LEGE
JF-Expert Member
- Oct 14, 2011
- 5,123
- 9,168
- Thread starter
- #141
: BEFORE I DIE
SEHEMU YA 50
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Oh Mungu wangu ! Latoya si binadamu wa kawaida.Mambo yake ni mazito na yanaogopesha.” akawaza Innocent huku akihisi baridi mwilini
Latoya aliingia katika jumba lile ambalo lilikuwa na giza nene ndani.Akawasha taa ndogo nyekundu iliyomuwezesha kuona.Akafungua chumba kimoja akangia.Akavua mavazi yake na kuvaa gauni refu jeupe.Akatoka mle chumbani na kuelekea katika ukumbi mpana.Alikuwa akitembea taratibu hadi katika meza yenye mishumaa sita na kuiwasha halafu akapiga magoti akainama na kusujudu
“ Atha.Lut pakta du mokaja,akta pata ovakoja du mapakta” alitamka taratibu maneno haya .Akayarudia mara tatu na mara moshi ukaanza kutoka katika madhabahu ile .Latoya akaendelea kuongea maneno aliyoyafahamu yeye mwenyewe na kila alipoongea moshi mwingi ulizidi kutoka.Ulikuwa ni moshi wenye harufu nzuri ya uturi.Chumba chote kilijaa moshi na mara ghafla ukatokea mwanga mkali sana ambao ulimulika eneo lile lote.Baada ya mwanga ule mkali kutokea,Latoya akainuka na kusimama .Mbele yake toka ndani ya moshi ule wakatokea watu wawili wenye mavazi meupe na ndevu nyingi
ENDELEA………………………..
“Innocent.!! Innocent !!!..” Ilikuwa ni sauti ya Latoya iliyomstua .Akafumbua macho na kuangaza huku na huku.Alikuwa ni kama mtu aliyechanganyikiwa.Latoya akamshika kichwani kwa mikono yake na mara fahamu zake zikamrejea
“ Latoya ..!!..” akasema Innocent
“ what happened?Nilisikia unalia nikataka kukufuata huko ndani lakini ghafla nika……” kabla hajamaliza sentensi yake Latoya akasema
“I know what happened.Twende tondoke”
Wakaingia garini na kuondoka
“Kwa masikio yangu nimesikia Latoya akipiga ukelele wa uchungu .Nilitaka kuingia mle ndani lakini kilichonitokea sintakisahau.I’m real scared” akawaza Innocent halafu akageuza shingo yake na kumtazama Latoya
“Huyu si binadamu wa kawaida.Kuna siri nzito katika maisha yake.Ouh Mungu wangu mambo yaliyoko hapa ni mazito .Natamani niondoke na kuachana na maisha haya lakini siwezi tena .I’m stuck in here and I cant leave this place anymore because I love Latoya.” Akawaza Innocent na kwa mbali macho yake yakatoa machozi
“ Latoya ni nani hasa? Natamani nimjue kiundani lakini naogopa.Maisha yake yametawaliwa na nguvu zisizo za kawaida.” akawaza halafu akageuka tena na kumtazama Latoya.Alikuwa ameinama analia
“ Latoya …..!!!!! akaita Innocent.Latoya hakuitika
“ Latoya ….!! akaita tena.Latoya akageuza shingo na kumtazama Innocent.
“ are you ok? Akauliza Inno
“ I’m ok Innocent.” Akajibu Latoya
“ You are crying.Whats your problem?
“ Never mind about me.I’m ok” akajibu Latoya Innocent hakumuuliza tena kitu chochote
“Naogopa kumuuliza tena kitu chochote.Anaonekana ana jambo zito, ngoja nimuache” akawaza Inno
“ Innocent” akaita Latoya
“ naam Latoya” akaitika Inno
“ Jiandae kesho kutwa tuanze ile safari yetu”
“ Usijali Latoya Mimi niko tayari muda wowote kuongozana nawe sehemu yoyote ile” akajibu Inno
“ ahsante sana Innocent.Thank you for being there for me” akasema Latoya halafu safari ikaendelea kimya kimya hadi wakafika nyumbani.Latoya hakuongea na mtu akapanda moja kwa moja ghorofani kwake.Innocent naye akapanda chumbani kwake.
“ Nimeogopa sana kwa kilichotokea leo.Kwa nini Latoya alikuwa analia.? Kuna mtu alikuwa anamuumiza?Kuna nini ndani ya jumba lile? Maswali haya yaliendelea kumuumiza kichwa Innocent lakini hakuweza kupata jawabu.
“ katika maisha yangu sijawahi kukutana na mauza uza kama haya.Inawezekana ni mipango yake nikutane na Latoya ili niweze kuufahamu upande wa pili wa mwanadamu ukoje.” akawaza Innocent akiwa kitandani.Alihisi joto sana akavua shati
“ Latoya anataka twende wapi kwa mapumziko?Niliwahi kumuuliza ni wapi tunakwenda lakini hakuwa tayari kuniambia.Kutokana na maisha haya anayoishi ananipa uoga hata mimi kuhusiana na safari hiyo ya sisi wawili pekee japokuwa ninatamani sana kuwa karibu naye nimueleze kilichomo moyoni mwangu.”
Innocent akastuliwa toka katika mawazo mengi na mlio wa simu
“hallo” akasema Innocent
‘ Innocent naomba tukutane bustanini” akasema Latoya
‘”Ok Latoya Nakuja sasa hivi” akajibu Innocent
“Wanasema kwamba Love is all about sacrifices.Because I love her I’ll sacrifice everything for her .I know its not going to be easy but even if it’s going to take my whole life I’ll die trying.” Akawaza Innocent halafu akavaa shati akatoka mle chumbani na kuelekea katika bustani ya Latoya iliyoko juu.Tayari Latoya alikwisha fika kule bustanini.
“ Unajisikiaje Innocent? akauliza Latoya
“ I’m ok Latoya.najisikia vizuri.Vipi kuhusu wewe? Unajisikiaje?
“ Najisikia vizuri Innocent” akajibu Latoya.
“Nikikuangalia machoni naona kama hauko sawa.Kitu gani kinakusumbua Latoya? Akauliza Innocent
“Ouh Innocent don’t mind about me.I’m ok.Ni uchovu ndio unaonisumbua .Hii ni sababu inayonipelekea kuamua kwenda mapumzikoni.Vile vile mambo mengi yametokea katika kipindi kifupi kwa hiyo ninahitaji kupumzika na kujaribu kuyasahau yote yaliyotokea. Nikiwa kisiwani husahau dunia kwa muda.No TV, no phone calls,no meetings,no any contact with the world.Its just me and the island.I talk to birds,animals and I go back to sleep.Hivyo ndivyo namna ninavyoishi nikiwa mapumzikoni” akasema Latoya
“Nimeipenda sana aina yako ya upumzikaji lakini kwa kuwa umezoea kuwa mwenyewe huoni kwamba nitakuwa mzigo kwako na kukuzuia usipumzike vile ulivyozoea? Akauliza Inno
“Innocent huwa ninakwenda mapumzikoni peke yangu kwa sababu sikuwa na mtu ninayemuamini ambaye ningeweza kwenda naye.Safari hii nimekupata wewe ambaye ninakuamini na kwa hiyo nitakuwa na mapumziko mazuri sana kuliko miaka yote ambayo nimekuwa nikipumzika peke yangu.Innocent wewe ni mtu wangu wa muhimu sana .Tumejuana katika kipindi kifupi lakini naomba ufahamu kwamba nilikujua kabla hata hatujakutana na ndiyo maana umetokea kuwa mtu muhimu mno kwangu.Duniani ninafahamika na mamilioni ya watu lakini sijawahi kupata rafiki kama wewe.Ninafurahi na kufarijika ninapokuwa nawe” akasema Latoya halafu akavua pete yake ya dhahabu na kumvalisha Innocent kidoleni
“ Innocent nakupatia pete hii, ambayo ni ya muhimu sana kwangu.Ninakuomba usiivue pete hii.Huu ni ukumbusho wangu kwako hata kama hatutakuwa pamoja kwa muda mrefu.Wakati mwingine inaweza ikawa na msaada mkubwa kwako “ akasema Latoya
“ahsante sana Latoya.Its a beautiful ring.I love it” akasema Innocent huku akifurahia pete ile nzuri
“ Utanikumbuka kila mara utakapoitazama pete hii” akasema Latoya huku akitabasamu
“Latoya bila hata ya pete hii,ninakukumbuka kila dakika ya maisha yangu.You are a wonderfull person I’ve ever met.Ninafurahi sana kuwa mmoja wa watu wako wa karibu”
“ Ouh Innocent,that’s so sweet.Ndiyo maana napenda kuwa nawe karibu muda wote.Ninapokuwa nawe ninasahau matatizo yangu.I forget death and everything..” akasema Latoya na ghafla akanyamaza na kumtazama Innocent ambaye alikuwa anatabasamu
“Innocent natamani watu wote duniani wangekuwa kama ulivyo wewe Dunia ingekuwa mahala pazuri sana pa kuishi lakini kwa bahati mbaya dunia hii imejazwa na watu makatili wasio na hata chembe ya huruma kwa wenzao” akasema Latoya
“ Kwa nini unasema hivyo Latoya? Akauliza Innocent
“Innocent bado hujajaliwa kuufahamu pande wa pili wa duna hii ukoje.Dunia hii ina sehemu mbili moja ni hii tunayoiona kwa macho ya kawaida nay a pili haionekani kwa macho ya kawaida.Siku ukijaliwa kuiona sehemu ya pili ya dunia hii utakubaliana na ninachokwambia kwamba binadamu ni kiumbe anayeweza kubadilik na kuwa mbaya sana kuliko hata mnyama wa mwitu” akasema Latoya
“nakubaliana nawe Latoya duniani humu kuna mambo mazito ambayo hatuwezi kuyaona,kuna watu makatili na ubinafsi umeitawala dunia siku hizi”
“ Thats my point.Mungu aliumba mwanadamu akamuweka duniani atawale kila kitu ,lakini mwanadamu huyo huyo amemgeuka hata muumba wake na kumpinga.Watu wanazivunja amri zake .Hawamuabudu tena.Wamewageukia miungu wengine.Wanaua wanadamu wenzao pamoja na kutenda dhambi nyingi zenye kuleta machukizo mbele za Mungu.Do you think its time now for God to put and end to this world? Akauliza Latoya
“ Latoya ni kweli dunia hii imejaa machukizo ya kila aina, makubwa na yasiyovumilika ,lakini pamoja na dhambi hizo za wanadamu Mwenyezi Mungu bado amezidi kutupa nafasi ya kubadilika na kumrudia yeye kutokana na sala na maombi ya wachamungu wachache wasiochoka kuomba.Nadhani Itakuwa Vyema kama Mungu ataendelea kutupa nafasi zaidi ya kujirekebisha.I don’t want to die” akasema Innocent halafu kimya kikatanda
“ Innocent you seem scared when you think of death..why? .Akauliza Latoya
“Latoya kifo kipo na kila mwanadamu atakufa lakini ninaogopa kufikiri kifo changu kwa sababu sipendi kufa.Kama ingetokea nikapewa nafasi ya kuchagua jambo moja tu na mwenyezi Mungu,basi ningeomba aniepushe na kifo..I don’t want to die.Naomba nife wakati nimekwisha zitimiza ndoto zangu kubwa” akasema Innocent
“ Me either.I don’t want to die especially this young. Lakini hata hivyo kama imeandikwa kwamba utakufa katika umri mdogo there is nothng you can do to change that.It hurt so much Innocent,kuiacha hii dunia na watu wake uliowapenda na kuwaozea.” Akasema Latoya
“ Inauma sana na ndiyo maana sitaki kufikiria kuhusu masuala ya kufa” akasema Innocent
‘ Ok Innocent lets not talk about death.Its so scary.Lets talk about something else like love” akasema Latoya na Innocent akatabasamu
“Innocent uliniambia kwamba hauna mpenzi.Je hakunamwanamke yeyote aliyewahi kukuvutia hadileo hii?
Swali lile likaonekana kuwa gumu kwa Innocent
“ Swali lako gumu Latoya lakini ukweli nikwamba wanawake wapo wengi wa kila aina na wenye kila sifa lakini kwa muda mrefu nilikuwa nikimtafuta yule ambaye nitamkabidhi moyo wangu bila mafanikio lakini nashukuru Mungu kwa kuniangazia na kwa sasa nina matumaini kwamba huenda siku za karibuni nikafanikiwa kumpata Yule ambaye anayafanya mapigo ya moyo wangu yaende kwa kasi ” akasema Innocent.Latoya akamuangalia halafu akatabasamu.
“Wow hongera kama tayari umekwisha pata mwangaza kuhusiana na mwnamke wa ndoto zako”akasema Latoya kwa sauti ya upole
“ Vipi kuhusu wewe? Akauliza Innocent
“ Innocent lets not talk about me.Lakini kuna jambo moja ambalo nataka kukushauri”
“ Jambo gani Latoya?
“Love don’t have a time to wait. Kama unafikiri kwamba tayari umekwisha mpata mtu ambaye unaamini ndiye unayempenda kwa moyo wako wote basi usipoteze muda,mueleze ukweli.Hakuna anayejua nini kitatokea katika dakika ijayo.Kwa maana hiyo tusisubiri na kujilaumu baadae kwa nini hatukuwaambia wale tuwapendao kwamba tunawapenda. Mariah carey na Boyz 2 men waliimba wimbo mmoja unaoitwa one sweet day.Do you know that song?
Innocent akaitika kwa kichwa ishara ya kwamba anaufahamu wimbo ule.taratibu Latoya akaanza kuimba
“Sorry, I've never told you, all I wanted to say
And now it's too late to hold you
'Cause you've flown away
So far away
Never had I imagined
Living without your smile
Feelin' and knowing you, hear me
It keeps me alive, alive
And I know you're shining down on me from Heaven
Like so many friends we've lost along the way
And I know eventually we'll be together
One sweet day…………………………………
“ wow sijawahi kukusikia ukiimba.Sauti yako tamu na laini kama ya malaika.Umebarikiwa mno Latoya kwa kila kitu.Laiti ungekuwa mwanamuziki nina hakika ungekuwa mmoja wa wanamuziki wakubwa mno duniani” akasema Innocent na kumfanya Latoya acheke kidogo
“ Innocent you real make me so happy.Sijawahi kuwa na furaha kama hii hapo kabla,ahsante kwa kuja katika maisha yangu” akasema Latoya
“Mimi pia.Ninajisikia furaha sana kuwapo mahala hapa,furaha ambayo siwezi kuielezea and that’s the reason I’ve sacrificed everything ,my job,my dreams,and everything just to be here only because I feel so connected to this place” akasema Innocent
“ Innocent be honnest with me.Are you happy with me as your friend? Akauliza Latoya
“Latoya naomba niwe muwazi kwako kwamba nina furaha tena kubwa sana na ndiyo maana nimeacha kila kitu kwa ajili ya kuwa na mtu kama wewe.You are a wonderfull friend,a friend that is worth to die for” akasema Innocent
Uso wa Latoya ukapambwa na tabasamu zito sana.Akamuangalia Innocent na kuuliza
“ Innocent unamaanisha hicho ulichokisema? Can you die for me?
“Ndiyo Latoya.Kama kuna mtu yeyote yule anayetaka kukudhuru mimi niko tayari kupambana hadi kufa kwa ajili yako”
“ Ouh Innocent you are like an angel to me.How can you die for a woman like me? Akasema Latoya huku machozi yakimlenga
“Latoya wewe ni mtu ambaye dunia inakuhitaji sana.Una moyo wa huruma na upendo usio na mfano.Wewe ni mkombozi na kimbilio la watu masikini kwa hiyo siko tayari kuona jambo lolote baya linakutokea na hii ndiyo sababu niko tayari kwenda hadi mwisho wa dunia kwa ajili ya kutafuta kitu ambacho kitakufanya uwe na furaha.Ninaumia kila niuonapo uso mzuri wa kimalaika kama huu ukiwa na machozi.Ninataka tabasamu hilo lililoko sasa hivi usoni pako liendelee kuwepo katika siku zote za maisha yako” akasema Innocent na uso wa Latoya ukazidi kuchanua kwa tabasamu
“ Ouh gosh ! Why I have to die?.Sitaki kumuacha Innocent. Ananipa furaha ambayo sijawahi kuipata katika maisha yangu.It hurt that I’ve found my happiness at my dying days.It hurt even more that I cant change anything now.It’s too late.Ninachotakiwa kufanya ni kutumia kila dakika iliyobaki vizuri.Nataka nife nikiwa na furaha na zaidi ya yote nikiwa msichana.sitaki kufa nikiwa bikira.Mwanaume pekee atakayenitoa bikira yangu ni Innocent” akawaza Latoya
Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwao wote.Hakuna aliyetamani kwenda kulala.Waliongea mambo mengi sana usiku ule na hadi ilipofika usiku wa saa tisa ndipo walipoagana na kila mmoja akaenda kulala.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………….
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 51
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Ouh Innocent you are like an angel to me.How can you die for a woman like me? Akasema Latoya huku machozi yakimlenga
“Latoya wewe ni mtu ambaye dunia inakuhitaji sana.Una moyo wa huruma na upendo usio na mfano.Wewe ni mkombozi na kimbilio la watu masikini kwa hiyo siko tayari kuona jambo lolote baya linakutokea na hii ndiyo sababu niko tayari kwenda hadi mwisho wa dunia kwa ajili ya kutafuta kitu ambacho kitakufanya uwe na furaha.Ninaumia kila niuonapo uso mzuri wa kimalaika kama huu ukiwa na machozi.Ninataka tabasamu hilo lililoko sasa hivi usoni pako liendelee kuwepo katika siku zote za maisha yako” akasema Innocent na uso wa Latoya ukazidi kuchanua kwa tabasamu
“ Ouh gosh ! Why I have to die?.Sitaki kumuacha Innocent. Ananipa furaha ambayo sijawahi kuipata katika maisha yangu.It hurt that I’ve found my happiness at my dying days.It hurt even more that I cant change anything now.It’s too late.Ninachotakiwa kufanya ni kutumia kila dakika iliyobaki vizuri.Nataka nife nikiwa na furaha na zaidi ya yote nikiwa msichana.sitaki kufa nikiwa bikira.Mwanaume pekee atakayenitoa bikira yangu ni Innocent” akawaza Latoya
Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwao wote.Hakuna aliyetamani kwenda kulala.Waliongea mambo mengi sana usiku ule na hadi ilipofika usiku wa saa tisa ndipo walipoagana na kila mmoja akaenda kulala.
ENDELEA………………………..
Saa mbili za asubuhi Innocent na Latoya walikwisha jiandaa tayari kwa ratiba ya siku hiyo.Latoya alimuomba Innocent aambatane naye katika mizunguko ya siku hiyo.Saa mbili na nusu waliingia garini na na msafara wa magari sita ukaondoka.
“ nataka nizungukie sehemu zote muhimu siku ya leo kabla ya kiza kuingia.This is my last day here.Ni siku yangu ya mwisho kuwepo hapa Tanzania kwa hiyo nataka nionane na wafanyakazi wangu pamoja na kufika sehemu zile zote ambazo nilipenda kuzitembelea .Sintaziona tena” akawaza Latoya ambaye siku hii alikuwa mkimya sana.
Kituo cha kwanza ilikuwa ni katika jengo lenye ofisi zake.Wafanyakazi wake walifurahi sana kumuona mkuu wao amefika kuwatembelea.Kwa siku kadhaa hawakuwa wamemuona kutokana na matatizo yaliyompata.Aliwaita wote katika ukumbi wa mikutano na kuwashukuru kwa namna waliyvomuunga mkono wakati wa matatizo.Aliwashukuru vile vile kwa kuendelea kuchapa kazi na kujituma hata pale ambapo yeye hayupo.Aliwataka waendelee na moyo huo wa kufanya kazi kwa kujituma hata kama hatakuwepo.Latoya aliongea maneno haya kwa uso wenye tabasamu lakini moyoni alikuwa na huzuni kubwa sana kwa kuwa alifahamu wazi hataonana nao tena wafanyakazi hawa wa ofisi yake kuu ya hapa Afrika.Kwa muda mrefu amekuwa akiishi nao kama ndugu.Baada ya kuongea nao alirejea ofisini kwake ,akaingalia ofisi yake kubwa na ya kupendeza machozi yakamtoka.Alizunguka sehemu mbali mbali za jengo lile kubwa la ghorofa nane kisha akaingia garini na msafara ukaelekea sehemu nyingine.Walizunguka sehemu mbali mbali ,na halafu wakafika katika hospitali kubwa ya magonjwa ya moyo ambayo ilikuwa imekamilika kwa asilimia tisini.Hospitali hii ambayo ilijengwa na Latoya mwenyewe ilikuwa ni kwa ajili ya kutoa tiba ya maradhi ya moyo bure kwa wagonjwa wote wenye maradhi ya moyo.Hapa alitoa machozi
“ nasikitika sintaweza kuifungua hospitali hii japokuwa nilitamani sana kushuhudia mgonjwa wa kwanza akipatiwa matibabu.Hii itabaki kumbu kumbu yangu kwa vizazi vingi vijavyo.”akawaza Latoya kisha wakaondoka.
Ratiba ilikuwa ndefu sana .Alitembelea miradi mingi anayoifadhili, mashule, zahanati,vikundi vya maendeleo vya akinamama na vijana, n.k Wengi walishangazwa na ziara ile ya ghafla aliyoifanya kwani siku zote anapotaka kutembelea mahala fulani huwa anatoa taarifa mapema.
“sehemu ya mwisho kutembelea siku hii ilikuwa ni katika kanisa moja kubwa sana alilokuwa analijenga ambalo nalo lilikuwa limekamilika.
