mara huyu anamwagiwa tindikali, yule nyumba yaungua karatasi inapona, huku katibu anasema kuna magaidi anawajua lakini polisi haiwajui, na huyu naye anapanda na siraha jukwaa la siasa kana kwamba ni vitan, mpaka kuisha kampen hizi tutasikia na kuona mengi pengine kuliko kampen zozote zile.
Halafu bado tunaendelea kubisha kati ya Magamba na Magwanda ni nani wanaofanya Siasa za Vitisho!!!
Angekua ni Mh. Kamanda Mbowe kafanya hivyo leo angekua ndani,
Polisi wetu wa ajabu sana, Wanaacha ku-deal na watu wa aina hii, wanabaki kuwashikilia watu waliofunua maovu ya yule Bibi, Muislamu uchwara DC
Naamini tulio wengi tumeona picha kubwa katika gazeti la mwananchi leo 23/9/2011 ikimuonesha mbunge wa Tabora mjini (ccm) Ismail Aden Rage akipanda jukwaani na bastola kiunoni. Ni ishara ya shari.
Lakini kwa upande mwingine katibu mkuu wa ccm, Mkama kaja na suala la ugaidi. Anadai CDM wamepeleka makomandoo waliopata mafunzo Libya na Afghanstan kwa ajili ya kufanya fujo igunga. Hii ni kauli nzito, si ya kuipuuza kwani imebeba dhamira hatari kwa usalama wa taifa letu. Japo Polisi wamekana kupewa vielelezo, nadhani iko haja ya vyombo vya usalama kuchukua hatua zaidi.
Binafsi napata hisia, zinazochochewa na vitendo vya ccm, kuwa chama chao kiko tayari kuivuruga amani ya nchi ili kulinda utawala wake. Sitashangaa wakileta makombora na mizinga siku chache kabla ya uchaguzi wa igunga tayari kuanzisha vita na watu wa igunga.
Watu wa Zambia wameonesha mfano, watanzania tusitishwe na propaganda za ccm wala tusikubali kugawanywa kwa misingi ya dini.
"Tukiamua kumuua panya kwa sumu, lazima tuwe tayari kunusa harufu ya mzoga wake kwani ni ya kitambo kidogo tu".
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.