mjunguonline
Member
- Mar 10, 2011
- 73
- 5
Msanii wa sanaa ya uchekeshaji Dickson Makwaya a.k.a "Bambo mzee wa kuchamandi" amepata ajali mbaya ya kugongwa na gari akiwa katika pikipiki maeneo ya Kigogo Mbuyuni jana usiku. Hali ya msanii huyo si nzuri sana na ameumia sehemu kubwa ya mwili wake na inasemekana kuwa amevunjika mfupa wa paja. Msanii huyo amelazwa wodi ya wagonjwa wa mifupa MOI na anatarajiwa kufanyiwa upasuaji Asubuhi hii. Mungu amsadie arudi katika hali yake ya zamani.Mzee wa "Aluuu....,Kukuluka mwanangu....Huwezi kupasua Godoro!