Inkoskaz
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 6,372
- 2,374
Kingunge ashindwa kumshukuru Kikwete
KADA Mkongwe wa CCM, Kingunge Ngombale Mwiru alishindwa kuzungumza "neno la shukurani" baada ya Rais Jakaya Kikwete kulihutubia taifa kupitia mkutano wa Wazee Mkoa wa Dar es Salaam.
Mzee Kingunge ambaye alikaa upande wa kushoto wa Rais Jakaya Kikwete wakati akihutubia Taifa juzi, alionekana kutokuwa tayari kusema neno hilo la shukrani licha ya Kaimu Mwenyekiti wa Wazee Mkoa wa Dar es Salaam, Brigedia Jenerali Hashim Mbita, kumsihi afanye hivyo.
Mbita aliyekuwa upande wa kulia wa Rais Kikwete, alisikika mara kadhaa kwenye kipaza sauti akimkaribisha Mwasisi huyo wa Chama, bila ya mafanikio .
Hata hivyo haikufahamika sababu za Kingunge kushindwa kutii ombi hilo ingawa alionyesha ishara ya kutokuwa tayari kufanya hivyo licha ya Mbita kuendelea kumsihi bila mafanikio.
Tukio hilo lilitokea wakati Brigedia Mbita alipokuwa akizingatia taratibu za kiitifaki za kutoa neno la shukrani baada ya Rais Kikwete kutoa hotuba.
Baada ya kitendo hicho kulionekana kuwepo kwa miguno kutoka kwa baadhi ya wazee waliohudhuria mkutano huo wakishindwa kuelewa kilichokuwa kikiendelea kwenye meza kuu.
Hatimaye baada ya jitihada za ushawishi kushindikana Mbita aliamua kutoa neno la shukrani kwa Rais Kikwete akibainisha kuwa hotuba yake imejaa nasaha nzuri na muhimu kwa Watanzania wote.
Katika hotuba hiyo Rais Kikwete alizungumzia mambo ambayo katika kipindi cha karibuni yamekuwa yanawagusa Watanzania wengi, yakiwemo yanayohusu matatizo ya kiuchumi na uundwaji wa katiba mpya.
Kuhusu uchumi, Kikwete aliwataka Watanzania kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho Tanzania na mataifa mengine duniani yanakabiliwa na athari za kiuchumi.
Miongoni mwa athari hizo alizozitaja ni pamoja na kasi ya mfumuko wa bei ambayo haijawahi kushuhudiwa katika historia ya nchi, kushuka kwa thamani ya shilingi, kupanda kwa bei ya mafuta na kuadimika kwa sukari inayozalishwa nchini kutokana na kuuzwa kimagendo kwa nchi jirani.
Alisema serikali yake iko mbioni kukabiliana na baadhi ya matatizo na moja wapo ni kuagiza sukari kutoka nje.
Lakini tatizo kama vile kupanda kwa bei ya mafuta na kushuka thamani ya sarafu huku dola ya kimarekani ikipaa, alisema ni tatizo kwa nchi nyingi duniani.
Kuhusu Katiba, Kikwete alipinga hoja zilizokuwa zikitolewa na Chadema pamoja na wanaharakati wa mabadiliko ya katiba.
Mojawapo ya hoja hizo, alisema wanapotosha kuwa suala la muungano limekatazwa kujadiliwa.
Ukweli alisema wanapinga kwenye mchakato wa kuandaa rasimu kujadili juu ya kuvunja muungano lakini wanaruhusu maoni ya namna ya kuuboresha.
Aliwahakikishia Watanzania kuwa katika mchakato wa kuandaa katiba hiyo, watakuwa huru katika kutoa maoni yao.
Lakini akaonyesha wasiwasi wake kuwa kuna makundi ya watu yanayoweza kuhamasisha watu juu ya mambo yenye maslahi kwao hivyo akaonya:
"Ninataka wananchi wawe huru. Mtu asilazimishwe la kusema."
Akijua wazi kuwa Chadema wamekuwa wakishinikiza mambo mbalimbali kwa maandamano kwa hoja ya kutumia nguvu ya umma, Kikwete akaonya:
"Jambo hili halihitaji maandamano… Vurugu hazina faida bali kuwaongezea machungu Watanzania. Hivyo naomba wawe na busara. Tuchague njia ya faraja. Tusichague njia ya machungu."
NIMEJIULIZA SIJAPATA JIBU HEBU WATAMBUZI NISAIDIENI MTAZAMO WENU!
