Barrick Gold wants tax refund from Tanzania Government!

Na bado wana airport ndani ya migodi, so we are not sure kama kweli hawasafirishi madini bila kuya account. Kaazi kweli kweli.

Hawa Jamaa hawata kaa na kuripoti faida hata siku moja kwenye mahesabu yao. Mimi nimeshakuwa consultant katika migodi ya Barrick and Angro, hawa ni wahuni sana. Wanatransfer faida mapema sana kwa kutumia manunuzi. Yaani wananunua spares na Equipment toka kwenye makampuni tanzu yao kwa bei za juu sana. As a result wanakuza expenses kwenye mahesabu, na kushusha faida. Mara nyingi wanatumia sana non tangible assets kama Computer Softwares na kadhalika, ambazo wanajua TRA au Watz wanashindwa kujua gharama halisi. Utakuta wanaweza kubadili software kila mwaka. Wanatumia consultancy services za kutoka kwenye kampunzi tanzu zao kwa bei kubwa hata kama utaalamu huo unaweza kupatikana nchini. Tatizo la Viongozi wetu hata ukiwatonya, ndio kwanza wao wanaenda kuvujisha siri iliwavute chochote. Kutrace hasabe zao ni vigumu sana kwani Ofisi za wahasibu zinafanywa nje ya nchi, hapa wahasibu kazi yao ni kuscan document na kusend basi.
 
Hapa dawa ni ku nationalize kama alivyofanya Hugo Shavez full stop! Maana kama hakuna faida kwa nini wanaendelea kununua new projects? Hata mtoto mdogo huwezi kumdanganya. Barrick kwa sasa ana migodi zaidi ya minne Tz kwa nini na hakuna faida. Kwa nini ana keep on investing?
 
Shamba la bibi hilooooooooo!!!!

Yaani haki ya nani unaweza kupatwa hasira mpaka ukashindwa ufanyeje! Utafikiri hatuna wasomi nchi hii, yaani watu wetu wa sheria usingizi tu! Inakuwaje wanasaini mikataba mibovu mibovu kama hii?? Eti unapewa mrahaba wa 3% halafu unawarudishia fedha yao waliyotumia kuzalishia umeme kwenye migodi yao, utafikiri umeme huo walikuwa wanauingiza kwenye grid ya Taifa ili wananchi nao wafidike. Haki ya nani nji hii hatuna Rais bali tuna mfano wa Rais.

Hata Mibunge yetu nayo hamzo!! Hivi hamwezi hata mkaiga kidogo tu kwa wenzetu Wa-Kenya? Eti akina Maji marefu nao Wabunge hivi hapo tutegemee nini kama siyo kupitisha mikataba fake kama hii!!!!!!
 
Mungu tunusuru na huu wizi wa mchana kweupe

Sijui kama kuna kunusurika kama CCM itaendelea kuwepo madarakani, labda wabadilike na kuamua kuanza kutetea maslahi ya nchi vinginevyo hali itaendelea kwa miaka mingi.
 
Wizi sasa umekufuru! Yote haya yanasababishwa ba viongozi wapumbavu ambao wanaingamiza nchi yetu mchana kweupe!! Hawa Barrick kwa kuchukua madini yetu bure kabisa nao wapo tayari kuongeza mrahaba wa 3% toka walipoanza kuchimba madini yetu hadi sasa? Je, wapo tayari kuilipa Tanzania baadhi ya faida kubwa waliyopata tangu waingie nchini wakati bei ya dhahabu ilikuwa $260 na sasa imefikia zaidi ya $1,500. Nashangaa kusikia hata Serikali imekubali kukaa nao chini eti kuwalipa refund ya $273.9 million! Hawa wanaosaini hii mikataba ni wendawazimu kabisa.

Hawa jamaa ni noma
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom