Barua ya Wazi kwa Spika wa Bunge

Advisor

Member
Jan 10, 2008
38
0
Nani “Chaplain” wa Bunge Letu?​

Je, watanzania tunaelekea wapi kama Taifa? Kinachonisukuma kwenye swali hilo ni mwenendo wetu wa kisiasa, kiuchumi na kijamii ambamo kila tukipiga hatua moja mbele, tunapiga hatua zingine kadhaa nyuma na kutereza. Hili limeendelea kutusumbua watanzania kwa zaidi ya miongo minne na nusu tangu tulipopewa uhuru wa kujitawala.

Leo nimetaka kujua jambo moja: Je, kwenye Bunge, Mahakama au Serikali yetu kuna kiongozi yeyote anayesimamia kutoa ushauri nasaha wa maadili mema na maswala ya kiroho? Kwa nini nauliza hili?
Kwa tafsiri ya afya ya Shirika la Afya Duniani (WHO), afya njema ni kuwa na siha nzuri kimwili, kiakili, na kiroho. Viongozi wetu wana afya nzuri sana kimwili kutokana na lishe na medical check-ups walizo nazo, hatuna shaka na hilo. Na hata kama kuna shida kidogo tumeshuhudia ndege zikipaa mara nyingi kwenda India, Ujerumani, Uingereza, Marekani na sehemu mbalimbali kuwaweka sawa kimwili. Wengi wao wanapata nafasi za mafunzo katika semina na short courses wanazozipata kila wakati, ingawa kwa kweli tuna wasi-wasi na muda wanaojitengea kwa kujisomea wao wenyewe. Haya yote ni katika kuweka sawa maeneo muhimu ya afya ya mwanadamu. Swali ni: je, viongozi hawa wana utaratibu uliowekwa na Bunge wa check-ups za afya zao kiroho ili wakamilike kwa tafsiri ya kuwa na afya njema na hatimaye utendaji bora? Kwa sababu kama mtu asipopata attention kwenye eneo moja kati ya hayo hataweza kudai kukamilika kiafya. Badala yake anaweza kuelemewa kwa namna moja au nyingine. Mtu anapoendelea kunawiri kimwili tu bila kuendelea kukumbushwa kwamba kuna nguvu kuu zaidi zinazompatia uwezo na hekima za mambo muhimu yanayohusiana na maadili na mwenendo mwema na kwamba anawajibika kwazo, kuna athari nyingi na zilizo dhahiri ni zile za kushuka uwezo wake kiutendaji, kushindwa kuutawala mwili na maamuzi yake na hivyo kuelemewa na ulafi, tamaa, uchu, kushindwa kuheshimu sheria na mambo mengi ambayo yanahitaji siha ya kiroho.

Lakini baya zaidi ni kujidanganya kwamba anaweza kutegemea uwezo wake binafsi. Na kama kiumbe huyu akibaki kutegemea uwezo wake binafsi, basi tarajia lolote, kwani ni kiumbe hatari kuliko wanyama wa mwituni.
Ninasema hivyo nikiwa na imani kubwa kwamba mwenendo na maadili aliyonayo mtu yana sehemu kubwa sana kwa utendaji wake kama kiongozi (bora).

Naamini kwamba maoni yangu hayatochukuliwa kama campaign ya kutaka kuwa na serikali ya wachungaji na mashehe. Hii sio hasa nia yangu kwani hata hao wanaweza kuwa na tatizo lile lile. Ninalopendekeza hapa ni kuwa na viongozi wenye msingi mzuri wa uadilifu, wenye elimu ya kutosha kujua tofauti ya baya na jema na kuwa na mfumo maalumu wa kuwawajibisha wale wanaopungukiwa na kiwango cha uadilifu tunachokihitaji.

Kama tukishindwa kulielewa hili na umuhimu wake, mambo kadhaa ni hakika kwetu watanzania:

1.Tutaunda kamati nyingi sana za uchunguzi na bado tusifike mbali.
2.Na tutaendelea kwa muda mrefu kushangaa matendo ya ajabu kabisa yafanywayo na wenzetu kila kukicha.

Kama elimu na uzoefu wa kisiasa vinatosha kumfanya mtu awe mwadilifu, basi tusingefikia hatua ya kuiona rushwa kama ni jambo la kawaida kiasi cha kulinganishwa rushwa ya mtu mmoja na mwingine ili tujue nani tumpigie kura, na tusingeifanya kigezo cha kupata huduma kwenye taasisi za serikali. Kama elimu na lishe tu vinatosha basi tusingesikia wale wenye shahada za udaktari wa falsafa za sheria wakighushi fedha nyingi za serikali ili waendelee kula. Hawa ndio ambao wangeweza kuwa wa kwanza kupinga jambo ambalo ni kinyume na sheria. Lakini si hivyo. Kama ni elimu na lishe tu tusingesikia wachumi wakilifirisi taifa lao wenyewe. Kama ni elimu na lishe tu basi tusingesikia viongozi wetu wakuu wa nchi wakiwa wao ndio “nyota ya mchezo” katika rushwa na ubadhirifu na kuwa na mabenki, mkampuni, nyumba za kifahari ndani na nje ya nchi, n.k na wala tusingesikia wake zao wakijihusisha na biashara haramu ili mradi tu wasipwaye kwenye tafsiri ya cheo chao cha “First Lady”. Kama elimu na lishe tu vinatosha tusingesikia viongozi wakiwafyatulia risasi wafuasi wao eti kwa sababu “wameudhiwa”. Lishe na elimu havitoshi. Tunahitaji viongozi waadilifu.

