Hauweze wapi huo urais,islaeri wametutukana yeye kakaa kimya hakujibu chochote,huyu si atakua kilaza zaidi ya mkuu wa kaya.
Huyu ni Waziri wa mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa(Minister of foreign affairs and international relations)
Huyu mtu anatajwa kuwa huenda akawa rais 2015 katika kujiaminisha kuwa ni mtu anaye faa hebu tuanze kukusanya maoni kutoka kona zote za nchi kwa wana JF wazalendo.
Na kama unavyojua, joka la mdimu lenyewe halili ndimu, lakini ukigusa mdimu tu... balaa...jina lake jingine ni joka la mdimu.
Ulianza na Nyalandu...ushamjua sasa?
Kesha utataka kumjua nani tuanze kukukusanyia taarifa
........umeiacha kazi moja nafikiri ni kwa makusudi, maalum ulishaanza, wewe malizia tu na ile.Mhe. Membe ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, toka 2007 hadi sasa. Amewahi kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani. Pia ni Mbunge wa Jimbo la Mtama tokea mwaka 2000 ambako akiwa Mbunge amekuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje. Amekuwa Mkuu wa Idara ya Siasa na Ushirikano wa Kimataifa ya CCM na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM tokea 2007 hadi 2011 Kamati Kuu ilipojiuzulu, na Mjumbe wa NEC tokea 2007 hadi sasa.
Nje ya siasa, Amefanya kazi katika Ofisi ya Rais hadi alipokwenda kugombea Ubunge mwaka 2000. Amekuwa Afisa Ubalozi katika Ubalozi wa Tanzania Canada kati ya mwaka 1992 hadi 2000. Ana elimu ya Shahada ya Uzamili(Masters) kwenye masuakpla ya Uhusiano wa Kimataifa, International Law and Economics kutoka moja ya vyuo bora nchini Marekani cha John Hopkins University (School of Advance International Studies). Ni Mkristo Mkatoliki na ana Mke mmoja na watoto watatu.
Ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa sio uhusiano wa kimataifa.
Thanx kwa kunifafanualia,je na hapo kwenye kingereza ni sawa au niweke international co-operations?
Mwaka jana amewezesha mashekhe kutoka kata zote za jimbo lake la Mtama kwenda kuhiji Mecca, pia viongozi wa dini ya kikristo kwenda kuhiji Jerusalem
Ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa sio uhusiano wa kimataifa.