Baraza la Mawaziri, sura mpya, uchakachuaji unaendelea

mwanakijiji sidhani kama tatizo la masha au ngeleja au kijana yeyote lilitokana na in experince yao ya siasa. Nitakubaliana na wewe ukisema masha na ngeleja walikuwa hawana experince ya kusafisha siasa na maamuzi mabovu yaonekane kama ni maamuzi mazuri machoni pa jamii.

Kusimamia haki, maadili ukweli na uzalendo hakuitaji experince . Kusimamia na kuongoza opposite yake ndio kunaweza kuhitaji experince. Hata huyo mama tibaijuka hiyo wizaraya ardhi hawezi kupewa kwa hofu ya kuwaumbua vigogo wengi. Ataishia kupewa wizara ya jinsia

Masha na Ngeleja walivimba sana vichwa wakajiona kama miungu watu na kudharau wananchi. Mnakumbuka issue ya ngeleja na yule masikini mlinzi wa atm aliyekuwa analinda eneo lenye atm?. Mlinzi baada ya kuona kuna mtu yuko kwenye atm anaongea na simu badala ya kuchukua pesa alienda akamwambia kuna watu wengi wanasubiri huduma wapishe. Yule mlinzi alikuwa na moyo safi wa kusaidia wateja wapite huduma. Lakini ngeleja kwa kulewa madaraka ya uwaziri alimtukana yule mlinzi matusi na kumtishia maisha. Kwa taarifa za mwisho tulizopata yule mlinzi alifukuzwa kazi.
 
Unaweka Title ya maana halafu habari zinakuwa za kizushi unaongea habari za pillow talk, umejuwaje undani wa huyo Mkwere?, acheni majungu bana,
Unamuita Rais wako Mkwere?!!! Duh utakamatwa wewe maana wanakujua, achana na majungu nenda kazini
 
Hata kwa watu wenye NAMBA sufuri wakikusanya kwa pamoja bado kutapatikana tu NAMBA MOJA wao.

Wao waendelee kujiandaa na sherehe na ULAJI huku sisi TUKIOENDELEEA kuomboleza kifo cha DEMOKRASIA nchini. Lakini ulaji wa wauaji wa demokrasia msibani, tonge halichelewi kukwama kwenye koo ya mtu, nakuambieni tena!!!
 
Ni kitu cha kawaida watu na makundi mbali mbali kulobby kupata nafasi kadhaa wa kadhaa serikalini. Politics is a game of influence. The more influential you are the more you get what you want. Ila wakuu naomba tu nionye kuhusu kuzidi kwa hizi "tetesi" la baraza jipya ya mawaziri. Tusubiri mkuu achague safu yake kisha ndiyo tuhoji kama watendaji hao wame chaguliwa kwenye nafasi stahili.
 
Wewe ni Jasusi wa umbea na chuki za kikabila. Yaani katika mawazili waliowekwa na mafisadi ni wale wa kutoka kanda ya ziwa?? Huna maana bora ukaimbe taarabu. Una uhakika gani kwamba Masha na Ngeleja waliwekwa na Rostam?? Acha upuuzi wako na siasa za maji taka. Mie nafuata siasa za mwalimu nyerere za kistaarabu na kiungwana. Na sio zako za kupaka watu matope. Mwalimu Nyerere hakuwahi kumpaka matope mtu kama wewe unavyofanya.

Mwalimu Nyerere alikua anadiscuss maswala, na sio watu kama wewe unavyofanya. Na ndio maana nikakuomba ushahidi wa kile unachokiropoka kuhusu Masha na Ngeleja. Na umeshindwa na umekuja na analysis ya kitoto namna hiyo. Badala ya kujiita Jasus nakushauri ujiite Khadija Kopa

Kwa haya unayoandika hapa hilo jina unalotumika halitaki jiite Kikwetelist
 
Sina shaka na uwezo wa mawaziri wote wa JK akiwamo Masha na Ngeleja, tatizo ni Influence ya mafisadi ktk CCM na serikali

Hatuhitaji kumung'unya maneno wala kupambapamba ni namna gani spade inafanana na big spoon. Ngeleja na Masha ni amongst the big failures in the fourth phase govt. Leadership sifuri na perfomance below average. Hii ya kushindwa kwao kupafom kwamba ni kutokana na external forces ndiyo inayooenyesha kwamba leadership ni zero!

Kama tunakumbuka vizuri mzee wa Kiraracha enzi zile alifanya kazi zake na alipogota the whole nation ilifahamu why! Sasa hawa the so called vijana Masha na Ngeleja kwa nini tutafute sababu za kufikirika? Na ni kwa nini viongozi wa CCM siku zote hawaishi visingizio such tht if they fail siyo wao ila kuna watu wengine wamesababisha.

