Barua ya wazi kwa rais Kikwete

Ngatuni

Member
Mar 10, 2006
5
30
Mheshimiwa Rais, nimefurahishwa vilivyo na jinsi ulivyoanza uongozi wako wa awamu ya nne kwa ziara za kushtukiza unazozifanya sehemu mbalimbali ambazo unahisi kuna matatizo yanayowaelemea wananchi. Kwa jambo hilo nakupa hongera sana. Wasiwasi wangu ni kwamba, je,baada ya ziara kama hizo ufumbuzi wa matatizo uliyoyaona utapatikana kwa wakati wake? Mfano; Muhimbili wagonjwa kulala chini, mpaka leo hatujasikia hatua zilizochukuliwa. Je, Vitanda vitapatikana lini?

Umeme bei juu lini utapunguzwa? Au ni kutokana na hii hali ya ukame…labda! Na kule kwenda sokoni na kuona bei ya vyakula kuwa juu, je kwa kauli yako wafanya biashara wamefanya lolote kupunguza bei? Mheshimiwa nafikiri wakati umefika wa kuwatumia wasaidizi wako wafanye kwanza utafiti wa kina wa matatizo ya sehemu unazoziona zina shida, ili unapotembelea sehemu hizo utoe hitimisho na kauli zilizofanyiwa utafiti wa kina. Kwa bahati mbaya Mheshimiwa rais nchi yetu ina matatizo mengi sana kila nyanja, nachelea kusema kwamba sehemu ambazo utakuwa hujatembelea wajanja watatumia kigezo hicho kwamba hawajaonekana hivyo kuzidi kutunyanyasa. Pia kama ziara hazitakuwa na ukali wa utekelezaji, basi wataona ni kawaida ya rais kututembelea na kuongea...!

Kuna jambo lingine tena Mtukufu Rais ambalo ni muhimu kwako kuliangalia, UWAJIBIKAJI WA PAMOJA (total responsibility). Serikali yako bado ni changa sana madarakakani hivyo inahitaji mawasilianao ya karibu sana katika utendaji wake ili kuimarisha msingi wa mtandao wa utekelezaji wa yale manayoyakusudia. Kitendo cha hivi karibuni cha wewe kwenda kutembelea daraja la muda bila kuwepo kwa mhusika yeyote wa ngazi za juu katika wizara inayohusika, ni cha kushangaza na kuacha maswali mengi nyuma.

Yako mengi sana Mheshimiwa yanayonipa mashaka na maswali mengi kichwani kama kauli zinazopingana kuhusu wafanyabiasha wadogo (wamachinga), Namna zoezi la ukamataji wa wafanyabiashara wanaohusishwa na ujambazi unavyofanyika na hatima yake….ni megi, mengi…nitarudi tena mhesimiwa rais.

ngatuni.
 
Hayo mengine tusubiri kikwete akujibu, ila hili la TANESCO siwezi nyamaza, bei ya umeme ipo juu hata kabla net Group hawajapewa tenda, yaani tuseme tangu shirika lilipo anzishwa, huwa gharama zingine zinatokana na ukweli kwamba baadhi ya watumiaji hawalipi bili, kama serikali, chama nk. Hili linasababisha wanaolipa walipe zaidi.

sababu ingine ni mikataba mibovu ya tangu enzi, ama waliingia hiyo mikataba kwa makusudi ili wapate takrima, ama waliingia hiyo mikataba kutokana na shinikizo la WAKOLONI (k.v. Benki ya dunia nk.) Hivyo usitegemee tanesco ishushe bei wakati bado inaingia mikataba ya kinyonyaji kama ya IPTL na SONGAS, tena shirika bado lina madeni zaidi ya bilioni tano! (utaambiwa walinunua vipuri, sijui kwanini hawakulipa "cash"?)

Suluhisho la yote ni kubadili sera ya nishati, lazima nchi ijitegemee katika nihati na tusibinafsishe au kuwapa wageni jukumu la kutuzalishia nishati.

Lolote lile lifanyike ili taifa liendelee na jukumu la kuzalisha umeme ndipo angalau bei inawaza pungua. vyanzo vya umeme wa uhakika tunavyo kama vile Gesi na makaa ya mawe, nahata maporomoko ya maji bado yapo mahala pengi tu nchini?

