Inkoskaz
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 6,372
- 2,374
Akizungumzia hitimisho la bunge lililopita ameainisha mambo mbalimbaliambayo hakika yamepambanua upeo wake kisiasa
1.amezungumzia utoro wa wabunge unavyowakosesha umakini wa kufuatilia hoja na uhalali wao wa kuwawakilisha wananchi
2.amezungumzia majibu ya mawaziri..hayalengi uhalisia wa mifumo ya nchi yetu bali yapo kibinafsi mno na kizimamoto zaidi ,amemchana naibu waziri wa Elimu mh Mulugo kwa namna anabyoyafanyia kazi matattizo ya walimu
3.Ameupongeza upinzani kwa hoja zao..hususani Mh Tundu lissu kuwa japo hoja yake ilipingwa lakini ina ukweli.hoja ilikuwa ni udhaifu katika uteuzi wa majaji ambao ni nguzo katika muhimili wa tatu wa dola,hili halina ubishi kuwa nguzo hii si imara tena kwani nondo zilizotumika kuijenga ni dhaifu,pia amepongeza hoja ya Zitto na na Chenge katika marekebisho ya vifungu vya bajeti ya wizara ya fedha,ambavyo waziri na naibu walishavifumbia macho licha ya kujadiliwa na kamati ya fedha na kutolewa maamuzi
4.amezungumzia tuhuma za rushwa kwa wabunge na kampeni za kukwamisha bajeti ya wizara ya nishati na madini kuwa ni jambo baya sana kwa bunge,japo tunasubiri taarifa ya kamati ya maadili iliyowahoji tayari ni dosari kubwa kwa watunga sheria
5.amezungumzia upimaji wa uwajibikaji wa wa maamuzi ya bunge..yaani maazimio na utekelezaji.yaani maazimio wanayopitisha hayafuatiliwi utekelezaji wake,na wanapoanza kikao kingine hakuna tathmini ya ya kuangalia milestone na waliyokubaliana awali
6.Ametoa rai yake kuwa kero yake kuu bungeni ni ileile tunayolia nayo hapa jf ya wabunge na mawaziri kupoteza muda wa bunge kutoa pongezi hadi kwa beki tatu na drivers na kuacha hoja za msingi
Pia kazungumzia mfumo wa uhitimishaji budget ya fedha kuwa mwishoni ili kuchambua wizara nyingine vizuri..haina maana kupinga wakati mlishakubaliana katika overall budget ya fedha
bravo Benson,kwa mtazamo huu umejipambanua
Source:clouds FM PB on saturday
1.amezungumzia utoro wa wabunge unavyowakosesha umakini wa kufuatilia hoja na uhalali wao wa kuwawakilisha wananchi
2.amezungumzia majibu ya mawaziri..hayalengi uhalisia wa mifumo ya nchi yetu bali yapo kibinafsi mno na kizimamoto zaidi ,amemchana naibu waziri wa Elimu mh Mulugo kwa namna anabyoyafanyia kazi matattizo ya walimu
3.Ameupongeza upinzani kwa hoja zao..hususani Mh Tundu lissu kuwa japo hoja yake ilipingwa lakini ina ukweli.hoja ilikuwa ni udhaifu katika uteuzi wa majaji ambao ni nguzo katika muhimili wa tatu wa dola,hili halina ubishi kuwa nguzo hii si imara tena kwani nondo zilizotumika kuijenga ni dhaifu,pia amepongeza hoja ya Zitto na na Chenge katika marekebisho ya vifungu vya bajeti ya wizara ya fedha,ambavyo waziri na naibu walishavifumbia macho licha ya kujadiliwa na kamati ya fedha na kutolewa maamuzi
4.amezungumzia tuhuma za rushwa kwa wabunge na kampeni za kukwamisha bajeti ya wizara ya nishati na madini kuwa ni jambo baya sana kwa bunge,japo tunasubiri taarifa ya kamati ya maadili iliyowahoji tayari ni dosari kubwa kwa watunga sheria
5.amezungumzia upimaji wa uwajibikaji wa wa maamuzi ya bunge..yaani maazimio na utekelezaji.yaani maazimio wanayopitisha hayafuatiliwi utekelezaji wake,na wanapoanza kikao kingine hakuna tathmini ya ya kuangalia milestone na waliyokubaliana awali
6.Ametoa rai yake kuwa kero yake kuu bungeni ni ileile tunayolia nayo hapa jf ya wabunge na mawaziri kupoteza muda wa bunge kutoa pongezi hadi kwa beki tatu na drivers na kuacha hoja za msingi
Pia kazungumzia mfumo wa uhitimishaji budget ya fedha kuwa mwishoni ili kuchambua wizara nyingine vizuri..haina maana kupinga wakati mlishakubaliana katika overall budget ya fedha
bravo Benson,kwa mtazamo huu umejipambanua
Source:clouds FM PB on saturday