Dangire
JF-Expert Member
- Oct 5, 2011
- 221
- 68
Miongoni mwa mambo yanayochelewesha kasi ya maendeleo ya nchi hii ni kile kinachojulikana kama 'mwamko mdogo wa watanzania juu ya nchi yao'. Ni zaidi ya miaka 50 sasa tangu nchi hii ipate uhuru, bado tungali tunaishi katika hali ya 'ukondoo' (wengi hawawezi kujenga hoja, kuuliza swali,nk...ni watu wa ndio mzee!!!!!!). Hii imetokana na sera ya kikoloni ya kuwafanya watawaliwa watawalike (pasification policy).walitujengea woga kwa watawala,;walitupa elimu ya kwao ili tusijitambue na kuwatukuza wao; walituambia tuwapende maadui zetu (wao), nk.
Matokeo yake, ijapokuwa tunasema kwa miaka ya hivi karibuni watz wameamka, ni wazi kuwa bado mwamko huu si wa kutufanya tuendelee.......we have to be more than active to respond to different happenings in our country. hebu fikiria, ripoti ya CAG ya hivi karibuni imeonesha ufisadi mkubwa sana serikalini, ambapo mabilioni na matrilioni ya pesa za wavuja jasho wa nchi hii zimeteketezwa na walafi wachache tu! huku hali ngumu na umasikini wa watanzania ukizidi kushamiri. Lakini bado watanzania tunasikiliza na kisha kusahau.......maisha yanasonga mbele!! hivi taarifa hizi hazitugusi???
nchi za wenzetu kama malawi, msumbiji, nigeria, zambia, nk. huandamana kwa kupanda bei mkate, mafuta, nk. kwa kiasi kidogo....sisi tunaridhika na hali hii iliyopo.......ama.........
Mkisikia kesho ninaandama peke yangu naomba mniunge mkono.........am tired!
Matokeo yake, ijapokuwa tunasema kwa miaka ya hivi karibuni watz wameamka, ni wazi kuwa bado mwamko huu si wa kutufanya tuendelee.......we have to be more than active to respond to different happenings in our country. hebu fikiria, ripoti ya CAG ya hivi karibuni imeonesha ufisadi mkubwa sana serikalini, ambapo mabilioni na matrilioni ya pesa za wavuja jasho wa nchi hii zimeteketezwa na walafi wachache tu! huku hali ngumu na umasikini wa watanzania ukizidi kushamiri. Lakini bado watanzania tunasikiliza na kisha kusahau.......maisha yanasonga mbele!! hivi taarifa hizi hazitugusi???
nchi za wenzetu kama malawi, msumbiji, nigeria, zambia, nk. huandamana kwa kupanda bei mkate, mafuta, nk. kwa kiasi kidogo....sisi tunaridhika na hali hii iliyopo.......ama.........
Mkisikia kesho ninaandama peke yangu naomba mniunge mkono.........am tired!