Barua ya wazi kwa dada zangu walio single...................!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Happy-Black-Woman-378x414.jpg


Leo nimeamua kuwaandikia barua dada zangu ambao wanatamani sana kuwa na mahusiano na wanaume lakini kwa bahati mbaya hawajabahatika kumpata anayewafaa. Kwa wale ambao wanaona kama muda unayoyoma na wanahisi kama wanaume wanawakwepa, kwa wale walio katika hatua ya mwisho ya kuvunja uhusiano, kwa wale ambao wanaona kwamba wao siku zote wanaishia kuwa wapambe wa maharusi na kamwe si mabibi harusi, kwa wale ambao mpaka sasa bado wanapewa mitoko (dating) lakini haizai matunda, kwa wale ambao wamejiondoa katika mahusiano yenye vurugu na wamefanikiwa kusonga mbele na maisha, kwa wale wenye hofu ya kuishi peke yao bila kuwa na mahusiano, kwa wale walioachwa na kukataa kufungua mioyo yao, na mwisho kwa wale ambao wamepoteza upendo na kuhisi kama kwamba kamwe hawataweza kupenda tena……………..

Nawaandikia barua hii ya wazi dada zangu wapendwa mlio single au mnaoelekea kuwa single nikiwaambia kwamba, huo sio mwisho wa dunia, na maisha bado ni zawadi kubwa kwenu na yenye thamani. Zawadi hii haipaswi tuichukulie kirahisi, kwani hutupa fursa ya kujitambua kuwa sisi ni nani na nini madhumuni ya kuwepo kwetu hapa duniani. Pale tunapopatwa na hali ya kujihisi upweke ni vyema tukawa na subira kwani mara nyingi subira hutuweka katika nafasi nzuri ya kujua kile kinachoingia na kutoka akilini mwetu.
black-woman-on-couch.jpg

Mara nyingi jamii yetu imekuwa ikiwatisha kwamba kutokuwa katika uhusiano au kutokuwa katika nafasi nzuri ya kuelekea kujenga mahusiano au kuchumbiwa au kuolewa iwapo utakuwa umefikisha umri fulani basi ni lazima utakuwa na matatizo ya kiakili, kimwili au kihisia na thamani zenu zinapungua……Ni bahati mbaya kwamba jamii mpaka sasa haimtendei haki mwanamke. Hata hivyo, kile ambacho watu wengi hushindwa kutambua ni kwamba, kuwa single ni sehemu ya maisha na inapaswa kusherehekea na kuiheshimu hali hiyo kama ilivyo pale inapotokea kuolewa. Hali hii ni lazima isherehekewe kwa sababu huu ndio wakati ambapo maarifa ya kujitambua kwamba wewe ni nani hukufanya ukue kifikra kila siku, na kuishi maisha uyapendayo na si vile watu wapendavyo uwe.

Najua wakati mwingine ni vigumu kukubaliana na hali hiyo, hasa pale muwaonapo wanandoa wanaopendana wakiwa na mtoko (dates) wakitembea huku wameshikana mikono, na ninajua ni vigumu kukubaliana na hali hiyo pale mtakapoalikwa na marafiki zenu mshiriki kwenye sherehe zao za kuvishana pete za uchumba. Pia ninajua kwamba itakuwa ni vigumu sana kwenu kukubaliana na hali hiyo, pale ambapo rafiki unayemfahamu mwenye tabia zisizofaa anapokutambulisha kwa mchumba wake unayemuona dhahiri kwamba ni mwenye tabia nzuri na mwadilifu lakini akiwa ameangukia mikononi mwa mwanamke unayemuaona dhahiri hamfai. Lakini pia utajisikia vibaya zaidi pale ambapo kila ufunguapo mitandao ya kijamii kama vile facebook na twitter unakutana na taarifa kutoka kwa baadhi ya marafiki zako wakitoa taarifa kwamba wamefunga ndoa au wamevishwa pete za uchumba…………….

