Tume ya Katiba
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,896
- 1,862
Wadau,
Huku baadhi ya watu, hasa wanasiasa ambao kitaaluma wengi sio wachumi wakionyesha kutoridhishwa na bajeti ya 2012/2013. Mchumi aliyebobea amesema bajeti inawajali sana watoto lkatika afya na elimu.
Na Ninaeli Masaki,
Imeelezwa kuwa bajeti mpya ya mwaka 2012/13 ina mwelekeo mzuri katika kuwajali watoto kwa kuwa imetoa kipaumbele katika sekta za elimu na afya.
Akizungumza katika warsha ya waandishi wa habari iliyohusu bajeti ya watoto, mchumi wa kujitegemea Dk. Daniel Ngowi, alisema nchi inatakiwa kupanga bajeti ambayo ni rafiki kwa mtoto kwasababu zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania ni watoto.
"Serikali inatakiwa kupanga bajeti inayokidhi mahitaji ya kundi kubwa la wananchi na zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania ni watoto naona ni vyema kwamba bajeti haijawasahau watoto katika sekta ya elimu na afya," alisema Dk. Ngowi.
sosi: :: IPPMEDIA
Huku baadhi ya watu, hasa wanasiasa ambao kitaaluma wengi sio wachumi wakionyesha kutoridhishwa na bajeti ya 2012/2013. Mchumi aliyebobea amesema bajeti inawajali sana watoto lkatika afya na elimu.
Na Ninaeli Masaki,
Imeelezwa kuwa bajeti mpya ya mwaka 2012/13 ina mwelekeo mzuri katika kuwajali watoto kwa kuwa imetoa kipaumbele katika sekta za elimu na afya.
Akizungumza katika warsha ya waandishi wa habari iliyohusu bajeti ya watoto, mchumi wa kujitegemea Dk. Daniel Ngowi, alisema nchi inatakiwa kupanga bajeti ambayo ni rafiki kwa mtoto kwasababu zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania ni watoto.
"Serikali inatakiwa kupanga bajeti inayokidhi mahitaji ya kundi kubwa la wananchi na zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania ni watoto naona ni vyema kwamba bajeti haijawasahau watoto katika sekta ya elimu na afya," alisema Dk. Ngowi.
sosi: :: IPPMEDIA