Kakke
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,883
- 1,482
Kero za Muungano Zatawala Mjadala wa Bajeti
Muwakilishi wa Kwantipura Hamza Hassan
Na Mwantanga Ame
HUKU wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakijadili bajeti ya mwaka wa fedha wa 2012/2013, kilio cha kero za Muungano kimetawala na kutikisa michango ya wajumbe wa Baraza hilo.
Wajumbe hao walisema kuwa kero za Muungano zimekuwa kero kubwa kwa uchumi wa Zanzibar na kwamba zinahitaji kurekebishwa hivi sasa badala ya kusubiri mchakato wa katiba mpya.
Akichangia bajeti hiyo, Mwenyekiti wa kamati ya Wenyeviti wa Baraza la Wawakilishi, Hamza Hassan Juma (Kwamtipura), alisema kuwa serikali inapaswa kuja na majibu mazuri juu ya namna ya kero za Muungano zitakavyomalizwa, kwani zinakandamiza uchumi wa Zanzibar.
Hamza alisema inasikitisha kuona serikali ya Muungano hivi sasa imekuwa na mambo mbali mbali ya serikali inayotakiwa kuyafanyia kazi lakini hakuna lililofanyika wakati serikali ya Muungano ikiwa inatekeleza vyema matakwa yake.
Mwenyekiti huyo alisema serikali ya Zanzibar inakosa majibu juu ya suala la mgao wa Muungano wa asilimia 4.5 ambao kwa muda mrefu yametolewa mapendekezo ya asilimia 11.5 lakini BOT bado halijatekelezeka hadi sasa.
Alisema jambo linaloshangaza kuona baada ya kupelekwa mapendekezo hayo serikali ya Muungano imeipatia gawio la asilimia 7.8 huku kukiwa hakuna muendelezo wa hatma ya suala hilo.
Alisema kuwapo kwa gawio hilo limeifanya serikali ya Zanzibar wakati ikisubiri suala hilo kumalizwa katika vikao vya kero za Muungano imekuwa ikikosa shilingi bilioni 7,000,000,000 kati ya shilingi bilioni 15, ambazo zilitakiwa kuingia katika mfuko wa hazina ya Zanzibar kama hilo lingekuwa limemalizwa.
Suali jengine linaloonesha kutokuwepo kwa utayari wa serikali ya Muungano kulifanyia kazi kwa haraka, ni kodi ya mishahara ya wafanyakazi wa Muungano ambao wanafanya kazi hapa Zanzibar ambapo inakosa shilingi bilioni 18.
Alisema kama mambo hayo yangeliweza kutolewa maamuzi ya haraka, kwa kiasi kikubwa zingeweza kuisaidia serikali ya Zanzibar kupata gawio lake kwa miaka mingi badala ya hivi sasa kuendelea kutolewa kwa fedha hizo kama ni huruma.
Aidha alisema kero pia ziko katika suala la elimu ya Juu ambapo serikali ya Zanzibar itapaswa kuona inadai serikali ya Muungano kwa mwaka ujao wa fedha kupatiwa asilimia ya gawio la Zanzibar ikiwa ni hatua itayoweza kujipanga vyema katika kutoa elimu ya juu.
Mwenyekiti huyo, aliikosoa bajeti hiyo, kwa kueleza kuwa kodi ya umeme ambapo alisema inaweza ikachangia kuongeza gharama za maisha kwa wananchi na kuiomba serikali kuiondoa hadi kamati ya Baraza la Wawakilishi litapomaliza kufanya uchunguzi wake katika shirika la Umeme.
Kutokana na hali hiyo Mwenyekiti huyo aliishauri serikali kufikiria kuwaangalia watendaji wake kwa kuhakikisha wanawatumikia wananchi huku serikali ikawachukulia hatua za kinidhamu wanaotajwa kuibia serikali.
Aidha, Mwenyekiti huyo pia alieleza dhamira ya Kamati hiyo kutaka kuwasilisha maombi ya kuifanyia uchunguzi Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) baada ya kujionesha baadhi ya Watendaji katika kitengo cha Bandarini kuonekana kujihusisha na uvujaji wa mapato.