Lakini hali hiyo isiwatishe kwani ni sehemu ya maisha, na hampaswi kuishi kwa kuangalia wenzenu wamepata nini bali lililo muhimu kwenu ni kuyafurahia maisha kwa sababu nyie ni binadamu kamili na mnazo sifa zote anazostahili kuwa nazo mwanamke na hampaswi kusubiri mkamilishwe na mtu yeyote………………..
 
Baada ya mahusiano mabaya, nilifurahia sana maisha ya kuwa peke yangu. Yaani uhuru, muda, pesa, friends vyote havikuwa tatizo. Weekend kwenda miji tofauti na kuenjoy bila kuulizwa (of course bila kuharibu) it was full burudani!

Lkn moyo ni kitu kingine bwana; l am in love again na kwa muda it is good lkn sijui itaendaje.

Maisha ni jinsi utakavyo na ndivyo yatakavyokuwa. Kuna furaha kwenye mahusiano kama kulivyo kusiko na commitment! Furaha ni wewe zaidi!

Thanks mtambuzi.
 
Mtambuzi, naamin ujumbe umewafikia. kwa waliokata tamaa na hata wasiojitambua
 


Baada ya mahusiano mabaya, nilifurahia sana maisha ya kuwa peke yangu. Yaani uhuru, muda, pesa, friends vyote havikuwa tatizo. Weekend kwenda miji tofauti na kuenjoy bila kuulizwa (of course bila kuharibu) it was full burudani!

Lkn moyo ni kitu kingine bwana; l am in love again na kwa muda it is good lkn sijui itaendaje.

Maisha ni jinsi utakavyo na ndivyo yatakavyokuwa. Kuna furaha kwenye mahusiano kama kulivyo kusiko na commitment! Furaha ni wewe zaidi!

Thanks mtambuzi.
 
Last edited by a moderator:
Da Marvelous.tena mtu unaweza ukawa umejiridhikia tu maisha yanaenda unakutana na mwanaume hata hakufahamu eti we mzuri hivyo mbona hujaolewa.?umeambiwa ni ticket ya kiama?Kaunga umenena am free for 3 years i can sllep any expensive hotel nikichoka kulala kwangu na nikitaka kwenda mbali mikoani i take flight?what if ningekua na jamaa miundombinu?aa life is what you make it bwana.Halafu jamii ndo huwa inaleta majungu hadi binti anaangukia kwa kwenye moto.Kila nikimwangalia dada yangu machozi yananitoka hasa nikifikiria aliamua aolewe kisa jamii.
 
Asante Mtambuzi kwa thread yako hii ambayo naamini imewatia moyo wadada wengi ambao walikuwa ktk hali ya kukataa tamaa kwa kukosa mtu wa kuolewa naye au kuwa na mahusiano ya kudumu.

Niwatie moyo wadada kuwa maisha bila ya kuolewa yanawezakana sana, na kwa kawaida hawapaswi kuharakisha au kuforce mahusiano maana Mungu aliyewaumba na kuwaleta hapa duniani amewapangia mahusiano mazuri sana ambayo kimsingi mara nyingi hupotea kwa kutokuwa wavumilivu au kuona umri unakimbia.

Ni vizuri kujipa moyo na kujiamini huku wakimuomba Mungu awaongoze kuwa na mahusiano ambayo hayatakuja kuleta majuto, ama laa wasiwe na mahusiano ya commitment endapo mwisho wake utakuwa m-baya.
Ni vizuri kutumia muda mwingi kujishughulisha na kazi na kutunza heshima na uaminifu ktk maisha yao ya kila siku. Wanaume wengi huvutiwa na wanawake wenye tabia njema kuwa wake zao na wale wenye kuruka ruka mara nyingi huishia kuwa ma-girl friend au watu wa kampani tu!

Kila la kheri wadada wote ambao mko kwenye hali ya namna hii. Tunawapenda na kuwaombea mema.
 
Back
Top Bottom