babu wa loliondo anazushiwa au kuna ukweli ndani yake?

MBUFYA

JF-Expert Member
Aug 15, 2011
445
68
nilikuwa mbeya siku moja watu niliokuwa nao wakaanza kujadili juu ya mchungaji mwaisapile eti kuwa wagonjwa wengi walio pata kikombe sasa wanakufa kwa kasi, wakaanza kutaja watu katika mtaa wao (uyole) walio toka kwa babu na mpaka sasa wamesha fariki.
pia nimewahi kusikiliza mahubiri ya msabato fulani kupitia cd yake naye anashuhudia mambo mengi ya kichawi na anasema watu wote waliopata kikombe kwa babu watakufa baada ya muda fulani, na akasema yeye anadawa ya kutoa sumu ya mchungaji.
wewe unasemaje?
 
kwani babu aliita mtu kule, kama walienda wao wenyewe kwa imani yao, kosa la babu liko wapi? hata kama amewapa dawa mchwara, hajaita mtu. Ukienda kwake ujue kitakachotokea kipo mikononi mwako, kwa sababu ulikuwa una uhuru wa kufanya vinginevyo, acheni kumsingizia babu wa watu, coz HAJAITA MTU KWAKE!
 
weka mambo waziwazi baba WANASEMA WATU WALIOKUNYWA KIKOMBE CHA BABU WATAKUFA BAADA YA MUDA GANI? Na sbb zitakazowaua ni nini?
 
siku za mwisho maandiko yanasema shetani ataleta magonjwa na kushusha miujiza ya kuyaponya ili watu waamini kwake soma Biblia na viatabu vya roho ya unabii na hasa kitabu cha matukio ya siku za mwisho utayaona haya na hasa uk 26 yanayomhusu babu na wenzake watakao jitokeza.
Mungu anatupenda na anataka tufungue akili zetu siku za mwisho zimefika.
naomba kuwasilishaaaaaaaaaaaaa
 
Back
Top Bottom