“ katika mambo yote niliyowahi kuyafanya katika maisha yangu,hili ndilo kubwa sana.Nimemjengea Mungu wangu nyumba .Kupitia nyumba hii ataabudiwa na kutukuzwa na kupewa sifa kwani ni yeye pekee anayestahili sifa na utukufu.” Akawaza Latoya huku akitabasamu kutokana na uzuri wa kanisa lile
Toka kanisani walielekea nyumbani kwa akina Innocent ambako walipokelewa kwa furaha kubwa.Hawakukaa sana wakaaga kwa dhumuni la kuondoka.Kabla hawajaondoka baba yake Innocent akamuita mwanae pembeni na kumvisha msalaba mdogo.
“ Huu utakulinda na hatari zote.Be safe my son” akasema baba yake Innocent.
Siku ilikwisha namna hii wakarejea nyumbani kwao saa tatu za usiku
“ Innocent jiandae.Saa sita kamili juu ya alama na mwanzo wa siku mpya safari yetu itaanza” akasema Latoya nakuelekea chumbani kwake huku akionekana ni mwenye majonzi mengi.
* * * *
Saa sita kasoro dakika ishirini,mlango wa chumba cha Innocent ukagonjwa akaufungua na kukutana na Latoya
“ Its time Innocent.are you ready? Akauliza Latoya
“I’m ready” akajibu Innocent.Wakaanza kushuka ngazi taratibu halafu wakatembea katika ujia moja mrefu ulioelekea baharini bila kukutana na mtu yeyote Yule.Kitu kilichomshangaza Innocent siku hii hakukuwa na mtu yeyote kulizunguka jumba la Latoya hata walinzi wake ambao huwa wanalizunguka jumba hili kwa saa ishirini na nne hakuwaona.Hakushangaa sana kwani mambo kama haya alikwisha anza kuyazoea.
“ are you nervous? Akauliza Latoya
“ No ! I’m not” Innocent akajibu
“ Good”
Walitembea katika gati kuiendea meli moja ya kifahari iliyokuwa imeegeshwa ukingoni mwa gati lile..Ilikuwa ni meli ya kupendeza na kuvutia mno
‘ welcome aboard madam Latoya” kijana mmoja aliyekuwa amevalia mavazi meupe akamkaribisha Latoya melini.Waliingia na kusalimiana na wafanyakazi kumi na nane wa meli ile na kisha wakaelekea juu kabisa ambako ndiko Latoya hupenda kukaa.
“ Latoya nimeipenda sana hii meli yako.Meli kama hizi nimekuwa nikiziona katika filamu na sikutegemea kama siku moja ningeweza kupanda meli nzuri kama hii”akasema Innocent.Latoya akatabasamu
“wanaiita meli ya maajabu kutokana na uzuri wake”
“ I wish I could live in here for the rest of my life.Hii ni meli inayoongoza kwa uzuri duniani.Sina hakika kama kuna meli ya kifahari ya kulinganisha na hii” akasema Innocent na wote wakacheka kwa nguvu
Saa sita kamili juu ya alama meli iling’oa nanga na safari ikaanza.
“ Bye bye Tanzania.nakupenda nchi yangu na watu wake.I’ll never see u again” akawaza Latoya wakati meli ikiondoka.Kwa kuwa ilikuwa bado usiku Latoya akamuomba Innocent waende kupumzika kwani bado walikuwa na safari ndefu majini.Inno akaonyeshwa chumba chake na kuingia kulala
* * * *
Saa mbili za asubuhi,Innocent aliamshwa na wahudumu.Baada ya kuoga na kujiweka safi akaenda kujumuika na Latoya kwa ajili ya kifungua kinywa.Ilikuwa ni asubuhi nzuri sana.Anga lilikuwa la bluu na kulikuwa na mawingu madogo madogo .Hakuna kilichokuwa kinaonekana mbele yao zaidi ya maji. Bahari ilikuwa kila upande.
“ Umeamkaje Innocent? akauliza Latoya ambaye uso wake ulikuwa umepambwa na tabasamu
“ Nimeamka salama Latoya.Sijui wewe”
“ Hata mimi nimeamka salama kabisa.How was your night?
“My night was so wonderfull.Nimelala usingizi mzito sana ambao sijawahi kuupata.Pengine ni kutokana na uzuri wa meli hii”
Waliendelea kupata kifungua kinywa na walipomaliza wakaenda kukaa sehemu ya kupumzika juu kabisa ya meli.Hali ya hewa ilikuwa nzuri na ya kupendeza.waliongea mambo mengi na ilipofika mchana wakaenda kupata chakula cha mchana halafu kila mmoja akaenda chumbani kwake kupumzika.Latoya alionekana kuwa na mawazo mengi mno
“ Muda unazidi kuyoyoma na muda wangu wa kuishi unakwisha .Usiku wa leo ni usiku wangu wa kipekee kabisa.Nitamwambia Innocent ukweli wa moyo wangu na usiku wa leo nitafanya mapenzi kwa mara ya kwanza.I’m prepared for that.Huu unaweza kuwa ndio usiku wangu wa mwisho kuwa na Innocent kwa hiyo kila kitu lazima kifanyike usiku wa leo.Ile ndoto yangu lazima itimie usiku wa leo.Nimeisubiri kwa muda mrefu sana siku hii ya leo ” Akawaza Latoya na kujilaza kitandani.Picha mbalimbali za maisha yake zikaanza kumjia kichwani .Alikumbuka mambo mengi sana na machozi yakamtiririka
“ Why I have to die? Latoya akasema kwa uchungu
“Sitaki kufa.Nataka niendelee kuishi.Kwa nini nife hasa katika wakati huu ambao tayari nimempata mwanaume wa ndoto zangu ? Sitaki kumuacha Innocent”
kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa Latoya kila alipofikiria kuhusiana na kifo chake.
“Nimekwisha chelewa.Siwezi tena kufanya kitu chochote kubadili ukweli huu kwamba nitakufa muda si mrefu.Ninachotakiwa kufanya ni kuutumia vizuri muda huu mchache niliobaki nao.”
Akafungua kabati lake na kuchagua nguo atakayoivaa usiku atakapokutana na Innocent kwa ajili ya chakula cha usiku
“Gauni hili nililiandaa miaka mingi kwa ajili ya kulivaa siku ya leo,usiku wangu wa kwanza na mwanaume ninayempenda.Nitalivaa kwa usiku wa leo ambao ni muhimu kwa mimi na Innocet.” Akatabasamu halafu akajilaza tena kitandani
Mlio wa saa ukiashiria ni saa kumi na mbili za jioni ulimstua Latoya toka usingizini.Akaelekea bafuni akaoga na kisha akaanza kujiandaa.Alijipaka mafuta mazuri yenye kunukia vizuri halafu akavaa gauni refu lile jekundu lililomkaa vyema.kama ilivyo kawaida yake hakuacha kuvaa koti jeusi
“ Nina hofu kubwa jinsi itakavyokuwa lakini sina namna nyingine .Usiku wa leo lazima nifanye mapenzi na Innocent.Akawaza Latoya akiwa bado amesimama anajiangalia katika kioo.Akavuta pumzi ndefu halafu akafungua mlango akatoka akaelekea katika chumba ambacho aliagiza kiandaliwe chakula maalum kwa ajili yake na Innocent usiku huo.Latoya akatabasamu baada ya kuona namna chumba kilivyokuwa kimeandaliwa na kuwekwa katika mandhari ya kimahaba kama alivyokuwa ameelekeza.Bila kupoteza muda akamtuma mmoja wa wahudumu wake akamchukue Innocent.Dakika tano baadae Innocent akawasili akiongozana na yule muhudumu
“wow ! amazing !
Akasema kwa mshangao Innocent akifurahia uzuri wa chumba kile
“Nimekipenda chumba hiki, kizuri sana” akasema Innocent na kumfanya Latoya atabasamu. Wale Wahudumu wakapewa ishara na Latoya wakaondoka na kuwaacha chumbani yeye na Innocent pekee.
“Umependeza sana usiku wa leo.Latoya you are amazing.Uzuri wako haulinganishwi na yeyote katika dunia hii“ akasema Innocent
“ Thank you Innocent’ Akajibu Latoya
“Latoya naomba niwe wazi kwako kwamba Mungu amekupendelea uzuri.Una uzuri wa kipekee kabisa.Mara ya kwanza nilipokuona nilistuka na kudhani labda wewe si binadamu wa kawaida.” Akasema Inno na kumfanya Latoya acheke kicheko kikubwa
“Thank you Innocent you always make me happy” akasema Latoya na kumkaribisha Innocent mezani
“Innocent chakula hiki cha leo ni maalum kwa ajili yetu.This is special night for me to say thank you for all that you’ve done for me” akasema Latoya
“Ouh Latoya,hakuna chochote ambacho nimekufanyia unachopaswa kushukuru.Wewe ndiye unayepaswa kushukuriwa kwa mambo ambayo umenifanyia.”
“ Innocent niruhusu nikushukuru kwa sababu pengine hufahamu thamani yako kwangu na mambo gani ambayo umenifanyia na ndiyo maana nataka kuutumia usiku huu kusema ahsante sana.Umenifanyia mambo ambayo hakuna binadamu yeyote aliyewahi kunifanyia.Umenitamkia maneno ambayo hakuna mwanadamu yeyote amewahi kunitamkia.Kwa hiyo kwa usiku wa leo nasema ahsante sana na japo kwa masaa haya machache naomba tuufanye usiku huu uwe wa aina yake.Lets forget the world for a while and make our own world” akasema Latoya halafu wakaendelea kula kwa furaha.Baada ya kumaliza kula wakaenda kuketi sofani.Latoya akamimina mvinyo katika glasi.Innocent akashangaa sana kwani toka amefahamiana naye hajawahi hata mara moja kumshuhudia akitumia mvinyo
“Latoya toka nimekufahamu sijawahi hata mara moja kukuona ukitumia mvinyo” akasema Innocent.Latoya akatabasamu halafu akanywa funda moja na kusema
“Kama nilvyokwambia awali kwamba usiku huu ni maalum kabisa kwa ajili yetu na ni usiku ambapo nina furaha ya ajabu sana na ndiyo maana nimeamua ninywe mvinyo kidogo kwa furaha niliyonayo”
“nakubaliana nawe Latoya kwamba usiku wa leo ni wa aina yake kwa sababu toka nimekufahamu sijawahi kukuona ukiwa umevaa nguo za rangi nyekundu.”
Latoya akacheka sana kusikia kauli ile ya Innoent
“Ni kweli Innocent, mimi si mpenzi sana wa rangi nyekundu, lakini leo hii imenilazimu kuvaa rangi hii kutokana na umuhimu wa usiku huu kwangu.Gauni hili nimelinunua miaka saba iliyopita na sijawahi kulivaa hata mara moja.Nilipanga nilivae gauni hili katika usiku kama huu wa leo ambao niliamini nitakutana na mtu muhimu sana katika maisha yangu.Leo ndoto yangu imetimia na ndiyo maana nimelivaa gauni hili” akasema Latoya
“.Innocent naomba ufahamu kwamba nimekwambia haya maneno toka ndani kabisa ya moyo wangu.Kwa usiku huu wa leo napenda niwe muwazi kwako kwa kila kilichopo moyoni mwangu.Vipi kuhusu wewe Innocent unaweza ukanieleza kile kilichopo moyoni mwako ambacho hujawahi kumweleza mtu yeyote? Ninamaanisha pengine kuna kitu ulipenda kunieleza lakini ulishindwa au kuogopa kutokana na mazingira? Kama unalo la kusema uwanja ni wako .Kuwa muwazi kwangu.Usiogope its just the two of us here at the middle of the ocean.” Akasema Latoya
Innocent akamtazama Latoya kwa muda halafu akataka kusema jambo lakini sauti ikakwama.Akakohoa kidogo ili kurekebisha koo lake.Latoya akamsogelea karibu akamtazama usoni na kumshika mikono,mwili wote wa Innocent ukasisimka kwa kushikwa na mikono ile laini sana.
“ Tell me Innocent,anything that you want to tell me” akasema Latoya kwa sauti laini ambayo ikampenya Innocent masikioni na kuyafanya mapigo ya moyo yaanze kwenda haraka
“Tell me Innocent” akasema tena Latoya.Mwili wa Innocent ulikuwa unatetemeka kwa hisia kalializokuwa nazo.Kitu pekee alichotaka kumweleza Latoya kwa wakati ule ni kwamba anampenda kwa moyo wake wote lakini kila alipotaka kusema ulimi ukawa mzito.Ghafla meli ikaanza kutikisika na radi kubwa ikapiga.Mvua kubwa ikaanza kunyesha.Innocent akastuka sana kwa mtikisiko ule wa meli
‘Whats that? Akauliza Innocent
“Relax Innocent.Hii ni hali ya kawaida katika safari za majini.Mara nyingi bahari huwa inachafuka” akasema Latoya
“Lakini mbona imekuwa ghafla sana? Akauliza Innocent
“ Usihofu Innocent.Meli hii ina uwezo mkubwa wa kuhimili dhoruba za baharini kama hizi.Ukiona imeyumba namna hii basi ujue kuna mawimbi makubwa sana jambo ambalo ni la kawaida baharini.Manahodha wanashughulikia suala hili na wako makini sana.” akasema Latoya kisha wakabaki wanaangaliana.Latoya akakohoa kidogo na kusema
“Innocent kama huna la kuniambia au unaogopa,mimi ninalo la kukwambia” akasema Latoya akamsogelea zaidi Innocent .Radi iliendelea kuunguruma huko nje na meli kutikisika.Latoya hakujali hilo akamsogelea zaidi Innocent na sasa nyuso zao zilikaribia kugusana.
“Innocent kuna jambo moja muhimu ambalo nataka kukwambia usiku wa leo” akanong’ona Latoya kwa sauti ndogo
“Innocent you………………” kabla hajamaliza sentensi yake ikapiga radi kubwa na meli ikatikisika kiasi kwamba vyombo vilivyokuwa mezani vikaanguka chini.Latoya akastuka na kusimama
“ Ouh gosh ! Ninafahamu sababu ya tufani hii.No ! I cant let that happen.I must do it tonight.Vyovyote itakavyokuwa usiku wa leo lazima nifanye mapenzi na Innocent.” akawaza Latoya na kisha akaenda katika meza yenye simu akawapigia manahodha wake.Aliongea nao kwa takribani dakika tatu na kisha akarejea kwa Innocent
“Nini kimetokea? Akauliza Innocent kwa wasi wasi
“relax Innocent.bahari imechafuka na sehemu hii kuna mkondo wa bahari .Usihofu tutavuka salama” akasema Latoya na kumkaribia tena Innocent
“ Innocent nataka ufahamu kwamba…….nataka ufahamu kwamba nin………….” Mara ikapiga radi kubwa na meli ikayumba .Innocent na Latoya wakajikuta wamekaribiana na midomo yao kugusana.Wote wawili walikuwa wakihema kwa kasi.
“Innocent……Inn…Innocent whatever happ…en…I..I….l..L..lo…….!!” kabla Latoya hajamaliza alichotaka kukisema ikapiga radi kubwa na kumzuia
“ Ouh gosh ! lazima nimwambie ukweli Innocent usiku huu” akawaza Latoya huku akitetemeka mwili.
“ Latoya hali inazidi kuwa mbaya..tutafanya nini? Akauliza Innocent
“Innocent naomba unisikilize.Please listen to me..” akasema Latoya huku akihema kwa kasi
“Latoya hali ni mbaya sana.Kwa nini tusiongee mambo hayo baadae wakati bahari imetulia? Akasema Innocent kwa woga huku upepo mkali sana ukiendelea kuvuma na mawimbi makubwa kuipiga na kuitikisa meli
“Innocent sikiliza kwanza.Kuna kitu unatakiwa ukifahamu.You have to know that I lo……….!!” Kabla hajamaliza sentensi yake, kishindo kikubwa cha radi kikasikika .Innocent hakuona tena kitu chochote zaidi ya giza nene.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………………
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 52
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Nini kimetokea? Akauliza Innocent kwa wasi wasi
“relax Innocent.bahari imechafuka na sehemu hii kuna mkondo wa bahari .Usihofu tutavuka salama” akasema Latoya na kumkaribia tena Innocent
“ Innocent nataka ufahamu kwamba…….nataka ufahamu kwamba nin………….” Mara ikapiga radi kubwa na meli ikayumba .Innocent na Latoya wakajikuta wamekaribiana na midomo yao kugusana.Wote wawili walikuwa wakihema kwa kasi.
“Innocent……Inn…Innocent whatever happ…en…I..I….l..L..lo…….!!” kabla Latoya hajamaliza alichotaka kukisema ikapiga radi kubwa na kumzuia
“ Ouh gosh ! lazima nimwambie ukweli Innocent usiku huu” akawaza Latoya huku akitetemeka mwili.
“ Latoya hali inazidi kuwa mbaya..tutafanya nini? Akauliza Innocent
“Innocent naomba unisikilize.Please listen to me..” akasema Latoya huku akihema kwa kasi
“Latoya hali ni mbaya sana.Kwa nini tusiongee mambo hayo baadae wakati bahari imetulia? Akasema Innocent kwa woga huku upepo mkali sana ukiendelea kuvuma na mawimbi makubwa kuipiga na kuitikisa meli
“Innocent sikiliza kwanza.Kuna kitu unatakiwa ukifahamu.You have to know that I lo……….!!” Kabla hajamaliza sentensi yake, kishindo kikubwa cha radi kikasikika .Innocent hakuona tena kitu chochote zaidi ya giza nene.
ENDELEA……………………
Moshi mkali uliomuingia puani ulimfanya apige chafya kwa nguvu mara tatu.Sauti za watu zikasikika.Walikuwa wakiongea lugha ambayo hakuifahamu.Macho yalimuuma na hakuweza kuona chochote kutokana na moshi mwingi uliokuwemo katika chumba kile.Alijaribu kufungua mdomo kutaka kuongea jambo lakini moshi mwingi ukamuingia mdomoni na kumfanya akohoe zaidi.Aliendelea kusikia watu wakiongea kwa lugha asiyoifahamu lakini hakuweza kuwaona watu hao kutokana na ,moshi mwingi.
“ Niko wapi? Ninafanya nini humu? Innocent akajiuliza huku akiendelea kukohoa na kupiga chafya mfululizo.Mwili haukuwa na nguvu na kila alipojaribu kuinua mkono alishindwa.
Mara mikono yenye nguvu ikamshika na kumnyanyua toka pale alipokuwa amelala na kumtoa ,kumpeleka sehemu nyingine yenye uwazi na upepo mzuri.Taratibu akafumbua macho na kujikuta amezungukwa na kundi la watu wanaume waliokuwa vifua wazi na viunoni mwao waljifunga ngozi za wanyama.Watu wale walikuwa wafupi wafupi na wenye miili iliyojengeka vyema.Nywele zao zilifanana na zile walizonazo watu wa bara Asia.
“ Hapa niko wapi? Hawa ni akina nani?
Akawaza Innocent akiwa amelazwa juu ya kitanda kilchosukwa kwa ngozi ya mnyama.Watu wale waliendelea kusemezana wao kwa wao huku wakimtazama .Baada ya kama dakika ishirini hivi toka awekwe pale nje, alitokea mzee mmoja mwenye ndevu nyingi nyeupe na shingoni alivaa meno mawili ya simba.Mzee yule ambaye alionekana kama ndiye mkubwa wao alimuinamia Innocent akamtazama machoni halafu akaubonyeza mkono wake.
“sukuchaa…!!!!!Kamulaping tcha..!!” akasema mzee yule na mara kikaletwa chungu ambacho ndani yake kulikuwa na vitu kama dawa.Akachota maji toka katika kile chungu akammwagia Innocent kichwani.Kilaletwa chungu cha pili kilichokuwa na kimimnika mithili ya mafuta.Mzee yule akayachota yale mafuta halafu wanaume wawili wenye nguvu wakamshika Innocent na kumpanua mdomo halafu yule mzee akayamimina mafuta yale yenye harufu mbaya mdomoni mwa Innocent ..mara tu baada ya kunywa mafuta yale Innocent akaanza kutapika huku watu wale wakishangilia.Aliendelea kutapika hatimaye nguvu zikamushia kabisa akaanza tena kuona giza akapoteza fahamu
* * * *
Alifumbua macho na kujikuta akiwa pembeni ya moto mkubwa huku idadi kubwa ya wale watu wakiwa wameuzunguka moto ule.Pembeni ya moto kulikuwa na wanyama wawili waliokuwa wakichomwa.Kiza tayari kilikuwa kimetanda lakini eneo lote lilikuwa na mwanga mkali uliotokana na ule moto mkubwa.Watu wale walikuwa wakipiga ngoma na kucheza kuuzunguka moto ule huku wakila nyama iliyokuwa inachomwa na kunywa kinywaji kilichokuwa ndani ya mitungi mikubwa.Ilikuwa ni kama sherehe kubwa
Mwili wa Innocent ulikuwa dhaifu sana na tumbo lake lilikuwa limeshinyaa kutokana na kutokuwa na kitu chochote ndani yake.Hakuwa amekula chochote.Pembeni ya pale alipokuwa amelazwa kulikuwa na watu wawili waliokuwa wamewekwa maalum kwa ajili ya kumuangalia.Walipomuona Innocent amefumbua macho wakawaita wenzao
“shukk hating ku la paochi…” akasema mzee yule.Akaushika mkono wa Innocent akauinua juu .Vijana wawili wakaleta vyungu viwili .Mzee yule akachota supu toka katika chungu kimojawapo ,Innocent akakalishwa na kunyweshwa supu ile.Baada ya supu ile akapewa uji uliochanganywa na nyama.Jasho jingi likamtiririka ,akajilaza tena kitandani akaendelea kutafakari na wale watu wakaendelea kucheza ngoma kwa furaha
“Hawa ni akina nani? Mbona wanaongea lugha ambayo siifahamu? Mimi si mtu wa maeneo haya.Sifanani kabisa watu hawa.Mimi ni nani? Nimetokea wapi? Jina langu nani? …..” akawaza Innocent
“ Ouh Mungu wangu,sikumbuki kitu chochote.Sikumbuki mimi ni nani,jina langu na nimetokea wapi.” Innocent akaogopa sana baada ya kugundua kwamba hakuwa na kumbu kumbu zozote kumhusu yeye.Alijaribu kuwaza lakini alishindwa kurejesha kumbu kumbu yoyote.
