Baregu: CUF wamelizwa tena Z'bar

Regia Mtema

R I P
Nov 21, 2009
2,970
863
na Deogratius Temba

MWELEKEO wa Chama cha Wananchi (CUF) kufanikiwa katika jitihada za kupata nafasi ya kushika madaraka, huenda ukagonga mwamba kutokana na uamuzi wa Baraza la Wawakilishi kutaka kuitisha kura za maoni kuamua hatma hiyo.

Pamoja na makubaliano yaliyofikiwa kwa kupitishwa na kuungwa mkono kwa hoja hiyo ndani ya Baraza la Wawakilishi, baadhi ya wadau wa siasa wana hofu kwamba huenda utekelezaji wake utakuwa mgumu kutokana na muda uliobaki.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano kwa nyakati tofauti umebaini kuwa, kuna uwezekano mkubwa mchakato wa kura za maoni unaotarajiwa kufanyika kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, kukwama au kuahirishwa.

Sababu ambazo zinatajwa kuwa zinaweza kuukwamisha mpango huo ni muda wa kupiga kura za maoni uliowekwa ambao ni kabla ya Oktoba mwaka huu, muda wa kubadilisha Katiba ya Zanzibar ili iruhusu serikali ya mseto na chombo cha kusimamia kura za maoni kitakachokuwa huru na orodha ya wapiga kura itakayotumika.

Pia wachambuzi wa siasa wanadai kuwa hoja ya Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff aliyoitaka siyo kuingia kwenye kura za maoni kwani suala hilo alilipinga Machi baada ya maazimio ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), kupendekeza hivyo katika mkutano wake wa Butiama.

Kwa upande mwingine inaelezwa kwamba hoja ya kiongozi wa upinzani katika baraza hilo, Aboubakar Khamis Bakar (CUF), iliyoungwa mkono na Baraza la Wawakilishi, haikutoa kile alichokuwa akikidai Maalim Seif, kwani alitaka Rais Amani Abeid Karume aongezewe muda baada ya kubadilisha katiba.

Aliyekuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mchambuzi wa masuala ya siasa barani Afrika, Profesa Mwesiga Baregu, akizungumza na Tanzania Daima Jumatano jana, alionyesha wasiwasi wake juu ya kufanikiwa kwa suala hilo kama ilivyopangwa.

“Hatua zozote zinazochukuliwa visiwani Zanzibar ni lazima ziwe za busara ili tusirudi kule tulikotoka. Ninashukuru kuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamekubali kuwa kitu kimoja na kukubali maazimio ya CCM Butiama, ambayo hapo awali CUF waliyapinga.

“Lakini katika kura za maoni ni lazima matokeo yake yawe ya kuaminika, na je tuna chombo cha kusimamia kura za maoni ili wasiibiwe? Suala hilo liwekwe kwa uangalifu, tusikurupuke kusema tunaenda kwenye kura za maoni halafu tukakwama kwa sababu mambo hayajakamilika na tukaahirisha uchaguzi itakuwa aibu. Suala hili lifanyike kwa umakini na kuaminiana,” alisema Profesa Baregu.

Alisema suala la Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) linakwenda sambamba na mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar ili iruhusu serikali ya mseto na yote yafanyike kwa njia ambayo haitaweza kufanya nchi kurudi kwenye migogoro.

Aidha alionyesha wasiwasi wake kwenye muda uliobaki ili kuingia katika uchaguzi huo na kufanya matukio yote kwa muda uliobaki kwani wahusika wasipokuwa makini, wanaweza kukwama.


Kazi kwenu wana CUF,jasho litawatoka mwaka huu
 
Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) amesema kura ya maoni ya kuamua Zanzibar kuunda serikali ya mseto ifanyike siku moja na uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.

Mkurugenzi wa ZEC, Salum Kassim Ali, alipokuwa akizungumza na Nipashe baada ya Baraza la Wawakilishi kupitisha hoja binafsi na kutaka kura ya maoni kuhusu serikali ya mseto iwe imefanyika kabla ya uchaguzi wa mwaka huu.

Alisema kura ya maoni ni jambo linalohitaji gharama na wananchi kupewa elimu ya kutosha wakati muda uliobakia kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu ni mdogo hivyo kuna haja ya kazi hizo kufanyika kwa wakati mmoja. Alisema ZEC inahitji muda wa miezi minne wa kutoa elimu ya uraia kwa wananchi kabla ya kura hiyo.

Aidha, alisema suala hilo linahitaji fedha za kutosha jambo ambalo linahitaji kuangaliwa kwa umakini hasa kwa kuzingatia uchumi wa Zanzibar utaathirika kwa kiwango kikubwa kutokana na athari ya kukosekana kwa umeme.

Alisema elimu ya uraia ni jambo la msingi kabla ya kufanyika kura hiyo ili wananchi wa Unguja na Pemba waweze kutoa maamuzi yatakayosaidia kujenga nchi na kuimarisha umoja wa kitaifa.

Alisema wananchi wa Zanzibar watapata usumbufu mkubwa iwapo kura ya maoni itafanyika siku tofauti na siku ya uchaguzi kwa vile mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi na watalazimika kupiga kura zisizopungua sita.

