Badilisha mfumo wa utoaji wa Leseni, Maisha yataokolewa mengi

Radical

JF-Expert Member
Jun 3, 2009
374
44
Hakuna siri kuwa utoaji wa leseni za udereva umegubikwa na rushwa tupu, ndio maana ajali ni nyingi mno. Mtu anayenunua leseni si sawa na yule anayepitia mafunzo halali na intensive, coz hajui dhamana anayobeba.
Tabia za kijinga za ku-ovateki, spidi kali, nk kwa muendesha gari (simuiti dereva) zinasababishwa na ukosefu wa mafunzo juu ya heshima ya chombo.

For once please, rekebisha huu mfumo otherwise tutafanya wiki nenda kwa usalama, semina, matamasha, nk lakini ajali zitaendelea kutuua...
 
Rushwa inatusumbua sana kuna vijana wanatamni wapate leseni zitakazowawezesha kuajiriwa kama madereva lakini hakuna proper channel ya kupata sijui class C. Responsible authority dont even bother to educate tanzanians on how and when they can get Class C. Red tapism shit!!!!!!!!!!
 
Ni kweli kabisa kama Fullgadiva J, alivyosema hapo juu.Chanzo cha tatizo la ajali nchini ni uendeshaji mbaya unaotokana na utoaji wa leseni kwa njia ya rushwa.Pili wanategemewa kusimamia usalama barabarani ndio hao wala rushwa wakubwa na pia wana magari yao binafsi ya biashara kwa hiyo wanawaajira watu wasio na sifa ya udereva kwa kuwa hawawalipi mishahara kabisa.Kutatua tatizo ni lazima kumaliza tatizo la rushwa kwanza!
 
Mkuu unaposema mfumo ubadilishwe kwa Tanzania inabeba maana kubwa, inabidi wahusika wote waondolewe wawekwe watu wengine, kuna sheria imewekwa ili kuweza kupata license class C, lakini ukiihitaji unaweza kumalizana na wahusika ndani ya siku moja na ukapata leseni yako.. NIT sijui kitu gani imetengeneza tu mwanya mwingine wa rushwa, vyeti vinapatikana mtaani mradi pesa yako tu..!
 
Tatizo la Tanzania ni kuwa tunaegemea sheria sana kuliko kuegemea maadili.
''sometimes something can be legally accepted but not ethically accepted''
 
Back
Top Bottom