I agree, this man should come and show us the money. Ingawa system nzima imeoza bado niko positive kwamba tunaweza kupata pa kuanzia.eti nilikuwa natumiwa? mpuuzi sana huyu na bora aje aseme ukweli tujue who/where is the money? akiwa mkweli wananchi tunaweza kumpa immunity maana atakuwa ametusaidia kuondoa mafisadi wengi sana
Breaking News toka Iringa ni kwamba mganga wa kienyeji wa Balali anayejulikana kwa jina GM (nafupisha kutomharibia soko) amethibitisha kuwa ndugu Balali ni mzima wa afya na atarudi Tanzania kusafinya jina lake baada ya yeye Mganga kukamilisha shughuli za maandalizi ya ujio wake!
NB: This is not a Joke
Mambo ya mganga wa Jadi siyaingilii lakini NI KWELI kwamba Ballali anajiandaa kurudi (si kurudishwa) nchini wakati wowote na katika mambo mengine anataka achunguzwe kwa undani na afikishwe mahakamani ili huko ndio mambo yajulikane. Anataka mali zake zichunguzwe na zilinganishwe na kipato chake na pia kama mali zake zinalingana na hizo fedha zilizoibwa.
Halisi, nimekusoma vyema ama? una maana Balali anataka arudi kumkoma nyani??
Hapa litakuwa limesanuka hasaaaaa!
Wasi wasi wangu ni je mahakama zetu zitatenda haki?? ama yatakuwa yale yale ya slayer Ditto??
Mdogo wa Ballali ambaye anaishi naye Boston, Marekani ameliambia gazeti hili kuwa kaka yake ambaye sasa anaendelea vyema baada ya kushambuliwa na maradhi, anatarajia kuuweka ukweli wa kile alichoeleza kuwa uongo unaosambazwa dhidi yake.