Ngoma ziliendelea kuchezwa huku nyama na vinywaji vikiendelea pia hadi walipochoka.Innocent ambaye nguvu zilianza kumrejea alikuwa amekaa akiwatazama namna walivyokuwa wanacheza .Kuna nyakati alijikuta akitabasamu baada ya kuvutiwa na uchezaji wa watu wale.Hatimaye baada ya kucheza kwa muda mrefu watu wale walipumzika na kuendelea kunywa kinywaji kile kilichokuwa katika mtungi mkubwa.Taratibu wakaanza kusinzia isipokuwa watu wale wawili waliokuwa wakimlinda.Bado aliendelea kuumiza kichwa kuhusiana na watu wale.Taratibu naye akaanza kuhisi usingzi akalala
* * * *
Sauti za watu wakizunguma karibu yake ndizo zilizomstua usingizini.Alifumbua macho na kitu cha kwanza alichokutana nacho ni anga la bluu lisilokuwa na mawingu lililong’arishwa na kijua kitamu cha asubuhi.Milio ya ndege wenye sauti mbali mbali za kuvutia ilisikika.Kwa mbali aliweza kusikia sauti za mawimbi ya bahari.Innocent alizungukwa na kundi kubwa la watu.Nyuso zao zilionyesha kuchoka kutokana na kazi kubwa ya kucheza waliyoifanya usiku uliopita.Taratibu Innocent akainuka na kukaa akaendelea kuwaangalia wale watu waliokuwa wanaongea lugha ambayo hakuifahamu.Yule mzee mkubwa wao akamsogelea na kumtazama machoni halafu akaongea maneno fulani na mara vijana wawili wakaleta chungu kilichokuwa na uji uliochanganywa na nyama Innocent akapewa akaunywa wote.Baada ya kunywa uji ule alitokwa na jasho jingi na kuanza kujisikia kupata nguvu.Watu wale waliendelea bado kumuangalia huku wakiongea kwa lugha yao.
“Nyie ni akina nani? Innocent akawauliza.Badala ya kujiibiwa watu wale wakacheka na kufurahi sana
“Hawa watu mbona wamefurahi baada ya kuisikia sauti yangu? Hawa ni akina nani? Akaendelea kujiuliza maswali ambayo hakuwa na majibu yake
Kitu kingine ambacho kiliendelea kumshangaza Innocent ni kwamba toka amejikuta katika mikono ya watu hawa hajamuona mwanamke yeyote maeneo haya
“Sijamuona mwanamke yeyote hapa.Jamii hii haina wanawake? Akajiuliza .Watu wale wakaanza kumsogelea na kumgusa ngozi yake kana kwamba walikuwa wanamshangaa.Walikuwa wanabonyeza mikono yake huku wakicheka na kufurahi.Mzee kiongozi akatamka maneno fulani halafu vijana wanne wakajitokeza na kukibeba kitanda kile alicholazwa Innocent na kuondoka huku wengine wote wakifuata kwa nyuma wakiimba na kucheza
Walitoka katika eneo lile la ufukweni na kuingia katika msitu mnene wenye kiza.Baada ya mwendo wa kama dakika ishirini hivi wakawasili katika sehemu moja iliyoonekana kama kijiji kilichokuwa na nyumba za miti.Vilikuwa ni vijumba vidogo vidogo.Innocent akawekwa ndani ya kijumba kimoja na kufungwa mikono na miguu ili asiweze kutoroka.Baada ya kama dakika kumi hivi mlango ukafunguliwa na watu wanne wakaingia ndani. Walikuwa na bakuli lililojaa nyama.Mmoja wa wale watu akamsemesha lakini Inno hakuweza kumjibu kutokana na kutoifahamu lugha yao.Watu wale wakamfungua mikono na kumsogezea bakuli la nyama akaanza kula kwa pupa.Alipomaliza kula nyama zile wale watu wakamfunga tena mikono na kuondoka zao.
“ Nimepoteza kumbu kumbu zote.Sikumbuki mimi ni nani ,nimetoka wapi na nimefikaje mikononi mwa watu hawa.Sifahamu lugha yao na siwezi kuwauliza chochote.Kwa sasa nahisi mwili wangu kuanza kupata nguvu natakiwa kufanya kitu.Lazima nifahamu hapa niko wapi na nimefikaje na ikiwezekana niweze kuondoka na kutafuta nilikotoka.” Akawaza Innocent .Watu wale waliendelea kuja mara kwa mara kumtazama na kila mara walikuwa wakimbonyeza mikono yake..Hatimaye kiza kikaingia na Innocent akalala
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………….
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 53
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Walitoka katika eneo lile la ufukweni na kuingia katika msitu mnene wenye kiza.Baada ya mwendo wa kama dakika ishirini hivi wakawasili katika sehemu moja iliyoonekana kama kijiji kilichokuwa na nyumba za miti.Vilikuwa ni vijumba vidogo vidogo.Innocent akawekwa ndani ya kijumba kimoja na kufungwa mikono na miguu ili asiweze kutoroka.Baada ya kama dakika kumi hivi mlango ukafunguliwa na watu wanne wakaingia ndani. Walikuwa na bakuli lililojaa nyama.Mmoja wa wale watu akamsemesha lakini Inno hakuweza kumjibu kutokana na kutoifahamu lugha yao.Watu wale wakamfungua mikono na kumsogezea bakuli la nyama akaanza kula kwa pupa.Alipomaliza kula nyama zile wale watu wakamfunga tena mikono na kuondoka zao.
“ Nimepoteza kumbu kumbu zote.Sikumbuki mimi ni nani ,nimetoka wapi na nimefikaje mikononi mwa watu hawa.Sifahamu lugha yao na siwezi kuwauliza chochote.Kwa sasa nahisi mwili wangu kuanza kupata nguvu natakiwa kufanya kitu.Lazima nifahamu hapa niko wapi na nimefikaje na ikiwezekana niweze kuondoka na kutafuta nilikotoka.” Akawaza Innocent .Watu wale waliendelea kuja mara kwa mara kumtazama na kila mara walikuwa wakimbonyeza mikono yake..Hatimaye kiza kikaingia na Innocent akalala
ENDELEA…………………………
Sauti za watu zikamstua Innocent toka usingizini.Akaamka na kukuta watu sita wakiwa mle kibandani.Miongoni mwao alikuwemo yule mzee kiongozi.Akamsogelea akamshika mkono akaubonyeza halafu akatabasamu na kuwageukia wenzake.Akawasemesha kwa lugha yao halafu wakaweka bakuli la nyama pembeni ya Innocent kisha wakamfungua mikono halafu wakatoka na kumuacha Innocent akiendelea kula nyama zile.Mara tu walipotoka akasikia sauti kama ya tarumbeta likipigwa na vishindo vya watu wakikimbia vikasikika halafu eneo lote likawa kimya kabisa
“Wamekwenda wapi? Tarumbeta hilo ni la nini?.Hawa jamaa wana maisha ya ajabu ajabu sana.Vitendo vyao vinanishangaza.Kila wajapo kuniangalia lazima wanibonyeze mikono yangu.Wanaangalia kitu gani katika mikono? Akawaza Innocent halafu akaanza kuzifungua kamba za miguuni baada ya kuchungulia na kuhakikisha kwamba pale hapakuwa na mtu yeyote.Kabla hajatoka mle kibandani mara mlango ukasukumwa na msichana mmoja mzuri sana mwenye nywele ndefu akaingia.Innocent akastuka asiamini macho yake.Wote wakaangaliana kwa sekunde kadhaa .Inno akataka kusema kitu lakini yule msichana akamzuia
“ shhhhhh…!!!!!!!.dont say anything.Can you speak English? Yule msichana akauliza.Innocent akatabasamu halafu akatikisa kichwa ishara ya kwamba anaweza kuzungumza kiingereza
“ Good..now follow me” akasema yule msichana huku akitoka mle kibandani.
“ where are we going? Akauliza Innocent.Msichana yule akamgeukia na kumuangalia kwa macho makali
“Stop asking question.You want to die here?
“ die here? What do you mean? Akauliza Innocent
“ C’mon guy,stop asking questions.If you want to get out of here this is the only chance you have now follow me” akasema yule msichana mzuri .Huku akiogopa Innocent akaanza kumfuata msichana yule.Walizunguka nyuma ya yale mabanda halafu wakaanza kukimbia kuelekea msitu mnene wakikimbia na kupita chini ya miti mirefu
“ Msichana huyu naye ni nani? Ananipeleka wapi? Mbona hafanani na watu hawa? Anafanya nini mahala hapa? Kwa nini ni yeye pekee anayezungmza kiingereza?
Maswali haya alijiuliza Innocent huku akiendelea kumfuata yule msichana.Mwili wake bado haukuwa na nguvu za kutosha lakini alijitahidi kwa kadiri alivyoweza kutembea kwa kasi katika msitu ule mnene.Baada ya dakika kama ishirini hivi wakajikuta wametokea ufukweni
“ Hurry up ! hurry up ! akasema yule msichana akimuongoza Innocent kuelekea sehemu kulikokuwa na boti ndogo nyeupe.waliifuata boti ile na kando yake kulikuwa na mitumbwi sita mikubwa.Wakaisukuma boti ile na kuiingiza majini
“ Hurry ..!! get in the boat” akasema yule msichana huku akimsaidia Innocent kupanda halafu akaiwasha na kuondoka kwa kasi huku Inno akishangaa.Msichana yule alionekana kuimudu vyema boti ile iliyokuwa ikienda kwa kasi kubwa.Mambo yaliyotokea Innocent aliyaona ni kama ndoto vile.Hakujua walikukokuwa wanaelekea hivyo akalazimika kumuuliza yule msichana
“ wewe ni nani na unanipeleka wapi?
“ naomba usiniulize maswali mengi tafadhali.Bado hatuko salama.Subiri hadi hapo tutakapokuwa salama na nitakujibu maswali yako yote” akasema yule msichana na kuendelea kuendesha ile boti .Bahari ilikuwa tulivu na hakukuwa na mawimbi yoyote.
Walitembea majini mwendo mrefu na hatimaye wakakiona kwa mbali kisiwa kidogo.Yule msichana akatabasamu na kusema
“ Pale ndipo tunakwenda”
“ Pale ndipo unapoishi? Akauliza Innocent lakini yule msichana hakumjibu kitu.Toka kwa mbali uzuri wa kisiwa kile ulionekana.Safari ikaendelea hadi walipofika katika kile kisiwa cha kupendeza mno.Walishuka na kuifunga boti katika kisiki cha mnazi .Kilikuwa ni kisiwa chenye uzuri wa kustaajabisha mno.Innocent akaustaajabia uzuri wa kisiwa kile kilichokuwa na miti ya kuvutia,majani mazuri na maua ya kupendeza sana.Msichana yule akamuomba Innocent amfuate na kuanza kutembea kuelekea ndani kabisa mwa kisiwa kile chenye uzuri wa kipekee.Ndege wa kila aina walikuwa wakiruka ,maua ya kila aina yalikuwa yanapatikana katika kisiwa hiki.Baada ya dakika kama kumi na tano za kutembea kwa miguu wakafika katika bustani yenye matunda mazuri yaliyoiva
“ Sijawahi kuona sehemu nzuri na ya kipekee kama hii” akasema Innocent huku akiendelea kushangaa bustani ile nzuri.
“ Ninahisi kama sipo duniani” akasema tena Innocent.
“Jina lako nani? Unatokea wapi? Yule msichana akamuuliza Innocent swali ambalo lilimbabaisha na kumfanya ashidwe kujibu
“nakuuliza jina lako nani na umetokea wapi? Akauliza tena yule msichana
“sikumbuki chochote,sina kumbukumbu zozote mimi ni nani na ninatokea wapi” akajibu Innocent
“Ulifikaje mikononi mwa wale watu? Akauliza tena yule msichana
“sina kumbu kumbu zozote nilifikaje pale.” Akajibu Innocent na kuinama chini.Yule msichana akamuangalia na kusema
“ pole sana.Usijali kumbu kumbu zitarejea taratibu.Hilo ni tatizo la kawaida katika eneo hili .Naitwa Naya” akasema yule msichana huku akimpa Innocent mkono
Kwa mra ya kanza Innocent akalishuhudia tabasamu pevu la Naya linalomfanya naye atabasamu.Uzuri wa binti huyu ulimsisimua .Akakitazama kifua chake kilichobeba titi ndogo zilizosimama akaitazama midomo laini akashusha macho yake chini na kukutana na kiuno kilichobeba miguu iliyojaa na kuzidi kumfanya binti huyu awe na uzuri wa kipekee kabisa
”nafurahi kukutana nawe Naya.U mkarimu sana” akasema Innocent
“karibu katika kisiwa hiki kijulikanacho kama black queen island.Ni kisiwa cha kipekee kabisa ulimwenguni.Upekee wake unatokana na kwamba hakimo katika ramani ya dunia” akasema Naya na kumshangaza sana Innocent
“Hakimo katika ramani ya dunia? Basi kitakuwa ni kisiwa cha kipekee kabisa.Uzuri uliomo katika kisiwa hiki haupatikani sehemu nyingine yoyote..Ukiwa ndani ya kisiwa hiki unajihis kama hauko katika dunia hii ya kawaida tuliyoizoea.Ni nani wanaishi hapa?
Naya akatabasamu na kusema
“Kisiwa hiki hakikaliwi na mtu yeyote kwa sasa.Hii ni sehemu ambayo malkia mweusi huja mara moja kila mwaka kupumzika.Majira kama haya kila mwaka huja hapa kupumzika yeye peke yake.Kuhusu wale watu kule tulikokua wanaitwa Albaque.Ni kabila dogo na wanaishi katika kisiwa kimoja kidogo mbali na hapa.Watu wale wanasifa moja kubwa tofauti na binadamu wengine. Wao wanakula binadamu wenzao”
Innocent akastuka sana na kutetemeka
“wanakula watu?! Akauliza
“Ndiyo.Wanakula watu.Huwa wanazunguka majini na katika visiwa vidogo vidogo na kuteka watu kisha huwapeleka katika kisiwa kile kuwachinja na kuwala.Ni watu makatili sana” akasema Naya
“ouh Mungu wangu..!! Nakumbuka walikuwa wakija na kunibonyeza mkono wangu lakini sikujua lengo lao lilikuwa nini”
“Hufanya vile ili kuangalia kama unafaa kuliwa.” Akasema Naya na kuzidi kumuogopesha Innocent
“Ilikuaje na wewe ukafika katika kisiwa kile? Akauliza Innocent
“ Ni hadithi ndefu kidogo lakini mimi sikutekwa.Nilifika mwenyewe katika kisiwa kile.Sikufahamu kama pale kuna watu wa aina ile .Wakati nikizunguka zunguka mle kisiwani nilijikuta nimekamatwa na wale jamaa na wakaenda kunifungia katika banda lililokuwa watu wengine wawili.Watu wale waliofungwa pamoja nami mle kibandani walianza kuliwa mmoja baada ya mwingine.Kabla ya zamu yangu kufika walikupata wewe na ukayaokoa maisha yangu.Walianza kukuandaa kwa ajili ya kuliwa .Kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja niliokaa nao nimewasoma vya kutosha.Kila siku asubuhi huwa wanakwenda katika sehemu yao ya kuabudu na baada ya hapo ndipo shughuli nyingine hufuata.Leo hii ndiyo ilikuwa siku yako ya kuliwa. Nilipowaona wameshuka bondeni, nilitoka haraka katika kibanda walichonifungia ambacho hakikuwa mbali na kibanda walichokufungia wewe.Ile boti tuliyoondoka nayo ni boti yangu ambayo nilifika nayo pale kisiwani.Najua hivi sasa watakuwa na hasira sana baada ya kukuta hatupo .” akasema Naya.Innocent alikuwa anaogopa na kutetemeka mwili
“Unahakika hawawezi kutufuata huku tulipo? Akauliza Innocent kwa wasiwasi.Naya akatabasamu na kusema
“Hapana.Hawawezi kufika huku.Kisiwa hiki hakuna mtu wa kawaida ambaye anaruhusiwa kuingia hapa.” Akasema Naya
“ Mbona mimi nimeingia? Akauliza Innocent
“ Unaonekana una muunganiko fulani na sehemu hii kwa sababu usingeweza kuingia katika kisiwa hiki wala hata kukiona.Kisiwa hiki huonekana kwa watu wachache tu ambao wanamuunganiko nacho.”.akasema Naya .Innocent akamtazama kwa mshangao
“ Kwani wewe ni nani Naya? Unaishi wapi? Katika kisiwa hiki kuna nini hadi mtu wa kawaida asiruhusiwe kuingia? Akauliza Innocent ..Naya hakumjibu kitu akachuma maembe mawili na kumpatia Innocent
“Twende upande wa pili wa kisiwa” akasema Naya.Wakaanza kutembea kuelekea upande wa pili wa kisiwa kile.Kila sehemu waliyopita ilikuwa na uzuri wa kipekee.
“Huyu Naya ni nani? Anaishi wapi? Mbona anaonekana kuyafahamu vyema maeneo haya? Kisiwa hiki kina siri gani kiasi kwamba hakuna mtu wa kawaida anayeweza kukiona wala kuruhusiwa kufika hapa? Nadhani kuna haja ya kukifahamu kiundani kisiwa hiki na kwa nini nina muunganiko nacho kama anavyosema Naya.Hisia zinakuja ni kama nimewahi kuwa na urafiki na msichana mmoja mrembo kama huyu Naya.” Akawaza Innocent wakati wakipanda kilima
TUKUTANE SEHEMU ILIYOPITA
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 54
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Mbona mimi nimeingia? Akauliza Innocent
“ Unaonekana una muunganiko fulani na sehemu hii kwa sababu usingeweza kuingia katika kisiwa hiki wala hata kukiona.Kisiwa hiki huonekana kwa watu wachache tu ambao wanamuunganiko nacho.”.akasema Naya .Innocent akamtazama kwa mshangao
“ Kwani wewe ni nani Naya? Unaishi wapi? Katika kisiwa hiki kuna nini hadi mtu wa kawaida asiruhusiwe kuingia? Akauliza Innocent ..Naya hakumjibu kitu akachuma maembe mawili na kumpatia Innocent
“Twende upande wa pili wa kisiwa” akasema Naya.Wakaanza kutembea kuelekea upande wa pili wa kisiwa kile.Kila sehemu waliyopita ilikuwa na uzuri wa kipekee.
“Huyu Naya ni nani? Anaishi wapi? Mbona anaonekana kuyafahamu vyema maeneo haya? Kisiwa hiki kina siri gani kiasi kwamba hakuna mtu wa kawaida anayeweza kukiona wala kuruhusiwa kufika hapa? Nadhani kuna haja ya kukifahamu kiundani kisiwa hiki na kwa nini nina muunganiko nacho kama anavyosema Naya.Hisia zinakuja ni kama nimewahi kuwa na urafiki na msichana mmoja mrembo kama huyu Naya.” Akawaza Innocent wakati wakipanda kilima
ENDELEA……………………….
“Ni kweli kumbu kumbu fulani zinakuja kwamba niliwahi kuwa na urafiki na msichana mmoja lakini simkumbuki ni nani na wapi.Ouh Mungu wangu nisaidie niweze kuzirejesha kumbu kumbu zangu.Nahitaji kukumbuka mimi ni nani,nimetoka wapi, na kwa nini niko hapa.” Akawaza Innocent.Hisia kwamba aliwahi kuwa na urafiki na msichana mrembo zikaendelea kuutesa ubongo wake
Hatimaye wakafika juu ya kilima na ghafla Innocent akapatwa na mshangao mkubwa baada ya kuushuhudia uzuri wa ajabu uliokuwa upande wa pili wa kisiwa kile.
“Haya ni maajabu.Sijawahi kuona sehemu nzuri kama hii” akasema Inno
“Jumba lile unaloliona ni la Malkia mweusi” akasema Naya
“Anatoka wapi huyo malkia mweusi? Akauliza Innocent
“Malkia mweusi hana nchi.Yeye ni malkia wa dunia nzima.Alitakiwa kuwepo hapa katika jumba lake mida hii lakini alifaya makosa makubwa katika utawala wake makosa ambayo adhabu yake ni kifo”
“Alifanya makosa gani? Kwa nini awe ni malkia wa dunia? Mbona mimi sijawahi kumsikia huyo malkia wa dunia?
“Hata kama umewahi kumsikia lakini huwezi kumkumbuka tena.Kuhusu makosa aliyoyafanya hata mimi sifahamu”
“Umewahi kuonana na malkia mweusi? Akauliza Inno
“Ndiyo.Nimewahi kuonana naye.Ni mrembo mno.Ana uzuri wa ajabu sana” akasema Naya halafu akasita kama mtu anayekumbuka kitu .Innocent akamuangalia na kuuliza
“Nani wanaishi pale katika jumba lile malkia mweusi asipokuwepo?
“Jumba lile halikaliwi na mtu yeyote .Ni malkia mweusi pekee ambaye anaruhusiwa kukaa ndani ya lile jumba”
“Kuna nini ndani ya jumba lile kiasi kwamba haruhusiwi kuingia mtu mwingine ?
“Mimi sifahamu chochote kuhusiana na kilichomo mle ndani.Hakuna mtu mwingine zaidi ya malkia mweusi anayeruhusiwa kuingia mle ndani.” akajibu Naya
Innocent akalitazama jumba lile na kusema
“Nataka kuingia ndani ya lile jumba.Nataka kuona kilichomo ndani yake.” Akasema Innocent huku akiinua mguu tayari kwa kuanza kushuka kilima.Naya akamzuia
“Hapana usithubutu kufanya hivyo.Usithubutu kuingia ndani ya jumba lile” akasema Naya
“ kama hutaniambai kuna nini ndani ya ile nyumba ,mimi naenda kuangalia mwenyewe.Nataka nifahamu siri za kisiwa hiki na kwa nini nina muunganiko nacho kama unavyosema” akasema Innocent na kuanza kupiga hatua.Naya akamkimbilia na kumshika mkono.Mara akastuka ghafla kama kwamba ameona kitu ha kutisha sana.Innocent naye akastuka wakabaki wanatazamana.Naya alikuwa anahema haraka haraka
“Naya una tatizo gani? Akauliza Innocent.Midomo ya Naya ilikuwa inatetemeka.Alishindwa kuongea.Innocent akamsogelea karibu na kumuuliza
“ Naya una tatizo gani? Mbona umebadilika ghafla?
