Zakumi
JF-Expert Member
- Sep 24, 2008
- 5,063
- 2,471
Ndugu Wazalendo,
Kwa mara ya kwanza nilimuona Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania, JK, nchi Marekani miaka mitano iliyopita katika mkutano wa waTanzania waishio Marekani ya kaskazini uliofanyika mjini Washington DC baada ya kuchaguliwa kuwa rais.
Katika mkutano huo, rais alisema alikabiliwa na mambo matatu makubwa: Ujambazi, matatizo ya umeme na mvua. Leo hii ni mwaka wa tano kamili. Tatizo la umeme bado lipo palepale. Na katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka amesema kuwa moja ya sababu za kushindwa kwa kutafutiwa ufumbuzi tatizo hilo ni kujitoa kwa mwekezaji kwa sababu ya matatizo ya uchumi wa kidunia. Ifuatayo ni maoni yangu kwa ndugu rais.
Ndugu rais, ngoja nikupe vipande vyangu vya mawazo. Kama Ndugu Basil Mramba aliweza kusema kuwa ndege ya rais ni lazima kununuliwa hata kama wananchi watakula nyasi. Na mimi nakwambia kuwa watanzania tunao uwezo wa kujenga mitambo ya umeme hata kama gharama zake zitatufanya tule udongo.
Na kwa kutumia msemo wa baba wa taifa kuhamasisha watanzania kupigana vita. Nitasema uwezo wa kujenga mitambo tunao, sababu ya kujenga mitambo zipo. Kinachoshindikana ni nia ya nyinyi viongozi kuwa waadilifu na wakweli.
Vifuatazo ni sababu za kuonyesha kuwa uwezo na sababu kuwa tunazo. Idadi ya watanzania ni 40milioni wenye vipato vyenye kutofautiana. Pamoja na tofauti yao, wapo watanzania wenye kipato cha kuweza kuchangia ujenzi wa vinu vya uwezo tofauti. Kwa kuanzia watanzania wanaweza kuchangia kinu cha 40MW. Na mafanikio ya kinu hicho yatahamasisha watu kuchangia vinu vyenye uwezo mkubwa.
Najua mtashangaa ni jinsi gani watu wanaweza kuchangia. Tanzania tunalo soko la share, Dar Es Salaam Stock Exchange. Ianzishwe kampuni ya wenye SHARE na yenye kuongozwa na wazalendo waadilifu na wenye kuaminika. Na baada ya hapo zitangazwe share. Manunuzi ya share hizo zitumike kujenga kinu. Mapato yatakayotokana na uzalishaji wa umeme wa kinu hicho yarudi kwa wawekezaji na vilevile yatumike kuongeza tija ya kampuni hilo.
Ndugu rais umetumia miaka mitano mitakatifu kuzunguka duniani kutafuta wawekezaji. Ukweli wa mambo wawekezaji wengi waliopo nje watafanya yale niliyokwambia. Watachukua pesa kutoka kwenye mifuko ya share, au mifuko ya kustaafu na kuleta mitambo Tanzania. Na sababu ya mwekezaji kujitoa kwenye mradi wa Mtwara ni kushindwa kupata pesa kwenye mifuko mbalimbali kutoka mifuko hiyo kuathiriwa na matatizo ya uchumi.
Sioni sababu ya mwekezaji kuja na mtaji na kupata faida ya zaidi ya 25% kwa pesa zitokanazo stocks, mifuko ya uwekezaji au mifuko ya kustaafu. Hiyo mifuko inaweza kuchangiwa hapohapo na faida kubaki hapohapo Tanzania. Hivyo kwanini mzunguke nje kutafuta misaada na wawekezaji wakati mkijisafisha tu katika safu zenu vitu hivyo vitapatikana hapo hapo nyumbani?
Ndugu rais sababu za kuwa mitambo ya umeme hipo. Kwanza umeme ni biashara nzuri na yenye kuitajiwa na watanzania wengi. Utaongeza matumizi mazuri ya gesi na makaa ya mawe na kutoa ajira kwa watanzania. Utaimarisha ubora wa maisha yetu.
Nia ya kununua share hazipo kwa sababu ya uongozi mbaya toka tumepata uhuru. Siku zote viongozi wetu mmetufanya watanzania kuwa ni watu wa kufanya vitu vidogovidogo tu. Mkitaka ujenzi wa shule au uwanja wa michezo mtatulazimisha tuchangie. Lakini kwenye vitu vya maana mnaona kutembeza mabakuli nje ya nchi ni sifa kubwa sana.
Vilevile mnaogopa kutuchangisha kwenye miradi mikubwa kwa sababu mnaogopa kuwa mkishindwa tutaandamana pale mkiboronga. Wale wazee waliofanya kazi kwenye shirikisho la Afrika mashariki wanawasumbua. Hivyo mnaogopa kuchukua dhamana, kwa sababu nikitoa mchango wangu mkubwa na ukashindwa kuleta umeme nitakufanyizia kwa njia yoyote hile. Iwe kwe uchaguzi, uchawi, au sayansi nitakufanyizia tu.
Ndugu rais kama tungekuwa na uongozi imara katika mambo ya biashara, ninakuakikishia kuwa watanzania wanao uwezo wa kununua share zenye uwezo wa kuanzisha kampuni la kuzalisha umeme. Na kama wazo ili lingeanza miaka mitano iliyopita, kwa sasa hivi taifa lisingekuwa kwenye matatizo ya umeme.
