BAKWATA: Hatuutambui waraka wa Waislamu

Mbalamwezi

JF-Expert Member
Sep 30, 2007
800
171
Bakwata imetangaza leo kuwa haiutambui waraka uliotolewa na Shura ya Maimamu jana.

Imesema hakuna mantiki kwa waislamu kuupinga waraka uliotolewa na Wakristo, halafu waislamu hao hao nao waamue kutoa wao. Watakuwa wametenda jema lipi kama waliona wakristo wamekosea?
 
Bakwata imetangaza leo kuwa haiutambui waraka uliotolewa na Shura ya Maimamu jana.

Imesema hakuna mantiki kwa waislamu kuupinga waraka uliotolewa na Wakristo, halafu waislamu hao hao nao waamue kutoa wao. Watakuwa wametenda jema lipi kama waliona wakristo wamekosea?

Hata ule wa wakatoliki haukuwa wa Wakristo wote! Ngoma droo!
 
KANISA Katoliki nchini limeanzisha programu maalumu yenye lengo la kuwafundisha waumini wake namna ya kupata viongozi bora katika uchaguzi mkuu ujao mwakani.

Mbali na hilo, kanisa hilo limeonya baadhi ya wanasiasa ambao wamekuwa wakipinga viongozi wa dini kuingilia masuala ya siasa na kueleza kuwa kamwe vitu hivyo haviwezi kutenganishwa.

Kanisa hilo limesema Serikali imepoteza imani yake kwa wananchi kutokana na kuendelea kukumbatia mafisadi kwa kushindwa kufikia maamuzi ya haraka ya kesi za tuhuma za ufisadi, jambo ambalo kanisa hio limesema litazidi kukemea bila woga.

Akizungumza katika maadhimisho ya Ibada ya Misa Takatifu ya Kutoa Komuniyo ya Kwanza kwa vijana wa Parokia ya Manzese, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Baptiste Mapunda wa Shirika la Wamisionari wa Africa, alisema wakati umefika chama tawala CCM kukubali kubalika kwani Watanzania sasa wameelimika na hawako tayari kuendelea kuburutwa.

"Maovu ni mengi sana katika nchi hii na yanasababisha kuporomoka kwa maadili, ambapo vyombo vya habari vinafanya kazi kubwa kuyagundua na kuhabarisha umma na sasa wananchi wameshaamka na wanataka demokrasia ya kweli hivyo utawala lazima ubadilike," alisema Padri Mapunda.


Akifafanua kuhusu uchaguzi mkuu ujao mwakani, Padri Mapunda alisema viongozi wa kanisa hilo wamekubaliana umuhimu wa kufundisha waumini wao na tayari wameanza kutoa mafunzo na semina mbalimbali kuwaelimisha namna ya kupata viongozi bora na kwamba viongozi hao watapatikana kutokana na uwezo wao si kwa kutoa rushwa.

"Viongozi wasio na uwezo ndio wanaotumia nguvu kubwa (rushwa) kupata nafasi za kuingia madarakani ambapo badala ya kulitumikia Taifa wanafikiria kujilimbikizia mali ili kufidia gharama walizotumia wakati wa uchaguzi, hivyo tuwe makini nao,"alisisitiza Padri Mapunda.


Alisema wakati wa mabadiliko ukifika hauepukiki hivyo kama viongozi hawako tayari kubadilika mabadiliko yatawabadilisha kwa lazima kwani huo ndiyo mfumo wa maisha ya binadamu.

Alisema suala la ufisadi limekuwa wimbo usio na mwitikio kwa wananchi kutokana na Serikali kuchukua muda mrefu kumaliza kesi za ufisadi jambo ambalo linaweza kupatiwa ufumbuzi mapema.

Alisema maovu yanayoendelea kutokea hapa nchini kama yale ya ufisadi na mengine yanatokana na ubinafsi, mmomonyoko wa maadili na matumizi mabaya ya madaraka miongoni mwa watu wachache wenye nafasi za juu Serikalini.

