Kilembwe
JF-Expert Member
- Aug 19, 2009
- 2,056
- 1,598
Jana nilikuwa naangalia kipindi kimoja katika kituo cha Televisheni cha TBC1 kiitwacho MCHAKATO MAJIMBONI, na jana walikuwa jimbo la Arusha mjini, niliwaona wagombea wote wa ubunge jimbo lile, alikuwepo Lema ( Chadema) Lyimo (TLP) , Salim (CUF) na yule bwana mdogo wa Chama cha Demokrasia Makini (CDM?), lakini ajabu sikumuona Mh Batilda Buriani Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM. Nilijiuliza na napenda pia wana JF mnisaidie hili, je Buriani kutotokea pale hakuwa na taarifa, aliogopa kuulizwa maswali, alidharau au hakuwa na jipya la kuwaambia wana Arusha?