Kama kilichoandikwa ni sahihi, kiasi kinachodaiwa kinatokana na nursing services alizopatiwa Balali nyumbani kwake hadi anakutwa na mauti baada ya kutoka hospitalini. Na kama kumbukumbu zangu ni sahihi, Balali aliandika barua ya kuresign kabla rais hajatengua uteuzi wake wa ugavana. BOT inawajibika vipi kulipia hizo nursing services? Lakini pia baada ya vyombo vya habari kutoa taarifa kuwa Balali kaenda kutibiwa Marekani, alipoulizwa waziri wa fedha Meghji alisema hana taarifa na jambo hilo. Kwa taratibu za kawaida, kabla ya kuondoka lazima kuna mtu aliyekaimishwa nafasi hiyo. Nani anayeteua mtu wa kukaimu nafasi hiyo sijui, lakini kitu ninachokifahamu kwa hakika ni kuwa miongoni mwa watu waliojulishwa uteuzi huo waziri wa fedha ni miongoni mwao. Ni vipi waziri huyo hakujua kuwa gavana wake wa benki kuu yuko nje kwa matibabu? Kukanganya mambo huku ndiko kunafanya watu wengine waendelee kuamini kuwa Balali yu hai!