Baraza la usalama UN lachakachua sheria kuivamia Libya

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Jan 22, 2011
1,221
1,788
Ndugu wanaJf
wakati mataifa ya magharibi walipoanza kuishambulia Libya,nililaani mashambulizi na nilipost thread nikilaani mashambulizi hayo,pamoja na upinzani mkali nilioupata,bado naendelea kulaani kwa kuwa yamekiuka sheria za kimataifa,kwa kuwa Libya haijaishambulia nchi yoyote.kwa mujibu wa sheria ya UN kifungu cha 2 (7) ni marufuku kwa taifa lolote kulishambulia taifa lingine kijeshi.
sote ni mashahidi kuwa waandamanaji wa libya,au tunisia na kwingineko hawakuomba msaada wa mataifa ya nje,
Siafiki hata kidogo wala siamini kuwa raia wa libya ni bora kuliko wa Ivory coast,Bahrain,Somalia,na kwingineko wanapopigana..mbona wakati Waisraeli wameua zaidi ya watoto 300 wa kipalestina hamna hatua zozote zilizochukuliwa?
Kamwe haijawi kuwa sera ya America kuwapenda raia hata kutumia gharama kubwa kiasi hiki.Ghadafi ametoa mwito wa kukaa meza moja wamekataa...
huu ni ubeberu mpya africa na
Ni wazi mifumo ya afya,elimuni bora kuliko ya magharibi amefanya kile ambacho kimewashinda
lazima tupinge kwa nguvu zetu wote
Nalaani na nitaendelea kulaani mashambulizi haya ambayo ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa
 
Ndugu wanaJf
wakati mataifa ya magharibi walipoanza kuishambulia Libya,nililaani mashambulizi na nilipost thread nikilaani mashambulizi hayo,pamoja na upinzani mkali nilioupata,bado naendelea kulaani kwa kuwa yamekiuka sheria za kimataifa,kwa kuwa Libya haijaishambulia nchi yoyote.kwa mujibu wa sheria ya UN kifungu cha 2 (7) ni marufuku kwa taifa lolote kulishambulia taifa lingine kijeshi.
sote ni mashahidi kuwa waandamanaji wa libya,au tunisia na kwingineko hawakuomba msaada wa mataifa ya nje,
Siafiki hata kidogo wala siamini kuwa raia wa libya ni bora kuliko wa Ivory coast,Bahrain,Somalia,na kwingineko wanapopigana..mbona wakati Waisraeli wameua zaidi ya watoto 300 wa kipalestina hamna hatua zozote zilizochukuliwa?
Kamwe haijawi kuwa sera ya America kuwapenda raia hata kutumia gharama kubwa kiasi hiki.Ghadafi ametoa mwito wa kukaa meza moja wamekataa...
huu ni ubeberu mpya africa na
Ni wazi mifumo ya afya,elimuni bora kuliko ya magharibi amefanya kile ambacho kimewashinda
lazima tupinge kwa nguvu zetu wote
Nalaani na nitaendelea kulaani mashambulizi haya ambayo ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa
Kweli. Na mimi nitakuwa moja kati ya sauti chache zinazopinga uvamizi wa Libya. Siku hizi ulimwengu wote umetishwa kufungua midomo yao dhidi ya nchi za magharibi ambazo zimejibatiza jina la kujipamba la (Jumuiya ya Kimataifa). Zamani tukiziita nchi za kibeberu (imperialists). Siku hizi hakuna anayethubutu tusema hilo neno, hasa viongozi wetu uchwara. Wanaogopa yanayompata Gaddafi sasa hivi. Amerika na wenzake wakiisha amua basi 'Jumuiya ya Kimataifa' imeamua. Tumerudi miaka hamsini nyuma. Ni ukoloni wa kificho.
 
napinga pia hilo la uvamizi! lakini juz clinton kasema neno flan imebidi nifikiri mara nyingine. majeshi ya gadafi yangeruhusiwa kuingia bengazi si angewachinja wote maana alikuwa tayari ameizunguka! je kusingekuwa na mauaji ya halaiki.
 