Umeme wa maji ndio ulio nafuu baada ya ule wa atomoki, juhudi zifanyike ili kuzalisha umeme mdogo mdogo wa maji katika mito yote nchini.

Pia umeme wa nguvu ya upepo na wa mionzi ya jua unafaa sana hasa vijijini ambako miundombinu ya gridi ya taifa haijafika.
 
Jamberi,

Hayo uliyoeleza ndiyo haswa kiini cha mimi kuandika hii post. Kiongozi wetu amekuwa anafanya/kusema mambo bila kuchunguza kwanza na kuona impact yake kwa jamii, kwa muda mfupi na mrefu. Mfano mmoja ni huo wa Tanesco, alipowaambia wasipandishe bei ya umeme na badala yake waangalie namna ya kupunguza bei, ilinishangaza ingawa wananchi wengi walishangilia. Inaelekea kushangilia huko ni kutokuelewa. Laiti kama rais angepata muda kidogo wa kupata maelezo kama haya uliyoyatoa hapo juu, nina imani angetoa kauli tofauti. Ninavyoelewa ni kwamba serikali ikitaka kuingilia sector ya kibiashara inayojitahidi kujiendesha yenyewe kama Tanesco, inaingia katika mtizamo huohuo wa kibiashara. Badala ya kuwaambia punguza bei kwa mdomo, wanatoa ruzuku kufidia zile gharama za uendeshaji ili kuzuia kupandisha bei kwa mlaji.


ngatuni.
 
Nngatuni,

Great thinking. Lakini sasa haya mawazo ni makubwa sana kwa kiongozi anayetaka sifa na kupigiwa makofi.

Japokuwa muda ni mfupi kutoa tathmini makini, kuna kila dalili kuwa viongozi waliopo hawana uthubutu wa kutenda jambo zuri in the long term perspective japokuwa linaweza lisiwape sifa sasa hivi.

Kikwete akitaka aende mbele katika umeme, ni muhimu atatue kitendawili cha IPTL. Sasa kama yeye ni mojawapo waliokitega hicho kitendawili itakuwa kazi kukitegua
 
Ndugu zangu,
Inasikitisha sana kuona kwamba nchi za magharibi kwa kupitia benki kuu wanataka kuhakikisha kwamba nguvu zote za Umeme na mashiika ya maji yanapewa makampuni yao makubwa. Hatupewi wala hatutapewa mkopo kuendesha Tanesco kama hatukubinafsisha kwao. Swala la Tanesco ni zito kuliko tunavyolielewa na wala sio TZ peke yake. Nchi nyingi maskini ambazo bado zimeshikilia maji, umeme na benki zinapigwa vita kishenzi wakati kama huu wa utandawazi - Mtaji hatuna na tukijifanya wajanja mali zetu zitawekwa ktk kutokuwa na quality standard inayotakiwa kwao, kwa hiyo hamuuzi kitu nje. Pesa itoke wapi?
Na inasikitisha sana kuona kwamba nchi zetu maskini leo hii eti hatuna budi kukubali UTANDAWAZI ambao ni Ukoloni mamboleo. Yaani tumekubali kurudi ktk kutawaliwa na wasomi wetu wanautangaza kwa nguvu kuwa ndio njia pekee ya mwananchi kujikomboa. Well, tuliutaka Uhuru wetu kwa sababu gani?
Baba wa Taifa, marehemu JKN alijenga mabwawa zaidi ya matano kwa malengo ya kujitegemea na umeme wake hauna gharimu kubwa, leo hii tunafikiria kuyaacha mabwawa hayo kuwa magofu kama tulivyoacha viwanda na kuzalisha umeme wa matumizi nyumbani kwa kutumia gas!...mwanamke mpya tumeacha mbachao. Hali nchi nzima imezungukwa na maziwa yenye maji matamu na masafi yasiyoweza kuozesha vipuri.. Hizo generators watakazo funga nchi nzima zitagharimu wananchi kwa muda mrefu kuliko uvutaji wa maji toka maziwa yetu. Mbona Bulyanhulu mmevuta maji toka ziwa Nyanza na kupeleka huko?..Mnashindwa nini kuvuta maji toka ziwa Nyasa, Nyanza ama Tanganyika, Rukwa, Edward n.k, KUJAZIA mito inayokuwa na upungufu wa maji. Mabwawa haya hayahitaji maji mengi sana ni wakati wa mgumu tu kwani mito yetu sii kwamba haina maji kabisa!
Pia uvutaji wa maji utasaidia maji ya matumizi ya wananchi na ktk kilimo. hapa tutakuwa tumeua ngede watatu kwa jiwe moja kuliko matumizi ya gas... hii ni biashara ya mwarabu mwenye duka la kona, chakula chake nyumbani hutoka humohumo dukani mwake.
 