Naya akamtazama Innocent usoni halafu akauliza kwa sauti yenye kitetemeshi
“ Hiyo pete kidoleni umeipata wapi?
Innocent akastuka na kuinua kiganja cha mkono wa kushoto .Ni kweli alikuwa na pete ya dhahabu kidoleni.Picha moja ikapita kichwani kwake ghafla lakini akashindwa kutambua picha ile.Kuna kumbu kumbu ilikuwa inakuja na kupotea
“ Sikumbuki pete hii nimeipata wapi.Kwani ina nini? Akauliza Innocent.Naya akamshika mabegani na kusema
“Tafadhali naomba ujitahidi kukumbuka pete hii umeipata wapi? Ni muhumu sana kwangu na kwako pia”
“Sikumbuki kitu chochote Naya.Sikumbuki nimeipata wapi hii pete.” akajibu Innocent halafu akakumbuka kwamba alikuwa na msalaba shingoni.Akaupeleka mkono wake na kuushika na mara kumbu kumbu fulani ikaja na kupotea.Akastuka
“ Umekumbuka kitu chochote ? akauliza Naya
“ Kuna kumbu kumbu inakuja na kupotea” akajibu Inno
“Ouh jamani.Jitahidi ukumbuke.Kumbuka chochote kuhusiana na pete hii.Kuna mtu aliwahi kukupa pete hii? Ni nani ?
“Sikumbuki chochote Naya na wala sikumbuki kama kuna mtu aliwahi kunipa hii pete ingawa kuna kumbu kumbu inanijia na kutoweka..Hii medali nakumbuka kama….kama ..k….ouh sikumbuki tena chochote” akasema Inno na kuinama chini
“ Sikumbuki chochote kuhusu hii pete wala chochote kuhusiana na maisha yangu.Kwa nini Naya amestuka baada ya kuiona pete hii ? Pete hii ina nini? Ina mahusiano yoyote na mahala hapa? Akawaza Innocent halafu akainua kichwa na kumtazama Naya
“Naya naomba uniambie pete hii ina nini?Nahitaji kufahamu tafadhali ili kama ni ya hatari basi niitoe mara moja” akasema Inno.Naya akamshika mkono na kumketisha katika majani na kusema
“Unaiona pete hii katika kidole changu? Akauliza Naya
“Ndiyo.Mbona inafanana na hii ya kwangu?
“Hicho ndicho kitu ambacho nataka kukifahamu.Pete hizi mbili zina utofauti.Hii ya kwangu ina nyota yenye rangi ya bluu na hii ya kwako ina nyota yenye rangi nyekundu.Pete hizi hazivaliwi wala kupatikana kwa mtu ambaye hahusiki.Mtu wa kawaida haruhusiwi kuwa na pete hizi” akasema Naya
“Sijakuelewa Naya.Nini maana ya pete hizi? Zinatoka wapi? Kwa nini huvaliwa na watu maalum tu? Hao watu maalum ni akina nani?Wewe ni nani Naya? Pete hii imefikaje kidoleni kwangu? Innocent akauliza maswali mfufulizo.Naya akavuta pumzi ndefu na kusema
“Mpaka pete hii imefika kidoleni mwako lazima utakuwa unafahamu mambo mengi makubwa” akasema Naya na kuzidi kumchanganya Innocent
“Naya sikumbuki kama ninafahamu chochote kuhusu pete hii” akasema Inno
“Ni kwa sababu umepoteza kumbu kumbu lakini kuna mambo mazito ambayo lazima umeyashuhudia” akasema Naya na kuushika msalaba ule shingoni kwa Inno
“Huu umekusaidia .Umekuokoa” akasema Naya
“Umeniokoaje? Akauliza Inno
“Ulitakiwa ufe lakini msalaba huu umekuokoa” Naya akazidi kumchanganya Innocent
“Nilitakiwa nife? Kwanini nife? Nani alitaka kuniua? Umefahamu vipi kama nilitakiwa kufa? Akauliza Inno kwa wasi wasi.Naya akamshika mkono na kusema
“Pete hii ulipewa na malkia mweusi.”
‘Mimi ?!! Innocent akashangaa
“Sifahamiani na huyo malkia mweusi na wala sijawahi kumuona na hajawahi kunivisha pete hii”akasema Inno.Naya akamuangalia halafu akatabasamu
“Hatimaye nimefanikiwa kukuona.Ni wewe !! “ akasema Naya huku akitabasamu halafu akamkumbatia Inno kwa nguvu
“Ouh ahsante Mungu.Nimefanikiwa kuonana na mkombozi wetu” akasema Naya huku machozi yakimtoka .Inno akashangaa
“Naya sikuelewi kwa haya maneno unayoyasema.Mimi nitakuwaje mkombozi wenu? Wewe na nani?
Naya hakujibu kitu akaendelea kufuta machozi
“Naya tafadhali naomba unieleze ukweli kuhusu maneno hayo unayoyasema.” Innocent akasisitiza.Naya akainama kwa sekunde kadhaa na kusema
“Nilikuwa na umri wa miaka kumi na miwili baba yangu aliponichukua na kunipeleka katika hekalu fulani ambako alinitoa sadaka.Nakumbuka tulikuwa watu wawili siku hiyo .Mimi na malkia mweusi.Baada ya ibada ile ya kutolewa sadaka nilichukuliwa na wazazi wangu na sikuelewa maana ya kutolewa sadaka.Nilipofikisha miaka kumi na minne,nililetwa katika kisiwa kitukufu kwa ajili ya kujifunza kuhusu maisha yetu na kujiandaa kwa ajili ya kuwa mrithi wa malkia mweusi.Nimeishi kisiwani kwa miaka kumi sasa.Nimejifunza mambo mengi .Nimeiva katika imani yetu na tayari nilitegemewa kumrithi malkia mweusi lakini sikuwa tayari kwa hilo.Niliamua kutoroka na badala yake nikaishia mikononi mwa wale wala watu.Safari yangu haikuwa ya bure kwani nimefanikiwa kukutana nawe mtu muhimu sana ambaye umekuwa ukisubiriwa na watu wengi kwa muda mrefu” akasema Naya
“Naya unazidi kunichanganya.Mimi nina umuhimu gani kwenu? Sielewi chochote Naya” akasema Inno
“Huwezi kuelewa Innocent kwa sababu kumbu kumbu zako hazitarudi kamwe hadi hapo utakapokuwa umekamilisha kazi unayotakiwa kuifanya”
“Kazi ninayotakiwa kuifanya? Ni kazi gani hiyo? Akashangaa Inno
“Unatakiwa ukamuokoe malkia mweusi ambaye muda wowote atauawa.Adhabu yake imeshatolewa lakini haiwezi kutekelezwa pasipokuwapo pete hii”
“ Yuko wapi malkia mweusi? Nitamuokoa vipi ? akauliza Inno
“Iko hivi” .akasema Naya halafu akamuangalia Inno aliyekuwa kimya akisikiliza kwa makini
“Kuna kitabu ambacho unatakiwa ukipate na uichane sura ya sita kati kati.Kitabu hicho kitukufu kimehifadhiwa katika pango lenye nyoka mkubwa na katika chumba kilimo kitabu hicho kuna moto mkali sana na kati kati ya huo moto kuna jiwe kubwa ambalo juu yake ndipo kipo kitabu hicho” akasema Naya na kumuogopesha Inno
“Hilo haliwezekani Naya.Siwezi kufanya kitu kama hicho.Sehemu hiyo haiingiliki hata kidogo na hakuna uwezekano wowote wa kukichukua kitabu hicho kitukufu.Nitawezaje kupambana na huyo nyoka mkubwa? Nitawezaje kuingia katika chumba chenye moto mkali? akasema Inno
“Lazima uende.Lazima umuokoe malkia mweusi na sisi sote na huo ndio utakuwa mwisho wao.” Akasema Naya huku ameukunja uso wake.Innocent akauliza
“ Naya kwa nini mimi nikaifanye kazi hiyo ya hatari na si mtu mwingine? “
“Kwa sababu wewe ndiye uliyechaguliwa.Wewe ndiye uliyepewa nguvu za kuwamaliza hawa watu”
“Nimechaguliwa na nani? Nguvu gani nilizonazo? Ni watu gani ambao natakiwa kuwamaliza? Akauliza Inno
“Ni hadithi ndefu sana lakini nina imani haya yote yalikwisha fanyika lakini hukumbuki chochote”
“Naya bado sijakuelewa vizuri.Nani huyo aliyenichagua? Amenifahamu vipi mimi? Akauliza Inno.Naya akamtazama na kusema
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………….
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 55
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Kuna kitabu ambacho unatakiwa ukipate na uichane sura ya sita kati kati.Kitabu hicho kitukufu kimehifadhiwa katika pango lenye nyoka mkubwa na katika chumba kilimo kitabu hicho kuna moto mkali sana na kati kati ya huo moto kuna jiwe kubwa ambalo juu yake ndipo kipo kitabu hicho” akasema Naya na kumuogopesha Inno
“Hilo haliwezekani Naya.Siwezi kufanya kitu kama hicho.Sehemu hiyo haiingiliki hata kidogo na hakuna uwezekano wowote wa kukichukua kitabu hicho kitukufu.Nitawezaje kupambana na huyo nyoka mkubwa? Nitawezaje kuingia katika chumba chenye moto mkali? akasema Inno
“Lazima uende.Lazima umuokoe malkia mweusi na sisi sote na huo ndio utakuwa mwisho wao.” Akasema Naya huku ameukunja uso wake.Innocent akauliza
“ Naya kwa nini mimi nikaifanye kazi hiyo ya hatari na si mtu mwingine? “
“Kwa sababu wewe ndiye uliyechaguliwa.Wewe ndiye uliyepewa nguvu za kuwamaliza hawa watu”
“Nimechaguliwa na nani? Nguvu gani nilizonazo? Ni watu gani ambao natakiwa kuwamaliza? Akauliza Inno
“Ni hadithi ndefu sana lakini nina imani haya yote yalikwisha fanyika lakini hukumbuki chochote”
“Naya bado sijakuelewa vizuri.Nani huyo aliyenichagua? Amenifahamu vipi mimi? Akauliza Inno.Naya akamtazama na kusema
ENDELEA…………………..
“Sophie alikuwa bibi mzee ambaye naye alishi maisha yake yote katika imani hii.Hakuwahi kuufurahia usichana wake hata kidogo.Nilipoletwa huku kisiwani,kwa mafunzo Sophie alinipokea na akatokea kunipenda sana .,Alinionea huruma na hakutaka niishi maisha kama aliyoishi yeye.Siku zote alinisihi kwamba nisikubaliane na chochote kile watakachoniamuru nifanye.Alikuwa ndiye mtetezi wangu.Alinikingia kifua katika kila jambo.Kwa bahati mbaya Sophie alifariki.Alifia mikononi mwangu.Kabla hajafariki aliniita chumbani kwake na kunipa siri kubwa.Aliniambia kwamba siku moja nitakutana na mtu ambaye atatukomboa.Hakuniambia kwamba mtu huyo nitakunata naye wapi lakini aliniambia kwamba mtu huyo nitakayekutana naye tayari atakuwa amejazwa nguvu za kuweza kupambana na kutukomboa.Alinipa ishara tatu ambazo zingeniwezesha kumtambua mtu huyo na ishara mojawapo ni pete hii uliyoivaa.Hii ni pete yenye nguvu sana na nina hakika lazima kuna sababu nzito sana iliyomfanya malkia mweusi akaitoa kidoleni mwake na kukupa.Inawezekana mlikuwa katika mapenzi mazito na hivyo akaona ni vyema kama atakulinda “
“mapenzi ?!! Innocent akashanga
“Sijawahi kuwa katika mapenzi na mwanamke yeyote achilia mbali huyo malkia mweusi.” Akasema Innocent ghafla kumbukumbu fulani ikamjia na kupotea
“Kuna kitu umekumbuka? Akauliza Naya
“Kuna kumbukumbu inakuja na kutoweka.Sikumbuki chochote tena lakini kuna hisia ninaanza kuzipata ni kama niliwahi kuwa mapenzini na mtu fulani” akasema Inno
“Usijali.Kumbu kumbu zote zitarejea.Kitu kikubwa ambacho tunatakiwa kukifanya sasa ni kwenda katika kituo cha kwanza alichonielekeza Sophie.Sehemu hii na zote tutakazozipitia ni za hatari lakini hatuna budi kwenda” akasema Naya.Innocent hakujibu kitu akabaki amesimama akitafakari
“Uko tayari kwenda? Unahitaji kuzirejesha kumbu kumbu zako? Akauliza Naya
“Niko tayari Naya japokuwa sielewi nitaiwezaje kazi hii ngumu “
“ahsante .Umefanya maamuzi ya busara na kwa maamuzi hayo utatukomboa sisi sote.Twende tuondoke” akasema Naya na kumshika mkono Innocent wakaanza kushuka kilima kuelekea ufukweni hadi mahala walikoiacha boti waliyokuja nayo.
“Tunaeleka wapi? Akauliza Innocent
“katika kituo cha kwanza kama alivyonielekeza Sophie”
Safari ikaanza na Naya alionekana kuyafahamu vyema mazingira yale ya bahari.Kadiri walvyozidi kusonga mbele ndivyo hali ya bahari ilivyozidi kuchafuka.Innocent akaogopa
“Naya hatuwezi kwenda zaidi ya hapa.Geuza boti turudi.bahari imechafuka na tunaweza kupoteza maisha.Twende turudi tulikotoka” akasema Inno
“Hatuwezi kurudi.Vyovyote itakavyokuwa lazima tusonge mbele.Hatuwezi kurudi nyuma.” Akasema Naya kwa ukali.Boti ile iliendelea kuchana mawimbi makubwa .Upepo mkali na ngurumo vikatawala bahari.Hali ya bahari ilikuwa mbaya sana.
“Karibu tutafika.” Akasema Naya na kumpa moyo Inno ambaye alikuwa akiogopa
Dakika kumi baadae wakasili katika kisiwa kidogo.Mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali na radi ilikuwa inanyesha.Innocent alikuwa anatetemeka mwili mzima kwa baridi kali aliyoisikia.Taratibu akaanza kukata tamaa ya kuendelea mbele
“Naya siwezi kuendelea tena zaidi ya hapa.Mwili wangu hauna nguvu hata kidogo” akasema Innocent na kuanguka chini
“Jitahidi .Tumeshafika ! Tafadhali usikate tamaa” akasema Naya.Mvua kubwa ikaendelea kunyesha.Alimshika mkono Innocent aliyekuwa ameanguka pake chini kwa lengo la kumnyanyua lakini ghafla akasukumwa na kitu kama upepo mkali na kuanguka katika jiwe.Alijilaza pale juu ya jiwe huku akisikia maumivu makali .Mvua kubwa iliendea kunyesha pamoja ngurumo za kutisha za radi
“lazima nimfikishe ndani.Lazima atukomboe” akawaza Naya halafu akainuka huku akipepesuka kutoka na upepo mkali na kumfuata Innocent. Akajaribu kunyanyua lakini akashindwa.Hakukata tamaa akaanza kumvuta huku akisukumwa na upepo mkali
Hatimaye Naya akafanikiwa kumfikisha Innocent katika pango.Ndani ya pango lile kulikuwa na mwanga na joto kali tofauti na nje kulikokuwa na baridi kali mno.Mbele kabisa ya pango lile kulikuwa na jiwe mfano wa meza ndogo ambalo juu yake kulikuwa na kitu fulani chenye umbo la duara mfano wa tufe ambalo lilikuwa linatoa mwanga ule mkali.Naya akazidi kupata nguvu na kumvuta Innocent hadi katika lile jiwe mfano wa meza.Akauinua mkono wa Innocent uliokuwa na ile pete halafu akauweka katika lile tufe lenye kutoa mwanga mkali
Mara tu mkono wa Innocent ulipowekwa juu ya lile tufe,radi kubwa ikapiga na kisiwa chote kikatikisika.Pete ile ya Innocent ikaanza kutoa mwanga mwekundu na mara mwili wa Innocent ambao ulikuwa dhaifu sana ukapatwa na nguvu za ghafla.Ngurumo za radi zikaendelea kusikika na ghafla kitu cha ajabu kikamtokea.Mbele yake alisimama mzee mmoja mwenye ndevu nyingi na aliyevaa nguo ndefu nyeupe na kujifunga mshipi mwekundu kiuononi.Mkononi mwake alikuwa ameshika ubao wenye maandishi.Akamtaka Innocent ayasome maandishi yale.Mara tu alipomaliza kuyasoma maandishi yale kumbukumbu fulani ikamjia.Alikumbuka aliwahi kumuona mahala mzee yule.Wakati akijaribu kutaka kukumbuka mahala alikomuona yule mzee,lile jiwe ambalo juu yake kulikiwa na tufe alilokuwa ameliwekea mkono likaanza kutikisika halafu ,likafunguka.Naya aliogopa sana kwa mambo aliyoyaona mle pangoni
Mara mtetemeko ule ukakoma Innocent ambaye tayari alikwisha rejewa na nguvu akalitazama jiwe lile lililofunguka.Ndani yake kulikuwa na upanga wenye kumeremeta.Wakati anaendelea kuushangaa upanga ule ,mara mbele yake akasimama tena yule mzee mwenye ndevu nyingi
“Chukua huo upanga.Nenda sasa kamuokoe Latoya” akasema yule mzee na kutoweka.
“Latoya!!....? Latoya ..?!! Jina hili si geni kwangu.Nakumbuka ni jina ambalo nimezoea kulitamka.Latoya ni nani ambaye natakiwa kumuokoa? Innocent akajiuliza na kukosa majibu.Taratibu akainama na kuushika upanga ule kwa mikono yake.Mara tu alipousika ule upanga vitu kama chaji za umeme vikamuingia mwilini na kupiga ukekele mkubwa.Baada ya dakika tano akajisikia mzima .Huku akiwa na upanga wake mkononi Innocent akageuka na kumtazama Naya aliyekuwa amejikunyata kwa uoga katika pembe moja ya pango
“twende tuondoke” akasema Inocent
“Nipeleke sehemu ya pili”
Naya akamtazama Innocent akataka usema kitu lakini kabla hajatamka chochote kukatokea tetemeko kubwa.Mawe yakaanza kuporomoka
“Twende tuondoke humu haraka” akasema Innocent na kwa kasi akamshika Naya mkono wakaanza kukimbia kutoka ndani ya lile pango huku mawe yakiendelea kuporomoka nyuma yao.Walifanikiwa kutoka salama ndani ya pango lile na.Bado mvua iliendea kunyesha ikiambata na upepo mkali ngurumo na tetemeko.Miti na mawe vikaendelea kuanguka kutokana na mtikisiko ule mkubwa. Wakaingia katika boti yao na kuanza kuondoka kwa kasi
“Tazama nyuma” akasema Naya wakati wakiendelea na safari .Inno akageuza kichwa na kutazama nyuma.Kisiwa kilikuwa kinazama.
“Ouh Mungu wangu .Haya ni maajabu.Sijawahi kuona mambo ya ajabu kama haya” akasema Inno.Hakuwahi kushuhudia kitu cha namna ile katika maisha yake.Aliogopa sana
Naya aliendelea kuendesha boti ile kwa kasi kubwa.Kwa sasa hali ya bahari ilizidi kuwa mbaya na wingu zito jeusi lilitanda na kupafanya baharini kuwe na kiza.Mawimbi makubwa yalitokea na upepo mkali ukaendelea kuvuma.Ilikuwa ni hali ya kutisha sana .
“ Nashindwa kuona tunakoelekea.Hali imekuwa mbaya sana” akasema Naya.Innocent akamkumbuka yule mzee mwenye ndevu nyingi halafu kumbukumbu fulani ikamjia ghafla.Alimuona mzee yule akimuelekeza maneno fulani na kumwambia ayatamke pale anapokuwa katika matatizo.Inno akayakumbuka maneno yale na kuyatamka na mara tu alipomaliza kuyatamka pete aliyovaa ikaanza kutoa mwangaza mkubwa.Naya akatabasamu na safari ikaendelea kwani aliweza kuona walikokuwa wakielekea.
Kwa mbali waliona kitu mithili ya moto
“Pale ndipo tunalekea” akasema Naya kwa uoga
“Mbona kama kunawaka moto ? akauliza Inno
“Kisiwa kile huwa kimezungukwa na moto unaowaka masaa yote.Ni sehemu ambayo hakuna mtu wa kawaida anaweza kufika wala kupaona.Pale ndipo kinahifahiwa kitabu kitukufu” akasema Naya.Innocent akastuka sana
Kadiri walivyozidi kukikaribia kisiwa ndivyo joto lilivyozidi kuongezeka.hata maji nayo yalianza kuwa ya moto.
“ Hapa lazima tufanye kitu.Hatuwezi kuingia salama pale kisiwani” akasema Innocent.Naya hakujibu kitu akabaki anamtazama Inno.Innocent akayatamka kimya kimya maneno yale ambayo aliambiwa ayatamke mara apatapo shida na mara tu alipomaliza kuyatamka ,upepo mkali ukavuma na kusababisha mawimbi makubwa kutokea
“Ee Mungu wangu naomba utulinde na hali hii ya kutisha.Sijawahi katika maisha yangu kushuhudia mambo ya kutisha kama haya” Innocent akaomba kimya kimya akiwa ameushikilia msalaba aliouvaa shingoni.Ghafla likatokea wimbi kubwa mfano wa mlima na kuwafunika kukawa na kiza kinene .