Mara nyingi watu wakiongelea mauaji ya halaiki Rwanda, lazima wailaumu jumuia ya kimataifa sbb waliangalia tu wakati watu wanateketezwa, kila mtu ana haki ya kutoa maoni, lkn mara nyingine tujitendee haki, Gadaffi alitangaza mapema kuwa atawateketeza wapinzani wake wote, na kweli akawashambulia kwa ndege waandamanaji! Isingekuwa busara ateketeze watu wa miji ile huku mataifa yanaangalia tu, Arab League ilishinikiza sana azimio la UN kuhusu libya lipitishwe, leo hii watu hawataji hilo! Ivory Coast kuna mgogoro mkubwa lkn kuna mchakato AU na ECOWAS unaendelea, Somalia US walipeleka majeshi huko ikashindikana, na kwa wenye kumbukumbu US walipingwa sana na mataifa ya Middle East. Mi nadhani mara nyingine tuwe tunawalaumu mataifa ya kiarabu na nchi kama China, wana uwezo wa kuingilia baadhi ya migogoro lkn kazi yao ni kupiga makelele tu na kulaumu!!
 
Mkuu clinton ni nani hata aweze kutabiri kuwa Gadafi angewachinja wote?siamini hata kidogo hizi ni propaganda just to justfy the means
 
napinga pia hilo la uvamizi! lakini juz clinton kasema neno flan imebidi nifikiri mara nyingine. majeshi ya gadafi yangeruhusiwa kuingia bengazi si angewachinja wote maana alikuwa tayari ameizunguka! je kusingekuwa na mauaji ya halaiki.

Hebu rudia hapo kwenye red, ni nani kasema? Act yew great thinker!
 
ghadafi hapo kabla alichukua miji ya las-ranuf, al-zuwahiya, brega na adjibiya, huko kote hakufanya mauaji ya halaiki, ni vipi basi hayo mauaji angeyafanya Benghazi?.

Kitu kingine ni kwamba, kama wao wanawalinda Raia mbona basi wanawaacha waasi wanasonga mbele na kuteka miji, kwa maana hiyo jamaa wanatake sides!.
 
Nakumbuka hata Iraq walikuwa na madai mengine km silaha za maangamizi na mauaji ya wapinzani. Kilichotokea ni uharibifu wa miundombinu, raia walikufa wengi kuliko kabla ya vita na wanaendelea kuuana, huduma za kijamii kama maji na matibabu zilikuwa za kuridhisha kuliko sasa na kinachoendelea ni kunyonya mafuta kama vile hawana akili timamu.
Hali ya Libya: Walibya walikuwa na hali nzuri kimaisha kuliko baadhi ya watu wa hizo nchi hizo zinazoishambulia Libya. Huduma za kijamii km maji, umeme, nyumba, gharama za kuoa, elimu mpaka chuo kikuu vyote hivyo ni bure, je nchi hizo zinafanya hivyo kwa raia wao??

Kitakachotokea: kama ilivyo Iraq na Afganistan yatakayojiri ni mauaji ya raia kuuana kwa mabomu ya kujilipua, kuvurugika kwa huduma za kijamii nk. Raia watakufa wengi kuliko ilivyokuwa kabla ya uvamizi wa nchi za magharibi.

Gharama za Vita: Gharama ya kurusha ndege moja ya kivita, bei ya makombora,meli za kivita, kuweka askari kule Mediteranian ni gharama sana, nani atalipa gharama hizo?? Ni kweli walipa kodi wa nchi hizo wako tayari kugharamia vita bure eti kwa ajili ya raia wa nchi nyingine?? Je gharama za maisha hazitapanda huko mkwao?? Majibu ni rahisi; Mafuta ya Libya.

Kusudio la vita hivi linajulikana, tusijibaraguze kwa majibu rahisi.
 
Ndugu wanaJf
wakati mataifa ya magharibi walipoanza kuishambulia Libya,nililaani mashambulizi na nilipost thread nikilaani mashambulizi hayo,pamoja na upinzani mkali nilioupata,bado naendelea kulaani kwa kuwa yamekiuka sheria za kimataifa,kwa kuwa Libya haijaishambulia nchi yoyote.kwa mujibu wa sheria ya UN kifungu cha 2 (7) ni marufuku kwa taifa lolote kulishambulia taifa lingine kijeshi.
sote ni mashahidi kuwa waandamanaji wa libya,au tunisia na kwingineko hawakuomba msaada wa mataifa ya nje,
Siafiki hata kidogo wala siamini kuwa raia wa libya ni bora kuliko wa Ivory coast,Bahrain,Somalia,na kwingineko wanapopigana..mbona wakati Waisraeli wameua zaidi ya watoto 300 wa kipalestina hamna hatua zozote zilizochukuliwa?
Kamwe haijawi kuwa sera ya America kuwapenda raia hata kutumia gharama kubwa kiasi hiki.Ghadafi ametoa mwito wa kukaa meza moja wamekataa...
huu ni ubeberu mpya africa na
Ni wazi mifumo ya afya,elimuni bora kuliko ya magharibi amefanya kile ambacho kimewashinda
lazima tupinge kwa nguvu zetu wote
Nalaani na nitaendelea kulaani mashambulizi haya ambayo ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa



pamoja na mambo mengine na hasira za kuangushwa ile ndege ya pan american airline kule scotland, wanadai gaddafi is the sponsor of terrorist. By the way what is terrorism?
 
Nami napingana na uvamizi wa nchi za kimagharibi kwa Libya kwani sio sawa na kama yule jamaa hafai basi ilikuwa ni juu ya walibya wao wenyewe kuamua namna ya kumtoa na si kuomba msaada wa toka nje ili kumuondoa raisi aliyeko madarakani, nasikia wameonekana kwenye Tv hao waasi wakishangalia ushindi huku wakiwa wanapeperusha bendara ya mmarekani je hii inatufundisha kitu gani? TAFAKARI
 
Napata kigugumizi kuzungumzia tena masuala ya Libya kwa kua tokea awali nimekua against sana na mataifa ya Magharibi kuhusu uvamivi wa kijeshi dhidi ya Libya,na kwa mtazamo wangu nilidhani kwamba kuna zaidi ya kuwaokoa raia...
Well,baada ya kuona wengi wanaunga mkono mashambulizi ya Western niliamua kukaa aside na kuperuzi kurasa..kwa mara nyingine tena napata utata kuhusu mahala pa kusimama kwa kua kwa mtazamo wa haraka haraka Gadaffi ni kiongozi shupavu na mpenda so called maendeleo ya wananchi wake wakati huo huo akiwa silent killer kwa wale wote walio against na utawala wake,na kweli aliwaua na anaua as well!
Sina hakika km ilikua sahihi kwa mataifa ya kigeni kuingilia mapigano ya Libya lakini najiuliza ni nini ingekua hatma ya mji uliokaliwa na waasi km askari wanaomtii Col Gadaffi wangeufikia mji huu!
 
Ndugu wanaJf
wakati mataifa ya magharibi walipoanza kuishambulia Libya,nililaani mashambulizi na nilipost thread nikilaani mashambulizi hayo,pamoja na upinzani mkali nilioupata,bado naendelea kulaani kwa kuwa yamekiuka sheria za kimataifa,kwa kuwa Libya haijaishambulia nchi yoyote.kwa mujibu wa sheria ya UN kifungu cha 2 (7) ni marufuku kwa taifa lolote kulishambulia taifa lingine kijeshi.
sote ni mashahidi kuwa waandamanaji wa libya,au tunisia na kwingineko hawakuomba msaada wa mataifa ya nje,
Siafiki hata kidogo wala siamini kuwa raia wa libya ni bora kuliko wa Ivory coast,Bahrain,Somalia,na kwingineko wanapopigana..mbona wakati Waisraeli wameua zaidi ya watoto 300 wa kipalestina hamna hatua zozote zilizochukuliwa?
Kamwe haijawi kuwa sera ya America kuwapenda raia hata kutumia gharama kubwa kiasi hiki.Ghadafi ametoa mwito wa kukaa meza moja wamekataa...
huu ni ubeberu mpya africa na
Ni wazi mifumo ya afya,elimuni bora kuliko ya magharibi amefanya kile ambacho kimewashinda
lazima tupinge kwa nguvu zetu wote
Nalaani na nitaendelea kulaani mashambulizi haya ambayo ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa

Angalia concept nzima ya R2P (Responsibility To Protect) na implication yake katika International Relations after Rwanda.
 
Waafrika wote ni omba omba, mbona China haki za binadamu hazifuatwi na hamna nchi za magharibi inayodhubutu kutia neno. Halafu wa magharibi wana tamaa, na waarabu hawana umoja pia mpaka gaddaf anatumia ndege kuua waandamanaji wao wamekaa kimya, sasa sijui kwa sababu wamezoea kuuwana.
 