Hivi jamani, hatuwezi Waafrika kuungana na kuanzisha Makampuni Mama kwa vitu kama Umeme, Simu, Reli, Ndege, Barabara na kadhalika?
 
Rev Kishoka,

Waafrika tunaweza kuungana na kufanikiwa kufanya makubwa sana. Kuna katatizo kadogo Bongo, ka kuatamia umasikini, na kudhani mzawa yoyote akiwa na fedha ameiba. Kenya lakini, wanafanya makubwa.

Fedha nyingi za miradi mikubwa hupatikana kwenye masoko. In Nairobi, $119.4 million worth of bonds was traded in their money markets, in the first 3 months of this year. Kenya Energy Generating Company (KenGen) has issued shares recently, and a subscription level of $250 million has been reached so far.

Kwa upande wetu, tulianza kusimama wakati wa Mkapa. Na hata Balozi wa Uganda Tanzania aliwahi kusema kama tungeendelea na hali ilyokuwepo mwishoni mwa kipindi cha Mkapa kwa miaka 10 zaidi, basi Tanzania ingeipiku Kenya na kuwa ndiyo kitovu cha uchumi wa Afrka Mashariki.

Kwa staili ya viongozi wetu wa sasa, we are quickly returning into our former position of being the economic backwater of East Africa.

Nimekuwa nikisikitika sana ninapoona Watanzania wengi, hata waliosoma, wanawashangilia Rais Kikwete na Waziri Mkuu Lowasa kama vile watu wanavyoshangilia mpira. These guys are running around looking for publicity only! They ought to sit down and do some strategic planning.

Augustine Moshi
 
Mimi kama wengi walivyosema juu ya JK na EL .Hwa viongozi wetu wanapenda sana sana sifa na nimeingiwa zaidi na wasi wasi baada ya kuona kwamba hata wasomi sasa wamebadilika na kuwa wapiga makofi badala ya kuchambua mambo kwa undanoi na kuwa msaad kwa Taifa na hata kumsaidia Rais kutenda kazi zake .There are no Critics na kwa hiyo ndugu JK he will never learn from his mistakes .Magazeti ni mali yake na sasa watu wenye akili za kuchambua mambo wanaishia kumwaga sifa kisa Majambazi ya Ubungo kufukuzwa kw akutumia Helikopta .Ni Balaa ya ajabu maana hata hilo helikopta kutumia bado majambazi wamekimbia na wanatafutwa kwa njia nyingine.

JK wacha kauli ahadi fanya kweli tueleze mikataba iko kwa usahihi, sikiliza kilo cha Watanzania na umeme , Njaa inaua watu Tanzania , rushwa bado na wako walio jitajirisha ni pia ni watu wako wa Mtandao chukua action bila ya kujali maslahi yako wewe binafsi maana wewe ni Rais wa sisi Watanzania na top layer yako .
 