No wonder hilo linchi litaendelea kuwa hivyohivyo au hata kudidimia zaidi kama the best we have ni watu kama Ngeleja na Masha.
 
Napingana na Mtazamo wa mwanakijiji

Mie binafsi sijaona kama Ngeleja na Masha walishindwa kazi,, kwa sayinsi ipi uliyotumia mwanakijiji?? Hizo analysis za kizamani za kujudge mtu kwa kuangalia mvuto wake wa kuongea na vyombo vya habari na umma kwa ujumla. Mie nadhani Masha na Ngeleja walifanya kazi vizuri sana na hukukutokea matatizo yoyote yaliyosababishwa na wao,, hizo judgement za hisia kwa vile mtu haumpendi binafsi sio nzuri.

Tukikubaliana na analysis, hisia na mtazamo wako, basi Kina David cameron, kina Obama, Kina Nick Craig, Ed Milliband, n.k n.k ni wabovu. Kitu ambacho utakipinga kwa sababu hao unapata information na utendaji wao ki-sayansi na kimahesabu. sio ki hisia. mambo ya kizamani. Vijana ni muhimu na wacha wapewe wachape kazi. Wazee wabaki kua consultants tu. Na hii pia iende mpaka CHADEMA, CCM, TLP, NCCR n.k maana kuna majina tumekua tukiyasikia yapata miaka 20 na hayajatusaidia chochote badala yake wamegeuza siasa biashara. Ni wakati wa Dr Slaa, Mrema, Msekwa, Mbowe, Kihwelu, Mbatia, Marando, Lipumba, safari, nk wote hawa they have to step out of the front offices of our political parties. Ni wakati wa siasa na uongozi kwa ujumla kuachiwa vijana ambao wanaonyesha wanaweza.

Mitizamo na uongozi mpya ndio kitu tanzania inachohitaji. Sio kuendeleza siasa na mitazamo ile ile ambayo imekua ikitumiwa kwa miaka 50. Eti wazee, ooh Uzoefu. Obama, Cameron, Tony Blair, walikua na uzoefu gani?? Kwa bahati mbaya sana falsafa hii imedakwa na kukumbatiwa na vyama vyote vya siasa. Kuanzia CHADEMA hadi TADEA, wote wanaendekeza mawazo mabovu yaliyojaa ubabe wa kizee.

Its time waachie hizo kazi, zimeshawashinda kwa miongo kibao. Tena kwa kutoa mfano, napendekeza aanze Dr Slaa ambaye amekua katibu wa CHADEMA karibia miaka 200 iliyopita. Kila siku ubabe na kufukuza vijana wanaoleta mitazamo mipya au wanaopingana nae.

Kile kinachodaiwa kuwa ni Sheria ya Madini Na. 14 ya 2010 ambacho Ngeleja amesimamia kutungwa kwake kumeonyesha wazi kuwa ana lengo la kulinda ufisadi. Kwa msingi hakuna walichobadilisha bali kuzuga watu kwa kuweka vipengele vya mabadiliko vichache huku vikiendeleza hai za Wachukuaji. Kibaya zaidi ni kusikia kauli zake za kutetea wachukuaji hao. Hiyo imenisikitisha sana. Faulo za Masha hazina upatu na mtu mwenye dhamira hai hawezi kumtetea. Anatetewa na wale ambao ni marafiki zake ambao wamenufaika na faulo zake.
 
Kuna taarifa kwamba JK amejifungia kuchakachua mapendekezo ya watu wa usalama na washauri wake (sio Sheikh Yahya na Maji Marefu).

Wizara zinazoumiza vichwa ni Mambo ya Nje, Mambo ya Ndani, Fedha na Uchumi, Maliasili na Utalii, Elimu, Afya na Ardhi.

Prof Anna Tibaijuka alitaka kumpa Mambo ya Nje,watu wakasema anafaa ardhi na makazi maana kuwa UN haina mana ni mwanadiplomasia. Hoja hiyo inatokana na Membe kuzidiwa na mizengwe ya kutaka kumtoa, kwa kigezo kile kile cha kumtoa Sitta kwamba eti makundi na wakose yote Membe na Lowassa!!!

Jina la January Makamba nalo liko juu, huku majina mapya ya vijana kibao yakijitokeza, baadhi wakiwa ni kutoka visiwani na mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Bado tatizo la ukubwa wa baraza haliepukiki kwa sasa. Ila kwa kweli kundi la mafisadi lina nguvu kubwa kwa CCM na JK anapata shida sana kujitenga na nguvu hizo na sasa zinamtesa sana.

Wizara ya Miundombinu nayo inatakiwa na mafisadi kwa nguvu zote.

More to come from Msoga.

Kama JK katuchoka na anataka viwanja vitolewe kikabila basi ampe huyo mama hiyo wizara.. Hawa jamaa zetu kwa ardhi huwa wana matatizo sana.
 