Nimeuliza swali hili hali nikijua fika kwamba Serikali yetu haina dini na yumkini vivyo hivyo kwa Bunge letu “tukufu” na Mahakama pia. Lakini ni imani yangu kwamba viongozi wengi na kiasi kikubwa cha wananchi wa Tanzania wana dini.

Kwa sababu kila kabla ya kuanza kwa vikao vya Bunge “tukufu” husomwa sala kwa dini kuu za Tanzania. Viongozi wa serikali yetu wanapoteuliwa kwa nyadhifa mbali-mbali za juu hulazimika kuapa wakiwa na vitabu vitakatifu kabla kuanza majukumu yao. Mashahidi wanapotaka kutoa ushahidi mahakamani hufanya vivyo hivyo pia. Na mara kadhaa tunapokumbwa na majanga tusiyoweza kuyatatua au kuyaelewa kwa busara zetu, viongozi wa serikali yetu isiyo na dini huwaomba wananchi kwa umoja wao na tofauti za dini zao kumwomba Mungu atusaidie. Mara zote tumelifanya hili kwa uaminifu mkubwa bila ushuru wala rushwa yoyote. Kwa mfano, mwezi wa Oktoba mwaka 1999 tuliombwa sana kumuombea Baba wa Taifa na tukaitikia kwa moyo mmoja.

Katika majanga makubwa kama ajali, ukame, mafuriko, njaa, magonjwa ya kutisha, n.k tumelazimika kutumia dini zetu kuisaidia serikali yetu isiyokuwa na dini yake.

Sasa kuna janga kubwa ambalo linahitaji maombezi ya wananchi wenye dini kuisaidia serikali ingawa viongozi wetu hawajaliona kabisa. Janga hili ni janga la ufisadi lililovikumba vyombo vya uongozi kama Serikali, Bunge, na Mahakama.

Tatizo hili ni kubwa kuliko tunavyodhani. Ni kubwa kwa sababu janga hili halikuanza jana na nasikitika kusema kwamba halitaisha kesho! Sisemi hivyo kwa sababu siipendi nchi yetu, la hasha! Ninaipenda sana Tanzania. Ninasema hivyo kwa sababu sioni nuru yoyote mwisho wa shimo hili tulilomo.

Sioni nuru kwa kuwa viongozi wetu ni wale wale jana, leo na hata kesho ambao waliotusababishia janga hili – wanabadilishana na kupumzishana tu kama wachezaji wa timu ya mpira wa kikapu. Tangu miaka ya 1980 viongozi wa juu wamekuwa wakijigamba kuandaa mazingira mazuri ya kiuchumi lakini hili limebaki kama swala la kujitafutia kura na umaarufu wa kisiasa na kuwaacha wananchi wapiga kura hao wakitaabika na kunyanyasika kila siku hali wakishuhudia miondoko ya ajabu ya viongozi waliowachagua.

Kila mwanadamu ameumbwa na utashi wa asili wa kuabudu hata kama ni kwa mapungufu ya hapa na pale katika imani hiyo. Na ndio maana wale wasioamini Mungu hukidhi utashi huu kwa kuabudu viumbe wengine kama Ng’ombe, Mbuzi, Kondoo, Miamba, Jua, n.k. Hii ni kwa sababu mwanadamu ameumbwa kama kiumbe tegemezi – anategemea uwezo wa asili mkubwa zaidi ya ule alionao na kapewa kiu ya asili ya kutaka kuwa na kiumbe wa kuabudu.

Swala hili la kuamini Mungu na viumbe wengine si swala la imani tupu. Ni swala linaoendana pia na mkusanyiko wa taratibu (maadili) mbali-mbali ambazo kwa kawaida huwa kanuni za maisha ya yule anayeamini. Kwa hivyo imani na maadili haya huwa msingi mkuu wa tabia na chaguzi za mtu na hatimaye mwenendo na matendo yake. Na kwa mantiki hii iliyo wazi kwa wengi ni dhahiri kwamba kuna uhusiano wa karibu sana kati ya imani ya mtu na mwenendo na utendaji wake. Kwa maana nyingine utu wa mtu unategemea sana kile anachokiamini na kukiabudu. Katika hali ya kawaida mtu asiyeamini Mungu utategema atende kama mtu asiyemuamini Mungu na vivyo hivyo kinyume chake.