kumbe malalamiko yalianza toka alipoanza kuongoza
Mheshimiwa Rais, nimefurahishwa vilivyo na jinsi ulivyoanza uongozi wako wa awamu ya nne kwa ziara za kushtukiza unazozifanya sehemu mbalimbali ambazo unahisi kuna matatizo yanayowaelemea wananchi. Kwa jambo hilo nakupa hongera sana. Wasiwasi wangu ni kwamba, je,baada ya ziara kama hizo ufumbuzi wa matatizo uliyoyaona utapatikana kwa wakati wake? Mfano; Muhimbili wagonjwa kulala chini, mpaka leo hatujasikia hatua zilizochukuliwa. Je, Vitanda vitapatikana lini? Umeme bei juu lini utapunguzwa? Au ni kutokana na hii hali ya ukame…labda! Na kule kwenda sokoni na kuona bei ya vyakula kuwa juu, je kwa kauli yako wafanya biashara wamefanya lolote kupunguza bei? Mheshimiwa nafikiri wakati umefika wa kuwatumia wasaidizi wako wafanye kwanza utafiti wa kina wa matatizo ya sehemu unazoziona zina shida, ili unapotembelea sehemu hizo utoe hitimisho na kauli zilizofanyiwa utafiti wa kina. Kwa bahati mbaya Mheshimiwa rais nchi yetu ina matatizo mengi sana kila nyanja, nachelea kusema kwamba sehemu ambazo utakuwa hujatembelea wajanja watatumia kigezo hicho kwamba hawajaonekana hivyo kuzidi kutunyanyasa. Pia kama ziara hazitakuwa na ukali wa utekelezaji, basi wataona ni kawaida ya rais kututembelea na kuongea...!
Kuna jambo lingine tena Mtukufu Rais ambalo ni muhimu kwako kuliangalia, UWAJIBIKAJI WA PAMOJA (total responsibility). Serikali yako bado ni changa sana madarakakani hivyo inahitaji mawasilianao ya karibu sana katika utendaji wake ili kuimarisha msingi wa mtandao wa utekelezaji wa yale manayoyakusudia. Kitendo cha hivi karibuni cha wewe kwenda kutembelea daraja la muda bila kuwepo kwa mhusika yeyote wa ngazi za juu katika wizara inayohusika, ni cha kushangaza na kuacha maswali mengi nyuma.
Yako mengi sana Mheshimiwa yanayonipa mashaka na maswali mengi kichwani kama kauli zinazopingana kuhusu wafanyabiasha wadogo (wamachinga), Namna zoezi la ukamataji wa wafanyabiashara wanaohusishwa na ujambazi unavyofanyika na hatima yake….ni megi, mengi…nitarudi tena mhesimiwa rais.

ngatuni.
 
Nngatuni,

Great thinking. Lakini sasa haya mawazo ni makubwa sana kwa kiongozi anayetaka sifa na kupigiwa makofi.

Japokuwa muda ni mfupi kutoa tathmini makini, kuna kila dalili kuwa viongozi waliopo hawana uthubutu wa kutenda jambo zuri in the long term perspective japokuwa linaweza lisiwape sifa sasa hivi.

Kikwete akitaka aende mbele katika umeme, ni muhimu atatue kitendawili cha IPTL. Sasa kama yeye ni mojawapo waliokitega hicho kitendawili itakuwa kazi kukitegua

Na akitegua hapo kwenye IPTL nadhani ishu ya umeme inaweza ikawa imepata solution maana hiyo IPTL ilikuja wakati yeye akiwa waziri wa mambo ya nje mimi naona kuna siri kubwa sana kati ya JK na IPTL.
 
Huu uzi ni wa 2006 lakini ukiangalia yaliyoguswa humu na yaliyotokea tangu hiyo 2006, duuh mdau alibashiri kila kitu. Kweli JK ni dhaifu sana.
 
Rev Kishoka,

Waafrika tunaweza kuungana na kufanikiwa kufanya makubwa sana. Kuna katatizo kadogo Bongo, ka kuatamia umasikini, na kudhani mzawa yoyote akiwa na fedha ameiba. Kenya lakini, wanafanya makubwa.

Fedha nyingi za miradi mikubwa hupatikana kwenye masoko. In Nairobi, $119.4 million worth of bonds was traded in their money markets, in the first 3 months of this year. Kenya Energy Generating Company (KenGen) has issued shares recently, and a subscription level of $250 million has been reached so far.

Kwa upande wetu, tulianza kusimama wakati wa Mkapa. Na hata Balozi wa Uganda Tanzania aliwahi kusema kama tungeendelea na hali ilyokuwepo mwishoni mwa kipindi cha Mkapa kwa miaka 10 zaidi, basi Tanzania ingeipiku Kenya na kuwa ndiyo kitovu cha uchumi wa Afrka Mashariki.

Kwa staili ya viongozi wetu wa sasa, we are quickly returning into our former position of being the economic backwater of East Africa.

Nimekuwa nikisikitika sana ninapoona Watanzania wengi, hata waliosoma, wanawashangilia Rais Kikwete na Waziri Mkuu Lowasa kama vile watu wanavyoshangilia mpira. These guys are running around looking for publicity only! They ought to sit down and do some strategic planning.

Augustine Moshi
Zamani JF ilikuwa kisima cha watu makini...hii miamba sijui iko wapi siku hizi.

Hii inadhihirisha wazi kwamba OLD IS GOLD.
 
Back
Top Bottom