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………………….
SEHEMU YA 50
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Oh Mungu wangu ! Latoya si binadamu wa kawaida.Mambo yake ni mazito na yanaogopesha.” akawaza Innocent huku akihisi baridi mwilini
Latoya aliingia katika jumba lile ambalo lilikuwa na giza nene ndani.Akawasha taa ndogo nyekundu iliyomuwezesha kuona.Akafungua chumba kimoja akangia.Akavua mavazi yake na kuvaa gauni refu jeupe.Akatoka mle chumbani na kuelekea katika ukumbi mpana.Alikuwa akitembea taratibu hadi katika meza yenye mishumaa sita na kuiwasha halafu akapiga magoti akainama na kusujudu
“ Atha.Lut pakta du mokaja,akta pata ovakoja du mapakta” alitamka taratibu maneno haya .Akayarudia mara tatu na mara moshi ukaanza kutoka katika madhabahu ile .Latoya akaendelea kuongea maneno aliyoyafahamu yeye mwenyewe na kila alipoongea moshi mwingi ulizidi kutoka.Ulikuwa ni moshi wenye harufu nzuri ya uturi.Chumba chote kilijaa moshi na mara ghafla ukatokea mwanga mkali sana ambao ulimulika eneo lile lote.Baada ya mwanga ule mkali kutokea,Latoya akainuka na kusimama .Mbele yake toka ndani ya moshi ule wakatokea watu wawili wenye mavazi meupe na ndevu nyingi
ENDELEA………………………..
“Innocent.!! Innocent !!!..” Ilikuwa ni sauti ya Latoya iliyomstua .Akafumbua macho na kuangaza huku na huku.Alikuwa ni kama mtu aliyechanganyikiwa.Latoya akamshika kichwani kwa mikono yake na mara fahamu zake zikamrejea
“ Latoya ..!!..” akasema Innocent
“ what happened?Nilisikia unalia nikataka kukufuata huko ndani lakini ghafla nika……” kabla hajamaliza sentensi yake Latoya akasema
“I know what happened.Twende tondoke”
Wakaingia garini na kuondoka
“Kwa masikio yangu nimesikia Latoya akipiga ukelele wa uchungu .Nilitaka kuingia mle ndani lakini kilichonitokea sintakisahau.I’m real scared” akawaza Innocent halafu akageuza shingo yake na kumtazama Latoya
“Huyu si binadamu wa kawaida.Kuna siri nzito katika maisha yake.Ouh Mungu wangu mambo yaliyoko hapa ni mazito .Natamani niondoke na kuachana na maisha haya lakini siwezi tena .I’m stuck in here and I cant leave this place anymore because I love Latoya.” Akawaza Innocent na kwa mbali macho yake yakatoa machozi
“ Latoya ni nani hasa? Natamani nimjue kiundani lakini naogopa.Maisha yake yametawaliwa na nguvu zisizo za kawaida.” akawaza halafu akageuka tena na kumtazama Latoya.Alikuwa ameinama analia
“ Latoya …..!!!!! akaita Innocent.Latoya hakuitika
“ Latoya ….!! akaita tena.Latoya akageuza shingo na kumtazama Innocent.
“ are you ok? Akauliza Inno
“ I’m ok Innocent.” Akajibu Latoya
“ You are crying.Whats your problem?
“ Never mind about me.I’m ok” akajibu Latoya Innocent hakumuuliza tena kitu chochote
“Naogopa kumuuliza tena kitu chochote.Anaonekana ana jambo zito, ngoja nimuache” akawaza Inno
“ Innocent” akaita Latoya
“ naam Latoya” akaitika Inno
“ Jiandae kesho kutwa tuanze ile safari yetu”
“ Usijali Latoya Mimi niko tayari muda wowote kuongozana nawe sehemu yoyote ile” akajibu Inno
“ ahsante sana Innocent.Thank you for being there for me” akasema Latoya halafu safari ikaendelea kimya kimya hadi wakafika nyumbani.Latoya hakuongea na mtu akapanda moja kwa moja ghorofani kwake.Innocent naye akapanda chumbani kwake.
“ Nimeogopa sana kwa kilichotokea leo.Kwa nini Latoya alikuwa analia.? Kuna mtu alikuwa anamuumiza?Kuna nini ndani ya jumba lile? Maswali haya yaliendelea kumuumiza kichwa Innocent lakini hakuweza kupata jawabu.
“ katika maisha yangu sijawahi kukutana na mauza uza kama haya.Inawezekana ni mipango yake nikutane na Latoya ili niweze kuufahamu upande wa pili wa mwanadamu ukoje.” akawaza Innocent akiwa kitandani.Alihisi joto sana akavua shati
“ Latoya anataka twende wapi kwa mapumziko?Niliwahi kumuuliza ni wapi tunakwenda lakini hakuwa tayari kuniambia.Kutokana na maisha haya anayoishi ananipa uoga hata mimi kuhusiana na safari hiyo ya sisi wawili pekee japokuwa ninatamani sana kuwa karibu naye nimueleze kilichomo moyoni mwangu.”
Innocent akastuliwa toka katika mawazo mengi na mlio wa simu
“hallo” akasema Innocent
‘ Innocent naomba tukutane bustanini” akasema Latoya
‘”Ok Latoya Nakuja sasa hivi” akajibu Innocent
“Wanasema kwamba Love is all about sacrifices.Because I love her I’ll sacrifice everything for her .I know its not going to be easy but even if it’s going to take my whole life I’ll die trying.” Akawaza Innocent halafu akavaa shati akatoka mle chumbani na kuelekea katika bustani ya Latoya iliyoko juu.Tayari Latoya alikwisha fika kule bustanini.
“ Unajisikiaje Innocent? akauliza Latoya
“ I’m ok Latoya.najisikia vizuri.Vipi kuhusu wewe? Unajisikiaje?
“ Najisikia vizuri Innocent” akajibu Latoya.
“Nikikuangalia machoni naona kama hauko sawa.Kitu gani kinakusumbua Latoya? Akauliza Innocent
“Ouh Innocent don’t mind about me.I’m ok.Ni uchovu ndio unaonisumbua .Hii ni sababu inayonipelekea kuamua kwenda mapumzikoni.Vile vile mambo mengi yametokea katika kipindi kifupi kwa hiyo ninahitaji kupumzika na kujaribu kuyasahau yote yaliyotokea. Nikiwa kisiwani husahau dunia kwa muda.No TV, no phone calls,no meetings,no any contact with the world.Its just me and the island.I talk to birds,animals and I go back to sleep.Hivyo ndivyo namna ninavyoishi nikiwa mapumzikoni” akasema Latoya
“Nimeipenda sana aina yako ya upumzikaji lakini kwa kuwa umezoea kuwa mwenyewe huoni kwamba nitakuwa mzigo kwako na kukuzuia usipumzike vile ulivyozoea? Akauliza Inno
“Innocent huwa ninakwenda mapumzikoni peke yangu kwa sababu sikuwa na mtu ninayemuamini ambaye ningeweza kwenda naye.Safari hii nimekupata wewe ambaye ninakuamini na kwa hiyo nitakuwa na mapumziko mazuri sana kuliko miaka yote ambayo nimekuwa nikipumzika peke yangu.Innocent wewe ni mtu wangu wa muhimu sana .Tumejuana katika kipindi kifupi lakini naomba ufahamu kwamba nilikujua kabla hata hatujakutana na ndiyo maana umetokea kuwa mtu muhimu mno kwangu.Duniani ninafahamika na mamilioni ya watu lakini sijawahi kupata rafiki kama wewe.Ninafurahi na kufarijika ninapokuwa nawe” akasema Latoya halafu akavua pete yake ya dhahabu na kumvalisha Innocent kidoleni
“ Innocent nakupatia pete hii, ambayo ni ya muhimu sana kwangu.Ninakuomba usiivue pete hii.Huu ni ukumbusho wangu kwako hata kama hatutakuwa pamoja kwa muda mrefu.Wakati mwingine inaweza ikawa na msaada mkubwa kwako “ akasema Latoya
“ahsante sana Latoya.Its a beautiful ring.I love it” akasema Innocent huku akifurahia pete ile nzuri
“ Utanikumbuka kila mara utakapoitazama pete hii” akasema Latoya huku akitabasamu
“Latoya bila hata ya pete hii,ninakukumbuka kila dakika ya maisha yangu.You are a wonderfull person I’ve ever met.Ninafurahi sana kuwa mmoja wa watu wako wa karibu”
“ Ouh Innocent,that’s so sweet.Ndiyo maana napenda kuwa nawe karibu muda wote.Ninapokuwa nawe ninasahau matatizo yangu.I forget death and everything..” akasema Latoya na ghafla akanyamaza na kumtazama Innocent ambaye alikuwa anatabasamu
“Innocent natamani watu wote duniani wangekuwa kama ulivyo wewe Dunia ingekuwa mahala pazuri sana pa kuishi lakini kwa bahati mbaya dunia hii imejazwa na watu makatili wasio na hata chembe ya huruma kwa wenzao” akasema Latoya
“ Kwa nini unasema hivyo Latoya? Akauliza Innocent
“Innocent bado hujajaliwa kuufahamu pande wa pili wa duna hii ukoje.Dunia hii ina sehemu mbili moja ni hii tunayoiona kwa macho ya kawaida nay a pili haionekani kwa macho ya kawaida.Siku ukijaliwa kuiona sehemu ya pili ya dunia hii utakubaliana na ninachokwambia kwamba binadamu ni kiumbe anayeweza kubadilik na kuwa mbaya sana kuliko hata mnyama wa mwitu” akasema Latoya
“nakubaliana nawe Latoya duniani humu kuna mambo mazito ambayo hatuwezi kuyaona,kuna watu makatili na ubinafsi umeitawala dunia siku hizi”
“ Thats my point.Mungu aliumba mwanadamu akamuweka duniani atawale kila kitu ,lakini mwanadamu huyo huyo amemgeuka hata muumba wake na kumpinga.Watu wanazivunja amri zake .Hawamuabudu tena.Wamewageukia miungu wengine.Wanaua wanadamu wenzao pamoja na kutenda dhambi nyingi zenye kuleta machukizo mbele za Mungu.Do you think its time now for God to put and end to this world? Akauliza Latoya
“ Latoya ni kweli dunia hii imejaa machukizo ya kila aina, makubwa na yasiyovumilika ,lakini pamoja na dhambi hizo za wanadamu Mwenyezi Mungu bado amezidi kutupa nafasi ya kubadilika na kumrudia yeye kutokana na sala na maombi ya wachamungu wachache wasiochoka kuomba.Nadhani Itakuwa Vyema kama Mungu ataendelea kutupa nafasi zaidi ya kujirekebisha.I don’t want to die” akasema Innocent halafu kimya kikatanda
“ Innocent you seem scared when you think of death..why? .Akauliza Latoya
“Latoya kifo kipo na kila mwanadamu atakufa lakini ninaogopa kufikiri kifo changu kwa sababu sipendi kufa.Kama ingetokea nikapewa nafasi ya kuchagua jambo moja tu na mwenyezi Mungu,basi ningeomba aniepushe na kifo..I don’t want to die.Naomba nife wakati nimekwisha zitimiza ndoto zangu kubwa” akasema Innocent
“ Me either.I don’t want to die especially this young. Lakini hata hivyo kama imeandikwa kwamba utakufa katika umri mdogo there is nothng you can do to change that.It hurt so much Innocent,kuiacha hii dunia na watu wake uliowapenda na kuwaozea.” Akasema Latoya
“ Inauma sana na ndiyo maana sitaki kufikiria kuhusu masuala ya kufa” akasema Innocent
‘ Ok Innocent lets not talk about death.Its so scary.Lets talk about something else like love” akasema Latoya na Innocent akatabasamu
“Innocent uliniambia kwamba hauna mpenzi.Je hakunamwanamke yeyote aliyewahi kukuvutia hadileo hii?
Swali lile likaonekana kuwa gumu kwa Innocent
“ Swali lako gumu Latoya lakini ukweli nikwamba wanawake wapo wengi wa kila aina na wenye kila sifa lakini kwa muda mrefu nilikuwa nikimtafuta yule ambaye nitamkabidhi moyo wangu bila mafanikio lakini nashukuru Mungu kwa kuniangazia na kwa sasa nina matumaini kwamba huenda siku za karibuni nikafanikiwa kumpata Yule ambaye anayafanya mapigo ya moyo wangu yaende kwa kasi ” akasema Innocent.Latoya akamuangalia halafu akatabasamu.
“Wow hongera kama tayari umekwisha pata mwangaza kuhusiana na mwnamke wa ndoto zako”akasema Latoya kwa sauti ya upole
“ Vipi kuhusu wewe? Akauliza Innocent
“ Innocent lets not talk about me.Lakini kuna jambo moja ambalo nataka kukushauri”
“ Jambo gani Latoya?
“Love don’t have a time to wait. Kama unafikiri kwamba tayari umekwisha mpata mtu ambaye unaamini ndiye unayempenda kwa moyo wako wote basi usipoteze muda,mueleze ukweli.Hakuna anayejua nini kitatokea katika dakika ijayo.Kwa maana hiyo tusisubiri na kujilaumu baadae kwa nini hatukuwaambia wale tuwapendao kwamba tunawapenda. Mariah carey na Boyz 2 men waliimba wimbo mmoja unaoitwa one sweet day.Do you know that song?
Innocent akaitika kwa kichwa ishara ya kwamba anaufahamu wimbo ule.taratibu Latoya akaanza kuimba
“Sorry, I've never told you, all I wanted to say
And now it's too late to hold you
'Cause you've flown away
So far away
Never had I imagined
Living without your smile
Feelin' and knowing you, hear me
It keeps me alive, alive
And I know you're shining down on me from Heaven
Like so many friends we've lost along the way
And I know eventually we'll be together
One sweet day…………………………………
“ wow sijawahi kukusikia ukiimba.Sauti yako tamu na laini kama ya malaika.Umebarikiwa mno Latoya kwa kila kitu.Laiti ungekuwa mwanamuziki nina hakika ungekuwa mmoja wa wanamuziki wakubwa mno duniani” akasema Innocent na kumfanya Latoya acheke kidogo
“ Innocent you real make me so happy.Sijawahi kuwa na furaha kama hii hapo kabla,ahsante kwa kuja katika maisha yangu” akasema Latoya
“Mimi pia.Ninajisikia furaha sana kuwapo mahala hapa,furaha ambayo siwezi kuielezea and that’s the reason I’ve sacrificed everything ,my job,my dreams,and everything just to be here only because I feel so connected to this place” akasema Innocent
“ Innocent be honnest with me.Are you happy with me as your friend? Akauliza Latoya
“Latoya naomba niwe muwazi kwako kwamba nina furaha tena kubwa sana na ndiyo maana nimeacha kila kitu kwa ajili ya kuwa na mtu kama wewe.You are a wonderfull friend,a friend that is worth to die for” akasema Innocent
Uso wa Latoya ukapambwa na tabasamu zito sana.Akamuangalia Innocent na kuuliza
“ Innocent unamaanisha hicho ulichokisema? Can you die for me?
“Ndiyo Latoya.Kama kuna mtu yeyote yule anayetaka kukudhuru mimi niko tayari kupambana hadi kufa kwa ajili yako”
“ Ouh Innocent you are like an angel to me.How can you die for a woman like me? Akasema Latoya huku machozi yakimlenga
“Latoya wewe ni mtu ambaye dunia inakuhitaji sana.Una moyo wa huruma na upendo usio na mfano.Wewe ni mkombozi na kimbilio la watu masikini kwa hiyo siko tayari kuona jambo lolote baya linakutokea na hii ndiyo sababu niko tayari kwenda hadi mwisho wa dunia kwa ajili ya kutafuta kitu ambacho kitakufanya uwe na furaha.Ninaumia kila niuonapo uso mzuri wa kimalaika kama huu ukiwa na machozi.Ninataka tabasamu hilo lililoko sasa hivi usoni pako liendelee kuwepo katika siku zote za maisha yako” akasema Innocent na uso wa Latoya ukazidi kuchanua kwa tabasamu
“ Ouh gosh ! Why I have to die?.Sitaki kumuacha Innocent. Ananipa furaha ambayo sijawahi kuipata katika maisha yangu.It hurt that I’ve found my happiness at my dying days.It hurt even more that I cant change anything now.It’s too late.Ninachotakiwa kufanya ni kutumia kila dakika iliyobaki vizuri.Nataka nife nikiwa na furaha na zaidi ya yote nikiwa msichana.sitaki kufa nikiwa bikira.Mwanaume pekee atakayenitoa bikira yangu ni Innocent” akawaza Latoya
Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwao wote.Hakuna aliyetamani kwenda kulala.Waliongea mambo mengi sana usiku ule na hadi ilipofika usiku wa saa tisa ndipo walipoagana na kila mmoja akaenda kulala.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………….
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 51
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Ouh Innocent you are like an angel to me.How can you die for a woman like me? Akasema Latoya huku machozi yakimlenga
“Latoya wewe ni mtu ambaye dunia inakuhitaji sana.Una moyo wa huruma na upendo usio na mfano.Wewe ni mkombozi na kimbilio la watu masikini kwa hiyo siko tayari kuona jambo lolote baya linakutokea na hii ndiyo sababu niko tayari kwenda hadi mwisho wa dunia kwa ajili ya kutafuta kitu ambacho kitakufanya uwe na furaha.Ninaumia kila niuonapo uso mzuri wa kimalaika kama huu ukiwa na machozi.Ninataka tabasamu hilo lililoko sasa hivi usoni pako liendelee kuwepo katika siku zote za maisha yako” akasema Innocent na uso wa Latoya ukazidi kuchanua kwa tabasamu
“ Ouh gosh ! Why I have to die?.Sitaki kumuacha Innocent. Ananipa furaha ambayo sijawahi kuipata katika maisha yangu.It hurt that I’ve found my happiness at my dying days.It hurt even more that I cant change anything now.It’s too late.Ninachotakiwa kufanya ni kutumia kila dakika iliyobaki vizuri.Nataka nife nikiwa na furaha na zaidi ya yote nikiwa msichana.sitaki kufa nikiwa bikira.Mwanaume pekee atakayenitoa bikira yangu ni Innocent” akawaza Latoya
Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwao wote.Hakuna aliyetamani kwenda kulala.Waliongea mambo mengi sana usiku ule na hadi ilipofika usiku wa saa tisa ndipo walipoagana na kila mmoja akaenda kulala.
ENDELEA………………………..
Saa mbili za asubuhi Innocent na Latoya walikwisha jiandaa tayari kwa ratiba ya siku hiyo.Latoya alimuomba Innocent aambatane naye katika mizunguko ya siku hiyo.Saa mbili na nusu waliingia garini na na msafara wa magari sita ukaondoka.
“ nataka nizungukie sehemu zote muhimu siku ya leo kabla ya kiza kuingia.This is my last day here.Ni siku yangu ya mwisho kuwepo hapa Tanzania kwa hiyo nataka nionane na wafanyakazi wangu pamoja na kufika sehemu zile zote ambazo nilipenda kuzitembelea .Sintaziona tena” akawaza Latoya ambaye siku hii alikuwa mkimya sana.
Kituo cha kwanza ilikuwa ni katika jengo lenye ofisi zake.Wafanyakazi wake walifurahi sana kumuona mkuu wao amefika kuwatembelea.Kwa siku kadhaa hawakuwa wamemuona kutokana na matatizo yaliyompata.Aliwaita wote katika ukumbi wa mikutano na kuwashukuru kwa namna waliyvomuunga mkono wakati wa matatizo.Aliwashukuru vile vile kwa kuendelea kuchapa kazi na kujituma hata pale ambapo yeye hayupo.Aliwataka waendelee na moyo huo wa kufanya kazi kwa kujituma hata kama hatakuwepo.Latoya aliongea maneno haya kwa uso wenye tabasamu lakini moyoni alikuwa na huzuni kubwa sana kwa kuwa alifahamu wazi hataonana nao tena wafanyakazi hawa wa ofisi yake kuu ya hapa Afrika.Kwa muda mrefu amekuwa akiishi nao kama ndugu.Baada ya kuongea nao alirejea ofisini kwake ,akaingalia ofisi yake kubwa na ya kupendeza machozi yakamtoka.Alizunguka sehemu mbali mbali za jengo lile kubwa la ghorofa nane kisha akaingia garini na msafara ukaelekea sehemu nyingine.Walizunguka sehemu mbali mbali ,na halafu wakafika katika hospitali kubwa ya magonjwa ya moyo ambayo ilikuwa imekamilika kwa asilimia tisini.Hospitali hii ambayo ilijengwa na Latoya mwenyewe ilikuwa ni kwa ajili ya kutoa tiba ya maradhi ya moyo bure kwa wagonjwa wote wenye maradhi ya moyo.Hapa alitoa machozi
“ nasikitika sintaweza kuifungua hospitali hii japokuwa nilitamani sana kushuhudia mgonjwa wa kwanza akipatiwa matibabu.Hii itabaki kumbu kumbu yangu kwa vizazi vingi vijavyo.”akawaza Latoya kisha wakaondoka.
Ratiba ilikuwa ndefu sana .Alitembelea miradi mingi anayoifadhili, mashule, zahanati,vikundi vya maendeleo vya akinamama na vijana, n.k Wengi walishangazwa na ziara ile ya ghafla aliyoifanya kwani siku zote anapotaka kutembelea mahala fulani huwa anatoa taarifa mapema.
“sehemu ya mwisho kutembelea siku hii ilikuwa ni katika kanisa moja kubwa sana alilokuwa analijenga ambalo nalo lilikuwa limekamilika.
“ katika mambo yote niliyowahi kuyafanya katika maisha yangu,hili ndilo kubwa sana.Nimemjengea Mungu wangu nyumba .Kupitia nyumba hii ataabudiwa na kutukuzwa na kupewa sifa kwani ni yeye pekee anayestahili sifa na utukufu.” Akawaza Latoya huku akitabasamu kutokana na uzuri wa kanisa lile
Toka kanisani walielekea nyumbani kwa akina Innocent ambako walipokelewa kwa furaha kubwa.Hawakukaa sana wakaaga kwa dhumuni la kuondoka.Kabla hawajaondoka baba yake Innocent akamuita mwanae pembeni na kumvisha msalaba mdogo.
