Barafu ilisababisha kuanguka kwa ndege uwanjani heathrow

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
Ndege hiyo ya British Airways 777 ilikuwa ina abiria 136 kutoka Beijing ilipokosa nguvu wakati inatua katika uwanja wa Hearthrow, magharibi mwa London, mita 330 kabla ya kufika kwenye njia ya kukimbilia ndege.

Kuongezeka kwa barafu katik matenki ya mafuta kulikuwa kumevuruga mzunguko wa mafuta kwenda kwa injini zake.
Baada ya kutua, ndege hiyo iliteleza mita 372 kwa kutumia tumbo lake (kwa vile magurudumu yalikuwa hayajatoka) kabla ya kusimama.

Abiria wote waliokolewa salama, mmoja akiwa amevunjika mguu.
Kwa jumla, abiria 34 na wafanyakazi 12 katika ndege hiyo walipata majeraha madogo, hususani migogoni na shingoni.
http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/1265724326_2.jpg
 
Back
Top Bottom