Kuna mtu hapo pembeni ya bango kashika maji ya Kilimanjaro. Amenifurahisha maana inaonesha jinsi hawa watu walivyo na low IQ
Wametumia uhuru wao wa kikatiba kueleza ujumbe wao kwa hiyo sidhani kama wana kosa. Makosa makubwa ni kwa viongozi wa Chadema kwa kuwakaririsha watu waamini kwamba vurugu ndiyo suluhisho la matatizo yetu.
Sasa kila mtu anajua kuwa Arusha ndiyo mji unaoongoza kwa vurugu na maandamano Afrika Mashariki kiasi cha kupunguza idadi ya watalii wanaotembelea mji huo na hivyo kupunguza pato la taifa linalotokana na utalii. Hivi niwaulize MAGWANDA mnaitakia mema hii nchi kweli? Au mnataka Tanzania igeuke Somalia?
Tazama sura zao ni za watu walio kata tamaa.
Halafu wamevaa T-shirt za bure!
naona wamekwenda arusha kweli na kufanya vurugu
Bango limeandikwa hivi;
''vurugu zenu mkafanye arusha na kilimanjaro
hatuwapi kura''
Bado wamelala, wanadanganywa ni mapambano ya ukabila na udini huku wanazidishiwa ufukara kwa unyonyaji. Arusha nyumbani kwa azimio la wanyonge haitatulia hadi mizimu ya azimio itulie hasira. Baragumu linalia kutokea arusha nchi inahitaji matumaini mapya ya wanyonge. Ufisadi umetamalaki kama ndio sera rasmi ya chama tawala.