"Tatizo ni ubinafsi wa watu wachache wenye tamaa ya kujilimbikizia mali ndio unaoumiza Watanzania wengi,"
alisema na kuongeza kuwa ni "Nguvu za Mungu pekee ndizo zitakazosaidia kupiga vita ufisadi huu unaoshamiri kwa kasi"

Alisema neno, 'ufisadi' na 'rushwa' sasa yamekithiri katika vinywa vya Watanzania na kuonya kuwa hali hiyo inaonesha kuwa sasa wamechoka na wakiamua kupambana na uovu huo wataweza.

Alisema ipo haja ya kufanyika mabadiliko Katiba kwa ya sasa imejaa viraka na haitoshelezi mahitaji ya demokrasia ya kweli.Alieleza kuwa hali hiyo inayotoa nafasi kwa watu kufanya maovu wanavyotaka bila ya kuchukuliwa hatua stahiki.

Alisema kuwa Katiba hiyo ni ya muda mrefu na ina maelekezo yaliyopitwa na wakati hivyo haikidhi mahitaji ya ulimwengu wa sayansi na teknolojia na inachangia kukwamisha maendeleo ya Taifa.

''Tunahitaji mapinduzi ya kikatiba wakati tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu kwani hata mtu asiye msomi anaweza kugundua udhaifu wa Katiba yetu na kama viongozi hawatakuwa tayari nguvu ya watu italeta mabadiliko,"alisema.

Padri Mapunda aliongeza kuwa Serikali ya Tanzania imeshindwa kuonesha demokrasia ya kweli kwa kushindwa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi jambo ambalo linasababisha vyama vya siasa kulalamika kila uchaguzi unapofanyika kwa kutotendewa haki.

Alisema NEC inateuliwa na viongozi wa chama tawala na wakati huo huo inasimamia uchaguzi wa viongozi wa vyama vyote ambapo mwanya wa kupendelea CCM unakuwa mkubwa.


"Hakutakuwa na amani hadi mabadiliko haya yafanyike kama jipu litaendelea kupakwa mafuta ipo siku litapasuka tu, hivyo ni bora marekebisho yakafanyika mapema kuliko kusubiri misukumo kutoka kwa wananchi waliochoshwa na Katiba hiyo," alisema.

Amevitaka vyama vya siasa kuacha ubinafsi kwani ni vigumu kwa chama kimoja kuchukua nchi kwa sasa ikiwa havina ushirikiano na badala yake vinapaswa kuweka malengo ya muda mrefu kwa kuzingatia maeneo ambayo vinaweza kuunganisha nguvu na kuweka mgombea anayekubalika na wengi.

Alisema kuwa malumbano baina ya vyama vya upinzani yamezidi kushamiri kutokana na mamluki walio ndani ya vyama hivyo kukwamisha mikakati endelevu na kushindwa kufikia malengo na kupoteza imani kwa wananchi hata pale wanapokuwa na malengo mazuri.

"Malumbano hayo yameikumba hadi CCM kufikia kiasi cha kupigana wakigombe madaraka hali ambayo inadhihirisha kuwa utawala sasa unahitaji mabadiliko kwani baadhi ya viongozi wamekosa uadilifu,'' alisema Padri Mapunda.


SOURCE: Majira







Shura ya Maimamu Tanzania, imezindua ‘Muongozo' kwa ajili ya waumini wa Kiislamu ambao itawaongoza wakati Watanzania wakielekea katika Uchaguzi Mkuu wa 2010.

Uzinduzi wa Muongozo huo unafanyika miezi michache baada ya Kanisa Katoliki nchini kutoa waraka unaowaelekeza waumini wake namna ya kuwachagua viongozi waadilifu wakati wa uchaguzi huo.