Tusemapo kwamba serikali haina dini – tulielewa hili vema katika mazingira ya kisiasa ambayo Baba wa Taifa alitaka kuyatumia katika kujenga msingi wa umoja usio na ubaguzi wa dini ambao kwake (na baadaye wengi wetu) ulikuwa muhimu sana. Wasi-wasi wangu leo ni pale falsafa hii inapowaingia baadhi yetu kinyume na maana tarajiwa na hivyo kuanza kujiona na kutenda kana kwamba na wao pia, kama watu binafsi, hawana dini.

Baba wa Taifa aliwahi kukemea swala la rushwa lililokithiri kwenye uongozi wa serikali wa awamu ya pili. Uongozi wa serikali ya awamu ya tatu ukaingia kwa staili ya “kubweka bila kung’ata”. Ikaendeleza rushwa zaidi kuliko awamu ya pili japo kwa staili tofauti. Uongozi wa awamu ya nne ukaamua kuendeleza yale ya awamu ya tatu. Watu wale wale. Leo hali ya rushwa ni mara dufu. Viongozi wa serikali hubadili tu staili ya ufisadi bila kupunguza makali.

Ninapoyatafakari haya yote ninajaribiwa kuamini kwamba matatizo yaliyopo katika taifa hili kamwe hayatatuliwa na serikali iliyopo madarakani. Ni kumtwisha mzigo asiouweza Rais wetu kama tutadhani kwamba umaarufu uliomuweka kwenye nafasi hiyo unaweza kututalia matatizo haya makubwa tuliyojiingiza kwa miaka yote huku tukichekeana na kupeana vizawadi vya uongo na kweli ili kuzibana midomo kwenye uhalifu wetu.

Taifa letu linahitaji wito kwa wale wenye dini za kweli kutuombea ili Mungu atupe viongozi wa kweli na wasio wafisadi.

Tunahitaji kukumbushana maadili mema na kuogopa ufisadi. Tunahitaji kuheshimiana .

Tunahitaji kuheshimu haki za kila mmoja wetu na sheria ya nchi.

Tunahitaji kutumia utawala wa sheria badala ya ushoga.

Tunahitaji kudumisha amani. Tunahitaji kuomba maadili yafufuke Tanzania.

Tunahitaji kuomba viongozi wapya Tanzania.

Ukweli ni kwamba akina Mkullo na akina Wassira hawana jipya la kutupatia watanzania, wangekuwa nalo Tanzania ingekuwa ni taifa bora zaidi. Akina Balali bado wapo wengi sana. Akina Mahalu tunazunguka nao humu-humu kila siku.

Akina Ditopile wamejaa kila mahala. Wameruhusiwa kununua silaha, na wanazo fedha za kuweka wanasheria. Na hawa watu tusiwakandamize sana kwani wamejikuta katika jamii iliyotoka kwenye msiba – msiba wa maadili. Taifa ambalo limesahau tofauti ya mema na mabaya. Likitendwa baya tunacheka na magazeti yetu yananunuliwa zaidi. Likifanywa zuri tunashangaa! Hivyo walijioona kama wako sawa.

Tunachohitaji sasa ni kujenga Taifa jipya. Tunahitaji mabadiliko makubwa zaidi. Mpaka wakati huo utakapotimu watanzania tukae tayari kusikia vituko vingi zaidi.

Raia Mpenda Mema,
 
Tunahitaji mabadiliko makubwa zaidi. Mpaka wakati huo utakapotimu watanzania tukae tayari kusikia vituko vingi zaidi.

Pole sana ndugu yangu, kama walivyowengine wengi, unaonekana umekata tamaa na jinsi mfumo wetu wa maisha unavyokwenda. Na kweli kwa sasa ni vituko vingi sana tunaviona.

Mabadiliko makubwa yanaweza kutokea pale tu viongozi wakuu watakapoamua kuleta serious changes bila kuangalia maslahi ya wachache.

Kwa sasa, Watanzania wanachoweza kufanya ni kuendelea kujikwamua kiuchumi kupitia fursa ziliozopo. Wengi wakifanya hivyo inawezekana wakajenga uwezo wa kiuchumi ambao unaweza ukaleta mabadiliko.

Otherwise . . . Let us watch and see . . .
 
Likitendwa baya tunacheka na magazeti yetu yananunuliwa zaidi. Likifanywa zuri tunashangaa! Hivyo walijioona kama wako sawa. Tunachohitaji sasa ni kujenga Taifa jipya. Tunahitaji mabadiliko makubwa zaidi. Mpaka wakati huo utakapotimu watanzania tukae tayari kusikia vituko vingi zaidi.

