Hi wana JF! Kama ilivyo desturi yetu watanzania huwa hatuachi kupongezana hasa pale panapoonekana kuna jambo zuri limefanyika. Wengi mtakubaliana na mimi kuwa babu ni mjasiliamali alieibadilisha samonge na kuitangaza loliondo duniani kwa muda mfupi,babu amesababisha kushughulikiwa huduma muhimu kijamii kama vile umeme,maji,huduma za afya, mawasiliano na barabara. Ni vema wajasiliamali tuwe wabunifu kwa kuiga mfano wa babu ili tuharakishe maendeleo ktk maeneo yetu.