Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
wapendwa,
nimehuzunishwa na habari za kuchomwa moto makanisa huko Zanzibar!
napenda kusema kuwa, kanisa laweza kuchomwa moto na hata biblia pia!
kisichoweza kuchomwa moto ni Mungu tu. wale maaskari wa kiyahudi walipijitahidi kumuua Mwana wa Mungu kwa ruhusa ya pilato aliyeshinikizwa na wakuu wa mafarisayo, lakini waliishia kukiri kuwa "alikuwa Mwana wa Mungu"
sasa niwatoe hofu kabisa wapendwa, acheni makanisa yachomwe moto. nyie kesheni katika sala mkijua kuwa shetani katoka kifungoni na anajiua kuwa ana muda mchache tu!!
zaidi sana nawakazia mzitazame siasa! wanasiasa wetu wamekosa weledi wa kufanya siasa na sasa nawafanya "mambo ya siasa"!! muungano wetu umeachwa bila maelezo ya kuwa una faida gani? vijana wasio na kazi, pesa wala akili, wanadanganywa kuwa wakivunja muungano watapata pesa toka OIC na jumuiya nyingine za kiislamu; na zitawawezesha kuwa matajiri!
viongozi wetu wanachekelea anasa za mashangingi waliyolazimisha kujinunulia kwa jasho la wananchi masikini. wanajiita waheshimiwa, wanajitutumua kuchoma nyavu za kuvulia samaki ili waonekane "wachapa kazi", lakini mwisho wa siku hawana cha kujishaua mbele ya watanzania kuwa wamelitumikia taifa lao.
siasa yetu imekufa, imebaki "biashara ya siasa"!
hebu tuamke, tuamke kuipigania nchi yetu!
Mungu ibariki Tanzania, ibariki Afrika,
Kidumu Chama Cha Mapinduzi!
bado nakiamini Chama Cha Mapinduzi, kinaweza kutukomboa!
Glory to God!
nimehuzunishwa na habari za kuchomwa moto makanisa huko Zanzibar!
napenda kusema kuwa, kanisa laweza kuchomwa moto na hata biblia pia!
kisichoweza kuchomwa moto ni Mungu tu. wale maaskari wa kiyahudi walipijitahidi kumuua Mwana wa Mungu kwa ruhusa ya pilato aliyeshinikizwa na wakuu wa mafarisayo, lakini waliishia kukiri kuwa "alikuwa Mwana wa Mungu"
sasa niwatoe hofu kabisa wapendwa, acheni makanisa yachomwe moto. nyie kesheni katika sala mkijua kuwa shetani katoka kifungoni na anajiua kuwa ana muda mchache tu!!
zaidi sana nawakazia mzitazame siasa! wanasiasa wetu wamekosa weledi wa kufanya siasa na sasa nawafanya "mambo ya siasa"!! muungano wetu umeachwa bila maelezo ya kuwa una faida gani? vijana wasio na kazi, pesa wala akili, wanadanganywa kuwa wakivunja muungano watapata pesa toka OIC na jumuiya nyingine za kiislamu; na zitawawezesha kuwa matajiri!
viongozi wetu wanachekelea anasa za mashangingi waliyolazimisha kujinunulia kwa jasho la wananchi masikini. wanajiita waheshimiwa, wanajitutumua kuchoma nyavu za kuvulia samaki ili waonekane "wachapa kazi", lakini mwisho wa siku hawana cha kujishaua mbele ya watanzania kuwa wamelitumikia taifa lao.
siasa yetu imekufa, imebaki "biashara ya siasa"!
hebu tuamke, tuamke kuipigania nchi yetu!
Mungu ibariki Tanzania, ibariki Afrika,
Kidumu Chama Cha Mapinduzi!
bado nakiamini Chama Cha Mapinduzi, kinaweza kutukomboa!
Glory to God!