Wewe ni Jasusi wa umbea na chuki za kikabila. Yaani katika mawazili waliowekwa na mafisadi ni wale wa kutoka kanda ya ziwa?? Huna maana bora ukaimbe taarabu. Una uhakika gani kwamba Masha na Ngeleja waliwekwa na Rostam?? Acha upuuzi wako na siasa za maji taka. Mie nafuata siasa za mwalimu nyerere za kistaarabu na kiungwana. Na sio zako za kupaka watu matope. Mwalimu Nyerere hakuwahi kumpaka matope mtu kama wewe unavyofanya.

Mwalimu Nyerere alikua anadiscuss maswala, na sio watu kama wewe unavyofanya. Na ndio maana nikakuomba ushahidi wa kile unachokiropoka kuhusu Masha na Ngeleja. Na umeshindwa na umekuja na analysis ya kitoto namna hiyo. Badala ya kujiita Jasus nakushauri ujiite Khadija Kopa
Advise: Usiwe hata siku moja uwe na matumaini kutoka kwa mawaziri kama Rais ni mpuuzi, kihiyo, kichwamaji etc. What do you expect from a cabinet while a president is stupid? Mininisters go by orders from the President; a good job is directed by the president! I don't expect anything new from this cabinet even if an angel is appointed a minister!

Another 5 years wasted!!!!
 
Kama JK katuchoka na anataka viwanja vitolewe kikabila basi ampe huyo mama hiyo wizara.. Hawa jamaa zetu kwa ardhi huwa wana matatizo sana.
Huo ndio ukabila. Je unaweza kuniambia Marehemu Jaji Lugakingira alipokuwa Kamishna wa Ardhi aliondoka na viwanja vingapi? (Jibu Sifuri) Je, Mama Sijaona (sasa Balozi Japan) ambaye si wa kabila la huo Mama je si ndiye amepora viwanja vya watu Mbweni, Bunju na sasa Luguruni. Kauli hizi zisizo za kuzungumza vitu kwa ujumla jumla ndizo zinaendeleza upuuzi wa ukabila, udini na urangi. Ni upuuzi na ni ujinga. Kama una hoja dhidi yake iweke katika matendo yake na si ukabila na maneno ya jumla jumla yanayojenga na kuendeleza chuki dhidi ya kabila au dini fulani.
 
Mwanakijiji sidhani kama tatizo la Masha au Ngeleja au Kijana yeyote lilitokana na in experince yao ya siasa. Nitakubaliana na wewe ukisema Masha na Ngeleja walikuwa hawana experince ya kusafisha siasa na maamuzi mabovu yaonekane kama ni maamuzi mazuri machoni pa jamii.

Kusimamia Haki, Maadili ukweli na Uzalendo hakuitaji experince . Kusimamia na kuongoza opposite yake ndio kunaweza kuhitaji experince. Hata Huyo Mama Tibaijuka Hiyo wizaraya ardhi hawezi kupewa kwa hofu ya kuwaumbua Vigogo wengi. Ataishia kupewa Wizara ya Jinsia

Mkuu umeongea ukweli tupu. katika kuunda serikali maswahiba wote huwa na mkono wao kwa kutaka kuweka watu ambao watalinda masilahi yao binafsi. Unapomuweka mtu huru na mfuata sheria huwa anaonekana ni kikwazo, Mfano mzuri ni kwa Dr Pombe Magufuli, huyu jamaa wizara ya ujenzi na miuondombinu aliiweza sana ila alikuja tolewa kipindi cha wanamtandao kwa ajili ya masilahi. Kama JK anahitaji kukumbukwa kuwa ni rais aliyeingia kipindi cha pili kwa chakachua lakini akaweza kufanya kazi kwa umahiri mkubwa mpaka wananchi wakamkubali basi ninamshauri asisikilie majungu ya usalama wa Taifa ambao wengi ni ma-agent wa mafisadi.

Kama anataka kufanya vetting basi ni bora hata awatumie EY au KPMG kuwa interview potential wote halafu achague anaoona kuwa kweli ni pro bono. Tatizo la katiba yetu haitoa muda wa transition yaani miezi kama miwili baada ya uchaguzi wa kuunda serikali yaani serikali zinaundwa kwa zimamoto kutokana na muda mchache tokea uchaguzi mpaka kuapishwa rais. Hii ni hatari sana hasa kama unahitaji kupata wachapa kazi badala ya wachumia tumbo
 
Wewe ni Jasusi wa umbea na chuki za kikabila. Yaani katika mawazili waliowekwa na mafisadi ni wale wa kutoka kanda ya ziwa?? Huna maana bora ukaimbe taarabu. Una uhakika gani kwamba Masha na Ngeleja waliwekwa na Rostam?? Acha upuuzi wako na siasa za maji taka. Mie nafuata siasa za mwalimu nyerere za kistaarabu na kiungwana. Na sio zako za kupaka watu matope. Mwalimu Nyerere hakuwahi kumpaka matope mtu kama wewe unavyofanya.