Eneo jengine ambalo kamati hiyo imetishia kuizuia bajeti hiyo ni juu ya suala la ajira kwa vijana kutokana na hivi sasa kuwepo kwa taarifa za wageni kuajiriwa kwa wingi katika mahoteli ya kitalii huku Wazanzibari wakikoseshwa nafasi hizo.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Uzini (CCM), Mohammed Raza alisema uchumi wa Zanzibar unaweza ukakosa kunawiri ikiwa baadhi ya mambo yakiachiwa moja kwa moja kutekelezwa na serikali ya Muungano likiwemo suala la kujiunga na taasisi ya kimataifa ya Kiislamu (OIC).
Aidha Mwakilishi huyo alihoji juu ya suala la Afrika Mashariki nalo linahitaji kuangaliwa katika haki ambazo itaweza kuzipata kama Zanzibar bila ya kuingia kama ipo chini ya mwamvuli wa Tanzania.
Naye Mwakilishi wa Kitope Makame Mshimba Mbarouk alisema serikali itapaswa kujiangalia katika miradi ya uwekezaji kutokana na baadhi ya wawekezaji kufutiwa miradi yao ikiwa analipia gharama kubwa na kupewa watu wanaolipiwa kiasi kidogo cha fedha.
Alisema hivi sasa kuna watu wamekuwa wakiondolewa kwa chuki katika baadhi ya miradi hiyo jambo ambalo linapoteza imani ya wawekezeji kuwekeza Zanzibar na kuahidi kuizuiya bajeti hiyo hadi atapopewa maelezo ya kija juu ya suala hilo.
Nae Mwakilishi wa Chonga (CUF), Abdalla Juma Abdalla, aliiomba serikali kuona inatekeleza vyema bajeti hiyo na kuahidi kuwa hatoacha kuiziya hadi atapopewa maelezo ya kina kutokana na kujitokeza mambo mbali mbali katika serikali.
Mwakilishi wa Ziwani, Rashid Seif, akitoa mchango wake aliitaka serikali kuona inajipanga vyema katika suala la kusimamia sekta ya elimu kutoka an akuanza kuonekana eneo hilo huenda kukawa na wajanja wanaotumia vibaya nafasi zao.
Muwakilishi wa Kwantipura Hamza Hassan
Na Mwantanga Ame
HUKU wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakijadili bajeti ya mwaka wa fedha wa 2012/2013, kilio cha kero za Muungano kimetawala na kutikisa michango ya wajumbe wa Baraza hilo.
Wajumbe hao walisema kuwa kero za Muungano zimekuwa kero kubwa kwa uchumi wa Zanzibar na kwamba zinahitaji kurekebishwa hivi sasa badala ya kusubiri mchakato wa katiba mpya.
Akichangia bajeti hiyo, Mwenyekiti wa kamati ya Wenyeviti wa Baraza la Wawakilishi, Hamza Hassan Juma (Kwamtipura), alisema kuwa serikali inapaswa kuja na majibu mazuri juu ya namna ya kero za Muungano zitakavyomalizwa, kwani zinakandamiza uchumi wa Zanzibar.
Hamza alisema inasikitisha kuona serikali ya Muungano hivi sasa imekuwa na mambo mbali mbali ya serikali inayotakiwa kuyafanyia kazi lakini hakuna lililofanyika wakati serikali ya Muungano ikiwa inatekeleza vyema matakwa yake.
Mwenyekiti huyo alisema serikali ya Zanzibar inakosa majibu juu ya suala la mgao wa Muungano wa asilimia 4.5 ambao kwa muda mrefu yametolewa mapendekezo ya asilimia 11.5 lakini BOT bado halijatekelezeka hadi sasa.
Alisema jambo linaloshangaza kuona baada ya kupelekwa mapendekezo hayo serikali ya Muungano imeipatia gawio la asilimia 7.8 huku kukiwa hakuna muendelezo wa hatma ya suala hilo.
Alisema kuwapo kwa gawio hilo limeifanya serikali ya Zanzibar wakati ikisubiri suala hilo kumalizwa katika vikao vya kero za Muungano imekuwa ikikosa shilingi bilioni 7,000,000,000 kati ya shilingi bilioni 15, ambazo zilitakiwa kuingia katika mfuko wa hazina ya Zanzibar kama hilo lingekuwa limemalizwa.
Suali jengine linaloonesha kutokuwepo kwa utayari wa serikali ya Muungano kulifanyia kazi kwa haraka, ni kodi ya mishahara ya wafanyakazi wa Muungano ambao wanafanya kazi hapa Zanzibar ambapo inakosa shilingi bilioni 18.
Alisema kama mambo hayo yangeliweza kutolewa maamuzi ya haraka, kwa kiasi kikubwa zingeweza kuisaidia serikali ya Zanzibar kupata gawio lake kwa miaka mingi badala ya hivi sasa kuendelea kutolewa kwa fedha hizo kama ni huruma.
Aidha alisema kero pia ziko katika suala la elimu ya Juu ambapo serikali ya Zanzibar itapaswa kuona inadai serikali ya Muungano kwa mwaka ujao wa fedha kupatiwa asilimia ya gawio la Zanzibar ikiwa ni hatua itayoweza kujipanga vyema katika kutoa elimu ya juu.
Mwenyekiti huyo, aliikosoa bajeti hiyo, kwa kueleza kuwa kodi ya umeme ambapo alisema inaweza ikachangia kuongeza gharama za maisha kwa wananchi na kuiomba serikali kuiondoa hadi kamati ya Baraza la Wawakilishi litapomaliza kufanya uchunguzi wake katika shirika la Umeme.
Kutokana na hali hiyo Mwenyekiti huyo aliishauri serikali kufikiria kuwaangalia watendaji wake kwa kuhakikisha wanawatumikia wananchi huku serikali ikawachukulia hatua za kinidhamu wanaotajwa kuibia serikali.
Aidha, Mwenyekiti huyo pia alieleza dhamira ya Kamati hiyo kutaka kuwasilisha maombi ya kuifanyia uchunguzi Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) baada ya kujionesha baadhi ya Watendaji katika kitengo cha Bandarini kuonekana kujihusisha na uvujaji wa mapato.
Eneo jengine ambalo kamati hiyo imetishia kuizuia bajeti hiyo ni juu ya suala la ajira kwa vijana kutokana na hivi sasa kuwepo kwa taarifa za wageni kuajiriwa kwa wingi katika mahoteli ya kitalii huku Wazanzibari wakikoseshwa nafasi hizo.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Uzini (CCM), Mohammed Raza alisema uchumi wa Zanzibar unaweza ukakosa kunawiri ikiwa baadhi ya mambo yakiachiwa moja kwa moja kutekelezwa na serikali ya Muungano likiwemo suala la kujiunga na taasisi ya kimataifa ya Kiislamu (OIC).
Aidha Mwakilishi huyo alihoji juu ya suala la Afrika Mashariki nalo linahitaji kuangaliwa katika haki ambazo itaweza kuzipata kama Zanzibar bila ya kuingia kama ipo chini ya mwamvuli wa Tanzania.
Naye Mwakilishi wa Kitope Makame Mshimba Mbarouk alisema serikali itapaswa kujiangalia katika miradi ya uwekezaji kutokana na baadhi ya wawekezaji kufutiwa miradi yao ikiwa analipia gharama kubwa na kupewa watu wanaolipiwa kiasi kidogo cha fedha.
Alisema hivi sasa kuna watu wamekuwa wakiondolewa kwa chuki katika baadhi ya miradi hiyo jambo ambalo linapoteza imani ya wawekezeji kuwekeza Zanzibar na kuahidi kuizuiya bajeti hiyo hadi atapopewa maelezo ya kija juu ya suala hilo.
Nae Mwakilishi wa Chonga (CUF), Abdalla Juma Abdalla, aliiomba serikali kuona inatekeleza vyema bajeti hiyo na kuahidi kuwa hatoacha kuiziya hadi atapopewa maelezo ya kina kutokana na kujitokeza mambo mbali mbali katika serikali.
Mwakilishi wa Ziwani, Rashid Seif, akitoa mchango wake aliitaka serikali kuona inajipanga vyema katika suala la kusimamia sekta ya elimu kutoka an akuanza kuonekana eneo hilo huenda kukawa na wajanja wanaotumia vibaya nafasi zao.