Mkuu Advisor,

Hapo juu ndio kwenye utata wa taifa letu, tuache kuwachagua viongozi wabovu, maana ni sisi wananchi ndio tunawapa uongozi kwa kutumia kura zetu, tuwaamshe wananchi ili tubadilike, maana taifa haliwezi kubadilika bila ya sisi wananchi kubadilika kwanza, na hakuna muujiza wa kuja kutubadilisha ila tutajibadilisha sisi wenyewe kwa kuamshana usingizini, bunge limeanza sasa wananchi tufuate nyuma!
 
mama Lwakatare nnategemea yupo kule tuhamasishe na wengine wawe wengi wajitahidi kutoa elimu hiyo mnayoisema au vp?
 
Roho ipo ndio maana kuna uroho

Hayo mawili hayahusiani kabisa, usitake nimfungulie kifimbocheza.

Roho ni kile wenzetu wanachokiita soul, ambacho kama si shorthand ya kuelezea psyche basi hakuna roho actual.Uroho unaotaka wewe kuuhusisha na roho hauhusiani hata kidogo na roho, unataka kuhusisha roho na uroho kama vile kulivyo na uhusiano kati ya kubwa na ukubwa, uroho (gluttony) ni neno linalojitegemea na halina uhusiano na roho (soul).I personally do not believe in the existence of the soul.It is a fabrication just like many other religious fabrications.

Not to be seen as going on a tangent and diverging from the point, my point is that the spiritual approach is seldom transparent and honestly effective.Kuna wanasiasa wachungaji wameingia mpaka bungeni lakini integrity zero, na kuna wasio na werevu wa kiroho lakini wachapa kazi wazuri.

Mambo ya kiroho yanasaidia lakini yana mipaka yake, kwani kuna mijitu imezaliwa katika familia za kichungaji/kiustaadh na mifirauni ya kwanza, na wengine wamezaliwa na kukulia katika madanguro ya Manzese kwa mfuga mbwa lakini ni watu safi sana.Lets keep it secular, especially when it comes to the state.


Advisor

Kila mwanadamu ameumbwa na utashi wa asili wa kuabudu hata kama ni kwa mapungufu ya hapa na pale katika imani hiyo. Na ndio maana wale wasioamini Mungu hukidhi utashi huu kwa kuabudu viumbe wengine kama Ng'ombe, Mbuzi, Kondoo, Miamba, Jua, n.k. Hii ni kwa sababu mwanadamu ameumbwa kama kiumbe tegemezi – anategemea uwezo wa asili mkubwa zaidi ya ule alionao na kapewa kiu ya asili ya kutaka kuwa na kiumbe wa kuabudu.

Kuna watu hatuamini mungu wala supernatural powers zozote, kwa hilo mkuu "Advisor" uki-assume kuwa ni lazima kuabudu unakosea.Na ukiassume kuwa integrity na morality haziji bali kwa njia ya dini na kuabudu vitu visivyoonekana au vilivyo "supernatural" unakosea.Morality na integrity inaweza kupatikana bila kuabudu.Actually wengine tunaweza kusema kuwa kuabudu ni sehemu ya tatizo kwa maana binadamu anawatupia mzigo wake mungu na shetani.Akifanya ushenzi anakimbilia kanisani na msikitini kutubu eti shetani kamkwaza, only kurudia tena over and over.Laiti angekubali kwamba ni yeye na yeye tu aliye responsible kwa matendo yake pengine angeweza kuwa na rsponsibility ya juu zaidi.
 
Kuna watu hatuamini mungu wala supernatural powers zozote, kwa hilo mkuu "Advisor" uki-assume kuwa ni lazima kuabudu unakosea.Na ukiassume kuwa integrity na morality haziji bali kwa njia ya dini na kuabudu vitu visivyoonekana au vilivyo "supernatural" unakosea.Morality na integrity inaweza kupatikana bila kuabudu.Actually wengine tunaweza kusema kuwa kuabudu ni sehemu ya tatizo kwa maana binadamu anawatupia mzigo wake mungu na shetani.Akifanya ushenzi anakimbilia kanisani na msikitini kutubu eti shetani kamkwaza, only kurudia tena over and over.Laiti angekubali kwamba ni yeye na yeye tu aliye responsible kwa matendo yake pengine angeweza kuwa na rsponsibility ya juu zaidi.

