Barua ya wazi kwa zitto kabwe

barua hii ataiweka kapuni... his head has grow too big for that mkuu

sorry if i disappoint you on this
 
Tatizo kijana anamaslahi na hiyo serikali kwa hiyo ni kazi kukubali kuwa na msimamo mmoja na chadema, kale kamtambo kake ka kusaga kokoto katakosa tender .
 
Asiyekwenda pamoja nasi, yu kinyume nasi, asiyekusanya pamoja nasi hutawanya...huyu hatufai kabisa wanachadema. tutaishi naye kwa machale tu na hataaminika kamwe.
 
nami ningependa kuongezea haya;
  • mhe mkuu zitto asipende sana kujibia masuala ya ndani ya chama chake kwenye press conference
  • mhe mkuu zitto, (endapo hakubaliani na maamuzi ya ndani ya chama chake), afuate hatua zinazofaa kuliko kufanya upinzani wa wazi.
 
huyu bwana mdogo asipokuwa makini atakwisha kisiasa mapema sana bora mrema alidumu kwa muda mrefu then akafulia!
 
Napata auheni nkisikia ushauri wa thread hii. Uyu Zitto binafsi namheshimu na ngependa aendeleze kujenga chadema. Cdm sio zitto,ila zitto yupo chadema. Zingatia maneno yangu. Zitto ni silaa muhimu kwa cdm kuimaliza ccm ila ccm wakizidi ujanja wa kuibomoa chadema kweli pagumu. Mh.ZITTO chukua ushauri wa mtoa mada tuwakomboe maskin dhidi ya mafisadi.
 
ZITTO'S EGO IS TOO BIG TO TAKE THAT ADVICE...PERIOD, mimi pamoja na wengine wasio na uwezo wa kuja jf kuchangia mada mbali mbali we say ''we hate you zitto''
 
Thanks Mods for disciplining Kichaka by removing his post. I think you can punish him more than that by imposing a ban. Tunataka JF iwe ya kistaarabu na isiwe sehemu ya kutukanana.
 
I am sorry for crowding the forums with a mere ''thanks'' reply, but thank you INVISIBLE for giving a (probably LIFETIME) ban on that somebody KICHAKA! That's a nice x-mas gift,
 
mh zitto karibu chama kingine mwaya kama wanakusingizia mtoto wa watu usije pata presha bure ukakutwa na ya AMINA CHIFUPA.AU UNATAKA KUMFUATA SHOST MWENZAKO?TULIZA AKILI KAKA
 
atoswee tu, pamoja na mabaya ndani ya chadema ila hakustahili kuwa hypocrate alitakiwa akaechini na atushtakie wanachama ili maovu yaondolewe na wanachama, watu tulimwona kama mkombozi kumbe ni mkombezi tu wa mali za uma, timua,timuuuua, hatukutakiiiiiiiiiiiiiiii unadanganyika kirahisi na umetusaliti wananchi na chama chako aibu kwako, nenda kwa mafisadi wenzio huku hakukufai.
 
mie mshamsamehe amewashushua wale waliosema karishwa sumu hivi vijigazeti vya RA BWANA ! tumwombee kwa Kakobe ana mapepo yatapona tu
 
Huu ni ushauri mzuri tu kwa Zitto na changamoto kwake. Ikiwa ni mwana-msikivu atafuata ushauri na shauri nyengine zinazolingana na hizi. Sikubaliani ingawa ninaheshimu mawazo kuwa kutoka kwake CDM hakutokuwa pigo kwa chama. Kama ilivyoelezwa mara moja hapa, kuwa kuna watu wanafuata watu na sio chama na wako wanaofuata watu katika chama. Lakini kwa upande mwengine ninaamini kuwa ikiwa atajitoa CDM na kujiunga na chama chochote cha upinzani, hasa CCM, atakuwa anaudhihirishia umma juu ya yote yaliyokuwa yanasemwa dhidi yake. Kwa kuwakata kidomodomo waliokuwa wanafikiria hivyo, akubali ushauri aliopewa hapa. "Hewalla si utumwa" wala si kujidhalilisha bali ni kukubali makosa, wenye nadhari na nia njema na CDM watakufahamu.
Jengine, kwa mawazo yangu binafsi, ninakuwa na wasiwasi na wale wanaohamahama vyama. Sifikirii kuwa ni watu makini wenye msimamo na itikadi thabiti ya kisiasa, ingawaje mtu ana uhuru wa kuamua analotaka, lakini hili la kuhama chama kwangu ni sawa na kuisaliti itikadi yako.
Mwisho wa yote, uamuzi ni wako, lakini kabla ya kuamua "fikiria tena na tena" ili uamuzi wako utokane na sababu zako (moyoni) na sio kichwani.
 
Mheshimiwa Zito me ni mwenyeji wa Kigoma, kumbuka CHADEMA ndiyo imekufikisha hapo ulipo, ni vizuri mkahesihimiana na wote ndani ya chama. tunajua kuna watu ndani ya CHADEMA wanataka kuwa viongozi daima, but kumbuka kuwa tunajjua ya kwamba ukiondoka chadema hutaweza kumshinda mtu mmoja maarufu sana kuliko wewe tena ndiye aliyekufundisha siasa Bwana YARED FUBUSA. angalia usije ukapotea kwenye siasa.
 