KADA Mkongwe wa CCM, Kingunge Ngombale Mwiru alishindwa kuzungumza "neno la shukurani" baada ya Rais Jakaya Kikwete kulihutubia taifa kupitia mkutano wa Wazee Mkoa wa Dar es Salaam.
Mzee Kingunge ambaye alikaa upande wa kushoto wa Rais Jakaya Kikwete wakati akihutubia Taifa juzi, alionekana kutokuwa tayari kusema neno hilo la shukrani licha ya Kaimu Mwenyekiti wa Wazee Mkoa wa Dar es Salaam, Brigedia Jenerali Hashim Mbita, kumsihi afanye hivyo.
Mbita aliyekuwa upande wa kulia wa Rais Kikwete, alisikika mara kadhaa kwenye kipaza sauti akimkaribisha Mwasisi huyo wa Chama, bila ya mafanikio .
Hata hivyo haikufahamika sababu za Kingunge kushindwa kutii ombi hilo ingawa alionyesha ishara ya kutokuwa tayari kufanya hivyo licha ya Mbita kuendelea kumsihi bila mafanikio.
Tukio hilo lilitokea wakati Brigedia Mbita alipokuwa akizingatia taratibu za kiitifaki za kutoa neno la shukrani baada ya Rais Kikwete kutoa hotuba.
Baada ya kitendo hicho kulionekana kuwepo kwa miguno kutoka kwa baadhi ya wazee waliohudhuria mkutano huo wakishindwa kuelewa kilichokuwa kikiendelea kwenye meza kuu.
Hatimaye baada ya jitihada za ushawishi kushindikana Mbita aliamua kutoa neno la shukrani kwa Rais Kikwete akibainisha kuwa hotuba yake imejaa nasaha nzuri na muhimu kwa Watanzania wote.
Katika hotuba hiyo Rais Kikwete alizungumzia mambo ambayo katika kipindi cha karibuni yamekuwa yanawagusa Watanzania wengi, yakiwemo yanayohusu matatizo ya kiuchumi na uundwaji wa katiba mpya.
Kuhusu uchumi, Kikwete aliwataka Watanzania kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho Tanzania na mataifa mengine duniani yanakabiliwa na athari za kiuchumi.
Miongoni mwa athari hizo alizozitaja ni pamoja na kasi ya mfumuko wa bei ambayo haijawahi kushuhudiwa katika historia ya nchi, kushuka kwa thamani ya shilingi, kupanda kwa bei ya mafuta na kuadimika kwa sukari inayozalishwa nchini kutokana na kuuzwa kimagendo kwa nchi jirani.
Alisema serikali yake iko mbioni kukabiliana na baadhi ya matatizo na moja wapo ni kuagiza sukari kutoka nje.
Lakini tatizo kama vile kupanda kwa bei ya mafuta na kushuka thamani ya sarafu huku dola ya kimarekani ikipaa, alisema ni tatizo kwa nchi nyingi duniani.
Kuhusu Katiba, Kikwete alipinga hoja zilizokuwa zikitolewa na Chadema pamoja na wanaharakati wa mabadiliko ya katiba.
Mojawapo ya hoja hizo, alisema wanapotosha kuwa suala la muungano limekatazwa kujadiliwa.
Ukweli alisema wanapinga kwenye mchakato wa kuandaa rasimu kujadili juu ya kuvunja muungano lakini wanaruhusu maoni ya namna ya kuuboresha.
Aliwahakikishia Watanzania kuwa katika mchakato wa kuandaa katiba hiyo, watakuwa huru katika kutoa maoni yao.
Lakini akaonyesha wasiwasi wake kuwa kuna makundi ya watu yanayoweza kuhamasisha watu juu ya mambo yenye maslahi kwao hivyo akaonya:
"Ninataka wananchi wawe huru. Mtu asilazimishwe la kusema."
Akijua wazi kuwa Chadema wamekuwa wakishinikiza mambo mbalimbali kwa maandamano kwa hoja ya kutumia nguvu ya umma, Kikwete akaonya:
"Jambo hili halihitaji maandamano… Vurugu hazina faida bali kuwaongezea machungu Watanzania. Hivyo naomba wawe na busara. Tuchague njia ya faraja. Tusichague njia ya machungu."
NIMEJIULIZA SIJAPATA JIBU HEBU WATAMBUZI NISAIDIENI MTAZAMO WENU!