Imani ya kumhofu Mungu ndiyo sahihi ila idadi kubwa imebakia ni jina tu kuwa wanaamini. Wanaamini pasipo kutekeleza wanachoamini na hapo ndipo shida inakuja. Usipomwamini Mungu utajiamini wewe mwenyewe kwamba ni supernatural na chochote utakachofanya utakiamini hata kama ni uonevu kwa wengine ndiyo maana tunaona watu wanakula mabilioni bila hata hofu kuwa kuna watu maskini wanazihitaji hizo pesa kwa uhai wao. Kumwanini Mungu si kuitwa Mohamed au Isaya au kuingia msikitini au kaniasani wengi wanaingia lakini hawana Mungu. Laiti tungemwamini Mungu kweli tungelikuwa mbali kimaendeleo. Tusingekuwa na kamati za mwakyembe, Zitto, n.k Haya tunayoyaona ni matokeo ya kutomhofu Mungu na kutotenda yale ambayo Mungu anatuagiza. Na mtu asiye mwamini Mungu ni hatari sana kwani anajiamini mwenyewe na matendo yake anaona ni sahihi hata kama ni unyanyasaji, hana reference ya yale anayotenda. Ukiona mtu anaua, anakula rushwa, fisadi, n.k huyo hana Mungu hata kama anaitwa Abdallah/Petro au anaenda msikitini/kanisani.
 
Kuna watu hatuamini mungu wala supernatural powers zozote, kwa hilo mkuu "Advisor" uki-assume kuwa ni lazima kuabudu unakosea.Na ukiassume kuwa integrity na morality haziji bali kwa njia ya dini na kuabudu vitu visivyoonekana au vilivyo "supernatural" unakosea.


Hii ni ligi nyingine mpya. Nashauri ufungue thread tofauti. Tunalojadili hapa ni maadili kwa jamii yetu. Ligi hiyo mimi ni vigumu kushiriki kwani tuko katika ulimwengu tofauti.
Goodluck!
 
Imani ya kumhofu Mungu ndiyo sahihi ila idadi kubwa imebakia ni jina tu kuwa wanaamini. Wanaamini pasipo kutekeleza wanachoamini na hapo ndipo shida inakuja. Usipomwamini Mungu utajiamini wewe mwenyewe kwamba ni supernatural na chochote utakachofanya utakiamini hata kama ni uonevu kwa wengine ndiyo maana tunaona watu wanakula mabilioni bila hata hofu kuwa kuna watu maskini wanazihitaji hizo pesa kwa uhai wao. Kumwanini Mungu si kuitwa Mohamed au Isaya au kuingia msikitini au kaniasani wengi wanaingia lakini hawana Mungu. Laiti tungemwamini Mungu kweli tungelikuwa mbali kimaendeleo. Tusingekuwa na kamati za mwakyembe, Zitto, n.k Haya tunayoyaona ni matokeo ya kutomhofu Mungu na kutotenda yale ambayo Mungu anatuagiza. Na mtu asiye mwamini Mungu ni hatari sana kwani anajiamini mwenyewe na matendo yake anaona ni sahihi hata kama ni unyanyasaji, hana reference ya yale anayotenda. Ukiona mtu anaua, anakula rushwa, fisadi, n.k huyo hana Mungu hata kama anaitwa Abdallah/Petro au anaenda msikitini/kanisani.

Kuna ukweli katika hiyo sentensi niliyo ibold, lakini ni misleading half truth zaidi kuliko ukweli.Some communists did not believe in a god and were brutal killers (Stalin for example) but there were also principled communists who even warned the rest of the Soviet about the evil of Stalin.The Nazi's even used the support of the Catholic Church in their inhuman Holocaust.

Waisraeli wakoloni, settlers wa Marekani na Australia wote waliamini kuwa wanatekeleza kazi ya mungu walipocommit inhuman atrocities against native people.Mara nyingi kuamini katika supernatural powers kunaleta negative or at best non transparent distortions.

Watu wanaua, wanaiba kwa sababu organised religion imeshindwa, na wanaamini watatubu.Watu wengi ni "closet atheist" hawaamini kwamba Mungu aliumba ulimwengu miaka 7,000 iliyopita katika siku saba.Watu hawaamini kwamba Jonah aliliwa na nyangumi na kutapikwa.Watu hawaamini kwamba Musa alipasua bahari.Hizi habari za kuwadanganya watu kwamba kuna mungu in the sky atakaye wa punish au kuwareward zinashusha standards za morality na watu wanafanya uovu kwa kuona huu uzushi.Watu inabidi wajue kuwa hakuna mungu na inabidi kufanya mema for the sake of kufanya mema, it is best for everybody.Watu wanashtuka kuwa hakuna pie in the sky inn the afterlife, this was a bad incentive.
 
Hii ni ligi nyingine mpya. Nashauri ufungue thread tofauti. Tunalojadili hapa ni maadili kwa jamii yetu. Ligi hiyo mimi ni vigumu kushiriki kwani tuko katika ulimwengu tofauti.
Goodluck!

Umeongelea the spiritual aspect (chaplains in the parliament and what not) ya jamii yetu kama sababu iliyotufikisha hapa tulipo.Mimi naonyesha the fallacy in the foundations of the precepts of that spiritual aspect, na kwamba as long as the precepts are fallacious and pretentious, they cannot be effective.

Sasa nimetoka nje ya topic kivipi? Mimi ndiye ninakurudisha kwenye topic, kwamba lets keep it secular (tuongee morality siyo spirituality), ukileta mambo ya spirituality especially in the dimension ya organised religion kama mambo ya chaplains una complicate issues kwa sababu kuna watu hatuamini in the monopoly of organized religion kwenye morality, doing good and raising performance eventually.

Organised religion katika kuwa na usiri mkubwa, heshima nyingi kwa wakubwa na kutoweza kuuliza authorities haina tofauti sana na mafisadi wa CCM wanaotaka mikataba iwe siri na Waziri Mkuu asiulizwe maswali eti kwa sababu ni "kiongozi mkuu wa serikali".Kweli ndiyo tunayotaka hayo?
 
Kwa kuwa serikali imezidiwa, tuisaidie

Peter Nyanje
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


NILIKUWEPO Hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam, wakati Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema alipowaambia wahariri kuwa mafisadi wa EPA (akimaanisha watu wanaotuhumiwa kuiba fedha za umma kupitia akaunti ya malipo ya madeni ya nje iliyoko Benki Kuu), ni sawa na magaidi ambao wameiteka ndege.

Mwema alitoa mfano huu ili kuwaaminisha wahariri kuwa timu inayochunguza wizi huo, inashindwa, si tu kuyataja majina ya watuhumiwa ambao tayari wameshaanza kurejesha fedha walizoiba, bali pia kuwachukulia hatua za kisheria wakati huu.

Akitetea hatua zinazochukuliwa na timu hiyo inayoongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Johnson Mwanyika, na kumhusisha yeye na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Edward Hosea kama wajumbe alisema, iwapo timu yake haitokuwa makini, wezi wa fedha za EPA wanaweza kutenda kama magaidi ambao wanaweza kuilipua ndege waliyoiteka ikiwa na mateka wake ndani.

Nikiri kuwa wakati niliposikia kauli hiyo ya Mwema kwa mara ya kwanza pale Movenpick, sikuona mara moja ukubwa wake, mpaka siku ya pili, nilipoitafakari kwa kina na kubaini kuwa kuna uwezekano, Mwema, labda kwa lengo la kutaka kujikosha kuwa anachokifanya kipo juu ya uwezo wake, aliamua kuonyesha kimafumbo ni jinsi gani mafisadi wameikamata serikali.

Kwa vyovyote vile, katika hali ya kawaida, haiwezekani kwa vyombo vikubwa vilivyokabidhiwa dhamana ya kutunza sheria za nchi, kama ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Jeshi la Polisi na Takukuru, kupata ushahidi dhahiri dhidi ya wezi, halafu washindwe kuwachukulia hatua.

Hivi ndivyo inavyotokea katika uchunguzi unaofanywa na vyombo hivi.

Mwanasheria Mkuu, Polisi na Takukuru baada ya kuwahoji wezi hao na kupata ushahidi wa dhahiri kiasi kwamba baada ya mashauriano, wezi waliona kuwa hakuna njia nyingine ya kukataa kosa, wakaamua kuanza kurejesha fedha hizo.

Kwamba wamekubali kurejesha ni uthibitisho wa wazi kuwa waliiba, na ndio maana nimeamua bila kumung’unya maneno kuwaita wezi.

Kwamba fedha hizo ziliibwa ilishathibitishwa na Ernst & Young katika ukaguzi uliofanyika na hata Rais Jakaya Kikwete alishawishika na kuyakubali matokeo ya uchunguzi huo kiasi cha kufikia uamuzi wa kutengua uteuzi wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Dk. Daudi Ballali.

Katika mazingira ambayo wezi wameamua kurejesha fedha walizoiba, mwendesha mashitaka anahitaji ushahidi gani zaidi ili kujihakikishia ushindi katika kesi yake?

Ni dhahiri kuwa mwendesha mashitaka anapoeleza kuwa hawezi hata kuyataja majina ya wezi hao basi kuna nguvu za ajabu nyuma ya woga huo.

Kwa kuwa timu hii ilipewa kazi na rais, ninashawishika kuamini kuwa hawezi tena kuwageuka na kuwatisha ili wasifanye kazi yao ipasavyo. Hivyo, ni dhahiri kuwa nguvu hii haitoki katika mamlaka mahsusi zilizopo, na hapa ndipo kauli ya Mwema akiwafananisha wezi hawa na magaidi walioteka ndege ilipoanza kunikolea na kupata maana halisi.

Ndio maana sasa ninaamini kuwa serikali imezidiwa na mafisadi katika hili la EPA. Nachukua nafasi hii kuwashauri Watanzania wenzangu kuwa umefika wakati sasa wananchi kuisaidia serikali katika kupambana na mafisadi.

Nashauri tuangalie namna ya kutumia nguvu ya umma ili mafisadi wasiilipue serikali yetu na sisi tukiwa ndani yake, kama magaidi wanavyoweza kuilipua ndege na mateka wake.

Awali, kabla hatujalishuhudia hili la EPA, Rais Kikwete alipochagua Baraza jipya la Mawaziri mwezi Februari, watu wengi waliulalamikia uteuzi wa Andrew Chenge, wakimtuhumu kuwa ni mmoja wa mafisadi.

Tuhuma hizi zilimfikia mwenyewe Chenge na alipotakiwa aeleze ni kwa nini, licha ya tuhuma hizo zote, ameteuliwa, yeye aliwaambia wanaohoji hilo waende wakamuulize rais ambaye ndiye aliyemteua.

Nilikuwa mmoja wa watu waliomuuliza Chenge swali hilo siku ambayo baraza hilo liliapishwa pale Chamwino, Dodoma. Aliponijbu hivyo, nilijaribu kumsogelea Rais Kikwete kwa lengo la kulipenyeza swali hilo kutokana na ushauri wa Chenge.

Rais alikuwa amezungukwa na watu wengi na alipotuona waandishi tukimnyemelea, alituwahi na kutueleza kuwa asingeweza kusema lolote kwa wakati huo, kwa sababu alishasema sana, na kuwa atasema tena siku hiyo jioni kwenye hafla iliyokuwa imeandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Nilitarajia rais angelizungumzia hilo katika hotuba yake jioni hiyo, lakini hakuligusia. Nadhani alikuwa hajui kuwa tulitaka kumuuliza hilo.

Lakini siku zilizofuata, bila shaka alisoma kwenye vyombo vya habari kuhusu tuhuma dhidi ya Chenge na lawama kwake kwa nini aliamua kumteua kuwa waziri. Kwa bahati mbaya sana, hadi leo rais hajajibu hilo, licha ya kupata fursa kadhaa za kuzungumza na wananchi.

Sasa kama miujiza vile, habari zinapatikana kuwa kilichokuwa kinadhaniwa kuwa ni tuhuma tu, kinaweza kuwa ni habari ya uhakika; Chenge ni bilionea.

Katika hili tatizo si ubilionea wake bali ameupataje ubilionea huo wakati akiwa mtumishi wa serikali hii ambayo inanuka umasikini kushoto kulia, mbele nyuma, juu na chini?

Haiyumkini kuwa Rais Kikwete hakuwa na chaguo jingine badala ya Chenge. Nini kimemsukuma kuchagua mtu ambaye uadilifu wake una shaka, kinaweza kuwa ni nguvu zile zile zilizotajwa na Mwema?

Ninachohisi hapa ni kwamba, inawezekana rais naye amezidiwa, na ndio maana narejea ushauri wangu kwa Watanzania kuwa, umefika wakati sasa wananchi tujitoe muhanga kumsaidia kupambana na nguvu hizi. Naamini kuwa nguvu ya umma haitashindwa.

Uundwaji wa baraza jipya la mawaziri ulitokana na yale yaliyoibuka baada ya kuwasilishwa bungeni kwa ripoti ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu mradi wa kuzalisha umeme wa dharura uliotolewa kwa Kampuni ya Richmond ya Marekani. Aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa akajiuzulu na Baraza la Mawaziri likavunjika.

Kinachoonekana sasa ni kama kilikuwa ni kisa tu, mkasa wenyewe unaonekana huko huko bungeni kupitia kwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.

Wakati ripoti hiyo ilipowasilishwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati, Dk. Harrison Mwakyembe, ilijadiliwa kwa jazba kubwa. Katika mchango wake wa maandishi, Rostam alituhumu kuwa kamati ilikiuka misingi ya kuundwa kwake, kwa kufanya kazi nje ya muda iliyopangiwa, na hivyo kufanikisha kuandaa ripoti mbili, ikiwamo moja ambayo ni bandia (fake).

Hizi zilikuwa tuhuma nzito na zililitikisa Bunge kama taasisi na kamati kama chombo kilichotekeleza azimio la Bunge.

Kutokana na hilo, Bunge, kupitia tangazo lililotolewa na Spika, Samuel Sitta, lilimtaka Rostam, kuthibitisha kile alichokisema, kama inavyotakiwa katika moja ya kanuni za Bunge zinazokataza mbunge kusema uongo bungeni.

Rostam alitakiwa kuthibitisha ukweli wa aliyoyaeleza kwa kuwasilisha maelezo kuhusu kauli yake hiyo. Kwa kuwa muda wa mkutano uliojadili masuala hayo ulikuwa umemalizika, alitakiwa kufanya hivyo katika mkutano uliofuata.

Lakini tumeshuhudia maajabu kwani Spika huyo huyo, aliyetangaza kuwa Rostam anatakiwa kujieleza kwa mujibu wa kanuni, leo hii ameyazuia maelezo ya mbunge huyo kwa maelezo kuwa kuyawasilisha bungeni ni kukiuka kanuni, kwa sababu kamati inayotuhumiwa ilishamaliza kazi yake hivyo haiwezi kujitetea.

