Toka kuchaguliwa kwao uongozi wa BAVICHA na BAWACHA wamekuwa kimya sana kiasi cha kutukatisha tamaa sisi wasahabiki wa CDM. Inashangaza sana kuona kila jambo hata la kuhakikisha CDM inajijenga wameachiwa viongozi wa kitaifa.
Ni kutokana na BAVICHA na BAWACHA kutokuwa active CDM imeshindwa kutayarisha wagombea wazuri kugombea ubunge wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EALA), kama wenzetu NCCR walivyoweza kufanya.
Hivi sasa nilitarajia BAVICHA na BAWACHA wangekuwa active sana nchi nzima kuwahamasisha wananchi waliowachagua wabunge katika majimbo mbali mbali kuwatumia salamu wabunge wao wakiwataka wabunge wao hususan kutoka CCM waafiki na kuweka sahihi zao katika hoja iliyotolewa na wabunge wa upinzani bungeni ya kutaka wabunge 70 kuweka sahihi kuunga mkono kuwasilishwa kwa hoja ya kutaka Waziri Mkuu ajiuzuru kutokana na wizi mkubwa unaoendelea Serikalini.
Endapo hamasa ya iana hii inefanikiwa kujengwa nchi nzima ingewapatia fursa wabunge wa CCM kupata sababu ya kuweka sahihi katika hoja hiyo ikiwa kama shinikizo toka majimboni mwao.
Cha kusikitisha BAVICHA na BAWACHA viko kimya kabisa kana kwamba havipo kabisa. Je huku ndio asasi hizi kusaidia kukijenga chama?
Naomba kuwasilisha
Ni kutokana na BAVICHA na BAWACHA kutokuwa active CDM imeshindwa kutayarisha wagombea wazuri kugombea ubunge wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EALA), kama wenzetu NCCR walivyoweza kufanya.
Hivi sasa nilitarajia BAVICHA na BAWACHA wangekuwa active sana nchi nzima kuwahamasisha wananchi waliowachagua wabunge katika majimbo mbali mbali kuwatumia salamu wabunge wao wakiwataka wabunge wao hususan kutoka CCM waafiki na kuweka sahihi zao katika hoja iliyotolewa na wabunge wa upinzani bungeni ya kutaka wabunge 70 kuweka sahihi kuunga mkono kuwasilishwa kwa hoja ya kutaka Waziri Mkuu ajiuzuru kutokana na wizi mkubwa unaoendelea Serikalini.
Endapo hamasa ya iana hii inefanikiwa kujengwa nchi nzima ingewapatia fursa wabunge wa CCM kupata sababu ya kuweka sahihi katika hoja hiyo ikiwa kama shinikizo toka majimboni mwao.
Cha kusikitisha BAVICHA na BAWACHA viko kimya kabisa kana kwamba havipo kabisa. Je huku ndio asasi hizi kusaidia kukijenga chama?
Naomba kuwasilisha