Ndugu wanaJf
kwa mujibu wa sheria ya UN kifungu cha 2 (7) ni marufuku kwa taifa lolote kulishambulia taifa lingine kijeshi.

Lakini Semeni Ghadafi si na yeye ana sehemu ya lawama katika hili? Unawezaje kutumia ndege za kijeshi kushambulia waandamanaji? Mbona kule yemeni, Misri na Tunisia hayakutokea haya?

Then sheria ni suala pana unataka tuamini kuwa hicho kifungu tu ulichotaja hakina provision zingine? Ina maana hata nchi za Africa zinazotuwakilisha ktk Baraza la usalama la UN hajui hii? si Wangepinga basi hlafu ionekane kuwa wamelazimisha shinikizo la No FLY ZONE lakini walikubali.

Sasa kwa nini wasilaumiwe wote wawili ili tuonekana hatuko biased na itikadi fulani?
 
Waafrika wote ni omba omba, mbona China haki za binadamu hazifuatwi na hamna nchi za magharibi inayodhubutu kutia neno. Halafu wa magharibi wana tamaa, na waarabu hawana umoja pia mpaka gaddaf anatumia ndege kuua waandamanaji wao wamekaa kimya, sasa sijui kwa sababu wamezoea kuuwana.

Huwezi kulinganisha commonplace abuse of human rights na tyrant aliyesema "nitawasaka mlango kwa mlango" ambaye alikuwa tayari kuua makumi ya maelfu ya watu kama sio zaidi huko Benghazi.
 
Ndugu wanaJf
wakati mataifa ya magharibi walipoanza kuishambulia Libya,nililaani mashambulizi na nilipost thread nikilaani mashambulizi hayo,pamoja na upinzani mkali nilioupata,bado naendelea kulaani kwa kuwa yamekiuka sheria za kimataifa,kwa kuwa Libya haijaishambulia nchi yoyote.kwa mujibu wa sheria ya UN kifungu cha 2 (7) ni marufuku kwa taifa lolote kulishambulia taifa lingine kijeshi.
sote ni mashahidi kuwa waandamanaji wa libya,au tunisia na kwingineko hawakuomba msaada wa mataifa ya nje,
Siafiki hata kidogo wala siamini kuwa raia wa libya ni bora kuliko wa Ivory coast,Bahrain,Somalia,na kwingineko wanapopigana..mbona wakati Waisraeli wameua zaidi ya watoto 300 wa kipalestina hamna hatua zozote zilizochukuliwa?
Kamwe haijawi kuwa sera ya America kuwapenda raia hata kutumia gharama kubwa kiasi hiki.Ghadafi ametoa mwito wa kukaa meza moja wamekataa...
huu ni ubeberu mpya africa na
Ni wazi mifumo ya afya,elimuni bora kuliko ya magharibi amefanya kile ambacho kimewashinda
lazima tupinge kwa nguvu zetu wote
Nalaani na nitaendelea kulaani mashambulizi haya ambayo ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa

Tumekusikia, lakini wacha nikukumbushe pia hii kitu moja. Paul Kagame mpaka kesho bado analaani UN kama wewe. Ila kinyume na wewe, yeye anadai kwa nini UN haikuvamia Rwanda kuzuia ile chinjachija ya mwaka 1994.

Sasa fanya mdahalo na Kagame tupate mshindi mmoja.
 
Tumekusikia, lakini wacha nikukumbushe pia hii kitu moja. Paul Kagame mpaka kesho bado analaani UN kama wewe. Ila kinyume na wewe, yeye anadai kwa nini UN haikuvamia Rwanda kuzuia ile chinjachija ya mwaka 1994.

Sasa fanya mdahalo na Kagame tupate mshindi mmoja.
Kagame ni ngumu kumuelewa, anailaumu UN kwa kutochukua hatua kuzuia mauaji huko Rwanda (yupo sahihi kabisa kufanya hivyo na UN inastahili lawama).

Ila pia alitumia udhaifu huo wa UN kutoingilia kati kutwaa madaraka na kuidhibiti Rwanda mpaka kesho.

Ameendelea kutumia udhaifu huo wa UN kutochukua hatua huko Rwanda kuhalalisha uvamizi wake huko Drc kwa kisingizio cha kuwasaka wapiganaji wa FDLR waliohusika na mauaji huko Rwanda.
 
Back
Top Bottom