Kinachoshangaza ni kuwa, wakati uamuzi wa kumtaka Rostam ajieleze ulitolewa na Bunge, uamuzi wa kuyakataa maelezo yake wala haukulihusisha Bunge! Kilikuwa ni kikao cha viongozi wa CCM!

Na kwa maneno yake mwenyewe, Rostam amesema kuwa amekubaliana na hoja ya kumzuia kusema bungeni kutokana na kulinda maslahi ya chama chake.

Haya ni maajabu yaliyoje! Maamuzi ya Bunge yakaamriwe na kikao cha viongozi wa CCM!

Hatua hiyo inanilazimisha nijiulize; hivi Bunge lina uhusiano gani na CCM kiasi kwamba sehemu ya maamuzi yake yakafanywe na viongozi wa chama hicho? Ndiyo utaratibu tuliojiwekea huo? Kama ni hivyo basi niwe wa kwanza kutamka kadharani kuwa utaratibu huo haufai hata kidogo.

Namshanga pia Spika kwa kusema sasa kuwa Rostam kuwasilisha maelezo yake ni kukiuka kanuni wakati alipoamriwa akalete maelezo zilitumika kanuni hizo hizo. Nisaidie kujiuliza, ina maana Spika na CCM hawakujua kuwa kamati ilikuwa imemaliza muda wake?

Pia, mapendekezo ya kamati hiyo yalifikishwa serikalini kupitia azimio la Bunge. Serikali ikasema kuwa inakwenda kuyafanyia kazi na itakuja kutoa maelezo yake bungeni. Hili tunalisubiri. Cha kujiuliza hapa ni kwamba, iwapo katika maelezo yake, serikali itaituhumu kamati hiyo kwa jambo lolote, itakuwaje?

Mlolongo wa maswali haya ambayo kukosekana kwa majibu yake ya uhakika kunazua utata, kunaonyesha kuwa si bure, lazima kuna nguvu nyingine ambayo imesababisha kupindishwa kwa hoja ya Rostam na kuondolewa bungeni kinyemela hadi kwenye vikao vya viongozi wa CCM ambao walijipa nguvu ya kuamua hoja iliyotolewa bungeni.

Inaonekana wazi kuwa Bunge limezidiwa na nguvu kiasi kwamba limekubali kupokonywa hoja hii na CCM. Na ndiyo maana sitachoka kuwaomba Watanzania wenzangu kuwa nao wasichoke, tujitolee kulipigania Bunge letu.

Naamini kuwa kwa umoja wetu, tunaweza kuuondoa unyonge tulio nao na kupata nguvu ya kulisaidia Bunge kupambana na nguvu hizi zisizoonekana. Na hapa naomba tuitumie nguvu ya umma kulikomboa Bunge letu.

Kwa ujumla wake, serikali inaonekana kushikwa na kigugumizi tangu tuhuma za ufisadi dhidi ya watumishi wake na wafanyabishara wakubwa, zianze kutajwa hadharani.

Tangu wakati huo haijafanya lolote lililoonekana dhahiri, kuwa ni juhudi zake za kupambana na ufisadi.

Baadhi ya waliokuwa wametajwa katika orodha ya mafisadi na Dk. Willibrod Slaa walitishia kwenda mahakamani kwa kile walichoeleza kuwa wamekashifiwa. Hiyo ilikuwa ni hatua nzuri ambayo ingesaidia kuwasafisha, lakini kwa mshangao wa wengi, hadi hii leo wameshindwa kufanya hivyo.

Kushindwa kwao ni moja ya dalili kuwa kilichoelezwa na Dk. Slaa ni kweli, na kuwa iwapo mamlaka zinazohusika zingetaka ‘kulishikia bango’ suala hilo, hapo palikuwa mahali pazuri pa kuanzia.

Lakini hadi leo, si Jeshi la Polisi, Takukuru wala taasisi nyingine yoyote inayohusika na vita dhidi ya ufisadi ambayo imeonekana kuzifanyia kazi tuhuma zilizotolewa na Dk. Slaa, ambazo wahusika wameshindwa kuzikanusha.

Kwa ujumla inaonekana kuwa serikali na taasisi zake zinakwazwa na nguvu fulani ambayo haionekani wazi.

Na ndiyo maana narudia tena kuutaka umma wa Watanzania, tujifunge vibwebwe kwa ajili ya kuitetea serikali yetu dhidi ya nguvu hii kubwa ambayo tayari imeshajionyesha dhahiri.

Naamini kuwa katika umoja wetu tutashinda na kurudisha heshima ya serikali na nchi yetu.

Mungu atubariki katika harakati hizo.

pnyanje@gmail.com
 
Back
Top Bottom