Balali wa zamani Nigeria akiri mashtaka

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
Gavana wa zamani wa Nigeria James Ibori ameekiri katika mahakama moja nchini Uingereza kuiba takriban euro milioni 190 za serikali ya Nigeria na kuzitumia* kibinafsi na mambo ya kifahari. James Ibori alikiri mashtaka 10 pamoja na ufujaji wa fedha na njama ya kughushi wakati alipokuwa gavana wa jimbo la Delta mwaka wa 1999 na 2007. Jimbo la Delta ni jimbo lililo na utajiri mkubwa wa mafuta.* Gavana huyo wa zamani aliye na umri wa miaka 49 bado anazuiliwa nchini humo na atahukumiwa hivi karibuni. Ibori alikamatwa mwaka wa 2007 na shirika la kupambana na ufisadi la Nigeria baada ya kupoteza kinga ya mahakama alipotoka katika wadhfa wake.*
 
Naona hapa unachanganya mambo Balali alikuwa Gavana wa Bank Kuu huyo James Ibori alikuwa gavana wa Jimbo la Delta huko Nigeria na siyo gavana wa Bank kuu ya Nigeria utawafanaishaje? Shule zimeshusha sana kiwango cha ufahamu cha nyie wadogo zetu.
 
Back
Top Bottom