Baraza la mawaziri! Hata serikali ya mafisadi inapaswa kuwa na kanuni!

The Analyst

JF-Expert Member
Feb 26, 2011
464
246
Sijui hawa mawaziri wanasumbuliwa na nini?
Ninavyojua, serikali hata iwe ya kifisadi namna gani, mawaziri huendelea kuwajibika kwa pamoja hata kama wanatofautiana vyama.
Leo hii unawasikia mawaziri wanaisema serikali kwa kauli zinazopingana mfano Babu wa Loliondo anapigwa stop na waziri wa Afya kisha waziri mwingine anasema haiwezekani kumzuia. Halafu ujue mwana JF, wote wana sababu nzuri tu za kumsaidia mtanzania waliyemfilisi kwa ufisadi.
Mwingine anaisemea serikali eti wamegundua kuna balozi zinawafadhili CDM kuleta machafuko nchini. Kwa manufaa ya nani? Nchi gani hizo? Haijulikani.
Kwa nini serikali iliyo makini kiasi cha kugundua yote hayo haijamchukulia hatua hata mhusika mmoja? Mbona inakuwa vigumu kuzitaja nchi?
Kauli nyingi za binafsi na zinazotofautiana hazitakiwi under serikali moja. Hii ni bila kujali ni serikali ya kifisadi kama yetu au ni ile inayowajibika. Ndiyo maana nasema; Mawaziri wa JK acheni mikurupuko!
 
Jamani lazima kwenye ukweli tuseme ukweli, hivi ikibainika zile dawa zinazotolewa na mzee kule Longido zina madhara baada ya miaka mitatu kwa binadamu tutasemaje mbele ya umati, ni vema ikachunguzwa kama haina madhara yoyote ya kiafya siku za baadaye. Na hapa ndio tunasema kila wizara inamsemaji wake kwa maana ya waziri anayeshughulika na Wizara hiyo.

Kabla utafiti haujafanyika si vema kuwaacha watu wakiendelea kunywa, lamsingi utafiti na vipimo viharakishwe.
 
Jamani lazima kwenye ukweli tuseme ukweli, hivi ikibainika zile dawa zinazotolewa na mzee kule Longido zina madhara baada ya miaka mitatu kwa binadamu tutasemaje mbele ya umati, ni vema ikachunguzwa kama haina madhara yoyote ya kiafya siku za baadaye. Na hapa ndio tunasema kila wizara inamsemaji wake kwa maana ya waziri anayeshughulika na Wizara hiyo.

Kabla utafiti haujafanyika si vema kuwaacha watu wakiendelea kunywa, lamsingi utafiti na vipimo viharakishwe.
Nakubaliana na wewe! Ninacholaumu ni wao kukosa kauli moja na kuifanya serikali kuwa na mapande mapande kama kifusi cha bomoa bomoa.
 
nafkiri kwa sasa kila waziri ni independent hawawajibiki kokote thats why kila mmoja anaropoka tuu hovyo hovyo tena wakiongozwa na pinda issue za utendaji anaamua kisiasa. Where is collective respondibility? Yani ni kama timu ambayo haichezi kitimu kila mchezaji anadrible kivyake na kukaba kivyake no pasi wala nini kweli itashinda? JK ur cabinet will lead you to destruction
 
Waganga wote wa jadi Tanzania wanatoa mitishamba yao bila miti hiyo kuchunguzwa kwanza ubora.
Wanachanja chale na kuweka dawa zao bila dawa hizo kuchunguzwa.
Nyembe zao hazichunguzwi.
hata mikono yao wengine hawanawi.
Pamoja na yote hayo sijawahi kusikia serikali ikitaka kuanzisha zoezi la kupima dawa za waganga hawa wa jadi.

Kwa nini Ghafla inakuwa Noma kwa Babu kutoa Dawa??
Kwa vile kasema anatibu Ukimwi??
Angesema anatibu Nguvu za kiume serikali ingeaagiza dawa zipimwe??

DOUBLE STD? KUJIKANYAGA? AU NINI?
Jamani lazima kwenye ukweli tuseme ukweli, hivi ikibainika zile dawa zinazotolewa na mzee kule Longido zina madhara baada ya miaka mitatu kwa binadamu tutasemaje mbele ya umati, ni vema ikachunguzwa kama haina madhara yoyote ya kiafya siku za baadaye. Na hapa ndio tunasema kila wizara inamsemaji wake kwa maana ya waziri anayeshughulika na Wizara hiyo.

Kabla utafiti haujafanyika si vema kuwaacha watu wakiendelea kunywa, lamsingi utafiti na vipimo viharakishwe.
 
Sijui hawa mawaziri wanasumbuliwa na nini?
Ninavyojua, serikali hata iwe ya kifisadi namna gani, mawaziri huendelea kuwajibika kwa pamoja hata kama wanatofautiana vyama.
Leo hii unawasikia mawaziri wanaisema serikali kwa kauli zinazopingana mfano Babu wa Loliondo anapigwa stop na waziri wa Afya kisha waziri mwingine anasema haiwezekani kumzuia. Halafu ujue mwana JF, wote wana sababu nzuri tu za kumsaidia mtanzania waliyemfilisi kwa ufisadi.
Mwingine anaisemea serikali eti wamegundua kuna balozi zinawafadhili CDM kuleta machafuko nchini. Kwa manufaa ya nani? Nchi gani hizo? Haijulikani.
Kwa nini serikali iliyo makini kiasi cha kugundua yote hayo haijamchukulia hatua hata mhusika mmoja? Mbona inakuwa vigumu kuzitaja nchi?
Kauli nyingi za binafsi na zinazotofautiana hazitakiwi under serikali moja. Hii ni bila kujali ni serikali ya kifisadi kama yetu au ni ile inayowajibika. Ndiyo maana nasema; Mawaziri wa JK acheni mikurupuko!

Tatizo lao ni waongo na hawajui kanuni za uongo. Kanuni ya uongo ni kuwa ukiwa muongo usiwe msahaulifu utakutaunajipinga mwenyewe.
 
Back
Top Bottom