Muongozo huo uliopewa jina la "Muongozo kwa Waislamu", ulizinduliwa jijini Dar es Salaam jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja na Katibu wa Kamati Kuu ya Siasa ya Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, katika mkutano uliohudhuriwa na maelfu ya waumini wa jumuiya na taasisi za Kiislamu za Tanzania Bara na visiwani Zanzibar.

Muongozo huo ulio kwenye mfumo wa kijitabu chenye kurasa 45, umejikita zaidi katika kueleza maeneo 15, ikiwamo dhana ya maisha bora, hadaa za uchaguzi na dira ya Waislamu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Maeneo mengine ni taswira ya uchaguzi uliopita, dhana ya uchaguzi, uhuru wa kutoa maoni, tumefikaje hapa tulipo, maadili, elimu, afya, kilimo, fedha na uwezeshaji, umoja na amani, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na uwakilishi.

Akizindua Muongozo huo, Sheikh Ponda alisema wamefikia hatua hiyo kwa vile Waislamu ni jamii iliyodhulumiwa, ambayo inahitaji ukombozi na uhuru.

"Lakusikitisha Waislamu leo wanadai uhuru kutoka kwa ndugu zao weusi," alisema Sheikh Ponda.


Alisema anamshangaa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo, kuwataka Waislamu wasitoe Muongozo wao kwa vile waraka uliotolewa na Kanisa Katoliki umechafua mazingira na kuhoji: "Marmo alikuwa wapi hadi waraka ule ukachafua mazingira?"

Awali, akifungua mkutano huo, Amiri wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Mussa Kundecha, alisema kilichozinduliwa na Waislamu kisichukuliwe kuwa ni waraka kwa kuwa waraka ni kitu kinachotoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, bali walichozindua jana, ni Muongozo kwa Watanzania wote.

Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo serikali itaufuata Muongozo huo, itafanikiwa katika kutawala na ikiupuuza itawatawala Watanzania katika mazingira magumu, ambayo hayajapata kutokea.

Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania (Baraza Kuu), Sheikh Ramadhan Sanze, alisema Muongozo huo utaisaidia serikali kutawala vizuri, Watanzania kuishi kwa amani na waumini wa dini mbalimbali kutobaguana.

"Ni mwongozo kwa watu wote na si njama," alisema Sheikh Sanze.

Alisema tofauti na Muongozo huo, ipo hati ya makubaliano (MoU) iliyotiwa saini kati ya serikali na makanisa kwa lengo la kuwapendelea Wakristo nchini mwaka 1992.

Hata hivyo, Sheikh Sanze alisema anashangazwa namna MoU ilivyotiwa saini na aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa kwa niaba ya serikali.

Naye Sheikh Mohamed Issa akiwasilisha mada ya hali ya Waislamu kabla na baada ya uhuru Tanzania, alisema Muongozo huo hauna lengo la kuwabagua baadhi ya wanadini na kuwapendelea wengine, bali umejikita zaidi katika kuwataka Waislamu wasikubali kudhulumu na kudhulumiwa.

Alisema kwa kuzingatia hilo, katika uchaguzi ujao, Waislamu wako tayari kumchagua mgombea yeyote, asiyekuwa na chuki na Waislamu bila kujali anatoka chama gani cha siasa.

"Ila akiwa ana dalili za ufisadi hata akiwa Muislamu wa aina gani hatutamchagua," alisema Sheikh Issa.

Naye Imamu Mkuu wa Msikiti wa Idrisa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, Maalim Ally Bassaleh, alisema Waislamu wamekuwa wakidanganywa muda mrefu na kuwataka waumini hao katika uchaguzi mkuu mwakani kuhakikisha wanatamka: "Hatudanganyiki."

CHANZO: NIPASHE
Sijasoma Nyaraka hizo, lakini hizi hotuba za uzinduzi wa nyaraka hizo mbili zinaonyesha tofauti kubwa sana katika maudhui yao. Ingawa zote zimetolewa na viongozi wa dini kwa waumini wao, moja ina utaifa zaidi na nyingine ina udini zaidi.


