Baraza La Mitihani si shwari?

CHANGA

Member
May 26, 2008
99
27
Kuna habari kuwa kwa takribani miaka miwili sasa baraza la mitihani kuna hakukaliki kwa wafanyakazi wake aidha kuondolewa ama kujiondoa wenyewe kufuatia ubabe uliopo pale wa katibu wake Mtendaji Dr Joyce Ndalichako. habari za ndani zinasema kuwa mama huyu amekuwa na mtazamo wake kivyake badala ya mtazamo wa kitaasisi. Kila kukicha ni kubadili watendaji bila kujali maslahi ya watahiniwa. Inasemekana kuwa aliweza kubadili kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa wa kidato cha sita 2007 na kusababisha wanafunzi wengi kufeli licha ya wataalamu wake kushauri. Wanajf wenye habari hizo vipi? Taasisi hiyo inaelekea pabaya
 
aiseee kama waongelea matokeo ya kidato cha sita kuanzia 2007 na hata hawa wa 2008 sio utani nakuunga mkono kwa miguu yote miwili na kila kitu..maana kuna vipanga vilikua vyaaminika haswaaa hata pepa zimefanyika wao ndo wanatumika kwenye discussions kuelezea maswali yale yanavyotakiwa kufanywa lakini cha kushangaza matokeo yanatoka eti yule aliyekua kipanga hadi anaelezea mitego kwenye exams zile anapata marks sawa na wengine waliokubali kuwa mitihani haikuwaendea vyema..
 
aiseee kama waongelea matokeo ya kidato cha sita kuanzia 2007 na hata hawa wa 2008 sio utani nakuunga mkono kwa miguu yote miwili na kila kitu..maana kuna vipanga vilikua vyaaminika haswaaa hata pepa zimefanyika wao ndo wanatumika kwenye discussions kuelezea maswali yale yanavyotakiwa kufanywa lakini cha kushangaza matokeo yanatoka eti yule aliyekua kipanga hadi anaelezea mitego kwenye exams zile anapata marks sawa na wengine waliokubali kuwa mitihani haikuwaendea vyema..
Lakini tambua kuna waliopata A
Kwa nini huyo kipanga asingepata A
 
Back
Top Bottom