Baba yangu Mchawi... Anatuangamiza, nifanyeje?!

kifront

Member
Oct 29, 2011
6
1
Habarini wanajamvi,

Inahitaji moyo wa ujasiri sana kutokeza kwenye jukwaa lililojaa wasomi, wacha Mungu, na watu wenye exposure ya kutosha kuja na mada ya uchawi. Hadi naandika haya sijui am half confused. Mimi mwenyewe I don’t practice witchcraft and don’t believe in it lakini kuna sequence ya events zimekuwa zikiipata familia kwa almost 20years ambazo zimenifanya nianze kuona ukweli ndani yake. Here is the version of my story, will try to cut it short:
Baba ana mke wa ndoa kazaa watoto 5. Kaona bi mdogo kazaa 1. Katelekeza bi mkubwa na watoto japo anaishi karibu na wao. Baada ya miaka 4 kaachana na bibi mdogo karudi kwa mkubwa, kapokelewa kukaa nyumba moja japo vyumba tofauti. Kakasirika kaapa kuangamiza kizazi chake cha kiume kwa cost yeyote.

Kabla ya hayo yote, alikuwa mpenda ushirikina, kwa ajili ya kazi, kusafisha nyota, blab la ya kila aina, hila kwa wenzie, kugombea shamba na kila aina ya kitu unachojua uanweza apply uchawi. Begi lake limejaa makorokocho ya aina hiyo.

Anafungua biashara mkoa mwingine na kuondoka, anatelekeza familia tena na kuhakikisha hasomeshi motto yeyote wa kiume. Kwa hisani ya Mungu katika hali ya umaskini wa kifedha, najikuta nafaulu to gov schools from primary to university na kuanza support waliobaki(though baba aliwahi nitamkia “ Nikiamua hata ww hufiki popote”

Wakati nikiwa kidato cha kwanza tuliwahi ambiwa na mtu wa karibu kuwa kaka zenu hawatakaa wawe watu na akili zao timamu, watakuwa walevi wa kupindikia then wehu kama Mr. Y.

Mr. Y, aliwahifanya kazi na baba, akiwa timamu na familia yake, wakakorofishana, akapoteza kazi, kawa mlevi, mwehu kasha kafa.

Mr. Z, kaka angu, kawa mlevi wa kupindukia, kawa partial mwehu, ….
Mr. Q, kaacha chuo bila sababu, kawa mlevi wa kupindukia……
Mr. A, baada ya kuona yaliyowapata wenzie katoroka home kujiokoa, still doing good huko aliko

Kifront, kafanyiwa hila baada ya kununua shamba hadi alikose na baba yake, kalikosa na kurudishiwa pesa, kifront anamwuliza “kwa nini baba” Anajibiwa bado mdogo hizo hela wapata wapi? Mshangao !! Baba anatishia uhai wa watoto wa kifront kwa kusema “ Nikiamua hata hao watoto wako kesho hawaamki, kisa haelewani na mkwewe”

Nimeandika vitu vichache sana just kujaribu kuonesha picture.

Mitihani niliyonayo, nitasaidiaje hii familia?
  1. Kwenda kwa mganga sijawahi, and my conscious wont let me free
  2. Kuendelea kumtegemea Mungu kama ilivyo kawaida yangu, naona majibu yanachelewa na shetani anaendelea kula familia apendavyo

WHAT DO I DO PEOPLE? WOTE NYUMBANI WANANITEGEMEA MIMI KWA MASULUHISHO AND AM JUST 26YRS SINA EXPERIENCE YA MAISHA KIHIVYO.
 
Du, nakushauri endeleeni kumuomba mungu na hao ambao wameshachanganyikiwa wapelekeni kwenye majumba ya ibada wakapatiwe huduma ya maombi mara kwa mara. pia jaribuni kuwapeleka hospital muhimbili kitengo cha saikologia wanaweza kuwasaidia
 
Mimi kama mimi siamini uchawi upo na najua nikikaa na wewe ukanielewesha vizuri nitakupa sababu kwa most of hivyo vitu. NIngekushahuri uache uoga maana uoga wako wenyewe ndio utakusababishia matatizo.
Nauna unaamuni Mungu yupo, basi endelea kumtegemea. Usisemi jibu linachelewa, Jibu litakuja when needed, kwa sasa Mungu anajua bado unanguvu la kujishindia hapo, kupitia imani yako. Kumbuka Mungu hawezi kumwacha shetani akujaribu juu ya nguvu yako.
Jaribu kum-ignore na kuendelea maisha kama kawaida, achana nae kwa muda na wala usimuogope kabisa.
 
my dear mungu anajibu na unapoona unaaanza kukata tamaa ndo majibu ya maombi yako yanakuja na usipokuwa makini na kukata tamaa shetani lazima atazidi kufanya maisha yako magumu zaidi .endelea kusali tena ikiwezekana tafuta mtumishi mmoja akusaidie kukuongoza cause kunamisingi ya kuomba ili ujibiwe waganga watakuzidishia matatizo zaidi
 
Leo nakutana na madai yahusuyo uchawi kwa mara ya pili hapa JF!

