Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,799
- 59,263
Nawasalim wote dadazz na kakazz bila kuwasahau wamama na wababa!!!
Natumaini jumatatu mmeianza vyema na wiki itaendelea kua nzuri.
Kama wimbo tunasikia kila siku mwanamke alivyo na nafasi kubwa katika kuharibu/jenga nyumba yake (mahusiano).Ni kweli kwamba mwanamke anaweza kubomoa nyumba yake mwenyewe...ila tukiangalia hili swala bila upendeleo, mwanaume ndiye anayemuwezesha mkewe kuwa mjenzi au mharibifu wa nyumba yao!!!
Kwa kina baba mnaodhani small house ndio suluhisho la matatizo yaliyopo majumbani mwenu hua mnakosea sana.
Visingizio vikuu ni kwamba small house hanuni.. mapokezi mazuri....sijui anapendeza...mapenzi anatoa yote...heshima na maelewano vinakuwepo n.k kinyume na maisha yalivyo nyumbani!Mnajua kwanini???Kwasababu hata mnayofanya huko ni tofauti na mnayowafanyia wake zenu!
Unakuta mtu nyumbani unaombwa pesa ya ada au matumizi tu ya kawaida unafoka kwamba huna pesa...huku kwa nyumba ndogo unalipa kodi...gari yake unaweka mafuta ....shopping unamfanyia na matatizo yake unamtatulia!
Small house hufiki kwake ukaanza kumkemea au kumkaripia na kila anachotaka unampa...sasa akasirike kitu gani?Ukifika huko unaita sweety...baby sijui darling kwa kubembeleza...ukifika kwako ni ''we mama nanii kuja hapa''....mara sijui fanya hivi fanye vile kwa ukali utadhani sio mwenzako.
Small house hakulelei watoto wala hakuaangalizii nyumba na kujali familia yako...wala hana mawazo yanayohusiana na maendeleo yenu ya kifamilia kwahiyo anakua relaxed na muda zaidi wa kujijali yeye mwenyewe ndo maana kila saa kapendeza...bila kusahau wewe unavyompendezesha kwa kumpeleka shopping bila kusahau pesa za saloon zisizoisha kuombwa!
Nwyz my point is....BADILIKA!!!
Huwezi kulalamika mtu ananuna tu muda wote kama hujampa kitu cha kufurahia....au hakupokei vizuri ikiwa mwenyewe ukifika getini tu unageuka simba...lazima nae atakua katika hali ya woga na kukosa amani!!
Kua mzuri kwa mke wako..acha kurudi nyumbani na magadhabu maana hayo ndio yanayotengeneza tension.Kua mpole na mkarimu kwa mkeo.
Acha kumkaripia na kumgombeza kama mtoto akikosea ongea nae kama mtu mzima mwenzako.
Muonyeshe upendo kama unaodhamiria kuuonyesha au tayari unauonyesha huko kwa nyumba ndogo.
Mjali ....kama unaona hajijali sana mshawishi kufanya hivyo....mpeleke shopping mwenyewe..msukume ajiweke safi na katika hali ya kuvutia.
Kina mama/dada na sisi tusijisahau jamani!!Mpe mwenzio sababu ya kuwahi nyumbani na kutaka kuwa karibu na wewe!Sio mtu akiona muda wa kazi umeisha anahema kama katwishwa mzigo...hata hamu hana!
Nawakilisha!!!
Natumaini jumatatu mmeianza vyema na wiki itaendelea kua nzuri.
Kama wimbo tunasikia kila siku mwanamke alivyo na nafasi kubwa katika kuharibu/jenga nyumba yake (mahusiano).Ni kweli kwamba mwanamke anaweza kubomoa nyumba yake mwenyewe...ila tukiangalia hili swala bila upendeleo, mwanaume ndiye anayemuwezesha mkewe kuwa mjenzi au mharibifu wa nyumba yao!!!
Kwa kina baba mnaodhani small house ndio suluhisho la matatizo yaliyopo majumbani mwenu hua mnakosea sana.
Visingizio vikuu ni kwamba small house hanuni.. mapokezi mazuri....sijui anapendeza...mapenzi anatoa yote...heshima na maelewano vinakuwepo n.k kinyume na maisha yalivyo nyumbani!Mnajua kwanini???Kwasababu hata mnayofanya huko ni tofauti na mnayowafanyia wake zenu!
Unakuta mtu nyumbani unaombwa pesa ya ada au matumizi tu ya kawaida unafoka kwamba huna pesa...huku kwa nyumba ndogo unalipa kodi...gari yake unaweka mafuta ....shopping unamfanyia na matatizo yake unamtatulia!
Small house hufiki kwake ukaanza kumkemea au kumkaripia na kila anachotaka unampa...sasa akasirike kitu gani?Ukifika huko unaita sweety...baby sijui darling kwa kubembeleza...ukifika kwako ni ''we mama nanii kuja hapa''....mara sijui fanya hivi fanye vile kwa ukali utadhani sio mwenzako.
Small house hakulelei watoto wala hakuaangalizii nyumba na kujali familia yako...wala hana mawazo yanayohusiana na maendeleo yenu ya kifamilia kwahiyo anakua relaxed na muda zaidi wa kujijali yeye mwenyewe ndo maana kila saa kapendeza...bila kusahau wewe unavyompendezesha kwa kumpeleka shopping bila kusahau pesa za saloon zisizoisha kuombwa!
Nwyz my point is....BADILIKA!!!
Huwezi kulalamika mtu ananuna tu muda wote kama hujampa kitu cha kufurahia....au hakupokei vizuri ikiwa mwenyewe ukifika getini tu unageuka simba...lazima nae atakua katika hali ya woga na kukosa amani!!
Kua mzuri kwa mke wako..acha kurudi nyumbani na magadhabu maana hayo ndio yanayotengeneza tension.Kua mpole na mkarimu kwa mkeo.
Acha kumkaripia na kumgombeza kama mtoto akikosea ongea nae kama mtu mzima mwenzako.
Muonyeshe upendo kama unaodhamiria kuuonyesha au tayari unauonyesha huko kwa nyumba ndogo.
Mjali ....kama unaona hajijali sana mshawishi kufanya hivyo....mpeleke shopping mwenyewe..msukume ajiweke safi na katika hali ya kuvutia.
Kina mama/dada na sisi tusijisahau jamani!!Mpe mwenzio sababu ya kuwahi nyumbani na kutaka kuwa karibu na wewe!Sio mtu akiona muda wa kazi umeisha anahema kama katwishwa mzigo...hata hamu hana!
Nawakilisha!!!