engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Ebu fikiria,
Dar tuna bandari ya asili ( natural harbour) ambayo Mungu hatutozi kodi hata senti moja. Holland inategemea sana Roterdam kama kitega uchumi chake cha maana. ( Roterdam) ni bandari kama ilivyo Dar Es Salaam.
Wateja tunao wengi sana kuliko hata walivyo nao HOLLAND, wateja hao ambao wanatakiwa wailetee bandari yetu pesa nyingi za kigeni.
Zipo nchi kama Rwanda, Burundi, Uganda, Congo, na Zambia ambazo hazina bahari hivyo kutegemea sana bandari ya Salama kama geti la kuchukua na kupeleka mizigo yao nje ya nchi. Lakini cha ajabu Bandari ya salama inaonekana ni ya kuchumia watu matumbo yao na si kwa lengo lililokusudiwa la kukuza uchumi,hatuitumii bandari hii salama kama kitega uchumi kwa Taifa letu ila Bandari hii ya Salama inatumika kujaza vitambi vya watu wachache na kumfanya Raisi kulalamika kuwa KUONGOZA NCHI MASIKINI NI TAABU
Sisi si masikini jamani,tumekosa mtu wa kusimamia mali asili zetu tulizopewa bure na mungu,Tumekosa mipango iliyo bora na hata kama tunayo mipango hiyo basi tumekosa wasimamizi,walio wengi wameweka ubinafsi mbele
kwa nini tusiwe na mkakati mbadala kama wenzetu wa HOLLAND na kuifanya Bandari hii kuwa ni kitega uchumi cha Taifa na si kichumia tumbo cha wachache?
Angalia tumeua hadi chuo cha Bandari DSM Kilichopo pale Temeke
hivi tupewe nini wazungu weusi?
Dar tuna bandari ya asili ( natural harbour) ambayo Mungu hatutozi kodi hata senti moja. Holland inategemea sana Roterdam kama kitega uchumi chake cha maana. ( Roterdam) ni bandari kama ilivyo Dar Es Salaam.
Wateja tunao wengi sana kuliko hata walivyo nao HOLLAND, wateja hao ambao wanatakiwa wailetee bandari yetu pesa nyingi za kigeni.
Zipo nchi kama Rwanda, Burundi, Uganda, Congo, na Zambia ambazo hazina bahari hivyo kutegemea sana bandari ya Salama kama geti la kuchukua na kupeleka mizigo yao nje ya nchi. Lakini cha ajabu Bandari ya salama inaonekana ni ya kuchumia watu matumbo yao na si kwa lengo lililokusudiwa la kukuza uchumi,hatuitumii bandari hii salama kama kitega uchumi kwa Taifa letu ila Bandari hii ya Salama inatumika kujaza vitambi vya watu wachache na kumfanya Raisi kulalamika kuwa KUONGOZA NCHI MASIKINI NI TAABU
Sisi si masikini jamani,tumekosa mtu wa kusimamia mali asili zetu tulizopewa bure na mungu,Tumekosa mipango iliyo bora na hata kama tunayo mipango hiyo basi tumekosa wasimamizi,walio wengi wameweka ubinafsi mbele
kwa nini tusiwe na mkakati mbadala kama wenzetu wa HOLLAND na kuifanya Bandari hii kuwa ni kitega uchumi cha Taifa na si kichumia tumbo cha wachache?
Angalia tumeua hadi chuo cha Bandari DSM Kilichopo pale Temeke
hivi tupewe nini wazungu weusi?