Katika hotuba yake, Sheikh Ramadhan Sanze amedai kuwa mwaka 1992 serikali ilikubaliana na makanisa kuwa itawapendelea wakristo nchini. Hili ni jambo la ajabu sana na nadhani linaweza kusababisha msuguano usiokuwa wa lazima na serikali kwa maana tamko hilo linaweza kuchukuliwa kuwa lina lengo la kuleta uchochezi bila msingi wowote. Akumbuke kuwa mwaka huyo 1992 wakati wa serikali ya Mwinyi ndipo kulikuwa na matukio mengi ya kidini kama vile uvunjaji wa bucha za nguruwe. Sidhani kama ni kweli kuwa Rais Mwinyi wakati ule aligeuka na kuahidi kuwapendelea eti wakristo kwa gharama ya kuwadidimiza waislamu.

Naweza kuelewa kwa nini BAKWATA haitaki kuutambua waraka huo.
 
Bakwata imetangaza leo kuwa haiutambui waraka uliotolewa na Shura ya Maimamu jana.

Imesema hakuna mantiki kwa waislamu kuupinga waraka uliotolewa na Wakristo, halafu waislamu hao hao nao waamue kutoa wao. Watakuwa wametenda jema lipi kama waliona wakristo wamekosea?

Bakwata ni CCM, wanataka watu wakae kimya ili ufisadi wao uendelee.
 
Sijasoma Nyaraka hizo, lakini hizi hotuba za uzinduzi wa nyaraka hizo mbili zinaonyesha tofauti kubwa sana katika maudhui yao. Ingawa zote zimetolewa na viongozi wa dini kwa waumini wao, moja ina utaifa zaidi na nyingine ina udini zaidi.


Katika hotuba yake, Sheikh Ramadhan Sanze amedai kuwa mwaka 1992 serikali ilikubaliana na makanisa kuwa itawapendelea wakristo nchini. Hili ni jambo la ajabu sana na nadhani linaweza kusababisha msuguano usiokuwa wa lazima na serikali kwa maana tamko hilo linaweza kuchukuliwa kuwa lina lengo la kuleta uchochezi bila msingi wowote. Akumbuke kuwa mwaka huyo 1992 wakati wa serikali ya Mwinyi ndipo kulikuwa na matukio mengi ya kidini kama vile uvunjaji wa bucha za nguruwe. Sidhani kama ni kweli kuwa Rais Mwinyi wakati ule aligeuka na kuahidi kuwapendelea eti wakristo kwa gharama ya kuwadidimiza waislamu.

Naweza kuelewa kwa nini BAKWATA haitaki kuutambua waraka huo.

Usitegemee lolote la kimaendeleo la waislam litaletwa na Bakwata...Bakwata ni Taasis ya CCM/Serikali...Viongozi wake wanachaguliwa na Usalama wa Taifa/Viongozi wa Serikali...
Hawajafanya lolote tangu 1967 ilipoundwa...Walivyonavyo sasa ...Serikali ya Nyerere ilipora kutoka Taasis Rasmi ya waislam na kuwapa Bakwata....!!! Vingine wameuza....Walivyonavyo vimedumazwa...!!!

Kichuguu...Endelea kutaja mengine yaliyotokea wakati huo...!!!
 
Vilevile tukumbuke hawa Shura ya Maimamu ni taasisi ndogo ya kidini (NGO) na wanachama wake ni wanaharakati wachache lakini wenye uwezo wa kufanya kampeni ya nguvu.

Jambo la kufuatilia ni kujua ufadhili wao unatoka wapi? Source of their funding!
 
Hata ule wa wakatoliki haukuwa wa Wakristo wote!...
Unatakiwa utambue mantiki ya hii post, ni kwamba hakuna jumuiya yoyote ya Kikatoliki iliyoupinga ule wa Kikatoliki, ila hapa Jumuiya mojawapo ya Kiislamu ie Bakwata, imeupinga waraka wa Jumuiya nyingine ya Kiislamu. Nadhani utakuwa umegundua kwa nini mleta mada ameamua kuiweka humu !
 
Vilevile tukumbuke hawa Shura ya Maimamu ni taasisi ndogo ya kidini (NGO) na wanachama wake ni wanaharakati wachache lakini wenye uwezo wa kufanya kampeni ya nguvu.

Jambo la kufuatilia ni kujua ufadhili wao unatoka wapi? Source of their funding!
Kakalende mi nakuunga mkono.. TAFADHALI WANAJAMVI MWENYE INFORMATION KUHUSU HII TAASISI NA UFADHILI WAKE AWEKE JAMVINI.tunaweza kuwa tunapambana na mapapa hatujui.Anyway kama miongozo ni kwa ajili ya uchaguzi mkuu..meaning kuchagua viongozi waadilifu, ni vipi hawa wenzetu waislamu wawe kama wanajazba na hasira kwa wakristo huku wakijifanya eti ni muongozo..kwa mfano sheikh ponda anasema'Akizindua Muongozo huo, Sheikh Ponda alisema wamefikia hatua hiyo kwa vile Waislamu ni jamii iliyodhulumiwa, ambayo inahitaji ukombozi na uhuru.
waislamu wamedhulumiwa na nani? wamedhulumiwa na wakristo au mafisadi ?, kwani ni wasiseme watanzania wamedhulumiwa?mbona walaka wa wakatoliki umejumuisha watanzania wote?
“Lakusikitisha Waislamu leo wanadai uhuru kutoka kwa ndugu zao weusi,” alisema Sheikh Ponda.

hawa ndugu weusi wanaoongelewa hapa ni akina nani?
Jamani nionavyo mimi waislamu wamekuwa wa kulaumu kwamba wanaonewa..
sasa si swala la mafisadi tena bali ni ugomvi wao kwa wakristo, kuna sehemu nimesoma katika quotation kwamba ..eti serikali imetia saini na wakristo kuwapendelea.. that is nosense!!
mimi ninachosema badala ya waislamu kukaa na kulalamika wanaonewa ni bora wakafikiria kuithamini zaidi ELIMU DUNIA na kuacha kuendekeza hiyo wanayoiita elimu akhera..tunahitaji maprofessa wengi wa kiislamu..ukweli ni kwamba bila elimu hakuna maendeleo na bila maendeleo siku zote level yako itakuwa ya chini, na utaona unaonewa.
tunahitaji wawekeze zaidi kwenye mahospitali, mashule, vyuo n.k na siyo vinginevyo.
 
Vilevile tukumbuke hawa Shura ya Maimamu ni taasisi ndogo ya kidini (NGO) na wanachama wake ni wanaharakati wachache lakini wenye uwezo wa kufanya kampeni ya nguvu.

Jambo la kufuatilia ni kujua ufadhili wao unatoka wapi? Source of their funding!

Shura haina the so called wafadhili...Ndio maana wameamua kuuza waraka kwa Sh.2000, kufidia gharama zao...otherwise wangetoa bure kama wakatoliki...!!!
 
Unatakiwa utambue mantiki ya hii post, ni kwamba hakuna jumuiya yoyote ya Kikatoliki iliyoupinga ule wa Kikatoliki, ila hapa Jumuiya mojawapo ya Kiislamu ie Bakwata, imeupinga waraka wa Jumuiya nyingine ya Kiislamu. Nadhani utakuwa umegundua kwa nini mleta mada ameamua kuiweka humu !