Alitaja kura watakazolazimika kupiga mwaka huu kwanza kuchagua wagombea ndani ya vyama vyao, kupiga kura kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa, kuchagua Rais wa Zanzibar, wawakilishi na madiwani kabla ya kushiriki kura ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano na wabunge.

Alisema zoezi la kura ya maoni kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa linakabiliwa na changamoto nyingi kwa vile hadi sasa haijafahamika ni daftari gani litatumika kati ya daftari la wapiga kura wa kudumu la ZEC au daftari la vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi.

Alisema Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi watapaswa kueleza hilo katika marekebisho ya sheria namba 11 ya ZEC yanayotarajia kufanyika ili wananchi waelewe kuhusiana na suala hilo.

CHANZO: NIPASHE

Ukisikia changa la macho laja ndio hili sasa kweli zanzibar maskini mmungu atusaidie!!!!!
 
na Deogratius Temba

MWELEKEO wa Chama cha Wananchi (CUF) kufanikiwa katika jitihada za kupata nafasi ya kushika madaraka, huenda ukagonga mwamba kutokana na uamuzi wa Baraza la Wawakilishi kutaka kuitisha kura za maoni kuamua hatma hiyo.

Pamoja na makubaliano yaliyofikiwa kwa kupitishwa na kuungwa mkono kwa hoja hiyo ndani ya Baraza la Wawakilishi, baadhi ya wadau wa siasa wana hofu kwamba huenda utekelezaji wake utakuwa mgumu kutokana na muda uliobaki.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano kwa nyakati tofauti umebaini kuwa, kuna uwezekano mkubwa mchakato wa kura za maoni unaotarajiwa kufanyika kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, kukwama au kuahirishwa.

Sababu ambazo zinatajwa kuwa zinaweza kuukwamisha mpango huo ni muda wa kupiga kura za maoni uliowekwa ambao ni kabla ya Oktoba mwaka huu, muda wa kubadilisha Katiba ya Zanzibar ili iruhusu serikali ya mseto na chombo cha kusimamia kura za maoni kitakachokuwa huru na orodha ya wapiga kura itakayotumika.

Pia wachambuzi wa siasa wanadai kuwa hoja ya Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff aliyoitaka siyo kuingia kwenye kura za maoni kwani suala hilo alilipinga Machi baada ya maazimio ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), kupendekeza hivyo katika mkutano wake wa Butiama.

Kwa upande mwingine inaelezwa kwamba hoja ya kiongozi wa upinzani katika baraza hilo, Aboubakar Khamis Bakar (CUF), iliyoungwa mkono na Baraza la Wawakilishi, haikutoa kile alichokuwa akikidai Maalim Seif, kwani alitaka Rais Amani Abeid Karume aongezewe muda baada ya kubadilisha katiba.

Aliyekuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mchambuzi wa masuala ya siasa barani Afrika, Profesa Mwesiga Baregu, akizungumza na Tanzania Daima Jumatano jana, alionyesha wasiwasi wake juu ya kufanikiwa kwa suala hilo kama ilivyopangwa.

“Hatua zozote zinazochukuliwa visiwani Zanzibar ni lazima ziwe za busara ili tusirudi kule tulikotoka. Ninashukuru kuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamekubali kuwa kitu kimoja na kukubali maazimio ya CCM Butiama, ambayo hapo awali CUF waliyapinga.

“Lakini katika kura za maoni ni lazima matokeo yake yawe ya kuaminika, na je tuna chombo cha kusimamia kura za maoni ili wasiibiwe? Suala hilo liwekwe kwa uangalifu, tusikurupuke kusema tunaenda kwenye kura za maoni halafu tukakwama kwa sababu mambo hayajakamilika na tukaahirisha uchaguzi itakuwa aibu. Suala hili lifanyike kwa umakini na kuaminiana,” alisema Profesa Baregu.

Alisema suala la Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) linakwenda sambamba na mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar ili iruhusu serikali ya mseto na yote yafanyike kwa njia ambayo haitaweza kufanya nchi kurudi kwenye migogoro.

Aidha alionyesha wasiwasi wake kwenye muda uliobaki ili kuingia katika uchaguzi huo na kufanya matukio yote kwa muda uliobaki kwani wahusika wasipokuwa makini, wanaweza kukwama.


Kazi kwenu wana CUF,jasho litawatoka mwaka huu
Tulisha sema mapema kwamba wasije wanalialia tena hapa kuwa wameibiwa au kuonewa.
Kafu hawaishi kulia lia we subiri tu si muda mrefu wataaza kupita na kupiga kelele.
Karagabaho.
 
Hapana, hapa CCM ndiyo wanacheza rafu na pia inaweza ikawageuka! Lets wait and see!!
 
Cuf has no choice but press for this kind of "resolution". Baada ya uchaguzi CUF walisema hawamtambui Karume. Consequently, waligoma kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura. Sasa uchaguzi mwingine unakuja na wao hawajiandikisha na zoezi hilo supposedly limeshafungwa kwa hiyo kura zao zitatoka wapi? Ni lazima wajiingize kwenye coalition kama hii ya serikali ya mseto ili angalau wapate some representation kwani kwenye ballot box wamefulia big time.

BTW, where is Chairman Lipumba? Katika malumbano yoooote haya kuhusiana na hili yeye amekaa kimya - ajua jambo fulani wengine hatulijui?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom