DA HUSTLA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2012
- 3,663
- 3,881
Jaman wadau naomba mnisaidie kuhusu hili jambo,nlikua na mwanamke/mpenzi wangu nlikua nampenda sana kupita maelezo.Ikaja ikatokea akaanza kunibadilikia,visirani kila saa tukiwa na miadi haji bila sababu za msingi na wala hapokei simu baadae ukimuuliza anasema alikua tight alishindwa kuja vile vile angepokea simu nisingemuelewa kabisa n.k.Nliamua nipumzike kidogo japo roho iliniuma sana na sikupenda hali ile itokee.Ilipita kma miez miwili bila kuwasiliana nae siku moja nikakutana nae mahali fulan hivi akiwa na rafiki yake ambaye ni mtu wake wangu wa karibu,sikupiga nae sana stori na yeye aliondoka mapema sana akaniacha na rafiki yake,nikapotezea ila wiki iliyofuata akanipigia simu tukawa tunawasiliana mara mojamoja,kwa kuwa nlikua bado nampenda basi ikabidi nirudishe mahusiano ila baada ya muda mfupi tukaanza kuyumba yumba tena.Tulivyokuja kuzinguana tena akanichana akaniambia mi ni mnafiki na hataki kuendelea na mimi tena,me skupenda afikie uamuzi huo mapema but alisema its over roho iliniuma sana mpaka sasa na nampenda sana nashindwa nifanyeje niweze kumsahau kila nikikumbuka baadhi ya mambo moyo unaniuma sana,wadau nisaidien nifanyeje???na ni mwanamke nliyefikiria tuishie kwenye ndoa.