Sinkala,

Tambua kuwa Ukatoliki sio Dini bali ni dhehebu katika ukristu.Elewa ndani ya ukristu kuna Walutheri, Waanglicana, wasabato, n.k n.k

Sasa je unataarifa kuwa KKKT na Anglican wanataka kutoa waraka zao kila mmoja?
 
Nimekuwa najiuliza siku zote huko Tanzania. Je Bakwata ina wafuasi wowote ukilinganisha na jumuiya nyingine za waislamu huko Tanzania especially Tanzania Bara.

Mimi naona kuna Jumuiya kama Baraza Kuu, Shura ya maimamu .n.k Hizi zina misimamo ya kidini sana katika kutetea haki za waislamu na uislamu.

Kwanini Serikali ya TZ inaikumbatia Bakwata? Kuna agenda gani kwa serikali?
 
Sijasoma Nyaraka hizo, lakini hizi hotuba za uzinduzi wa nyaraka hizo mbili zinaonyesha tofauti kubwa sana katika maudhui yao. Ingawa zote zimetolewa na viongozi wa dini kwa waumini wao, moja ina utaifa zaidi na nyingine ina udini zaidi.


Katika hotuba yake, Sheikh Ramadhan Sanze amedai kuwa mwaka 1992 serikali ilikubaliana na makanisa kuwa itawapendelea wakristo nchini. Hili ni jambo la ajabu sana na nadhani linaweza kusababisha msuguano usiokuwa wa lazima na serikali kwa maana tamko hilo linaweza kuchukuliwa kuwa lina lengo la kuleta uchochezi bila msingi wowote. Akumbuke kuwa mwaka huyo 1992 wakati wa serikali ya Mwinyi ndipo kulikuwa na matukio mengi ya kidini kama vile uvunjaji wa bucha za nguruwe. Sidhani kama ni kweli kuwa Rais Mwinyi wakati ule aligeuka na kuahidi kuwapendelea eti wakristo kwa gharama ya kuwadidimiza waislamu.

Naweza kuelewa kwa nini BAKWATA haitaki kuutambua waraka huo.

Hili linajulikana kuwa Tanzania Udini hi suala linalohusu Uislamu. Mbona tumshasoma Thread nyingi hapa pale anapochaguliwa Muislamu kwenye Post nyeti. Au tunasahau kuwa kila siku tunaimba Uislamu CC ya CCM. Huu ni double standard iwapo Waislamu wanatowa madai yao basi na tuangalie na kuona kuna ukweli kiasi gani au nini chanzo cha hali hiyo.
TANZANIA HII UDINI NI UISLAMU
 
Vilevile tukumbuke hawa Shura ya Maimamu ni taasisi ndogo ya kidini (NGO) na wanachama wake ni wanaharakati wachache lakini wenye uwezo wa kufanya kampeni ya nguvu.

Jambo la kufuatilia ni kujua ufadhili wao unatoka wapi? Source of their funding!

Tukishajuwa iweje? Kwani kipi walichofanya kibaya? Nguvu ya hoja ndio inayoleta kukubalika na wala sio nani aliefadhili. BAKWATA wanafadhiliwa na Serikali lakini hawana hoja kwa Waislamu walichoweka mbele ni ngawira kutoka kwa JK.
 
Nimekuwa najiuliza siku zote huko Tanzania. Je Bakwata ina wafuasi wowote ukilinganisha na jumuiya nyingine za waislamu huko Tanzania especially Tanzania Bara.

Mimi naona kuna Jumuiya kama Baraza Kuu, Shura ya maimamu .n.k Hizi zina misimamo ya kidini sana katika kutetea haki za waislamu na uislamu.

Kwanini Serikali ya TZ inaikumbatia Bakwata? Kuna agenda gani kwa serikali?

NI rahisi kununuliwa kwani wote ni njaa tupu hakuna suala la dini pale!
 
hawa ndugu zetu inabidi wawe makini sana manake mtu akiwapinga wataanza hata kumuita kafiri!!!
 
Back
Top Bottom