Mlitika
JF-Expert Member
- Mar 23, 2012
- 457
- 260
Mabingwa watetezi wa kabumbu nchini Dar Y.A. leo/jana (samahani, sina hakika na saa yangu) walikuwa wageni wa Coastal Union huko ugosini ambapo muda wa mchezo uliisha kwa mabingwa hao watetezi kuwa mbele kwa bao moja. Katika mechi hiyo mabingwa hao watetezi walimchezesha Stephano Mwasika ambaye kwa kadiri ya sheria za kabumbu alikuwa bado anatumikia kifungo halali cha Kadi nyekundu kwa kosa la kumchapa makonde mwamuzi. Baada ya rapsha za mechi hiyo Kamati ya Mashindano ya TFF ilitembeza kibano kwa wachezaji watano wa Yanga ambapo bondia Mwasika pamoja na kifungo cha kawaida cha kadi nyekundu cha kuwa benchi kwa mechi zisizopungua tatu alilimwa ban ya kuwa nje ya ligi kwa MWAKA MMOJA.
Katika hali inayo-apply tu katika busara za soka la Kibongo Kamati ya Nidhamu ya TFF chini ya njagu mstaafu Tiba iliamua kuondoa vibano vya wanasoka hao. Yanga kwa ulevi wa ushindi wa kesi wakaamua kumchezesha Mwasika leo (jana) wakijisahaulisha kuwa ishu yake ilikuwa na adhabu mbili toka Mamlaka mbili tofauti
1. Kadi nyekundu which is indubitable kwa maana kwamba ktk sheria za kabumbu hakuna awezaye kutangua maamuzi ya refa halafu matokeo ya mechi yabaki halali. Mamlaka yoyote itakayotangua maamuzi ya refa hata katika tukio moja la mchezo basi maamuzi yoye ya refa kisheria yanapashwa kuwa batili na kwa sababu hiyo mechi inapashwa kurudiwa.
2. Kamati ya Mashindano ya TFF ilimpa Mwasika mezani hiyo ban ya mwaka 1 kama adabu ya pili (ambayo haifuti ile ya kwanza).
Ili iwe halali kwa adhabu ya kwanza hapo juu kufutwa na kamati ya Tiba ni lazima sentenso zifuatazo ziwe mantiki sahihi:
· Maamuzi ya refa siyo ya mwisho / maamuzi mbadala yanaweza kutolewa na mtu kama Tiba ambaye siyo lazima awe uwanjani wakati mechi inachezwa.
· Mwasika alikuwa sahihi kumpiga refa/ Mwasika kumpiga refa ilikuwa halali ndiyo maana kadi nyekundu aliyopewa siyo halali.
Kama tukifuata tu sheri za FIFA ili kujenga heshima yetu na kukuza nidhamu ya wachezaji wetu ambayo ni mbovu na ndiyo inayodidimiza soka letu, Yanga wana sababu ipi ya kutonyang'wanywa pointi tatu za mechi hii?
SOSI NI MIMI NA SHERIA ZA SOKA!
Katika hali inayo-apply tu katika busara za soka la Kibongo Kamati ya Nidhamu ya TFF chini ya njagu mstaafu Tiba iliamua kuondoa vibano vya wanasoka hao. Yanga kwa ulevi wa ushindi wa kesi wakaamua kumchezesha Mwasika leo (jana) wakijisahaulisha kuwa ishu yake ilikuwa na adhabu mbili toka Mamlaka mbili tofauti
1. Kadi nyekundu which is indubitable kwa maana kwamba ktk sheria za kabumbu hakuna awezaye kutangua maamuzi ya refa halafu matokeo ya mechi yabaki halali. Mamlaka yoyote itakayotangua maamuzi ya refa hata katika tukio moja la mchezo basi maamuzi yoye ya refa kisheria yanapashwa kuwa batili na kwa sababu hiyo mechi inapashwa kurudiwa.
2. Kamati ya Mashindano ya TFF ilimpa Mwasika mezani hiyo ban ya mwaka 1 kama adabu ya pili (ambayo haifuti ile ya kwanza).
Ili iwe halali kwa adhabu ya kwanza hapo juu kufutwa na kamati ya Tiba ni lazima sentenso zifuatazo ziwe mantiki sahihi:
· Maamuzi ya refa siyo ya mwisho / maamuzi mbadala yanaweza kutolewa na mtu kama Tiba ambaye siyo lazima awe uwanjani wakati mechi inachezwa.
· Mwasika alikuwa sahihi kumpiga refa/ Mwasika kumpiga refa ilikuwa halali ndiyo maana kadi nyekundu aliyopewa siyo halali.
Kama tukifuata tu sheri za FIFA ili kujenga heshima yetu na kukuza nidhamu ya wachezaji wetu ambayo ni mbovu na ndiyo inayodidimiza soka letu, Yanga wana sababu ipi ya kutonyang'wanywa pointi tatu za mechi hii?
SOSI NI MIMI NA SHERIA ZA SOKA!