Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,797
- 12,239
Harakati za Bashe kisiasa ndani ya CCM zinakabiliana na vikwazo vingi.
Baadhi ya vichache na vilivyoathiri maisha yake kisiasa ni kama vifuatavyo:
Maswali ya kujiuliza hapa ni:
Baadhi ya vichache na vilivyoathiri maisha yake kisiasa ni kama vifuatavyo:
- Ndani ya UVCCM anakabiliwa na upinzani kila kona na hivyo kuhatarisha nafasi yake kiuongozi!
- Madai ya kutokuwa raia wa Tanzania ambayo hadi sasa ufumbuzi wake unatia shaka. Hii ilipelekea kuenguliwa katika kugombea ubunge kupitia CCM pamoja na kushika nafasi ya kwanza katika kura za maoni na badala yake akateuliwa hasimu wake mkubwa kisiasa Bw. Kingwangwalla ambaye alishika nafasi ya tatu katika kura za maoni!
- Kuzuiliwa na hasimu wake mkubwa Bw. Kingwangwalla kurudisha fomu ya kugombea ujumbe wa NEC (CCM) kwa madai kuwa muda wa kurudisha fomu ulikwisha!
- Kutishiwa bastola na hasimu wake mkubwa Bw. Kingwangwalla, kitu ambacho si cha kawaida kwa watu walio chama kimoja!
Maswali ya kujiuliza hapa ni:
- Je Kingwangwalla anatumwa kumhujumu Bashe na wakubwa wake kichama?
- Je Kingwangwalla anatumiwa na vigogo na kwa lengo na manufaa gani ?
- Je Kingwangwalla alikuwa time keeper wakati wa kurudisha fomu?
- Je Kingwangwalla hastahili kuchukuliwa hatua kichama kwa kumtishia Bashe kwa bastola?