Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Hakuna cheo nisichokitambua na ambacho kina wababaisha watu wengi huku mtaani kwetu kama hiki cha balozi.Wengi hata wale waliokwenda shule bado wana endekeza enzi za chama kushika hatamu ambapo balozi wa nyumba kumi alikuwa na nguvu kubwa kwa watu japo sina uhakika kama ni cheo kilichokuwa kipo kisheria au la.Ninachokifahamu mimi ni kuwa huyu si kiongozi wa serikali.Mwenyekiti wa serikali za mitaa ndiye kiongozi mkuu katika mtaa husika.Lakini cha ajabu yupo huyu aitwae balozi naye anajionesha kama ana tambulika.
Binafsi kwangu nimekuwa nikiwakatalia kupokea amri zao kwa hoja hii kuwa yeye si kiongozi wa serikali.
Baada ya mauaji ya ovyo kutokea hapa Songea mkuu wa wilaya alipita na kuwaeleza wananchi kile kilichotokea.Katika mikutano yake yote hapa mjini alikuwa anakumbana na maswali mengi ambayo alikuwa hawezi kuyatolea ufafanuzi zaidi ya kuleta ubabe.Hivi sasa ametoa amri ya kulinda sungusung mitaani.Sasa zoezi hili limekuwa likiendeshwa na hawa jamaa wa kujiita mabalozi wa nyumba kumi kumi.Jambo hili kwenye mkutano mmojawapo Sabaya Mkuu wa wilaya alikataliwa kuwatumia hawa watu badala yake tulimwambia hiyo ni kazi ya serikali ya mitaa.Balozi hatambuliki hivyo hataweza kujibishwa pindi mambo yatakapokuwa ymeharibika.Lakini inaonekana ameendelea na ubabe huo wa kuwatumia.
Juzi mimi niliwatimua wajumbe walotumwa na balozi nikawaambia hilo ni jukumu la Mwenyekiti wa serikali za mitaa.Wakarudisha jibu kuwa nimekaidi amri ya serikali.Nikaletewa barua ya kuitwa ofisini.Huko akaitwa na huyo balozi,nikamwambia Mwenyekiti kuwa huyu simtambui na wala sitatii amri hiyo akitaka atangulie mahakamani.Nikamwambia kama ni kweli ana tawala kisheria basi barua ilitakiwa iandikwe na balozi huyu ya kuniita mimi lakini badala yake umeandika wewe.
Naandika hili ili kuwaeleza na wengine amabao bado hawajatambua kuwa cheo hiki ni batili.Hakipo.
Binafsi kwangu nimekuwa nikiwakatalia kupokea amri zao kwa hoja hii kuwa yeye si kiongozi wa serikali.
Baada ya mauaji ya ovyo kutokea hapa Songea mkuu wa wilaya alipita na kuwaeleza wananchi kile kilichotokea.Katika mikutano yake yote hapa mjini alikuwa anakumbana na maswali mengi ambayo alikuwa hawezi kuyatolea ufafanuzi zaidi ya kuleta ubabe.Hivi sasa ametoa amri ya kulinda sungusung mitaani.Sasa zoezi hili limekuwa likiendeshwa na hawa jamaa wa kujiita mabalozi wa nyumba kumi kumi.Jambo hili kwenye mkutano mmojawapo Sabaya Mkuu wa wilaya alikataliwa kuwatumia hawa watu badala yake tulimwambia hiyo ni kazi ya serikali ya mitaa.Balozi hatambuliki hivyo hataweza kujibishwa pindi mambo yatakapokuwa ymeharibika.Lakini inaonekana ameendelea na ubabe huo wa kuwatumia.
Juzi mimi niliwatimua wajumbe walotumwa na balozi nikawaambia hilo ni jukumu la Mwenyekiti wa serikali za mitaa.Wakarudisha jibu kuwa nimekaidi amri ya serikali.Nikaletewa barua ya kuitwa ofisini.Huko akaitwa na huyo balozi,nikamwambia Mwenyekiti kuwa huyu simtambui na wala sitatii amri hiyo akitaka atangulie mahakamani.Nikamwambia kama ni kweli ana tawala kisheria basi barua ilitakiwa iandikwe na balozi huyu ya kuniita mimi lakini badala yake umeandika wewe.
Naandika hili ili kuwaeleza na wengine amabao bado hawajatambua kuwa cheo hiki ni batili.Hakipo.