Hii ni stori ya upande mmoja of course hatujapata bado upande wa pili. Ukweli wa huyu mama utakuja kujulikana tu.
Lakini habari zinazotoka newsroom ya IPP-Media zinaonyesha kuwa mzee Mengi alimshtukia mama huyu Mdosi kwamba ni pandikizi wa wale mapapa aliyowataja akina RA. Wanavyosema wenyewe kule IPP ni kwamba alivuta mzigo kabambe kutoka kwao ili awe anawatolea siri za IPP Media nk.
Kwa hivyo Sakina sasa akiajiriwa Habari Corporation haitashangaza tusubiri tu.
Kuna uongo wa dhahiri katika barua yake hiyo ya kujiuzuru na hasa katika suala la kumkumbatia balozi wa Palestina kuwa ndiyo sababu ambayo ilimwondoa pale, kwani Mengi ana mahusiano mazuri na Israel.
Hii kaiweka kwa sababu eti tu Mengi ana uhusiano na kampuni ya Coca Cola ambayo inamilikiwa na Wayahudi. Sidhani kama sababu hii ni strong hasa ukiona bidhaa hizo za coca Cola zinavyouzwa katika nchi za Kiarabu, pamoja na sehemu za Wapalestina.
Lakini kikubwa ni kwamba Sakina katunga uongo, kwa sababu miaka kama miwili au mitatu nyuma, ITV ilitoa coverage ya tukio ambapo balozi wa zamani wa Palestina, akiandama na timu ya maripota wa ITV na Guardian walikwenda Mkuranga ku-cover tukio la kumtuza mtoto mmoja aliyezaliwa na ulemavu pale na ambaye wazazi wake walimpa jina la Arafat.
Balozi huyo alimvalisha medali yenye picha ya Arafat na pia kutoa misaada mingine ya pesa nk kwa mtoto huyo na wazazi wake. Hii coverage ilisimamiwa na Kyondo Mshana wa Guardian na ripota wengine wa ITV.
Mimi nadhani ITV itatoa hiyo footage kuonyesha jinsi balozi wa Palestina alivyokarimiwa na ITV ili ku-mprove Sakina wrong. Jee wakati huo Mengi hakuwa na uhusiano na Coca Cola?
Aidha kuna mwana JF mmoja hapo juu kasema eti Sakina amethibitisha habari kwamba Mengi anaamrisha habari zipi zitoke na zipi zisitoke kwenye magazeti. Pengine sipingi hilo, lakini ukijua jinsi RA anavyoamrisha wahariri wa magazeti yake kutoa habari anazotaka yeye, utaona ya Mengi ni cha mtoto.
Mnakijua kilichonfanya Atilio Tagalile aliyekuwa Mhariri Mkuu wake kujiuzulu? Mnakijua kilichomuondoa Rosemary Mwakitwange kama CEO wa New Habari Corporation? Ni hayo hayo kulazimisha kuwekwa kwa stori zisizokuwa na maadili kabisa - za kutetea ufisadi na mafisadi hakuna kingine. Mkiweza muulizeni Mama Mwakitwange.
RA amejaza ma-yesmen katika newsroom yake. Nani asiyejua u-spin doctor wa Muhimgo Rweyemamu, Manyerere Jackton na wengine?
Muongo mkubwa wewe,Rostam hana muda na vyombo vya habari vyake,lini uliona gazeti la Habari lina picha za Rostam? lakini Mengi kila siku ITV ina dakika 40 za habari zake na kila gazeti ni habari zake tu.
Sakina kafanya jambo zuri kuandika upuuzi wa MENGI wote humu ndani.