Infopaedia
JF-Expert Member
- Oct 28, 2011
- 1,231
- 1,487
Kampuni ya African Barrick Gold imeusimamisha mgodi wake wa Bulyanhulu kwa masaa 48, kuanzia jioni ya August 1st. Uongozi wa Bulyanhulu umechukuwa uamuzi huo jioni hii baada ya mgomo wa siku mbili wa wafanyakazi. Mgomo huo ambao ulianza jana asubuhi July 31st ulisababishwa na sheria ya kufuta fao la kujitoa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii. Baada ya wafanyakazi kuona uongozi wa Barrick Bulyanhulu umelala sana na hakuna jitihada zozote za kupata official reports from SSRA. Jana asubuhi wafanyakazi wakaamuwa kuanzisha mgomo mpaka hapo watakapoitiwa watendaji wa juu wa SSRA ili waelezwe na wafafanuliwa juu ya mafao yao na wao kutoa kilio chao juu ya hiyo sheria mpya. Baada ya wafanyakazi kukusanyika na kujadili. Ilionekana ni bora aje mbunge Jafu ambaye anakusanya maoni, au Waziri wa Kazi. Lakini uongozi ulifanya jitihada na kumleta Afisa uhusiano wa SSRA toka Dar office. Afisa uhusiano aliondoka bila kutowa jawabu la kuridhisha kwa wafanyakazi. Hivyo wafanyakazi waliamuwa waendelee na mgomo mpaka atakapoletwa Jafu au waziri mwenye dhamana. Hivyo wafanyakazi wakaendelea na mgomo mpaka wakati wa kutoka jioni. Jioni waliukabidhi mgomo kwa wafanyakazi wa zamu ya usiku. Zamu ya usiku waliupokea mgomo kwa mikoni miwili na kuahidi mgomo watauendeleza mpaka asubuhi na kuwarudishia waasisi wa mgomo huo. Kweli bwana, pamoja na vitisho vyote toka utawala, lakini jamaa wa usiku waliendelea kukaza uzi mpaka asubuhi. Ilipofika leo asubuhi, waanzilishi wa mgomo walikuja kupokea mgomo wao. Shift ya leo asubuhi iliendelea na mgomo huku mijadala na uongozi ikiwa inaendelea. Lakini wafanyakazi wakashikilia uamuzi wao wa kuonana na Jafu ama waziri mwenye dhamana. Ulipofika muda kama wa saa kumi na moja jioni, uongozi ukatoa taarifa kwa wafanyakazi wote. Kwamba uongozi umeamuwa kusimamisha shughuli za uchimbaji kwa masaa 48 kuanzia muda huo wa jioni. Wafanyakazi ambao ilibidi waingie kwa zamu ya usiku jioni hii hawakuingia kazini. Na waliokuwepo walirudi nyumbani kusubiri kwa masaa 48. Nje ya geti wafanyakazi walikuta police wakiwa wametawanywa. Lakini hakukuwa na tukio lolote la vurugu ama utumiaji nguvu. Wafanyakazi waliingia kwenye ma-bus ya kampuni na kurudi nyumbani kwa amani.
Source: Shuhuda wa tukio.
Source: Shuhuda wa tukio.