Wako katika ujenzi wa taifa,
Za10
Kwa mara ya kwanza nilimuona Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania, JK, nchi Marekani miaka mitano iliyopita katika mkutano wa waTanzania waishio Marekani ya kaskazini uliofanyika mjini Washington DC baada ya kuchaguliwa kuwa rais.
Katika mkutano huo, rais alisema alikabiliwa na mambo matatu makubwa: Ujambazi, matatizo ya umeme na mvua. Leo hii ni mwaka wa tano kamili. Tatizo la umeme bado lipo palepale. Na katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka amesema kuwa moja ya sababu za kushindwa kwa kutafutiwa ufumbuzi tatizo hilo ni kujitoa kwa mwekezaji kwa sababu ya matatizo ya uchumi wa kidunia. Ifuatayo ni maoni yangu kwa ndugu rais.
Ndugu rais, ngoja nikupe vipande vyangu vya mawazo. Kama Ndugu Basil Mramba aliweza kusema kuwa ndege ya rais ni lazima kununuliwa hata kama wananchi watakula nyasi. Na mimi nakwambia kuwa watanzania tunao uwezo wa kujenga mitambo ya umeme hata kama gharama zake zitatufanya tule udongo.
Na kwa kutumia msemo wa baba wa taifa kuhamasisha watanzania kupigana vita. Nitasema uwezo wa kujenga mitambo tunao, sababu ya kujenga mitambo zipo. Kinachoshindikana ni nia ya nyinyi viongozi kuwa waadilifu na wakweli.
Vifuatazo ni sababu za kuonyesha kuwa uwezo na sababu kuwa tunazo. Idadi ya watanzania ni 40milioni wenye vipato vyenye kutofautiana. Pamoja na tofauti yao, wapo watanzania wenye kipato cha kuweza kuchangia ujenzi wa vinu vya uwezo tofauti. Kwa kuanzia watanzania wanaweza kuchangia kinu cha 40MW. Na mafanikio ya kinu hicho yatahamasisha watu kuchangia vinu vyenye uwezo mkubwa.
Najua mtashangaa ni jinsi gani watu wanaweza kuchangia. Tanzania tunalo soko la share, Dar Es Salaam Stock Exchange. Ianzishwe kampuni ya wenye SHARE na yenye kuongozwa na wazalendo waadilifu na wenye kuaminika. Na baada ya hapo zitangazwe share. Manunuzi ya share hizo zitumike kujenga kinu. Mapato yatakayotokana na uzalishaji wa umeme wa kinu hicho yarudi kwa wawekezaji na vilevile yatumike kuongeza tija ya kampuni hilo.
Ndugu rais umetumia miaka mitano mitakatifu kuzunguka duniani kutafuta wawekezaji. Ukweli wa mambo wawekezaji wengi waliopo nje watafanya yale niliyokwambia. Watachukua pesa kutoka kwenye mifuko ya share, au mifuko ya kustaafu na kuleta mitambo Tanzania. Na sababu ya mwekezaji kujitoa kwenye mradi wa Mtwara ni kushindwa kupata pesa kwenye mifuko mbalimbali kutoka mifuko hiyo kuathiriwa na matatizo ya uchumi.
Sioni sababu ya mwekezaji kuja na mtaji na kupata faida ya zaidi ya 25% kwa pesa zitokanazo stocks, mifuko ya uwekezaji au mifuko ya kustaafu. Hiyo mifuko inaweza kuchangiwa hapohapo na faida kubaki hapohapo Tanzania. Hivyo kwanini mzunguke nje kutafuta misaada na wawekezaji wakati mkijisafisha tu katika safu zenu vitu hivyo vitapatikana hapo hapo nyumbani?
Ndugu rais sababu za kuwa mitambo ya umeme hipo. Kwanza umeme ni biashara nzuri na yenye kuitajiwa na watanzania wengi. Utaongeza matumizi mazuri ya gesi na makaa ya mawe na kutoa ajira kwa watanzania. Utaimarisha ubora wa maisha yetu.
Nia ya kununua share hazipo kwa sababu ya uongozi mbaya toka tumepata uhuru. Siku zote viongozi wetu mmetufanya watanzania kuwa ni watu wa kufanya vitu vidogovidogo tu. Mkitaka ujenzi wa shule au uwanja wa michezo mtatulazimisha tuchangie. Lakini kwenye vitu vya maana mnaona kutembeza mabakuli nje ya nchi ni sifa kubwa sana.
Vilevile mnaogopa kutuchangisha kwenye miradi mikubwa kwa sababu mnaogopa kuwa mkishindwa tutaandamana pale mkiboronga. Wale wazee waliofanya kazi kwenye shirikisho la Afrika mashariki wanawasumbua. Hivyo mnaogopa kuchukua dhamana, kwa sababu nikitoa mchango wangu mkubwa na ukashindwa kuleta umeme nitakufanyizia kwa njia yoyote hile. Iwe kwe uchaguzi, uchawi, au sayansi nitakufanyizia tu.
Ndugu rais kama tungekuwa na uongozi imara katika mambo ya biashara, ninakuakikishia kuwa watanzania wanao uwezo wa kununua share zenye uwezo wa kuanzisha kampuni la kuzalisha umeme. Na kama wazo ili lingeanza miaka mitano iliyopita, kwa sasa hivi taifa lisingekuwa kwenye matatizo ya umeme.
Wako katika ujenzi wa taifa,
Za10