Hii inanikumbusha uchaguzi wa chuo CBE wa mwaka huu. Aliye rais sasa Mr. Emmanuel alichagua jamaa 1 very famous awe mkt wa kampeni zake kumbe jamaa (Miraji) alikuwa mamluki.
 
Mheshimiwa Zitto Kabwe,
Mbunge wa Kigoma Kaskazini,
na Katibu Mkuu Msaidizi wa CHADEMA.
Mheshimiwa,
Kwa siku za karibuni jina lako limevuma sana katika vyombo vya habari kwa masuala mbali mbali na Watanzania hasa wanachama na wapenzi wa chama chako wamegawanyika ktk mapande mawili, wengine wakikushutumu na wengine wakikuunga mkono! Mimi leo kupitia JF ambako najua wewe ni mwanachama, naomba kupita mstari wa katikati na kukushauri kitu cha kufanya katika kipindi hiki kigumu kwa chama chako na wewe binafsi.

Kama sikosei mheshimiwa, umri wako bado ni mdogo hivyo kunipa imani kwamba bado unayo miaka mingi ya kufanya kazi hizi za kisiasa kuliko viongozi wenzako wengi mlioko CHADEMA. Najua na nina amini kuwa unao uwezo mkubwa wa kufanya siasa lakini kwa hakika wale wote tunaokupenda umetuweka roho juu na hatujui your next move. Lakini Mheshimiwa, kwa jinsi hali ilivyo nakuomba usifanye move yoyote itakayo kuumiza wewe binafsi, kuumiza chama chako au kutuumiza sisi tunaokupenda na kukushabikia!

Hivi sasa najua umekuwa lulu kwa wanaCCM, wanakutaka pia wanataka kukuchanganya kwa sababu wangependa kuona chama chako kikisambaratika ili ifikapo mwaka 2015 wasipate changamoto kama walizopata ktk uchaguzi uliopita. Najua pia kuwa vyama vya NCCR MAGEUZI na CUF wanakumezea mate na wangependa ufanye chochote ili uondokane na hawa CHADEMA na ikiwezekana uungane nao bila kujali maisha yako kisiasa.

Mheshimiwa Zitto,
Usikubali kupoteza mtaji wa kura zaidi ya Milion 2.5 zilizopatikana kwenye uchaguzi mkuu kwa chama chako. Najua kuwa ulichangia moja kwa moja au inderectly kupatikana kwa kura hizo ambazo mimi naona ni mtaji kwako wewe Mheshimiwa. CHADEMA siyo ya Mbowe, Slaa, Mtei wala Kiongozi yeyote. Naamini kuwa Chadema ni yetu sisi wananchi na wanachama wote hivyo mapambano yoyote yanayoendelea kwenye chama ni kielelezo cha mstakabali wetu na lazima historia itakuja tujuza pumba na mchele.

Mheshimiwa, nakuomba uvumilie kama kuna matatizo yoyote kwenye chama, nakuomba ufanye uamuzi wa kishujaa utoke hadharani uombe msamaha kwa yote unayotuhumiwa nayo haafu uchukue hatua ya kuwaandikia barua ya kuomba msamaha viongozi wenzako. Ukifanya hivyo, utakuwa umeshinda vita zote zilizoko mbele yako na utaonekana shujaa ktk chama chako. Najua kwa kufanya hivyo, CCM watasikitika na kukusema kuwa umeisha kisiasa lakini mimi nadhani kuwa utakuwa umezikumbatia zile kura milioni 2.5 zilizopatikana kwenye uchaguzi uliopita na utakuwa umejitengenezea njia nzuri ya kuelekea 2015.

Mheshimiwa, ni vema nikasema kuwa ni heri kupiga hatua moja mbili nyuma kuliko kurudi mwanzo na kuanza upya ili uweze kusonga mbele. Wanaokwambia ujiondoe CHADEMA hawakutakii mema wewe binafsi wala chama chako na wale wanaosema ufukuzwe hawajui mtaji uliowekeza kwenye chama na wala hawakitakii chama chako prosperity. Ndugu yangu Zitto, nakuomba utumie changamoto zilizoko sasa ufanye siasa ambyo itakuimarisha wewe na chama chako ili hata wapinzani wako waanze kukuamini na kujua kuwa wewe ni kijogoo wa siasa za Chadema.

CHADEMA for Life.
Sikiliza sauti kutoka kwa mama yako Mzazi,
Heshimu viongozi wenzako na kila anayekutakia mema kwenye Chama

Uwiwanyu Agukunda

tabu yote ya nini hiyo? akitaka mambo yake yawe safi basi abadilishe dini tuu.
 
Safi sana laiti tungekuwa na washauri wazuri kama wewe Tanzania yetu ingekuwa mbali sana tatizo Zitto ni mbishi kama unga wa ngano kila kitu anajua na anaweza.
 
Back
Top Bottom