Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,726
Kuna tetesi nzito kuwa kikao cha baraza la mawaziri cha dharula usiku huu. JK mwenyewe yuko Moshi lakini kaagiza kifanyike chini ya uenyekiti wa Makamu wa Rais.
Agenda kuu ni mgomo wa madaktari na kuona njia ya kuwaondoa Dr. Mponda na Nkya bila kusababisha political fallout. Lile zengwe la Pinda la hapo awali ilikuwa ni danganya toto ili kupima joto ya maji.
Mawaziri wengi matumbo yako moto. Kuku weusi, kondoo na ng'ombe wameteketea kwa kasi jana na leo katika familia za mawaziri.
Hili ni la kuvunda halina ubani. Amewanyima madaktari mgomo umerudi, akiwapa, walimu wanagoma. Afanyeje?
Agenda kuu ni mgomo wa madaktari na kuona njia ya kuwaondoa Dr. Mponda na Nkya bila kusababisha political fallout. Lile zengwe la Pinda la hapo awali ilikuwa ni danganya toto ili kupima joto ya maji.
Mawaziri wengi matumbo yako moto. Kuku weusi, kondoo na ng'ombe wameteketea kwa kasi jana na leo katika familia za mawaziri.
Hili ni la kuvunda halina ubani. Amewanyima madaktari mgomo umerudi, akiwapa, walimu wanagoma. Afanyeje?