“ Huu utakulinda na hatari zote.Be safe my son” akasema baba yake Innocent.
Siku ilikwisha namna hii wakarejea nyumbani kwao saa tatu za usiku
“ Innocent jiandae.Saa sita kamili juu ya alama na mwanzo wa siku mpya safari yetu itaanza” akasema Latoya nakuelekea chumbani kwake huku akionekana ni mwenye majonzi mengi.
* * * *
Saa sita kasoro dakika ishirini,mlango wa chumba cha Innocent ukagonjwa akaufungua na kukutana na Latoya
“ Its time Innocent.are you ready? Akauliza Latoya
“I’m ready” akajibu Innocent.Wakaanza kushuka ngazi taratibu halafu wakatembea katika ujia moja mrefu ulioelekea baharini bila kukutana na mtu yeyote Yule.Kitu kilichomshangaza Innocent siku hii hakukuwa na mtu yeyote kulizunguka jumba la Latoya hata walinzi wake ambao huwa wanalizunguka jumba hili kwa saa ishirini na nne hakuwaona.Hakushangaa sana kwani mambo kama haya alikwisha anza kuyazoea.
“ are you nervous? Akauliza Latoya
“ No ! I’m not” Innocent akajibu
“ Good”
Walitembea katika gati kuiendea meli moja ya kifahari iliyokuwa imeegeshwa ukingoni mwa gati lile..Ilikuwa ni meli ya kupendeza na kuvutia mno
‘ welcome aboard madam Latoya” kijana mmoja aliyekuwa amevalia mavazi meupe akamkaribisha Latoya melini.Waliingia na kusalimiana na wafanyakazi kumi na nane wa meli ile na kisha wakaelekea juu kabisa ambako ndiko Latoya hupenda kukaa.
“ Latoya nimeipenda sana hii meli yako.Meli kama hizi nimekuwa nikiziona katika filamu na sikutegemea kama siku moja ningeweza kupanda meli nzuri kama hii”akasema Innocent.Latoya akatabasamu
“wanaiita meli ya maajabu kutokana na uzuri wake”
“ I wish I could live in here for the rest of my life.Hii ni meli inayoongoza kwa uzuri duniani.Sina hakika kama kuna meli ya kifahari ya kulinganisha na hii” akasema Innocent na wote wakacheka kwa nguvu
Saa sita kamili juu ya alama meli iling’oa nanga na safari ikaanza.
“ Bye bye Tanzania.nakupenda nchi yangu na watu wake.I’ll never see u again” akawaza Latoya wakati meli ikiondoka.Kwa kuwa ilikuwa bado usiku Latoya akamuomba Innocent waende kupumzika kwani bado walikuwa na safari ndefu majini.Inno akaonyeshwa chumba chake na kuingia kulala
* * * *
Saa mbili za asubuhi,Innocent aliamshwa na wahudumu.Baada ya kuoga na kujiweka safi akaenda kujumuika na Latoya kwa ajili ya kifungua kinywa.Ilikuwa ni asubuhi nzuri sana.Anga lilikuwa la bluu na kulikuwa na mawingu madogo madogo .Hakuna kilichokuwa kinaonekana mbele yao zaidi ya maji. Bahari ilikuwa kila upande.
“ Umeamkaje Innocent? akauliza Latoya ambaye uso wake ulikuwa umepambwa na tabasamu
“ Nimeamka salama Latoya.Sijui wewe”
“ Hata mimi nimeamka salama kabisa.How was your night?
“My night was so wonderfull.Nimelala usingizi mzito sana ambao sijawahi kuupata.Pengine ni kutokana na uzuri wa meli hii”
Waliendelea kupata kifungua kinywa na walipomaliza wakaenda kukaa sehemu ya kupumzika juu kabisa ya meli.Hali ya hewa ilikuwa nzuri na ya kupendeza.waliongea mambo mengi na ilipofika mchana wakaenda kupata chakula cha mchana halafu kila mmoja akaenda chumbani kwake kupumzika.Latoya alionekana kuwa na mawazo mengi mno
“ Muda unazidi kuyoyoma na muda wangu wa kuishi unakwisha .Usiku wa leo ni usiku wangu wa kipekee kabisa.Nitamwambia Innocent ukweli wa moyo wangu na usiku wa leo nitafanya mapenzi kwa mara ya kwanza.I’m prepared for that.Huu unaweza kuwa ndio usiku wangu wa mwisho kuwa na Innocent kwa hiyo kila kitu lazima kifanyike usiku wa leo.Ile ndoto yangu lazima itimie usiku wa leo.Nimeisubiri kwa muda mrefu sana siku hii ya leo ” Akawaza Latoya na kujilaza kitandani.Picha mbalimbali za maisha yake zikaanza kumjia kichwani .Alikumbuka mambo mengi sana na machozi yakamtiririka
“ Why I have to die? Latoya akasema kwa uchungu
“Sitaki kufa.Nataka niendelee kuishi.Kwa nini nife hasa katika wakati huu ambao tayari nimempata mwanaume wa ndoto zangu ? Sitaki kumuacha Innocent”
kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa Latoya kila alipofikiria kuhusiana na kifo chake.
“Nimekwisha chelewa.Siwezi tena kufanya kitu chochote kubadili ukweli huu kwamba nitakufa muda si mrefu.Ninachotakiwa kufanya ni kuutumia vizuri muda huu mchache niliobaki nao.”
Akafungua kabati lake na kuchagua nguo atakayoivaa usiku atakapokutana na Innocent kwa ajili ya chakula cha usiku
“Gauni hili nililiandaa miaka mingi kwa ajili ya kulivaa siku ya leo,usiku wangu wa kwanza na mwanaume ninayempenda.Nitalivaa kwa usiku wa leo ambao ni muhimu kwa mimi na Innocet.” Akatabasamu halafu akajilaza tena kitandani
Mlio wa saa ukiashiria ni saa kumi na mbili za jioni ulimstua Latoya toka usingizini.Akaelekea bafuni akaoga na kisha akaanza kujiandaa.Alijipaka mafuta mazuri yenye kunukia vizuri halafu akavaa gauni refu lile jekundu lililomkaa vyema.kama ilivyo kawaida yake hakuacha kuvaa koti jeusi
“ Nina hofu kubwa jinsi itakavyokuwa lakini sina namna nyingine .Usiku wa leo lazima nifanye mapenzi na Innocent.Akawaza Latoya akiwa bado amesimama anajiangalia katika kioo.Akavuta pumzi ndefu halafu akafungua mlango akatoka akaelekea katika chumba ambacho aliagiza kiandaliwe chakula maalum kwa ajili yake na Innocent usiku huo.Latoya akatabasamu baada ya kuona namna chumba kilivyokuwa kimeandaliwa na kuwekwa katika mandhari ya kimahaba kama alivyokuwa ameelekeza.Bila kupoteza muda akamtuma mmoja wa wahudumu wake akamchukue Innocent.Dakika tano baadae Innocent akawasili akiongozana na yule muhudumu
“wow ! amazing !
Akasema kwa mshangao Innocent akifurahia uzuri wa chumba kile
“Nimekipenda chumba hiki, kizuri sana” akasema Innocent na kumfanya Latoya atabasamu. Wale Wahudumu wakapewa ishara na Latoya wakaondoka na kuwaacha chumbani yeye na Innocent pekee.
“Umependeza sana usiku wa leo.Latoya you are amazing.Uzuri wako haulinganishwi na yeyote katika dunia hii“ akasema Innocent
“ Thank you Innocent’ Akajibu Latoya
“Latoya naomba niwe wazi kwako kwamba Mungu amekupendelea uzuri.Una uzuri wa kipekee kabisa.Mara ya kwanza nilipokuona nilistuka na kudhani labda wewe si binadamu wa kawaida.” Akasema Inno na kumfanya Latoya acheke kicheko kikubwa
“Thank you Innocent you always make me happy” akasema Latoya na kumkaribisha Innocent mezani
“Innocent chakula hiki cha leo ni maalum kwa ajili yetu.This is special night for me to say thank you for all that you’ve done for me” akasema Latoya
“Ouh Latoya,hakuna chochote ambacho nimekufanyia unachopaswa kushukuru.Wewe ndiye unayepaswa kushukuriwa kwa mambo ambayo umenifanyia.”
“ Innocent niruhusu nikushukuru kwa sababu pengine hufahamu thamani yako kwangu na mambo gani ambayo umenifanyia na ndiyo maana nataka kuutumia usiku huu kusema ahsante sana.Umenifanyia mambo ambayo hakuna binadamu yeyote aliyewahi kunifanyia.Umenitamkia maneno ambayo hakuna mwanadamu yeyote amewahi kunitamkia.Kwa hiyo kwa usiku wa leo nasema ahsante sana na japo kwa masaa haya machache naomba tuufanye usiku huu uwe wa aina yake.Lets forget the world for a while and make our own world” akasema Latoya halafu wakaendelea kula kwa furaha.Baada ya kumaliza kula wakaenda kuketi sofani.Latoya akamimina mvinyo katika glasi.Innocent akashangaa sana kwani toka amefahamiana naye hajawahi hata mara moja kumshuhudia akitumia mvinyo
“Latoya toka nimekufahamu sijawahi hata mara moja kukuona ukitumia mvinyo” akasema Innocent.Latoya akatabasamu halafu akanywa funda moja na kusema
“Kama nilvyokwambia awali kwamba usiku huu ni maalum kabisa kwa ajili yetu na ni usiku ambapo nina furaha ya ajabu sana na ndiyo maana nimeamua ninywe mvinyo kidogo kwa furaha niliyonayo”
“nakubaliana nawe Latoya kwamba usiku wa leo ni wa aina yake kwa sababu toka nimekufahamu sijawahi kukuona ukiwa umevaa nguo za rangi nyekundu.”
Latoya akacheka sana kusikia kauli ile ya Innoent
“Ni kweli Innocent, mimi si mpenzi sana wa rangi nyekundu, lakini leo hii imenilazimu kuvaa rangi hii kutokana na umuhimu wa usiku huu kwangu.Gauni hili nimelinunua miaka saba iliyopita na sijawahi kulivaa hata mara moja.Nilipanga nilivae gauni hili katika usiku kama huu wa leo ambao niliamini nitakutana na mtu muhimu sana katika maisha yangu.Leo ndoto yangu imetimia na ndiyo maana nimelivaa gauni hili” akasema Latoya
“.Innocent naomba ufahamu kwamba nimekwambia haya maneno toka ndani kabisa ya moyo wangu.Kwa usiku huu wa leo napenda niwe muwazi kwako kwa kila kilichopo moyoni mwangu.Vipi kuhusu wewe Innocent unaweza ukanieleza kile kilichopo moyoni mwako ambacho hujawahi kumweleza mtu yeyote? Ninamaanisha pengine kuna kitu ulipenda kunieleza lakini ulishindwa au kuogopa kutokana na mazingira? Kama unalo la kusema uwanja ni wako .Kuwa muwazi kwangu.Usiogope its just the two of us here at the middle of the ocean.” Akasema Latoya
Innocent akamtazama Latoya kwa muda halafu akataka kusema jambo lakini sauti ikakwama.Akakohoa kidogo ili kurekebisha koo lake.Latoya akamsogelea karibu akamtazama usoni na kumshika mikono,mwili wote wa Innocent ukasisimka kwa kushikwa na mikono ile laini sana.
“ Tell me Innocent,anything that you want to tell me” akasema Latoya kwa sauti laini ambayo ikampenya Innocent masikioni na kuyafanya mapigo ya moyo yaanze kwenda haraka
“Tell me Innocent” akasema tena Latoya.Mwili wa Innocent ulikuwa unatetemeka kwa hisia kalializokuwa nazo.Kitu pekee alichotaka kumweleza Latoya kwa wakati ule ni kwamba anampenda kwa moyo wake wote lakini kila alipotaka kusema ulimi ukawa mzito.Ghafla meli ikaanza kutikisika na radi kubwa ikapiga.Mvua kubwa ikaanza kunyesha.Innocent akastuka sana kwa mtikisiko ule wa meli
‘Whats that? Akauliza Innocent
“Relax Innocent.Hii ni hali ya kawaida katika safari za majini.Mara nyingi bahari huwa inachafuka” akasema Latoya
“Lakini mbona imekuwa ghafla sana? Akauliza Innocent
“ Usihofu Innocent.Meli hii ina uwezo mkubwa wa kuhimili dhoruba za baharini kama hizi.Ukiona imeyumba namna hii basi ujue kuna mawimbi makubwa sana jambo ambalo ni la kawaida baharini.Manahodha wanashughulikia suala hili na wako makini sana.” akasema Latoya kisha wakabaki wanaangaliana.Latoya akakohoa kidogo na kusema
“Innocent kama huna la kuniambia au unaogopa,mimi ninalo la kukwambia” akasema Latoya akamsogelea zaidi Innocent .Radi iliendelea kuunguruma huko nje na meli kutikisika.Latoya hakujali hilo akamsogelea zaidi Innocent na sasa nyuso zao zilikaribia kugusana.
“Innocent kuna jambo moja muhimu ambalo nataka kukwambia usiku wa leo” akanong’ona Latoya kwa sauti ndogo
“Innocent you………………” kabla hajamaliza sentensi yake ikapiga radi kubwa na meli ikatikisika kiasi kwamba vyombo vilivyokuwa mezani vikaanguka chini.Latoya akastuka na kusimama
“ Ouh gosh ! Ninafahamu sababu ya tufani hii.No ! I cant let that happen.I must do it tonight.Vyovyote itakavyokuwa usiku wa leo lazima nifanye mapenzi na Innocent.” akawaza Latoya na kisha akaenda katika meza yenye simu akawapigia manahodha wake.Aliongea nao kwa takribani dakika tatu na kisha akarejea kwa Innocent
“Nini kimetokea? Akauliza Innocent kwa wasi wasi
“relax Innocent.bahari imechafuka na sehemu hii kuna mkondo wa bahari .Usihofu tutavuka salama” akasema Latoya na kumkaribia tena Innocent
“ Innocent nataka ufahamu kwamba…….nataka ufahamu kwamba nin………….” Mara ikapiga radi kubwa na meli ikayumba .Innocent na Latoya wakajikuta wamekaribiana na midomo yao kugusana.Wote wawili walikuwa wakihema kwa kasi.
“Innocent……Inn…Innocent whatever happ…en…I..I….l..L..lo…….!!” kabla Latoya hajamaliza alichotaka kukisema ikapiga radi kubwa na kumzuia
“ Ouh gosh ! lazima nimwambie ukweli Innocent usiku huu” akawaza Latoya huku akitetemeka mwili.
“ Latoya hali inazidi kuwa mbaya..tutafanya nini? Akauliza Innocent
“Innocent naomba unisikilize.Please listen to me..” akasema Latoya huku akihema kwa kasi
“Latoya hali ni mbaya sana.Kwa nini tusiongee mambo hayo baadae wakati bahari imetulia? Akasema Innocent kwa woga huku upepo mkali sana ukiendelea kuvuma na mawimbi makubwa kuipiga na kuitikisa meli
“Innocent sikiliza kwanza.Kuna kitu unatakiwa ukifahamu.You have to know that I lo……….!!” Kabla hajamaliza sentensi yake, kishindo kikubwa cha radi kikasikika .Innocent hakuona tena kitu chochote zaidi ya giza nene.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………………
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 52
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Nini kimetokea? Akauliza Innocent kwa wasi wasi
“relax Innocent.bahari imechafuka na sehemu hii kuna mkondo wa bahari .Usihofu tutavuka salama” akasema Latoya na kumkaribia tena Innocent
“ Innocent nataka ufahamu kwamba…….nataka ufahamu kwamba nin………….” Mara ikapiga radi kubwa na meli ikayumba .Innocent na Latoya wakajikuta wamekaribiana na midomo yao kugusana.Wote wawili walikuwa wakihema kwa kasi.
“Innocent……Inn…Innocent whatever happ…en…I..I….l..L..lo…….!!” kabla Latoya hajamaliza alichotaka kukisema ikapiga radi kubwa na kumzuia
“ Ouh gosh ! lazima nimwambie ukweli Innocent usiku huu” akawaza Latoya huku akitetemeka mwili.
“ Latoya hali inazidi kuwa mbaya..tutafanya nini? Akauliza Innocent
“Innocent naomba unisikilize.Please listen to me..” akasema Latoya huku akihema kwa kasi
“Latoya hali ni mbaya sana.Kwa nini tusiongee mambo hayo baadae wakati bahari imetulia? Akasema Innocent kwa woga huku upepo mkali sana ukiendelea kuvuma na mawimbi makubwa kuipiga na kuitikisa meli
“Innocent sikiliza kwanza.Kuna kitu unatakiwa ukifahamu.You have to know that I lo……….!!” Kabla hajamaliza sentensi yake, kishindo kikubwa cha radi kikasikika .Innocent hakuona tena kitu chochote zaidi ya giza nene.
ENDELEA……………………
Moshi mkali uliomuingia puani ulimfanya apige chafya kwa nguvu mara tatu.Sauti za watu zikasikika.Walikuwa wakiongea lugha ambayo hakuifahamu.Macho yalimuuma na hakuweza kuona chochote kutokana na moshi mwingi uliokuwemo katika chumba kile.Alijaribu kufungua mdomo kutaka kuongea jambo lakini moshi mwingi ukamuingia mdomoni na kumfanya akohoe zaidi.Aliendelea kusikia watu wakiongea kwa lugha asiyoifahamu lakini hakuweza kuwaona watu hao kutokana na ,moshi mwingi.
“ Niko wapi? Ninafanya nini humu? Innocent akajiuliza huku akiendelea kukohoa na kupiga chafya mfululizo.Mwili haukuwa na nguvu na kila alipojaribu kuinua mkono alishindwa.
Mara mikono yenye nguvu ikamshika na kumnyanyua toka pale alipokuwa amelala na kumtoa ,kumpeleka sehemu nyingine yenye uwazi na upepo mzuri.Taratibu akafumbua macho na kujikuta amezungukwa na kundi la watu wanaume waliokuwa vifua wazi na viunoni mwao waljifunga ngozi za wanyama.Watu wale walikuwa wafupi wafupi na wenye miili iliyojengeka vyema.Nywele zao zilifanana na zile walizonazo watu wa bara Asia.
“ Hapa niko wapi? Hawa ni akina nani?
Akawaza Innocent akiwa amelazwa juu ya kitanda kilchosukwa kwa ngozi ya mnyama.Watu wale waliendelea kusemezana wao kwa wao huku wakimtazama .Baada ya kama dakika ishirini hivi toka awekwe pale nje, alitokea mzee mmoja mwenye ndevu nyingi nyeupe na shingoni alivaa meno mawili ya simba.Mzee yule ambaye alionekana kama ndiye mkubwa wao alimuinamia Innocent akamtazama machoni halafu akaubonyeza mkono wake.
“sukuchaa…!!!!!Kamulaping tcha..!!” akasema mzee yule na mara kikaletwa chungu ambacho ndani yake kulikuwa na vitu kama dawa.Akachota maji toka katika kile chungu akammwagia Innocent kichwani.Kilaletwa chungu cha pili kilichokuwa na kimimnika mithili ya mafuta.Mzee yule akayachota yale mafuta halafu wanaume wawili wenye nguvu wakamshika Innocent na kumpanua mdomo halafu yule mzee akayamimina mafuta yale yenye harufu mbaya mdomoni mwa Innocent ..mara tu baada ya kunywa mafuta yale Innocent akaanza kutapika huku watu wale wakishangilia.Aliendelea kutapika hatimaye nguvu zikamushia kabisa akaanza tena kuona giza akapoteza fahamu
* * * *
Alifumbua macho na kujikuta akiwa pembeni ya moto mkubwa huku idadi kubwa ya wale watu wakiwa wameuzunguka moto ule.Pembeni ya moto kulikuwa na wanyama wawili waliokuwa wakichomwa.Kiza tayari kilikuwa kimetanda lakini eneo lote lilikuwa na mwanga mkali uliotokana na ule moto mkubwa.Watu wale walikuwa wakipiga ngoma na kucheza kuuzunguka moto ule huku wakila nyama iliyokuwa inachomwa na kunywa kinywaji kilichokuwa ndani ya mitungi mikubwa.Ilikuwa ni kama sherehe kubwa
Mwili wa Innocent ulikuwa dhaifu sana na tumbo lake lilikuwa limeshinyaa kutokana na kutokuwa na kitu chochote ndani yake.Hakuwa amekula chochote.Pembeni ya pale alipokuwa amelazwa kulikuwa na watu wawili waliokuwa wamewekwa maalum kwa ajili ya kumuangalia.Walipomuona Innocent amefumbua macho wakawaita wenzao
“shukk hating ku la paochi…” akasema mzee yule.Akaushika mkono wa Innocent akauinua juu .Vijana wawili wakaleta vyungu viwili .Mzee yule akachota supu toka katika chungu kimojawapo ,Innocent akakalishwa na kunyweshwa supu ile.Baada ya supu ile akapewa uji uliochanganywa na nyama.Jasho jingi likamtiririka ,akajilaza tena kitandani akaendelea kutafakari na wale watu wakaendelea kucheza ngoma kwa furaha
“Hawa ni akina nani? Mbona wanaongea lugha ambayo siifahamu? Mimi si mtu wa maeneo haya.Sifanani kabisa watu hawa.Mimi ni nani? Nimetokea wapi? Jina langu nani? …..” akawaza Innocent
“ Ouh Mungu wangu,sikumbuki kitu chochote.Sikumbuki mimi ni nani,jina langu na nimetokea wapi.” Innocent akaogopa sana baada ya kugundua kwamba hakuwa na kumbu kumbu zozote kumhusu yeye.Alijaribu kuwaza lakini alishindwa kurejesha kumbu kumbu yoyote.
Ngoma ziliendelea kuchezwa huku nyama na vinywaji vikiendelea pia hadi walipochoka.Innocent ambaye nguvu zilianza kumrejea alikuwa amekaa akiwatazama namna walivyokuwa wanacheza .Kuna nyakati alijikuta akitabasamu baada ya kuvutiwa na uchezaji wa watu wale.Hatimaye baada ya kucheza kwa muda mrefu watu wale walipumzika na kuendelea kunywa kinywaji kile kilichokuwa katika mtungi mkubwa.Taratibu wakaanza kusinzia isipokuwa watu wale wawili waliokuwa wakimlinda.Bado aliendelea kuumiza kichwa kuhusiana na watu wale.Taratibu naye akaanza kuhisi usingzi akalala
* * * *
Sauti za watu wakizunguma karibu yake ndizo zilizomstua usingizini.Alifumbua macho na kitu cha kwanza alichokutana nacho ni anga la bluu lisilokuwa na mawingu lililong’arishwa na kijua kitamu cha asubuhi.Milio ya ndege wenye sauti mbali mbali za kuvutia ilisikika.Kwa mbali aliweza kusikia sauti za mawimbi ya bahari.Innocent alizungukwa na kundi kubwa la watu.Nyuso zao zilionyesha kuchoka kutokana na kazi kubwa ya kucheza waliyoifanya usiku uliopita.Taratibu Innocent akainuka na kukaa akaendelea kuwaangalia wale watu waliokuwa wanaongea lugha ambayo hakuifahamu.Yule mzee mkubwa wao akamsogelea na kumtazama machoni halafu akaongea maneno fulani na mara vijana wawili wakaleta chungu kilichokuwa na uji uliochanganywa na nyama Innocent akapewa akaunywa wote.Baada ya kunywa uji ule alitokwa na jasho jingi na kuanza kujisikia kupata nguvu.Watu wale waliendelea bado kumuangalia huku wakiongea kwa lugha yao.
“Nyie ni akina nani? Innocent akawauliza.Badala ya kujiibiwa watu wale wakacheka na kufurahi sana
“Hawa watu mbona wamefurahi baada ya kuisikia sauti yangu? Hawa ni akina nani? Akaendelea kujiuliza maswali ambayo hakuwa na majibu yake
Kitu kingine ambacho kiliendelea kumshangaza Innocent ni kwamba toka amejikuta katika mikono ya watu hawa hajamuona mwanamke yeyote maeneo haya
“Sijamuona mwanamke yeyote hapa.Jamii hii haina wanawake? Akajiuliza .Watu wale wakaanza kumsogelea na kumgusa ngozi yake kana kwamba walikuwa wanamshangaa.Walikuwa wanabonyeza mikono yake huku wakicheka na kufurahi.Mzee kiongozi akatamka maneno fulani halafu vijana wanne wakajitokeza na kukibeba kitanda kile alicholazwa Innocent na kuondoka huku wengine wote wakifuata kwa nyuma wakiimba na kucheza
Walitoka katika eneo lile la ufukweni na kuingia katika msitu mnene wenye kiza.Baada ya mwendo wa kama dakika ishirini hivi wakawasili katika sehemu moja iliyoonekana kama kijiji kilichokuwa na nyumba za miti.Vilikuwa ni vijumba vidogo vidogo.Innocent akawekwa ndani ya kijumba kimoja na kufungwa mikono na miguu ili asiweze kutoroka.Baada ya kama dakika kumi hivi mlango ukafunguliwa na watu wanne wakaingia ndani. Walikuwa na bakuli lililojaa nyama.Mmoja wa wale watu akamsemesha lakini Inno hakuweza kumjibu kutokana na kutoifahamu lugha yao.Watu wale wakamfungua mikono na kumsogezea bakuli la nyama akaanza kula kwa pupa.Alipomaliza kula nyama zile wale watu wakamfunga tena mikono na kuondoka zao.
“ Nimepoteza kumbu kumbu zote.Sikumbuki mimi ni nani ,nimetoka wapi na nimefikaje mikononi mwa watu hawa.Sifahamu lugha yao na siwezi kuwauliza chochote.Kwa sasa nahisi mwili wangu kuanza kupata nguvu natakiwa kufanya kitu.Lazima nifahamu hapa niko wapi na nimefikaje na ikiwezekana niweze kuondoka na kutafuta nilikotoka.” Akawaza Innocent .Watu wale waliendelea kuja mara kwa mara kumtazama na kila mara walikuwa wakimbonyeza mikono yake..Hatimaye kiza kikaingia na Innocent akalala
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………….
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 53
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Walitoka katika eneo lile la ufukweni na kuingia katika msitu mnene wenye kiza.Baada ya mwendo wa kama dakika ishirini hivi wakawasili katika sehemu moja iliyoonekana kama kijiji kilichokuwa na nyumba za miti.Vilikuwa ni vijumba vidogo vidogo.Innocent akawekwa ndani ya kijumba kimoja na kufungwa mikono na miguu ili asiweze kutoroka.Baada ya kama dakika kumi hivi mlango ukafunguliwa na watu wanne wakaingia ndani. Walikuwa na bakuli lililojaa nyama.Mmoja wa wale watu akamsemesha lakini Inno hakuweza kumjibu kutokana na kutoifahamu lugha yao.Watu wale wakamfungua mikono na kumsogezea bakuli la nyama akaanza kula kwa pupa.Alipomaliza kula nyama zile wale watu wakamfunga tena mikono na kuondoka zao.
“ Nimepoteza kumbu kumbu zote.Sikumbuki mimi ni nani ,nimetoka wapi na nimefikaje mikononi mwa watu hawa.Sifahamu lugha yao na siwezi kuwauliza chochote.Kwa sasa nahisi mwili wangu kuanza kupata nguvu natakiwa kufanya kitu.Lazima nifahamu hapa niko wapi na nimefikaje na ikiwezekana niweze kuondoka na kutafuta nilikotoka.” Akawaza Innocent .Watu wale waliendelea kuja mara kwa mara kumtazama na kila mara walikuwa wakimbonyeza mikono yake..Hatimaye kiza kikaingia na Innocent akalala
ENDELEA…………………………
Sauti za watu zikamstua Innocent toka usingizini.Akaamka na kukuta watu sita wakiwa mle kibandani.Miongoni mwao alikuwemo yule mzee kiongozi.Akamsogelea akamshika mkono akaubonyeza halafu akatabasamu na kuwageukia wenzake.Akawasemesha kwa lugha yao halafu wakaweka bakuli la nyama pembeni ya Innocent kisha wakamfungua mikono halafu wakatoka na kumuacha Innocent akiendelea kula nyama zile.Mara tu walipotoka akasikia sauti kama ya tarumbeta likipigwa na vishindo vya watu wakikimbia vikasikika halafu eneo lote likawa kimya kabisa
“Wamekwenda wapi? Tarumbeta hilo ni la nini?.Hawa jamaa wana maisha ya ajabu ajabu sana.Vitendo vyao vinanishangaza.Kila wajapo kuniangalia lazima wanibonyeze mikono yangu.Wanaangalia kitu gani katika mikono? Akawaza Innocent halafu akaanza kuzifungua kamba za miguuni baada ya kuchungulia na kuhakikisha kwamba pale hapakuwa na mtu yeyote.Kabla hajatoka mle kibandani mara mlango ukasukumwa na msichana mmoja mzuri sana mwenye nywele ndefu akaingia.Innocent akastuka asiamini macho yake.Wote wakaangaliana kwa sekunde kadhaa .Inno akataka kusema kitu lakini yule msichana akamzuia
“ shhhhhh…!!!!!!!.dont say anything.Can you speak English? Yule msichana akauliza.Innocent akatabasamu halafu akatikisa kichwa ishara ya kwamba anaweza kuzungumza kiingereza
“ Good..now follow me” akasema yule msichana huku akitoka mle kibandani.
“ where are we going? Akauliza Innocent.Msichana yule akamgeukia na kumuangalia kwa macho makali
“Stop asking question.You want to die here?
“ die here? What do you mean? Akauliza Innocent
“ C’mon guy,stop asking questions.If you want to get out of here this is the only chance you have now follow me” akasema yule msichana mzuri .Huku akiogopa Innocent akaanza kumfuata msichana yule.Walizunguka nyuma ya yale mabanda halafu wakaanza kukimbia kuelekea msitu mnene wakikimbia na kupita chini ya miti mirefu
“ Msichana huyu naye ni nani? Ananipeleka wapi? Mbona hafanani na watu hawa? Anafanya nini mahala hapa? Kwa nini ni yeye pekee anayezungmza kiingereza?
Maswali haya alijiuliza Innocent huku akiendelea kumfuata yule msichana.Mwili wake bado haukuwa na nguvu za kutosha lakini alijitahidi kwa kadiri alivyoweza kutembea kwa kasi katika msitu ule mnene.Baada ya dakika kama ishirini hivi wakajikuta wametokea ufukweni
“ Hurry up ! hurry up ! akasema yule msichana akimuongoza Innocent kuelekea sehemu kulikokuwa na boti ndogo nyeupe.waliifuata boti ile na kando yake kulikuwa na mitumbwi sita mikubwa.Wakaisukuma boti ile na kuiingiza majini
“ Hurry ..!! get in the boat” akasema yule msichana huku akimsaidia Innocent kupanda halafu akaiwasha na kuondoka kwa kasi huku Inno akishangaa.Msichana yule alionekana kuimudu vyema boti ile iliyokuwa ikienda kwa kasi kubwa.Mambo yaliyotokea Innocent aliyaona ni kama ndoto vile.Hakujua walikukokuwa wanaelekea hivyo akalazimika kumuuliza yule msichana
“ wewe ni nani na unanipeleka wapi?
“ naomba usiniulize maswali mengi tafadhali.Bado hatuko salama.Subiri hadi hapo tutakapokuwa salama na nitakujibu maswali yako yote” akasema yule msichana na kuendelea kuendesha ile boti .Bahari ilikuwa tulivu na hakukuwa na mawimbi yoyote.
Walitembea majini mwendo mrefu na hatimaye wakakiona kwa mbali kisiwa kidogo.Yule msichana akatabasamu na kusema
“ Pale ndipo tunakwenda”
“ Pale ndipo unapoishi? Akauliza Innocent lakini yule msichana hakumjibu kitu.Toka kwa mbali uzuri wa kisiwa kile ulionekana.Safari ikaendelea hadi walipofika katika kile kisiwa cha kupendeza mno.Walishuka na kuifunga boti katika kisiki cha mnazi .Kilikuwa ni kisiwa chenye uzuri wa kustaajabisha mno.Innocent akaustaajabia uzuri wa kisiwa kile kilichokuwa na miti ya kuvutia,majani mazuri na maua ya kupendeza sana.Msichana yule akamuomba Innocent amfuate na kuanza kutembea kuelekea ndani kabisa mwa kisiwa kile chenye uzuri wa kipekee.Ndege wa kila aina walikuwa wakiruka ,maua ya kila aina yalikuwa yanapatikana katika kisiwa hiki.Baada ya dakika kama kumi na tano za kutembea kwa miguu wakafika katika bustani yenye matunda mazuri yaliyoiva
“ Sijawahi kuona sehemu nzuri na ya kipekee kama hii” akasema Innocent huku akiendelea kushangaa bustani ile nzuri.
“ Ninahisi kama sipo duniani” akasema tena Innocent.
“Jina lako nani? Unatokea wapi? Yule msichana akamuuliza Innocent swali ambalo lilimbabaisha na kumfanya ashidwe kujibu
“nakuuliza jina lako nani na umetokea wapi? Akauliza tena yule msichana
“sikumbuki chochote,sina kumbukumbu zozote mimi ni nani na ninatokea wapi” akajibu Innocent
“Ulifikaje mikononi mwa wale watu? Akauliza tena yule msichana
“sina kumbu kumbu zozote nilifikaje pale.” Akajibu Innocent na kuinama chini.Yule msichana akamuangalia na kusema
“ pole sana.Usijali kumbu kumbu zitarejea taratibu.Hilo ni tatizo la kawaida katika eneo hili .Naitwa Naya” akasema yule msichana huku akimpa Innocent mkono
Kwa mra ya kanza Innocent akalishuhudia tabasamu pevu la Naya linalomfanya naye atabasamu.Uzuri wa binti huyu ulimsisimua .Akakitazama kifua chake kilichobeba titi ndogo zilizosimama akaitazama midomo laini akashusha macho yake chini na kukutana na kiuno kilichobeba miguu iliyojaa na kuzidi kumfanya binti huyu awe na uzuri wa kipekee kabisa
”nafurahi kukutana nawe Naya.U mkarimu sana” akasema Innocent
“karibu katika kisiwa hiki kijulikanacho kama black queen island.Ni kisiwa cha kipekee kabisa ulimwenguni.Upekee wake unatokana na kwamba hakimo katika ramani ya dunia” akasema Naya na kumshangaza sana Innocent
“Hakimo katika ramani ya dunia? Basi kitakuwa ni kisiwa cha kipekee kabisa.Uzuri uliomo katika kisiwa hiki haupatikani sehemu nyingine yoyote..Ukiwa ndani ya kisiwa hiki unajihis kama hauko katika dunia hii ya kawaida tuliyoizoea.Ni nani wanaishi hapa?
Naya akatabasamu na kusema
“Kisiwa hiki hakikaliwi na mtu yeyote kwa sasa.Hii ni sehemu ambayo malkia mweusi huja mara moja kila mwaka kupumzika.Majira kama haya kila mwaka huja hapa kupumzika yeye peke yake.Kuhusu wale watu kule tulikokua wanaitwa Albaque.Ni kabila dogo na wanaishi katika kisiwa kimoja kidogo mbali na hapa.Watu wale wanasifa moja kubwa tofauti na binadamu wengine. Wao wanakula binadamu wenzao”
Innocent akastuka sana na kutetemeka
“wanakula watu?! Akauliza
“Ndiyo.Wanakula watu.Huwa wanazunguka majini na katika visiwa vidogo vidogo na kuteka watu kisha huwapeleka katika kisiwa kile kuwachinja na kuwala.Ni watu makatili sana” akasema Naya
“ouh Mungu wangu..!! Nakumbuka walikuwa wakija na kunibonyeza mkono wangu lakini sikujua lengo lao lilikuwa nini”
“Hufanya vile ili kuangalia kama unafaa kuliwa.” Akasema Naya na kuzidi kumuogopesha Innocent
“Ilikuaje na wewe ukafika katika kisiwa kile? Akauliza Innocent
“ Ni hadithi ndefu kidogo lakini mimi sikutekwa.Nilifika mwenyewe katika kisiwa kile.Sikufahamu kama pale kuna watu wa aina ile .Wakati nikizunguka zunguka mle kisiwani nilijikuta nimekamatwa na wale jamaa na wakaenda kunifungia katika banda lililokuwa watu wengine wawili.Watu wale waliofungwa pamoja nami mle kibandani walianza kuliwa mmoja baada ya mwingine.Kabla ya zamu yangu kufika walikupata wewe na ukayaokoa maisha yangu.Walianza kukuandaa kwa ajili ya kuliwa .Kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja niliokaa nao nimewasoma vya kutosha.Kila siku asubuhi huwa wanakwenda katika sehemu yao ya kuabudu na baada ya hapo ndipo shughuli nyingine hufuata.Leo hii ndiyo ilikuwa siku yako ya kuliwa. Nilipowaona wameshuka bondeni, nilitoka haraka katika kibanda walichonifungia ambacho hakikuwa mbali na kibanda walichokufungia wewe.Ile boti tuliyoondoka nayo ni boti yangu ambayo nilifika nayo pale kisiwani.Najua hivi sasa watakuwa na hasira sana baada ya kukuta hatupo .” akasema Naya.Innocent alikuwa anaogopa na kutetemeka mwili
“Unahakika hawawezi kutufuata huku tulipo? Akauliza Innocent kwa wasiwasi.Naya akatabasamu na kusema
“Hapana.Hawawezi kufika huku.Kisiwa hiki hakuna mtu wa kawaida ambaye anaruhusiwa kuingia hapa.” Akasema Naya
“ Mbona mimi nimeingia? Akauliza Innocent
“ Unaonekana una muunganiko fulani na sehemu hii kwa sababu usingeweza kuingia katika kisiwa hiki wala hata kukiona.Kisiwa hiki huonekana kwa watu wachache tu ambao wanamuunganiko nacho.”.akasema Naya .Innocent akamtazama kwa mshangao
“ Kwani wewe ni nani Naya? Unaishi wapi? Katika kisiwa hiki kuna nini hadi mtu wa kawaida asiruhusiwe kuingia? Akauliza Innocent ..Naya hakumjibu kitu akachuma maembe mawili na kumpatia Innocent
“Twende upande wa pili wa kisiwa” akasema Naya.Wakaanza kutembea kuelekea upande wa pili wa kisiwa kile.Kila sehemu waliyopita ilikuwa na uzuri wa kipekee.
“Huyu Naya ni nani? Anaishi wapi? Mbona anaonekana kuyafahamu vyema maeneo haya? Kisiwa hiki kina siri gani kiasi kwamba hakuna mtu wa kawaida anayeweza kukiona wala kuruhusiwa kufika hapa? Nadhani kuna haja ya kukifahamu kiundani kisiwa hiki na kwa nini nina muunganiko nacho kama anavyosema Naya.Hisia zinakuja ni kama nimewahi kuwa na urafiki na msichana mmoja mrembo kama huyu Naya.” Akawaza Innocent wakati wakipanda kilima
TUKUTANE SEHEMU ILIYOPITA
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 54
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Mbona mimi nimeingia? Akauliza Innocent
“ Unaonekana una muunganiko fulani na sehemu hii kwa sababu usingeweza kuingia katika kisiwa hiki wala hata kukiona.Kisiwa hiki huonekana kwa watu wachache tu ambao wanamuunganiko nacho.”.akasema Naya .Innocent akamtazama kwa mshangao
“ Kwani wewe ni nani Naya? Unaishi wapi? Katika kisiwa hiki kuna nini hadi mtu wa kawaida asiruhusiwe kuingia? Akauliza Innocent ..Naya hakumjibu kitu akachuma maembe mawili na kumpatia Innocent
“Twende upande wa pili wa kisiwa” akasema Naya.Wakaanza kutembea kuelekea upande wa pili wa kisiwa kile.Kila sehemu waliyopita ilikuwa na uzuri wa kipekee.
“Huyu Naya ni nani? Anaishi wapi? Mbona anaonekana kuyafahamu vyema maeneo haya? Kisiwa hiki kina siri gani kiasi kwamba hakuna mtu wa kawaida anayeweza kukiona wala kuruhusiwa kufika hapa? Nadhani kuna haja ya kukifahamu kiundani kisiwa hiki na kwa nini nina muunganiko nacho kama anavyosema Naya.Hisia zinakuja ni kama nimewahi kuwa na urafiki na msichana mmoja mrembo kama huyu Naya.” Akawaza Innocent wakati wakipanda kilima
ENDELEA……………………….
“Ni kweli kumbu kumbu fulani zinakuja kwamba niliwahi kuwa na urafiki na msichana mmoja lakini simkumbuki ni nani na wapi.Ouh Mungu wangu nisaidie niweze kuzirejesha kumbu kumbu zangu.Nahitaji kukumbuka mimi ni nani,nimetoka wapi, na kwa nini niko hapa.” Akawaza Innocent.Hisia kwamba aliwahi kuwa na urafiki na msichana mrembo zikaendelea kuutesa ubongo wake
Hatimaye wakafika juu ya kilima na ghafla Innocent akapatwa na mshangao mkubwa baada ya kuushuhudia uzuri wa ajabu uliokuwa upande wa pili wa kisiwa kile.
“Haya ni maajabu.Sijawahi kuona sehemu nzuri kama hii” akasema Inno
“Jumba lile unaloliona ni la Malkia mweusi” akasema Naya
“Anatoka wapi huyo malkia mweusi? Akauliza Innocent
“Malkia mweusi hana nchi.Yeye ni malkia wa dunia nzima.Alitakiwa kuwepo hapa katika jumba lake mida hii lakini alifaya makosa makubwa katika utawala wake makosa ambayo adhabu yake ni kifo”
“Alifanya makosa gani? Kwa nini awe ni malkia wa dunia? Mbona mimi sijawahi kumsikia huyo malkia wa dunia?
“Hata kama umewahi kumsikia lakini huwezi kumkumbuka tena.Kuhusu makosa aliyoyafanya hata mimi sifahamu”
“Umewahi kuonana na malkia mweusi? Akauliza Inno
“Ndiyo.Nimewahi kuonana naye.Ni mrembo mno.Ana uzuri wa ajabu sana” akasema Naya halafu akasita kama mtu anayekumbuka kitu .Innocent akamuangalia na kuuliza
“Nani wanaishi pale katika jumba lile malkia mweusi asipokuwepo?
“Jumba lile halikaliwi na mtu yeyote .Ni malkia mweusi pekee ambaye anaruhusiwa kukaa ndani ya lile jumba”
“Kuna nini ndani ya jumba lile kiasi kwamba haruhusiwi kuingia mtu mwingine ?
“Mimi sifahamu chochote kuhusiana na kilichomo mle ndani.Hakuna mtu mwingine zaidi ya malkia mweusi anayeruhusiwa kuingia mle ndani.” akajibu Naya
Innocent akalitazama jumba lile na kusema
“Nataka kuingia ndani ya lile jumba.Nataka kuona kilichomo ndani yake.” Akasema Innocent huku akiinua mguu tayari kwa kuanza kushuka kilima.Naya akamzuia
“Hapana usithubutu kufanya hivyo.Usithubutu kuingia ndani ya jumba lile” akasema Naya
“ kama hutaniambai kuna nini ndani ya ile nyumba ,mimi naenda kuangalia mwenyewe.Nataka nifahamu siri za kisiwa hiki na kwa nini nina muunganiko nacho kama unavyosema” akasema Innocent na kuanza kupiga hatua.Naya akamkimbilia na kumshika mkono.Mara akastuka ghafla kama kwamba ameona kitu ha kutisha sana.Innocent naye akastuka wakabaki wanatazamana.Naya alikuwa anahema haraka haraka
“Naya una tatizo gani? Akauliza Innocent.Midomo ya Naya ilikuwa inatetemeka.Alishindwa kuongea.Innocent akamsogelea karibu na kumuuliza
“ Naya una tatizo gani? Mbona umebadilika ghafla?
Naya akamtazama Innocent usoni halafu akauliza kwa sauti yenye kitetemeshi
“ Hiyo pete kidoleni umeipata wapi?
Innocent akastuka na kuinua kiganja cha mkono wa kushoto .Ni kweli alikuwa na pete ya dhahabu kidoleni.Picha moja ikapita kichwani kwake ghafla lakini akashindwa kutambua picha ile.Kuna kumbu kumbu ilikuwa inakuja na kupotea
“ Sikumbuki pete hii nimeipata wapi.Kwani ina nini? Akauliza Innocent.Naya akamshika mabegani na kusema
“Tafadhali naomba ujitahidi kukumbuka pete hii umeipata wapi? Ni muhumu sana kwangu na kwako pia”
“Sikumbuki kitu chochote Naya.Sikumbuki nimeipata wapi hii pete.” akajibu Innocent halafu akakumbuka kwamba alikuwa na msalaba shingoni.Akaupeleka mkono wake na kuushika na mara kumbu kumbu fulani ikaja na kupotea.Akastuka
“ Umekumbuka kitu chochote ? akauliza Naya
“ Kuna kumbu kumbu inakuja na kupotea” akajibu Inno
“Ouh jamani.Jitahidi ukumbuke.Kumbuka chochote kuhusiana na pete hii.Kuna mtu aliwahi kukupa pete hii? Ni nani ?
“Sikumbuki chochote Naya na wala sikumbuki kama kuna mtu aliwahi kunipa hii pete ingawa kuna kumbu kumbu inanijia na kutoweka..Hii medali nakumbuka kama….kama ..k….ouh sikumbuki tena chochote” akasema Inno na kuinama chini
“ Sikumbuki chochote kuhusu hii pete wala chochote kuhusiana na maisha yangu.Kwa nini Naya amestuka baada ya kuiona pete hii ? Pete hii ina nini? Ina mahusiano yoyote na mahala hapa? Akawaza Innocent halafu akainua kichwa na kumtazama Naya
“Naya naomba uniambie pete hii ina nini?Nahitaji kufahamu tafadhali ili kama ni ya hatari basi niitoe mara moja” akasema Inno.Naya akamshika mkono na kumketisha katika majani na kusema
“Unaiona pete hii katika kidole changu? Akauliza Naya
“Ndiyo.Mbona inafanana na hii ya kwangu?
“Hicho ndicho kitu ambacho nataka kukifahamu.Pete hizi mbili zina utofauti.Hii ya kwangu ina nyota yenye rangi ya bluu na hii ya kwako ina nyota yenye rangi nyekundu.Pete hizi hazivaliwi wala kupatikana kwa mtu ambaye hahusiki.Mtu wa kawaida haruhusiwi kuwa na pete hizi” akasema Naya
“Sijakuelewa Naya.Nini maana ya pete hizi? Zinatoka wapi? Kwa nini huvaliwa na watu maalum tu? Hao watu maalum ni akina nani?Wewe ni nani Naya? Pete hii imefikaje kidoleni kwangu? Innocent akauliza maswali mfufulizo.Naya akavuta pumzi ndefu na kusema
“Mpaka pete hii imefika kidoleni mwako lazima utakuwa unafahamu mambo mengi makubwa” akasema Naya na kuzidi kumchanganya Innocent
“Naya sikumbuki kama ninafahamu chochote kuhusu pete hii” akasema Inno
“Ni kwa sababu umepoteza kumbu kumbu lakini kuna mambo mazito ambayo lazima umeyashuhudia” akasema Naya na kuushika msalaba ule shingoni kwa Inno
“Huu umekusaidia .Umekuokoa” akasema Naya
“Umeniokoaje? Akauliza Inno
“Ulitakiwa ufe lakini msalaba huu umekuokoa” Naya akazidi kumchanganya Innocent
“Nilitakiwa nife? Kwanini nife? Nani alitaka kuniua? Umefahamu vipi kama nilitakiwa kufa? Akauliza Inno kwa wasi wasi.Naya akamshika mkono na kusema
“Pete hii ulipewa na malkia mweusi.”
‘Mimi ?!! Innocent akashangaa
“Sifahamiani na huyo malkia mweusi na wala sijawahi kumuona na hajawahi kunivisha pete hii”akasema Inno.Naya akamuangalia halafu akatabasamu
“Hatimaye nimefanikiwa kukuona.Ni wewe !! “ akasema Naya huku akitabasamu halafu akamkumbatia Inno kwa nguvu
“Ouh ahsante Mungu.Nimefanikiwa kuonana na mkombozi wetu” akasema Naya huku machozi yakimtoka .Inno akashangaa
“Naya sikuelewi kwa haya maneno unayoyasema.Mimi nitakuwaje mkombozi wenu? Wewe na nani?
Naya hakujibu kitu akaendelea kufuta machozi
“Naya tafadhali naomba unieleze ukweli kuhusu maneno hayo unayoyasema.” Innocent akasisitiza.Naya akainama kwa sekunde kadhaa na kusema
“Nilikuwa na umri wa miaka kumi na miwili baba yangu aliponichukua na kunipeleka katika hekalu fulani ambako alinitoa sadaka.Nakumbuka tulikuwa watu wawili siku hiyo .Mimi na malkia mweusi.Baada ya ibada ile ya kutolewa sadaka nilichukuliwa na wazazi wangu na sikuelewa maana ya kutolewa sadaka.Nilipofikisha miaka kumi na minne,nililetwa katika kisiwa kitukufu kwa ajili ya kujifunza kuhusu maisha yetu na kujiandaa kwa ajili ya kuwa mrithi wa malkia mweusi.Nimeishi kisiwani kwa miaka kumi sasa.Nimejifunza mambo mengi .Nimeiva katika imani yetu na tayari nilitegemewa kumrithi malkia mweusi lakini sikuwa tayari kwa hilo.Niliamua kutoroka na badala yake nikaishia mikononi mwa wale wala watu.Safari yangu haikuwa ya bure kwani nimefanikiwa kukutana nawe mtu muhimu sana ambaye umekuwa ukisubiriwa na watu wengi kwa muda mrefu” akasema Naya
“Naya unazidi kunichanganya.Mimi nina umuhimu gani kwenu? Sielewi chochote Naya” akasema Inno
“Huwezi kuelewa Innocent kwa sababu kumbu kumbu zako hazitarudi kamwe hadi hapo utakapokuwa umekamilisha kazi unayotakiwa kuifanya”
“Kazi ninayotakiwa kuifanya? Ni kazi gani hiyo? Akashangaa Inno
“Unatakiwa ukamuokoe malkia mweusi ambaye muda wowote atauawa.Adhabu yake imeshatolewa lakini haiwezi kutekelezwa pasipokuwapo pete hii”
“ Yuko wapi malkia mweusi? Nitamuokoa vipi ? akauliza Inno
“Iko hivi” .akasema Naya halafu akamuangalia Inno aliyekuwa kimya akisikiliza kwa makini
“Kuna kitabu ambacho unatakiwa ukipate na uichane sura ya sita kati kati.Kitabu hicho kitukufu kimehifadhiwa katika pango lenye nyoka mkubwa na katika chumba kilimo kitabu hicho kuna moto mkali sana na kati kati ya huo moto kuna jiwe kubwa ambalo juu yake ndipo kipo kitabu hicho” akasema Naya na kumuogopesha Inno
“Hilo haliwezekani Naya.Siwezi kufanya kitu kama hicho.Sehemu hiyo haiingiliki hata kidogo na hakuna uwezekano wowote wa kukichukua kitabu hicho kitukufu.Nitawezaje kupambana na huyo nyoka mkubwa? Nitawezaje kuingia katika chumba chenye moto mkali? akasema Inno
“Lazima uende.Lazima umuokoe malkia mweusi na sisi sote na huo ndio utakuwa mwisho wao.” Akasema Naya huku ameukunja uso wake.Innocent akauliza
“ Naya kwa nini mimi nikaifanye kazi hiyo ya hatari na si mtu mwingine? “
“Kwa sababu wewe ndiye uliyechaguliwa.Wewe ndiye uliyepewa nguvu za kuwamaliza hawa watu”
“Nimechaguliwa na nani? Nguvu gani nilizonazo? Ni watu gani ambao natakiwa kuwamaliza? Akauliza Inno
“Ni hadithi ndefu sana lakini nina imani haya yote yalikwisha fanyika lakini hukumbuki chochote”
“Naya bado sijakuelewa vizuri.Nani huyo aliyenichagua? Amenifahamu vipi mimi? Akauliza Inno.Naya akamtazama na kusema
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………….
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 55
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Kuna kitabu ambacho unatakiwa ukipate na uichane sura ya sita kati kati.Kitabu hicho kitukufu kimehifadhiwa katika pango lenye nyoka mkubwa na katika chumba kilimo kitabu hicho kuna moto mkali sana na kati kati ya huo moto kuna jiwe kubwa ambalo juu yake ndipo kipo kitabu hicho” akasema Naya na kumuogopesha Inno
“Hilo haliwezekani Naya.Siwezi kufanya kitu kama hicho.Sehemu hiyo haiingiliki hata kidogo na hakuna uwezekano wowote wa kukichukua kitabu hicho kitukufu.Nitawezaje kupambana na huyo nyoka mkubwa? Nitawezaje kuingia katika chumba chenye moto mkali? akasema Inno
“Lazima uende.Lazima umuokoe malkia mweusi na sisi sote na huo ndio utakuwa mwisho wao.” Akasema Naya huku ameukunja uso wake.Innocent akauliza
“ Naya kwa nini mimi nikaifanye kazi hiyo ya hatari na si mtu mwingine? “
“Kwa sababu wewe ndiye uliyechaguliwa.Wewe ndiye uliyepewa nguvu za kuwamaliza hawa watu”
“Nimechaguliwa na nani? Nguvu gani nilizonazo? Ni watu gani ambao natakiwa kuwamaliza? Akauliza Inno
“Ni hadithi ndefu sana lakini nina imani haya yote yalikwisha fanyika lakini hukumbuki chochote”
“Naya bado sijakuelewa vizuri.Nani huyo aliyenichagua? Amenifahamu vipi mimi? Akauliza Inno.Naya akamtazama na kusema
ENDELEA…………………..
“Sophie alikuwa bibi mzee ambaye naye alishi maisha yake yote katika imani hii.Hakuwahi kuufurahia usichana wake hata kidogo.Nilipoletwa huku kisiwani,kwa mafunzo Sophie alinipokea na akatokea kunipenda sana .,Alinionea huruma na hakutaka niishi maisha kama aliyoishi yeye.Siku zote alinisihi kwamba nisikubaliane na chochote kile watakachoniamuru nifanye.Alikuwa ndiye mtetezi wangu.Alinikingia kifua katika kila jambo.Kwa bahati mbaya Sophie alifariki.Alifia mikononi mwangu.Kabla hajafariki aliniita chumbani kwake na kunipa siri kubwa.Aliniambia kwamba siku moja nitakutana na mtu ambaye atatukomboa.Hakuniambia kwamba mtu huyo nitakunata naye wapi lakini aliniambia kwamba mtu huyo nitakayekutana naye tayari atakuwa amejazwa nguvu za kuweza kupambana na kutukomboa.Alinipa ishara tatu ambazo zingeniwezesha kumtambua mtu huyo na ishara mojawapo ni pete hii uliyoivaa.Hii ni pete yenye nguvu sana na nina hakika lazima kuna sababu nzito sana iliyomfanya malkia mweusi akaitoa kidoleni mwake na kukupa.Inawezekana mlikuwa katika mapenzi mazito na hivyo akaona ni vyema kama atakulinda “
“mapenzi ?!! Innocent akashanga
“Sijawahi kuwa katika mapenzi na mwanamke yeyote achilia mbali huyo malkia mweusi.” Akasema Innocent ghafla kumbukumbu fulani ikamjia na kupotea
“Kuna kitu umekumbuka? Akauliza Naya
“Kuna kumbukumbu inakuja na kutoweka.Sikumbuki chochote tena lakini kuna hisia ninaanza kuzipata ni kama niliwahi kuwa mapenzini na mtu fulani” akasema Inno
“Usijali.Kumbu kumbu zote zitarejea.Kitu kikubwa ambacho tunatakiwa kukifanya sasa ni kwenda katika kituo cha kwanza alichonielekeza Sophie.Sehemu hii na zote tutakazozipitia ni za hatari lakini hatuna budi kwenda” akasema Naya.Innocent hakujibu kitu akabaki amesimama akitafakari
“Uko tayari kwenda? Unahitaji kuzirejesha kumbu kumbu zako? Akauliza Naya
“Niko tayari Naya japokuwa sielewi nitaiwezaje kazi hii ngumu “
“ahsante .Umefanya maamuzi ya busara na kwa maamuzi hayo utatukomboa sisi sote.Twende tuondoke” akasema Naya na kumshika mkono Innocent wakaanza kushuka kilima kuelekea ufukweni hadi mahala walikoiacha boti waliyokuja nayo.
“Tunaeleka wapi? Akauliza Innocent
“katika kituo cha kwanza kama alivyonielekeza Sophie”
Safari ikaanza na Naya alionekana kuyafahamu vyema mazingira yale ya bahari.Kadiri walvyozidi kusonga mbele ndivyo hali ya bahari ilivyozidi kuchafuka.Innocent akaogopa
“Naya hatuwezi kwenda zaidi ya hapa.Geuza boti turudi.bahari imechafuka na tunaweza kupoteza maisha.Twende turudi tulikotoka” akasema Inno
“Hatuwezi kurudi.Vyovyote itakavyokuwa lazima tusonge mbele.Hatuwezi kurudi nyuma.” Akasema Naya kwa ukali.Boti ile iliendelea kuchana mawimbi makubwa .Upepo mkali na ngurumo vikatawala bahari.Hali ya bahari ilikuwa mbaya sana.
“Karibu tutafika.” Akasema Naya na kumpa moyo Inno ambaye alikuwa akiogopa
Dakika kumi baadae wakasili katika kisiwa kidogo.Mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali na radi ilikuwa inanyesha.Innocent alikuwa anatetemeka mwili mzima kwa baridi kali aliyoisikia.Taratibu akaanza kukata tamaa ya kuendelea mbele
“Naya siwezi kuendelea tena zaidi ya hapa.Mwili wangu hauna nguvu hata kidogo” akasema Innocent na kuanguka chini
“Jitahidi .Tumeshafika ! Tafadhali usikate tamaa” akasema Naya.Mvua kubwa ikaendelea kunyesha.Alimshika mkono Innocent aliyekuwa ameanguka pake chini kwa lengo la kumnyanyua lakini ghafla akasukumwa na kitu kama upepo mkali na kuanguka katika jiwe.Alijilaza pale juu ya jiwe huku akisikia maumivu makali .Mvua kubwa iliendea kunyesha pamoja ngurumo za kutisha za radi
“lazima nimfikishe ndani.Lazima atukomboe” akawaza Naya halafu akainuka huku akipepesuka kutoka na upepo mkali na kumfuata Innocent. Akajaribu kunyanyua lakini akashindwa.Hakukata tamaa akaanza kumvuta huku akisukumwa na upepo mkali
Hatimaye Naya akafanikiwa kumfikisha Innocent katika pango.Ndani ya pango lile kulikuwa na mwanga na joto kali tofauti na nje kulikokuwa na baridi kali mno.Mbele kabisa ya pango lile kulikuwa na jiwe mfano wa meza ndogo ambalo juu yake kulikuwa na kitu fulani chenye umbo la duara mfano wa tufe ambalo lilikuwa linatoa mwanga ule mkali.Naya akazidi kupata nguvu na kumvuta Innocent hadi katika lile jiwe mfano wa meza.Akauinua mkono wa Innocent uliokuwa na ile pete halafu akauweka katika lile tufe lenye kutoa mwanga mkali
Mara tu mkono wa Innocent ulipowekwa juu ya lile tufe,radi kubwa ikapiga na kisiwa chote kikatikisika.Pete ile ya Innocent ikaanza kutoa mwanga mwekundu na mara mwili wa Innocent ambao ulikuwa dhaifu sana ukapatwa na nguvu za ghafla.Ngurumo za radi zikaendelea kusikika na ghafla kitu cha ajabu kikamtokea.Mbele yake alisimama mzee mmoja mwenye ndevu nyingi na aliyevaa nguo ndefu nyeupe na kujifunga mshipi mwekundu kiuononi.Mkononi mwake alikuwa ameshika ubao wenye maandishi.Akamtaka Innocent ayasome maandishi yale.Mara tu alipomaliza kuyasoma maandishi yale kumbukumbu fulani ikamjia.Alikumbuka aliwahi kumuona mahala mzee yule.Wakati akijaribu kutaka kukumbuka mahala alikomuona yule mzee,lile jiwe ambalo juu yake kulikiwa na tufe alilokuwa ameliwekea mkono likaanza kutikisika halafu ,likafunguka.Naya aliogopa sana kwa mambo aliyoyaona mle pangoni
Mara mtetemeko ule ukakoma Innocent ambaye tayari alikwisha rejewa na nguvu akalitazama jiwe lile lililofunguka.Ndani yake kulikuwa na upanga wenye kumeremeta.Wakati anaendelea kuushangaa upanga ule ,mara mbele yake akasimama tena yule mzee mwenye ndevu nyingi
“Chukua huo upanga.Nenda sasa kamuokoe Latoya” akasema yule mzee na kutoweka.
“Latoya!!....? Latoya ..?!! Jina hili si geni kwangu.Nakumbuka ni jina ambalo nimezoea kulitamka.Latoya ni nani ambaye natakiwa kumuokoa? Innocent akajiuliza na kukosa majibu.Taratibu akainama na kuushika upanga ule kwa mikono yake.Mara tu alipousika ule upanga vitu kama chaji za umeme vikamuingia mwilini na kupiga ukekele mkubwa.Baada ya dakika tano akajisikia mzima .Huku akiwa na upanga wake mkononi Innocent akageuka na kumtazama Naya aliyekuwa amejikunyata kwa uoga katika pembe moja ya pango
“twende tuondoke” akasema Inocent
“Nipeleke sehemu ya pili”
Naya akamtazama Innocent akataka usema kitu lakini kabla hajatamka chochote kukatokea tetemeko kubwa.Mawe yakaanza kuporomoka
“Twende tuondoke humu haraka” akasema Innocent na kwa kasi akamshika Naya mkono wakaanza kukimbia kutoka ndani ya lile pango huku mawe yakiendelea kuporomoka nyuma yao.Walifanikiwa kutoka salama ndani ya pango lile na.Bado mvua iliendea kunyesha ikiambata na upepo mkali ngurumo na tetemeko.Miti na mawe vikaendelea kuanguka kutokana na mtikisiko ule mkubwa. Wakaingia katika boti yao na kuanza kuondoka kwa kasi
“Tazama nyuma” akasema Naya wakati wakiendelea na safari .Inno akageuza kichwa na kutazama nyuma.Kisiwa kilikuwa kinazama.
“Ouh Mungu wangu .Haya ni maajabu.Sijawahi kuona mambo ya ajabu kama haya” akasema Inno.Hakuwahi kushuhudia kitu cha namna ile katika maisha yake.Aliogopa sana
Naya aliendelea kuendesha boti ile kwa kasi kubwa.Kwa sasa hali ya bahari ilizidi kuwa mbaya na wingu zito jeusi lilitanda na kupafanya baharini kuwe na kiza.Mawimbi makubwa yalitokea na upepo mkali ukaendelea kuvuma.Ilikuwa ni hali ya kutisha sana .
“ Nashindwa kuona tunakoelekea.Hali imekuwa mbaya sana” akasema Naya.Innocent akamkumbuka yule mzee mwenye ndevu nyingi halafu kumbukumbu fulani ikamjia ghafla.Alimuona mzee yule akimuelekeza maneno fulani na kumwambia ayatamke pale anapokuwa katika matatizo.Inno akayakumbuka maneno yale na kuyatamka na mara tu alipomaliza kuyatamka pete aliyovaa ikaanza kutoa mwangaza mkubwa.Naya akatabasamu na safari ikaendelea kwani aliweza kuona walikokuwa wakielekea.
Kwa mbali waliona kitu mithili ya moto
“Pale ndipo tunalekea” akasema Naya kwa uoga
“Mbona kama kunawaka moto ? akauliza Inno
“Kisiwa kile huwa kimezungukwa na moto unaowaka masaa yote.Ni sehemu ambayo hakuna mtu wa kawaida anaweza kufika wala kupaona.Pale ndipo kinahifahiwa kitabu kitukufu” akasema Naya.Innocent akastuka sana
Kadiri walivyozidi kukikaribia kisiwa ndivyo joto lilivyozidi kuongezeka.hata maji nayo yalianza kuwa ya moto.
“ Hapa lazima tufanye kitu.Hatuwezi kuingia salama pale kisiwani” akasema Innocent.Naya hakujibu kitu akabaki anamtazama Inno.Innocent akayatamka kimya kimya maneno yale ambayo aliambiwa ayatamke mara apatapo shida na mara tu alipomaliza kuyatamka ,upepo mkali ukavuma na kusababisha mawimbi makubwa kutokea
“Ee Mungu wangu naomba utulinde na hali hii ya kutisha.Sijawahi katika maisha yangu kushuhudia mambo ya kutisha kama haya” Innocent akaomba kimya kimya akiwa ameushikilia msalaba aliouvaa shingoni.Ghafla likatokea wimbi kubwa mfano wa mlima na kuwafunika kukawa na kiza kinene .
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………………….