CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO. wajinga wameshaliwa. watu wanajifanya mabalozi wa kukijibia Chama humu, kumbe hawakijui chama wala hakiwajui wao. Unacheza wewe! Mtu ameshindwa kwenye dini ndo aje aweze kwenye siasa?
Watanzania wenye uchungu na nchi yetu, pesa yetu walipa kodi (Ruzuku) inakwenda tena kwenye maandamano wanakwenda kugawana posho za maandamano. Chadema wamefanya maandamano kama Sekta yao ya kugawania pesa zetu Watanzania.
Takwimu zinaonyesha kila maandamano yanatumia zaidi ya milioni 40, na nchi hii ilivyokua kubwa mpaka waimalize kwa maandamano sijui watatumia kiasi gani cha pesa zetu Watanzania.
Si bora hizo pesa wangechimba visima kila jimbo walioshinda uchaguzi au wangenunua madawati watoto wetu wapate pakusomea wananchi wangewapongeza.
ndugu tumia ubongo vizuri. Kama maandamano yanatumia mil40 kwa siku kadhaa alaf serikali ya ccm inatumia mil.50 ndani ya masaa36 kumsafirisha Aikaeli Mbowe kwenda Arusha kwa ulinzi mkali zaidi ya rais mtawala. Serikali yetu ni kama haina cost analysers. Acha kuhurumia ela inayojenga elimu ya uraia na ustawi wa jamii wakati tuliyopewa tuitumie tunaichezea.
Kweli mkuu, mambo ya ajabu kabisa kila kukicha wabunge wa Chadema wao na maandamano nchi aijengwe na maandamano
nape kawatuma eti, atachemka tu! Kama mvua ya masika imeshindwa umande utaweza? Dr. Slaa ni mtu makini ya mungu anayajua na hata ya dunia sasa ndie kiongozi bora na kiongoz bora ni yule anaechukia maovu na ufisadi wa viongoz wa ccm wasiomuogopa mungu.
Kaoge weweHalafu rushwa zenyewe walizianika humu JF mpaka za shillingi 1,500/= Wananchekeshaa!
Niliwaambia kwenye nyuzi nyingine kule watumie "scientific approach" kwenye siasa. Hawajui kuwa ngoma ikivuma sana hupasuka. Hawana jipya na hao wanaoandaa maamndamo wamejipatia njia moja ya kujipatia posho kiulaini.
Kweli mkuu, mambo ya ajabu kabisa kila kukicha wabunge wa Chadema wao na maandamano nchi aijengwe na maandamano
Mkuu Tukutuku, hoja kweli ni maandamano ya Bavicha, lakini hatuwezi kuganda hapo hapo kwenye maandamano tunaenda mbali zaidi mpaka tunagusa ahadi za wabunge, sababu kubwa ni malalamiko kutoka kwa wananchi. Kuwa wamewachagua wabunge wa Chadema ili wawafanyie yale ambayo CCM wameshindwa kuwafanyia kinyume chake wabunge wa Chadema kila siku wapo kwenye maandamano yasiokuwa na tija kwa waliowapigia kura, Lema alisema wakati kampeni atajenga Machinga Complex mbili Arusha.
Wenje nae aliwambia wakazi wa Mwanza wakimchagua Machinga wote wa Mwanza wafanya kazi zao maeneo ya Mjini, tunavyoengea hapa madiwani wengi wa Chadema wamepitisha sheria machinga wote wamefukuzwa maeneo
ya mjini