Juu ya hivyo sijawahi kusikia uchawi wa kuroga watu wakawa walevi

Binafsi naamini ni coincidence tu. Endelea kumtegemea Mungu na uendele na shughuli zako kama kawaida
 
Endelea Kumuomba Mungu na ufanye jitihada kubwa kumuwezesha huyo mzazi wako amjue Mungu, Matatizo yote yataisha.
 
@Gaijin;
Umechangia kiasi kwa mie ku-post hii thread baada ya kuona ulivyo-comment kwa mtu mmoja aliyesema kaka yake karogwa. Nikaona na mie nipost hiki kisa changu maana naona imani inaanza kutiswa na ibilisi. Jamani If I could give you details of my story, mtashngaa tunayofanyiwa na huyu mtu. Any way thanks for your comments, will help me to stand still and let God move katika kipindi hiki kigumu. So sad to see the people you grew up together happily going mud for no reason.
Imagine the position of our mom, I cant tell.
 
Achana na ushirikina ndugu yangu. Hauna msaada wowote zaidi ya kukufanya uwe mtumwa. Ukisikia au kuona chochote unachanganyikiwa. Huwezi amini wale wanaoiutumia wanapata shida za aina gani. Kuna mtu alikuwa anafanya ziara kwenye wizara mbalimbali nchi fulani siitaji jina, kwasababu ya kuogopa kulogwa na wale anaowaita wabaya wake alikuwa anabeba kiti toka nyumbani kwake. Imagine ni utumwa wa aina gani huo!!!
 
uchawi uko na hata kwenye vitabu vitakatifu vimeandika, Ushauri wangu kwako ni kumtumaini MUNGU kumwomba bila kukata tamaa kwani yeye pekee ndo anaweza kukulinda wewe na familia yako,
 
@Gaijin;
Umechangia kiasi kwa mie ku-post hii thread baada ya kuona ulivyo-comment kwa mtu mmoja aliyesema kaka yake karogwa. Nikaona na mie nipost hiki kisa changu maana naona imani inaanza kutiswa na ibilisi. Jamani If I could give you details of my story, mtashngaa tunayofanyiwa na huyu mtu. Any way thanks for your comments, will help me to stand still and let God move katika kipindi hiki kigumu. So sad to see the people you grew up together happily going mud for no reason.
Imagine the position of our mom, I cant tell.

Pole sana.

Jaribu kufuta kichwani kuwa uchawi unahusika na utizame Kama unaweza kuwasaidia kwa kupitia wataalamu wa tiba

Omba sana na mama pia nae aelekeze Shukrani zake na kumiachia Mungu yote yanayotokea
 
Pole sana,dogo ulipoambiwa kuwa uyaone ndo kama hayo!Kwa ushauri ni kwamba ili uwe salama ni kuwa opposite na uchawi,namna ya kufanya hivyo ni kuwa msafi wa matendo na kufikiri,kwa kufanya hivyo hataweza kukufanya kitu ma utaiokoa familia!
 
Pole sana mkuu,kwangu naweza kwambia mtegemee Mungu zaidi na jibidiishe na maombi kwa sana kwai Mungu atakuongoza vema
 
Muombe mungu kwa sana hakuna litakalo kufika mpaka mungu atake,usisahau kua yeye pia ni kiumbe wa mungu kama ulivyo wewe,na ni mwenyezi mungu peke yake mwenye uwezo akisema KUA INAKUA sio binadamu hata kidogo...
 
Hii kitu inaitwa uchawi mimi naisikia tu na nimekutana na watu wanauamini kama ambavyo wengine tunaamini katika Mungu. Mimi nadhani dawa ni wewe kuendelea na imani yako bila kuchakachua na waganga wa kienyeji kwani inawezekana ndio pekee inayokusaidia usiharibikiwe kama wenzako. Ukianza safari za kwenda kwa waganga watakuchanganya zaidi na wewe utaishia kuwa mlevi/mwehu.
 
pole mpendwa!! uchami mi nauogopa kuliko hata jambazi!! mtumainie mungu asie shindwa na kitu chochote!!
 
dawaa yake ndogooo...nguvu ziada itumikeeee,mkatee kidevuuu...mkoroogieni sumu afee au tumeni majambazii wamuuwe au tafutaa wataalamu wamfunzeee.ilaaa unaweza kutaa sio uchawiii kunaaa watu wanamidomo mibayaaa,akiongea kitu chake lazimaaa kitatokeaaa
 
Tumia Shinyanga / Tabora Technique ukiwa umevaa miwani ya Mbao umalize udhia.
 
Back
Top Bottom