
 
we mpotevu, brain washed.

Africa will be for Africans. wewe huko si mkimbizi?
nyote nyie hatuwaamini kamwe, mkatupigisha kura hapa kwa ajili ya DICOTA afu mkaingia mitini.
wachonganishi wakubwa.

Ukiacha abdel gamal, nyerere,nkurumah. idd amin, kenyata, kaunda, mandela etc ni nani mwafrika mwingine aliyebaki anayeweza kubishana na mataifa ya magharibi kwa kusimamia haki ya mwafrika zaidi ya MUGABE na Late Gaddaf?

Kagame is coming up, lakini si nyie ombaomba, masikini mnaotegemea kuhemea huko ili mje kujenga nyumba huku.

Kwenda zako
 
nyie sijui mpo dunia ya ngapi, napata shida kujua mnasomea nini na mnafanya nini kama hawa wanaowalea ndo washawapandikiza chuki kama hiyo! alafu nyie sio wazalendo ni kuongwa tu vidola mnasaliti nchi!nampongezaembe ameona mbali na hii itakuwa provrd baadae impact zikianza kuonekana very soon, subiri waanze kulipa deni la NATO. then Watu wote wanaoshabikia gadafi kuuwawa nadhani hawajui nini kinaendelea!gadafi ni mtu kama wewe, he was not perfect, hakuna raisi ambaye hajaua, na katika ukombozi na harakati zake lazima watu wafe hiyo ipo given, sacrife must be there bandugu, tunachojaribu kuangalia ni je, nato nia yao ni nini?kwa nini ni benghazi na sio serte,na je ni libya tu waliona kuna shida?kwanini ni ukanda wa watu wenye mambo sawa kimfanano?kwanini somalia hawaendi?kwa nini israel na parestina, je yanayotokea yemen hawayaoni??

kwanini sadam alishukiwa kuwa na siraha za maangamizi na hawakuziona??je marekani wameua wangapi kuanzia afghanistan, iraq, kongo,sudan, namibia,hata misri wapo nyuma ya hawa vibaraka waliopandikizwa mbegu za chuki??

marekani sio watu, uingereza sio haki!msimamo wa gadafi kukataa kuingia mkataba nao kuchimba mafuta, kukataa unyonyaji kwenye mikataba nchini kwake, kuonekana kuwa na nguvu sana barani afrika na kuwa na nia ya kutuunganisha waliona tutakuwa na nguvu ya maamuzi yetu,sio walibya wote wanaompinga gadafi ni kijisehem cha vibaraka wa magharibi! Na hii ni somalia mpya imetengenezwa afrika lengo ni kuona sisi sio wamoja ili wachume mali zetu zote!je watoto wetu wataishi vipi kama hali ndo hii?

utumwa unarudi polepole watu wasio na maono wanashangalia kuuawawa kinyama kwa gadafi!ipo siku magahribi watajutia tabia zao ambazo tushazijua na libya watamkumbuka sana gadafi, kwanza walipe deni la nato alafu tuanzie hapo ndani ya mwaka utaona!mungu katupa akili tupamnanue mambo na sio kuchukulia mambo kijuujuu!!!!!!!!!!!!!!!USITEGEMEE UTASOMA AU KUANGALIA TV ZA MAGHARIBI KAMA CNN,BBC NA ZINGINE UONE MAZURI YA GADAFI!!!!!!!!!! MARA MIA MUNGU AKUPE AKILI KULIKO SURA!!!!!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom