Bendera ya- Tanzania Kupeperushwa nusu mlingoti

SEAL Team 6

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
655
118
Kufuatia kifo cha Dictator Gaddafi serikali kupitia Waziri Membe itapeperusha bendera ya nchi nusu mlingoti. Hili jambo linanichanganya kidogo, ni kwa heshima gani aliyostahili Gaddafi kupewa hadi bendera ipepee nusu milngoti? Dunia nzima inajua kwamba Gaddafi alikuwa Dictator amehusika na mauaji ya watu kama siyo halaiki tena kwa kiburi tu.

Gaddafi huyo huyo alishirikiana na Dictator wa Uganda Amini kuvamia nchi yetu na Watanzania wengi waliuawa, sasa hapa kuna umuhimu gani wa serikali ya Tanzania kupeperusha bendera nusu mlingoti? Mbona wakati IDD AMINI alipokufa Tanzania hatukupeperusha bendera nusu mlingoti?

Inamaana ile misaada yake ya kujenga Miskit ndiyo imetufanya tuchukue maamuzi hayo? Kwa maana nyingine ni kwamba hata IDD AMINI kabla hajafa angejenga shule au Kanisa hapa Tanzania, siku ya kifo chake ingepeperusha bendera nusu mlingoti?

Kama ni suala la IMANI lingeachiwa viongozi wa dini ndiyo waeleze msimamo wao kuhusu uzuri na ubaya wa Gaddafi.

Gaddafi huyo huyo alikuwa ni mshirika wa Gaidi OSAMA BIN Laden, inakuwaje tunawashangilia watu hatari kama hawa. Tunachokiona hapa siyo sera za nchi bali ni SIASA KWA AJILI ya 2015, sasa huu ndiyo ujinga wa serikali yetu.

Serikali kukataa kuwatambua waasi inamaana inafanya maandalizi kwenda Libya kuwafurusha serikali ya mpito ya Lbya. Tujiulize tena au tumuulize Waziri membe nini kauli yake kuhusu MAZISHI ya GADDAFI kufanyika BAHARINI kama ilivyokuwa kwa OSAMA BINLaden???

Watanzania tunaliona hili kuwa maombolezo hayo ni maalumu kwa MAFISADI na Wenyeuchu wa Madaraka ( Wachakachuaji na wezi wa KURA)na wala hayawakilishi Watanzania wenye nia njema.
 
Mi sijui anatuhusu nini kitaifa (kama habari ni kweli) mpaka kustahili heshma ya namna hiyo.

Yawezekana 'mfalme wa wafalme' alishiriki kuiweka serikali yetu madarakani!

Siungi mkono hilo.
 
Anatutia aibu. Kweli Membe ni mkebe. Wateremshe bendera ya CCM nusu mlingoti. Wasichezee bendera ya Taifa letu tukufu.
 
Honestly am simply shocked. Nusu mlingoti kwa ajili ya Ghadafi. Yeye ni nani hapa Tz, tuambiwe.
 
Membe tunaomba mustuambukize roho za kivita.mkifanya hivyo mtajuta kwa matendo yenu na mzimu wa gadaff utawaandama.kama vipi ccm ungeni mkono gaddaf na sisi wengine tuunge mkono ntc halatu tulianzishe.Mia
 
Tangu jana kuna habari inanitatiza kwamba Tanzania yamlilia Gaddafi, nashindwa kuelewa hivi huyu Membe akitoa ya moyoni mwake kuhusu kifo cha Gaddafi anawakilisha watanzania wote? Hivi huyo Gaddafi ametusaidia nini watanzania mpaka tumlilie. Huyu Membe na viongozi waseme wao ndio wanamlialia. Mbona hao walibya zaidi ya Elfu 50, walio uliwa kwa amri yake sio binadamu, na wale watanzania walio uliwa na wanajeshi wa Gaddafi pale Kagera akimsaidia Dictator mwenzake Idd Amini vipi au viongozi wetu wamesahau au hawakujua wala kusikia. Jamani viongozi wetu waache unafiki.
 
Kama wanahamu ya kushusha bendera nusu mlingoti si washushe ya CCM? Wakishusha ya ccm wala hakuna atakae uliza maswali.
 
Nchi inaendeshwa kama toroli,haina sera ama iliyodhabiti ya ndani wala ya nje...ukiuliza ya ndani eti ujamaa na kujitegemea wakati ukweli hauko hivyo,ya nje eti ni kuendeleza mahusiano huru na ya kidemokrasia na kila nchi,wanahabudu misingi ya haki za binadamu huku wakiwatukuza magaidi na madikteta...Membe,sera zetu za nje zikoje?
 
Hongera Membe na serikali kwa ujumla. Gadaf alikuwa ni mmoja wa viongozi imara sana Afrika, wanaongozwa na misimamo yao imara, si wale wafata upepo.

Afrika nzima inapaswa kumlilia Gadaf, mungu ailaze mahali peponi.
 
Kufuatia kifo cha Dictator Gaddafi serikali kupitia Waziri Membe itapeperusha bendera ya nchi nusu mlingoti. Hili jambo linanichanganya kidogo, ni kwa heshima gani aliyostahili Gaddafi kupewa hadi bendera ipepee nusu milngoti? Dunia nzima inajua kwamba Gaddafi alikuwa Dictator amehusika na mauaji ya watu kama siyo halaiki tena kwa kiburi tu.

Gaddafi huyo huyo alishirikiana na Dictator wa Uganda Amini kuvamia nchi yetu na Watanzania wengi waliuawa, sasa hapa kuna umuhimu gani wa serikali ya Tanzania kupeperusha bendera nusu mlingoti? Mbona wakati IDD AMINI alipokufa Tanzania hatukupeperusha bendera nusu mlingoti?

Inamaana ile misaada yake ya kujenga Miskit ndiyo imetufanya tuchukue maamuzi hayo? Kwa maana nyingine ni kwamba hata IDD AMINI kabla hajafa angejenga shule au Kanisa hapa Tanzania, siku ya kifo chake ingepeperusha bendera nusu mlingoti?

Kama ni suala la IMANI lingeachiwa viongozi wa dini ndiyo waeleze msimamo wao kuhusu uzuri na ubaya wa Gaddafi.

Gaddafi huyo huyo alikuwa ni mshirika wa Gaidi OSAMA BIN Laden, inakuwaje tunawashangilia watu hatari kama hawa. Tunachokiona hapa siyo sera za nchi bali ni SIASA KWA AJILI ya 2015, sasa huu ndiyo ujinga wa serikali yetu.

Serikali kukataa kuwatambua waasi inamaana inafanya maandalizi kwenda Libya kuwafurusha serikali ya mpito ya Lbya. Tujiulize tena au tumuulize Waziri membe nini kauli yake kuhusu MAZISHI ya GADDAFI kufanyika BAHARINI kama ilivyokuwa kwa OSAMA BINLaden???

Watanzania tunaliona hili kuwa maombolezo hayo ni maalumu kwa MAFISADI na Wenyeuchu wa Madaraka ( Wachakachuaji na wezi wa KURA)na wala hayawakilishi Watanzania wenye nia njema.
soma history wacha kurukia mambo usiyoyajua qaddafi was a hero and an icon of africa countries
 
Sasa kijinchi kama tz kina msaada gan kwa libya hata kaitambue au kasiitambue hyo serikali ya waasi wa libya.mambo mengne akna jk wanajiaibsha wenyewe 2.
 
Kwa nini hakupewa hii support when he was alive?????

Tuliogopa kunyimwa misada na wale walio kuwa wanamshambulia wakiwasaidia NTC kumng'oa, muhimu zaidi sasa tumepata sababu ya msingi kumsupport, kwamba si utamaduni wetu kufurahia kifo cha mtu na sababu hii imefanyiwa uchunguzi haiwezi kuwachukiza wafadhili wetu.
 
Back
Top Bottom