Bado natafakari kauli ya Malima kwamba zile silaha ni mtaji mkubwa wa maisha!

Kuna Waziri wetu mwingine alishikwaga nje na Risasi za AK45. Hii yote Ni tabia ya viongozi wapagani waoga wasiojiamini na hawajui kabisa wamekuja duniani kufanya nini.
 
sasa hizo silaha zimemsaidia nini kama anaibiwa kiulaini namna hiyo?hata angekua na kifaru wangemchapa tuu
Kweli mkuu. Anajaribu kutunga story to kuficha ukweli. But kuna mambo mengi hayaeleweki, hajaipanga vizuri story yake.
 
Buchanan
Huyu ndugu ni muheshimiwa na ni mtu wa hotuba kwahiyo sitashangaa sana kama atasema vinasa sauti ni kwaajili ya ‘kujinasa’ sauti yake mwenyewe ya hotoba ili baada ya kusikiliza na kurudiarudia mara kwa mara (‘ku-rehearse’) huku akisahihisha, ‘atoke’ na toleo la hotuba nzuri na yenye ‘mvuto’ zaidi.

Lakini: haiingii akilini hata kama alikuwa anasafari kwenda nje ya nchi hicho kiasi cha hela kutembea nacho mfukoni kwa tekinolojia iliyopo sasa bado ni kikubwa, silaha ya kivita anakaa nayo hotelini kwa nini? anamlinda nani? anajilinda dhidi nini/nani? kwa nini? kama anahitaji ulinzi mkali kiasi hicho si angepewa ‘bodyguard’? wakati anaibiwa alikuwa wapi? kama ana maadui wengi kiasi hicho mbona basi alikuwa mbali na silaha yake ya kivita?

Jambo moja bado hamjalijua, kwamba yule bwana ni mtaalam wa kuwakamerun machali wenye njaa ya pesa. Sasa siku hiyo kama kawaida yake akamchukua dogo fulani mgozi. Sijui huko ndani dogo kafanikiwe kumchosha at the muximum na kwa kwa sababu ya uchovu jamaa kalala uzingizi wa pono. Dogo kasepa na kila kitu alichokiona kinamfaa. Baada ya masaa mengi jamaa ndiyo anaakuja kuzinduka, ndiyo kutunga draft ya dirisha kuvunjwa. Hilo litakkuwa fundisho kwake la kuachana na ukamerun la sivyo machali wataendelea kumliza.
 
SMG ni silaha inayojulikana kama "assault automatic weapon" ambayo kwa sheria za Tanzania ni vyombo vya majeshi ya serikali tu vinavyoruhusiwa kumiliki. Mtu binafsi huruhusiwi kuwa na "assault weapon". Hivyo tunataka IGP na Waziri wa ndani atupe majibu kamili kama Malima alikuwa na silaha hii kihalali, na huo uhalalishaji wa kumilikishwa "assault weapon" ulitoka wapi.

Mkuu, inavyoo onekana ni kwamba viongozi wa Tanzania wako juu ya sheria. Sheria inatumika tu pale ambapo mtenda kosa ni kapuku. Kimsingi kabisa, huyu bwana malima angetakiwa awe yuko mahabusu "kuisadia" polisi.
 
Kua na Bastola sio tatizo lakini alikua pia na kitu kama hii???????
kedr1.jpg
 
jamani tuliambiwa 1995 kuwa kama tunawapenda kwa sura zao tukanye kahawa nao na kama ni wahuni wakafanye uhuni wao huko mabarabarani lakini sio kuwapa nafasi watuongoze lakini hatukuweza kuyatafakari nakujua maana hivyo mpaka pale tukapo tafakari juu ya uongozi tunautaka kwa nchi yetu mbona viongozi waleo hamuishi VITUKO haya shauri yenu:flock:nie napita tuu
 
Mtumishi wa Uma una cash 4000$ na 1.5m! kama pocket money? mamamaeee walahi
 
Hivi hizi baraghashia hazipo kwenye orodha ya mabegi matatu ya nguo wangetutajia mpaka na idadi ya kufuli alizobeba na dhamani yake,mabegi matatu ya nguo na silaha za kivita huyu alikuwa safarini kwenda kujiunga na allshabab
Wanajamii habari ya Jumapili. Ninaamini ni wazima na mnaendelea vizuri. Nimesoma gazeti la mwananchi la leo kwenye kichwa cha habari kinachoeleza kuibiwa kwa naibu huyu wa waziri naomba kunukuu sehemu hii

Vitu alivyoibiwa ni pamoja na laptop tatu, aina ya Dell zenye thamani ya Sh5.6 milioni. Vinasa sauti viwili vya digitali na headphone zake zote ambavyo thamani yake ni Sh milioni moja, simu tatu, ya kwanza Nokia C6 ya Sh500,000, Nokia E200 ya Sh250,000 na Blackberry yenye thamani ya Sh5.5 milioni,” alisema kamanda huyo na kuongeza:

“Vitu vingine ni pete mbili za almasi zenye thamani ya Sh2.5 milioni, Dola za Marekani 4,000 ambazo ni sawa na Sh6.5milioni, fedha taslimu Sh1.5 milioni, kadi mbili za benki, mabegi matatu ya nguo, baraghashia mbili zenye thamani ya Sh50,000 na nyaraka mbalimbali za Serikali.”

Kaimu kamanda huyo alisema kuwa polisi waliokwenda kufanya uchunguzi wa awali walibaini kuwa mtu aliyeiba vitu hivyo hakuwa amevaa viatu kutokana na nyayo za miguu yake zilizoonekana nje ya chumba alichokuwa naibu waziri huyo.

Hata hivyo, Kaimu Kamanda huyo ambaye pia ni Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Morogoro, alisema mwizi aliyeiba vitu hivyo hakuiba bastola na bunduki aina ya SMG alizokuwa nazo Naibu Waziri huyo ambazo zilikuwa sehemu ya wazi
.""

Jamani naomba kujua huyu kiongozi silaha zote hizi ni za nini? Je viongozi wanaruhusiwa kuwa na sila za kivita na kutembea nazo kokote? hivi vitu vyote alikuwa anataka kuhama mkoa au nchi?

Naomba kuwasilisha!
 
Mtaji wa kimaisha alikuwa anamaanisha ukiwa nazo unakodisha kwa wazee wa kazi unapata mkwanja

hujakosea kabisa, kwanza jamaa nilivyomuona kwenye TV inaonyesha alikua anaulevi, kaziba haswa, ww inakuwaje ulale ndani halaf mwizi aingie hata usijue? Kama sio pombe ni nn? au usikute alitaka kutolipia huduma kiburudisho, ndo akaachwa saa amelala.
 
Mkuu huyu jamaa alikuwa na madini yenye thamani kubwa..ndio maana inabidi atumie bunduki mbili kuyalinda!
mbaya zaidi yule malaya aliondoka na baadhi ya madini.

Kumbe ulikuwa hujui...mh. alikuwa patner na papaaa Muzamir young milionaire, papaa Musofee, Ally Aurora biashara yao
kubwa ni madini mangumashi wakiwaliza wazungu kila wakati...nilifikiri amepata ubunge na uwaziri ameacha hizo deal, kumbe bado!!
 
Kumbe ulikuwa hujui...mh. alikuwa patner na papaaa Muzamir young milionaire, papaa Musofee, Ally Aurora biashara yao
kubwa ni madini mangumashi wakiwaliza wazungu kila wakati...nilifikiri amepata ubunge na uwaziri ameacha hizo deal, kumbe bado!!

Basi ndio maana ana silaha za kivita!
 
Ndugu zangu,

Mimi bado najiuliza hivi Malima alikuwa anamaanisha nini aliposema kwamba silaha mbili zilizokoswakoswa kuibwa ni mtaji mkubwa wa maisha. Binafsi kwa kiongoozi mkubwa kama yeye naona kama hakupaswa kuongea hivyo. Kama ndivyo anavyoamini basi nchi hii tuna laana kubwa sana. Sisi wananchi tunawezaje kumtofautisha yeye na hao wanaotumia zana hizo kama mtaji. Inavyoonekana, aliyeiba ni changudoa wake maana tangu lini changudoa akahitaji silaha.

Nitafurahi wanaharakati wakifungua kesi dhidi ya Malima ili atueleze silaha hizo anazitumia kwa biashara gani.

Naibu waziri amedhihirisha uwepo wa authorised crime. Kama wanajeshi na polisi wanolipwa mshahara wa kuwatosha siku kumi tu za mwezi wakati walinda na kuhifadhi maghala yenye 'Mtaji mkubwa wa maisha' ni dhahiri kuwa majambazi wanaochachafya wananchi ni miongoni mwa watu tuliowapatia dhamana ya kutulinda na viongozi kama kina Malima wanajua hilo.
 
Wizi mtupu....sasa kiongozi anamiliki silaha kama SMG yenye uwezo wa kubeba risasi 30 halafu anasema kwamba ndo mtaji wake wa maisha inaonyesha wazi kuwa huwa inatumika kwa shughuli za uhalifu mara nyingi sababu sidhani kama sheria za nchi zinaruhusu silaha kama hiyo kumilikiwa na mtu binafsi....napenda kuwasilisha mtazamo wangu kwa wanaJF...
 
Comrade kama wewe ambavyo hujapata majibu ktk hiyo tafakuri yako jadidu nami pia nimegubikwa na maswali mengi sana.Nimesoma kwenye mwananchi kwamba siraha mojawapo ilikua SMG. nijuavyo SMG NI siraha ya kivita ambayo mtu binafsi haruhusiwi kuimiliki hapa Comrades naombeni ufafanuzi wenu.Ni vipi Bwn Adam amiliki siraha hii?

Nafikiri wanajiandaa kwa vita,si unajua gap la wenye nacho na wasiokuwa nacho limekuwa kubwa sana,saa yoyote mambo yanaweza kubadirika,"USIMUONE KOBE KAINAMA......................................"
 
Nashukuru kama na nyinyi wenzangu mmeliona hili la vitu vya anasa.Kinachonishangaza zaidi ni hizi silaha hasa SMG au alibeba SMG UZIGURN?Maana navyofahamu ni kuwa smg ni silaha kubwa ya kivita.Kwa msingi huu inaonyesha anacho kibali cha kumiliki silaha ya kivita.
 
Vinasa sauti waziri????? alisahau camera za kiuchunguzi, maana anaonekana alikuwa kikazi zaidi.Serikali ikikaa kimya hapa nitaishangaa sana, Vuai nahodha aleleze umiliki huo wa SMG ulipitishwa na nani na kwa madhumuni gani na ilinunuliwa wapi.
Kwa uelewa wangu hiyo hoteli ya chumba cha 400,000 ni kubwa na lazima itakuwa na kamera za security, sijasikia popote wanazizungumzia maana najua wameshafuta hiyo part huyo mdada alipokuwa anatoka chumbani na mizigo yake
 
Back
Top Bottom