Mwalimu Nyerere alikua anadiscuss maswala, na sio watu kama wewe unavyofanya. Na ndio maana nikakuomba ushahidi wa kile unachokiropoka kuhusu Masha na Ngeleja. Na umeshindwa na umekuja na analysis ya kitoto namna hiyo. Badala ya kujiita Jasus nakushauri ujiite Khadija Kopa
Mimi mwenyewe natoka kanda ya Ziwa pia. Nitafutie tusi jingine.
 
Mkuu usiwe mbishi sana kama jambo hulifahamu vizuri. Ngeleja alikuwa mwanasheria wa Vodacom ambako Rostam ni mwana hisa. Ndo aliyemshauri akagombee ubunge Sengerema na Rostam ndo aliyegharimia kampeni zake mwaka 2005. Mara tu baada ya kuwa mbunge akapewa unaibu waziri wa nishati na madini na hatimaye waziri kamili wa wizara hiyo. Na huo ulikuwa mpango kamili wa Rosatm na rafiki yake Lowasa kufanikisha ufisadi wao katika sekta ya mishati na madini. Tumeona Dowans na Richmond. Pia Rostam kampuni yake ya Caspian ndo wenye mitambo ya kuchimba madini kwenye makampuni mengi yaliyopo hapa nchini. n.k.
Halafu anathubutu kujiita Nyerereist. My foot!
 
Mimi ninaamini kabisa kuwa kama hekima itapata nafasi basi kuna watu ambao japo wanaonekana "wanastahili" uwaziri wasipewe na wapo ambao wanaonekana hawawastahili wapewe. Kwa vile mawazirindio wasaidizi wakuu wa Rais basi kwa jinsi baraza litakavyokuwa ndivyo mwelekeo wa serikali utakavyokuwa.
 
Lakini kwa nini tunaendeleza upumbavu ule ule wa kudai tuwe na wasomi hata vijana lakini hakuna wanalozalisha? Kama kuna baraza la mawaziri lilikuwa limejaa wasomi ni hili lilokwisha, sasa mjiulize ni vipi wameshindwa kazi. Je ni Usomi, Jinsia, Ukabila, Umri au?

Ufanisi hauna umri, elimu, jinsia, dini wala rangi. Ni ufanisi tuu na hakuna lingine!
 
Lakini kwa nini tunaendeleza upumbavu ule ule wa kudai tuwe na wasomi hata vijana lakini hakuna wanalozalisha? Kama kuna baraza la mawaziri lilikuwa limejaa wasomi ni hili lilokwisha, sasa mjiulize ni vipi wameshindwa kazi. Je ni Usomi, Jinsia, Ukabila, Umri au?

Ufanisi hauna umri, elimu, jinsia, dini wala rangi. Ni ufanisi tuu na hakuna lingine!
Reverend,
Umesahau kuwa vijana wengi leo hawana ule moyo wa "what can I do for my country." Wanakimbilia CCM kwa sababu huko ni rahisi kupata ulaji. Wanagombea ubunge kwa sababu ndiyo tiketi ya kupata uwaziri. Na ukishapata uwaziri unajikuta umetajirika bila hata kujua utajiri umetoka wapi.
 
Lakini kwa nini tunaendeleza upumbavu ule ule wa kudai tuwe na wasomi hata vijana lakini hakuna wanalozalisha? Kama kuna baraza la mawaziri lilikuwa limejaa wasomi ni hili lilokwisha, sasa mjiulize ni vipi wameshindwa kazi. Je ni Usomi, Jinsia, Ukabila, Umri au?

Ufanisi hauna umri, elimu, jinsia, dini wala rangi. Ni ufanisi tuu na hakuna lingine!


Vijana wengi wasomi walioko CCM ni kwa sababu huko kuna shortcut ya kupatia madaraka. Ni vigumu kuamini kuwa kuna kijana msomi mwenye akili timamu aliyeona yote yaliyofanywa na serikali ya CCM katika kipindi cha kuanzia mwaka 1995 hadi leo atakayesema kuwa chama hiki ni cha kutumikia ili kuiendeleza Tanzania; ni afadhali wazeee waliokua na ile CCM tangu mwanzo wake kwa vile inawezekana wanaathiriwa na ile ostrich philosophy ya kuamini kuwa wako right kila siku. Ndiyo maana binafsi ninashindwa kutoa ushuari wowote kuhusu serikali ijayo kwa vile candidates wake karibu wote ni hovyo tu.
 
Yaani mnataka kusema mtu aliyetangazwa Rais wiki iliyopita mpaka leo hana orodha kamili ya Baraza lake la Mawaziri?
 
Back
Top Bottom